Kilichotokea kwa Zambians vs Chinese kwa ZESCO ndicho kilichopo kwa Tanzanians vs Chinese kwa TAZARA

kanewi

JF-Expert Member
Jun 12, 2012
298
199
Nimeandika hapa ni baada ya kupata habari toka humu jamvini inayohusu Uchina kutaka kulichukua na kuwa chini yao shirika mamlaka ya umeme la Zambia,na hii ni baada ya kushindwa kulipa mkopo usio na masharti toka kwa wachina. Hadithi hii haina tofauti na kilichotokea hapa kwetu kwa TAZARA,tulipatiwa mkopo mkubwa sana na wachina usio na riba wala masharti yoyote,tumeshindwa kulipa na ndio maana hata kufikiria kulibinafsisha inakuwa ngumu.

China ndio wenye kauri ya mwisho,tafakuri yangu inachagizwa na huu mkopo ulioahidiwa na Uchina ktk mkutano wa hivi karibuni,tuwe makini sana na hela za wachina,kama hakuna ulazima wa hela hizi ni bora tuachane nazo,tusikope bali wapewe fulsa ya kuwekeza tu.
 
Hayo unamwambia nani? Kumbuka msemo huu " sikio la kufa" sio kwamba huu msemo umeanza jana.
 
Ndugu Kanewi, mchina ameshatuondoa katika marafiki zake 5 bora barani Afrika, na yote hayo ni kwa sababu Raisi Magufuli aligomea kuendelea na mikopo miwili mikubwa.

1. BANDARI YA BAGAMOYO
2. RELI YA SGR KUTOKA DAR HADI MWANZA NA KIGOMA.

Magufuli alikataa mikopo hiyo kwani haikuwa mizuri kwa nchi, ilikuwa ghali sana na haikuendana na miradi yenyewe. Ilikuwa na dosari nyingi, hilo limemuudhi sana mchina.

Hata hivi juzi majaliwa amepewa muda mdogo sana wa kuona na Raisi wa china.
 
Kwa ile mikataba mibovu walioipitisha vichwa maji wa ccm tutegemee na hapa kwetu lolote linaweza tokea.
 
Mikopo isiyo na masharti sasa inakuwaje wanakuja kuchukua mashirika na makampuni waliyofinance?
 
Nimeandika hapa ni baada ya kupata habari toka humu jamvini inayohusu Uchina kutaka kulichukua na kuwa chini yao shirika mamlaka ya umeme la Zambia,na hii ni baada ya kushindwa kulipa mkopo usio na masharti toka kwa wachina. Hadithi hii haina tofauti na kilichotokea hapa kwetu kwa TAZARA,tulipatiwa mkopo mkubwa sana na wachina usio na riba wala masharti yoyote,tumeshindwa kulipa na ndio maana hata kufikiria kulibinafsisha inakuwa ngumu.

China ndio wenye kauri ya mwisho,tafakuri yangu inachagizwa na huu mkopo ulioahidiwa na Uchina ktk mkutano wa hivi karibuni,tuwe makini sana na hela za wachina,kama hakuna ulazima wa hela hizi ni bora tuachane nazo,tusikope bali wapewe fulsa ya kuwekeza tu.
Nashindwa kuelewa hapa "tulipatiwa mkopo mkubwa sana na wachina usio na riba wala masharti yoyote" inakuwaje hauna masharti yoyote ilakishindwa kulipa wajichagulie masharti? Wanasiasa wetu waache uhuni kutudanganya kisa kura huku wanauza nchi
 
Back
Top Bottom