babalao 2
JF-Expert Member
- Apr 6, 2012
- 5,399
- 3,243
Moshi. Mikoa ya Kilimanjaro na Tanga,
imeonyesha kuwa na matumani ya kuwa na
utajiri mkubwa wa mafuta.
Mkoa wa Kilimanjaro pia umeonekana kuwa
na dalili za kuwa na madini ya urani na
kuufanya mkoa huo wenye mlima mrefu
kuliko yote Afrika, kuwa na uwezekano wa
kuwa na utajiri wenye manufaa makubwa
kwa Tanzania.
Wakuu wa mikoa hiyo, jana walithibitisha
kuwa tafiti zilizofanyika kwa nyakati tofauti,
zimethibitisha matumaini ya utajiri huo.
Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro, Leonidas Gama
alisema katika mkoa wake mafuta
yamegundulika katika Bonde Pangani katika
vijiji vya wilaya za Moshi Vijijini, Mwanga na
Same.
Ni kweli kuna watu wanafanya utafiti wa
mafuta pale Chekereni Moshi Vijijini kuna
mwelekeo wa kupatikana kwa mfuta katika
bonde lote hilo kuanzia Same hadi Moshi
Vijijini, alisema Gama.
Gama alisema ishara za kuwepo kwa mafuta
ndizo zilizosukuma kuanza kwa utafiti huo.
Tusubiri tuone yakipatikana itakuwa ni
neema kwa Kilimanjaro na taifa, alisema.
Wakati mkuu wa mkoa akisema hivyo,
Mbunge wa Mwanga ambaye pia ni Waziri wa
Maji, Profesa Jumanne Maghembe, naye
alithibitisha kuwepo kwa dalili za kupatikana
kwa mafuta katika ukanda huo.
Ni kweli walianzia utafiti wao pale Ziwa
Chala na Ziwa Jipe halafu wakaenda hadi
Kijiji cha Butu mpaka Mkomazi pale jimboni
kwangu na kuna dalili za kuwapo kwa
mafuta, alisema Profesa Maghembe.
Profesa Maghembe alisema taarifa za
wataalamu wa miamba pia zinaonyesha
kugunduliwa kwa madini ya Urani katika
milima ya Kijiji cha Kivisini.
Hii ni neema kwa kweli kwa sababu
rasilimali zote hizi mbili zikigunduliwa hapa
kwetu ni manufaa makubwa ya kiuchumi si
kwa mkoa tu lakini kwa taifa zima hili si
jambo dogo, alisema waziri.
Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Chiku Gallawa
alisema dalili za kuwepo kwa mafuta katika
ukanda wa bahari ya mkoa wake, zimeanza
kuonyesha matumaini na utafiti kwamba
unatarajia kukamilika mwaka ujao.
imeonyesha kuwa na matumani ya kuwa na
utajiri mkubwa wa mafuta.
Mkoa wa Kilimanjaro pia umeonekana kuwa
na dalili za kuwa na madini ya urani na
kuufanya mkoa huo wenye mlima mrefu
kuliko yote Afrika, kuwa na uwezekano wa
kuwa na utajiri wenye manufaa makubwa
kwa Tanzania.
Wakuu wa mikoa hiyo, jana walithibitisha
kuwa tafiti zilizofanyika kwa nyakati tofauti,
zimethibitisha matumaini ya utajiri huo.
Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro, Leonidas Gama
alisema katika mkoa wake mafuta
yamegundulika katika Bonde Pangani katika
vijiji vya wilaya za Moshi Vijijini, Mwanga na
Same.
Ni kweli kuna watu wanafanya utafiti wa
mafuta pale Chekereni Moshi Vijijini kuna
mwelekeo wa kupatikana kwa mfuta katika
bonde lote hilo kuanzia Same hadi Moshi
Vijijini, alisema Gama.
Gama alisema ishara za kuwepo kwa mafuta
ndizo zilizosukuma kuanza kwa utafiti huo.
Tusubiri tuone yakipatikana itakuwa ni
neema kwa Kilimanjaro na taifa, alisema.
Wakati mkuu wa mkoa akisema hivyo,
Mbunge wa Mwanga ambaye pia ni Waziri wa
Maji, Profesa Jumanne Maghembe, naye
alithibitisha kuwepo kwa dalili za kupatikana
kwa mafuta katika ukanda huo.
Ni kweli walianzia utafiti wao pale Ziwa
Chala na Ziwa Jipe halafu wakaenda hadi
Kijiji cha Butu mpaka Mkomazi pale jimboni
kwangu na kuna dalili za kuwapo kwa
mafuta, alisema Profesa Maghembe.
Profesa Maghembe alisema taarifa za
wataalamu wa miamba pia zinaonyesha
kugunduliwa kwa madini ya Urani katika
milima ya Kijiji cha Kivisini.
Hii ni neema kwa kweli kwa sababu
rasilimali zote hizi mbili zikigunduliwa hapa
kwetu ni manufaa makubwa ya kiuchumi si
kwa mkoa tu lakini kwa taifa zima hili si
jambo dogo, alisema waziri.
Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Chiku Gallawa
alisema dalili za kuwepo kwa mafuta katika
ukanda wa bahari ya mkoa wake, zimeanza
kuonyesha matumaini na utafiti kwamba
unatarajia kukamilika mwaka ujao.