Hii imekaa safi saaaaaana.
Wakati sisi Bara tunapigana na CCM, wenzetu mko busy saaana mkiisaidia. Kama si CUF, Chadema wangelishinda Kigoma majimbo mengi sana.
Kama Lipumba na CUF wangelitoa msaada kwa Slaa na kutupa mgombea mwenza wa maana, mambo yangelikuwa mengine kabisa sasa hivi. Sasa wote tumeingizwa Jando na CCM. Ila nyie lenu ndiyo baya zaidi maana ni lile la Kimasai, bila ganzi na mbele ya wanawake na unalazimishwa USILIE maana wewe ni Mwanaume (ehh, Mapanga shashasha).
Cha ajabu hata mwaka 2015, bado mtataka kuisaliti Chadema na kujifanya mko karibu na CCM na CCM bila hiyana wataendelea kuwa-do. Mwiba na kundi lako kumshambulia Dr Slaa kiko wapi sasa? Kimekula kwenu. Mlijifanya mnawaamini sana CCM, ona sasa. Mmekuwa kama Manyumbu mnaita Fisi awe Mkunga wenu, kaaazi kwelikweli.
Maadamu Lisu, Sugu, Wenje, Mbowe, Zitto, Mnyika wanaingia bungeni, ngoja ninywe Gongo langu hapa Sikonge.
To hell all of you, bila kujali wewe ni CUF, CCM, Chadema au sijui nani.
Mwakani MOTO utawaka pale DODOMA na Dom patakuwa hapatoshi.
Ahhhh, dada yangu Halima Mdee, mwaka 2015 tunaweza kuwa wote Dodoma nikiwakilisha Sikonge na kuwa mbunge wa kwanza wa Upinzani wa Mkoa wa Tabora. Ila leo, All of you u can go to hell, gongo langu uko wapi? Nyama Pori kwa wingi hapa nikisherehekea. Kesho nikiamka, naanza vita na waliochakachua matokeo ya SLAA. SLAA wewe ni Rais wangu bila kujali matokeo.
LALI MPOLA nawaambia wote.
Duh! Hapo Sikonge nimekukubali!