Na Maggid Mjengwa
UKWELI ni majeruhi wa kwanza pande mbili zinapoingia kwenye mapambano. Ndivyo inavyokuwa. Maana, kwenye vita yeyote iwayo, risasi ya kwanza huelekezwa kwenye ukweli. Ndio, ukweli hufichwa na uongo hutamalaki hata kama utapewa jina jingine, kuwa ni propaganda.
Ni nini basi tafsiri ya kilichotokea Igunga?
Igunga kumejitokeza ishara za yanayotarajiwa kutokea huko twendako. Na tujipe kazi ya kuzisoma ishara hizo za nyakati. Kuna niliyoyaona na yanifanyayo niendelee kutafakari. Kuna mapya pia yanayojitokeza hata baada ya matokeo kutangazwa. Yanatutaka tufikiri kwa bidii zaidi.
Kubwa nililoliona ni pigo tulilolipata sote kama taifa. Kwamba Igunga imetudhihirishia, kuwa tuna safari ndefu katika ujenzi wa demokrasia yetu na kuifanya nchi yetu kuwa ya kisasa zaidi. Tumeingia kwenye siasa za vyama kukamiana na kuwa na ushabiki kama wa vilabu vya mpira. Kama ni ujenzi wa nyumba ya ghorofa hamsini, basi, tuko kwenye kukusanya kokoto. Hatujaanza hata kuchimba msingi.
Tumeona kule Igunga, kuwa vyama vikubwa vilivyoshiriki uchaguzi huo vimetumia fedha na rasilimali nyingi kugombania kiti kimoja. Hi isi ishara njema.
Na katika muktadha huo huo, nadiriki kuandika, kuwa kama CCM itaondolewa madarakani 2015 na CHADEMA inayoonekana sasa, basi , CHADEMA haitakuwa chama bora tawala ikiwa na CCM dhaifu kama ilivyo sasa kwenye kambi ya upinzani ifikapo 2015.
Labda si wengi walioona, lakini, kuna ukweli kuwa, kuna kubwa limetokea Igunga. Kuwa CUF imekwenda Igunga, imejichimbia kaburi na imejizika yenyewe. Walichovuna CUF Igunga si kingine bali ni janga la kisiasa. CUF wamefanya vibaya sana pamoja na kuanza na kinachoitwa mtaji wa kura 11,000. Na Naibu Katibu Mkuu wa CUF bara, Julius Mtatiro ameonyesha ujasiri wa kisiasa kukiri hadharani kilichowatokea.
Tumesikia, kuwa CUF wameitwa 'CCM B'. Si Wana Igunga tu, hata Watanzania wengi wanaonekana kukubaliana na CHADEMA na kuwaona CUF kwa na sura hiyo. Kama wanataka wafufuke, CUF wana lazima ya kujipanga upya.
Na kibaya hapo ni ukweli, kuwa CUF wamepoteza nafasi ya kuwa chama cha pili kikubwa cha upinzani bara baada ya CHADEMA. Na NCCR Mageuzi wajitafakari namna watakavyorudi tena kwenye ulingo wa siasa. Wakizicheza vibaya karata zao, basi, CHADEMA, wamekamata mhuri wa ' CCM C' na hawatakuwa na mkono mzito kwenye kuugonga kwenye paji la uso wa NCCR – Mageuzi.
Na si jambo jema kwa nchi kama ni CHADEMA tu itakayobaki kuwa chama kikubwa cha upinzani na kinachoaminika kuwa kina sura hiyo ya upinzani , kwamba CHADEMA si kibaraka wa chama tawala. Maana, siku ile CCM na CHADEMA watakapoamua kuunda Serikali ya Mseto , basi, nchi yetu itabaki bila ya chama cha upinzani. Hiyo ni hatari kwa demokrasia tuliyodhamiria kuijenga.
Igunga imetudhihirishia kuwa bado tuna viongozi wa hovyo hovyo, wanaoamini kuwa WaTanzania wote ni watu wa hovyo hovyo, bila kutambua kuwa ni wao, kama viongozi, ndio watu wa hovyo hovyo wanaotufanya WaTanzania wote tuonekane kuwa ni watu wa hovyo hovyo.
Na kuna taasisi tatu katika nchi hii ambazo zinaweza kabisa zikatufikisha kwenye kuwaona watu wetu wakichinjana na tukabaki kuililia nchi yetu huku tukijalumu kuwa tuliona ishara lakini hatukuwa wakweli kwa nchi yetu. Kwamba tuliamua kukaa kimya tukiendekeza njaa zetu na kuisaliti nchi yetu tuliyozaliwa.
Ni taasisi gani hizi zinazoweza kutufikisha kwenye umwagaji damu?
Tume ya Uchaguzi, Jeshi la Polisi na Vyombo vya habari. Siku zote nimesisitiza, kuwa historia ni mwalimu mzuri. Katika nchi zetu hizi, taasisi hizo tatu ndio zimekuwa chanzo cha maafa ya nchi nyingi za Kiafrika. Wahenga walisema; kujifunza kuanzie kwa jirani yako.
Ndio, tumeona hata kwa jirani zetu wa Kenya. Kwamba Tume ya Uchaguzi, Jeshi la Polisi na Vyombo vya habari vilichangia vurugu, mauaji na hasara kubwa kuafuatia matokeo ya uchaguzi mkuu wa Kenya uliopita.
Leo WaKenya wamepata Katiba mpya na kuanza kusonga mbele, lakini, wakiwa na makovu na hata machungu yaliyobaki kwa yaliyotokea huko nyuma. WaKenya walikuwa na uwezo wa kuzuia kilichotokea. Lakini, nao pia, walikuwa na viongozi wa hovyo hovyo waliodhani WaKenya wote ni watu wa hovyo hovyo. Na matokeo ya dhania hiyo dunia nzima imeyaona.
Hivyo basi, kule Igunga WaTanzania tumeshaziona ishara, kuwa kama nchi yetu itakwenda kwenye Uchaguzi Mkuu wa 2015 bila kuufanyia mabadiliko ya kimsingi mfumo wetu wa uchaguzi ikiwamo uwepo wa Tume Huru ya Uchaguzi, bila kuwa na Katiba itakayolifanya Jeshi la Polisi kutenda haki kwa raia na vyama vyote vya siasa kwa wakati wote na bila kuwa na vyombo huru vya habari , basi , sihitaji kuwa na maarifa ya elimu ya nyota kuweza kutabiri machafuko ya kisiasa yakayopelekea madhara makubwa ya kijamii na kiuchumi kwa nchi yetu.
Maana, WaTanzania kwa asili ni watu watulivu na wenye kupenda amani. WaTanzania hawa kwa kawaida watakwenda kwenye mikutano ya siasa na watawasikiliza wanasiasa. Na siku ya kupiga kura watakwenda kupiga kura kwa amani.
Ni vyama vya siasa na baadhi ya wanasiasa ndio wenye kutumia hila , ghilba na hata , kwa kutumia fedha, hutokea wakagharamia vurugu ili baadae kwa kuvilipa vyombo vya habari na hata baadhi ya wana habari, watajenga taswira ya uongo juu ya uwepo wa vurugu na hata kusukuma lawama kwa wapinzani wao wa kisiasa.
Kisha , jeshi la polisi nalo, kwa ama kutojiamini kwa baadhi ya viongozi wa jeshi hilo au kusukumwa kisiasa, nao wataingia kwenye mapambano na wafuasi wa vyama na hata viongozi wa vyama. Na hapo ndipo chuki inapozaa chuki na silaha inapozaa silaha. Ni balaa.
Na uwepo wa Tume ya Uchaguzi isiyo huru unapelekea Tume kuwa na viongozi wasiojiamini, hivyo basi, kuendesha shughuli za uchaguzi katika hali ya mashaka na hata kuegemea upande mmoja. Na katika nchi zetu hizi, siku zote, tabu inakuja kwenye shughuli ya kuhesabu kura na kutangaza matokeo. Joseph Stalin wa Urusi ya zamani alipata kutamka; Katika uchaguzi wowote ule, mpiga kura si anayeamua matokeo, bali mhesabu kura!
Tunachojifunza kwenye kauli hiyo ya Jeseph Stalini ni ukweli, kuwa kikubwa katika mchakato wa uchaguzi ni uwepo wa imani kwa wanaondesha mchakato huo. Kama vyama vya siasa na hata wapiga kura watakosa imani na aliyeteuliwa kuendesha mchakato na hata kuhesabu kura zao, basi, matokeo ya chaguzi yanaweza kuwa chanzo cha vurugu za kisiasa.
Na si tuliona? Kuwa nchi nzima ilihamia Igunga. Kuna wengi tuliopumua kwamba ya Igunga yamepita bila madhara makubwa. Turudi sasa kwenye mengine ya kila siku. Maana, hata msomaji wangu, mchuuzi wa samaki pale Soko Kuu Igunga naye amepumua. Ni baada ya kukoswakoswa panga alipokuwa akipita nje ya Hotel ya Peak pale Igunga siku ile vurugu zilipoanza.
Na hapo ndipo tulipofikia WaTanzania, kwamba chaguzi zetu zimekuwa chanzo cha mashaka badala ya kutupa matumaini ya kwenda mbele. Na sasa ni kuanzia ngazi ya udiwani. Haya ndio mambo ya hovyo hovyo yanayotufanya tuonekane kuwa ni watu wa hovyo hovyo. Tuna uwezo na kila sababu ya kuandaa taratibu za kuendesha mambo yetu kistaarabu. Nahitimisha.
MJENGWA - Picha, Habari & Matangazo
UKWELI ni majeruhi wa kwanza pande mbili zinapoingia kwenye mapambano. Ndivyo inavyokuwa. Maana, kwenye vita yeyote iwayo, risasi ya kwanza huelekezwa kwenye ukweli. Ndio, ukweli hufichwa na uongo hutamalaki hata kama utapewa jina jingine, kuwa ni propaganda.
Ni nini basi tafsiri ya kilichotokea Igunga?
Igunga kumejitokeza ishara za yanayotarajiwa kutokea huko twendako. Na tujipe kazi ya kuzisoma ishara hizo za nyakati. Kuna niliyoyaona na yanifanyayo niendelee kutafakari. Kuna mapya pia yanayojitokeza hata baada ya matokeo kutangazwa. Yanatutaka tufikiri kwa bidii zaidi.
Kubwa nililoliona ni pigo tulilolipata sote kama taifa. Kwamba Igunga imetudhihirishia, kuwa tuna safari ndefu katika ujenzi wa demokrasia yetu na kuifanya nchi yetu kuwa ya kisasa zaidi. Tumeingia kwenye siasa za vyama kukamiana na kuwa na ushabiki kama wa vilabu vya mpira. Kama ni ujenzi wa nyumba ya ghorofa hamsini, basi, tuko kwenye kukusanya kokoto. Hatujaanza hata kuchimba msingi.
Tumeona kule Igunga, kuwa vyama vikubwa vilivyoshiriki uchaguzi huo vimetumia fedha na rasilimali nyingi kugombania kiti kimoja. Hi isi ishara njema.
Na katika muktadha huo huo, nadiriki kuandika, kuwa kama CCM itaondolewa madarakani 2015 na CHADEMA inayoonekana sasa, basi , CHADEMA haitakuwa chama bora tawala ikiwa na CCM dhaifu kama ilivyo sasa kwenye kambi ya upinzani ifikapo 2015.
Labda si wengi walioona, lakini, kuna ukweli kuwa, kuna kubwa limetokea Igunga. Kuwa CUF imekwenda Igunga, imejichimbia kaburi na imejizika yenyewe. Walichovuna CUF Igunga si kingine bali ni janga la kisiasa. CUF wamefanya vibaya sana pamoja na kuanza na kinachoitwa mtaji wa kura 11,000. Na Naibu Katibu Mkuu wa CUF bara, Julius Mtatiro ameonyesha ujasiri wa kisiasa kukiri hadharani kilichowatokea.
Tumesikia, kuwa CUF wameitwa 'CCM B'. Si Wana Igunga tu, hata Watanzania wengi wanaonekana kukubaliana na CHADEMA na kuwaona CUF kwa na sura hiyo. Kama wanataka wafufuke, CUF wana lazima ya kujipanga upya.
Na kibaya hapo ni ukweli, kuwa CUF wamepoteza nafasi ya kuwa chama cha pili kikubwa cha upinzani bara baada ya CHADEMA. Na NCCR Mageuzi wajitafakari namna watakavyorudi tena kwenye ulingo wa siasa. Wakizicheza vibaya karata zao, basi, CHADEMA, wamekamata mhuri wa ' CCM C' na hawatakuwa na mkono mzito kwenye kuugonga kwenye paji la uso wa NCCR – Mageuzi.
Na si jambo jema kwa nchi kama ni CHADEMA tu itakayobaki kuwa chama kikubwa cha upinzani na kinachoaminika kuwa kina sura hiyo ya upinzani , kwamba CHADEMA si kibaraka wa chama tawala. Maana, siku ile CCM na CHADEMA watakapoamua kuunda Serikali ya Mseto , basi, nchi yetu itabaki bila ya chama cha upinzani. Hiyo ni hatari kwa demokrasia tuliyodhamiria kuijenga.
Igunga imetudhihirishia kuwa bado tuna viongozi wa hovyo hovyo, wanaoamini kuwa WaTanzania wote ni watu wa hovyo hovyo, bila kutambua kuwa ni wao, kama viongozi, ndio watu wa hovyo hovyo wanaotufanya WaTanzania wote tuonekane kuwa ni watu wa hovyo hovyo.
Na kuna taasisi tatu katika nchi hii ambazo zinaweza kabisa zikatufikisha kwenye kuwaona watu wetu wakichinjana na tukabaki kuililia nchi yetu huku tukijalumu kuwa tuliona ishara lakini hatukuwa wakweli kwa nchi yetu. Kwamba tuliamua kukaa kimya tukiendekeza njaa zetu na kuisaliti nchi yetu tuliyozaliwa.
Ni taasisi gani hizi zinazoweza kutufikisha kwenye umwagaji damu?
Tume ya Uchaguzi, Jeshi la Polisi na Vyombo vya habari. Siku zote nimesisitiza, kuwa historia ni mwalimu mzuri. Katika nchi zetu hizi, taasisi hizo tatu ndio zimekuwa chanzo cha maafa ya nchi nyingi za Kiafrika. Wahenga walisema; kujifunza kuanzie kwa jirani yako.
Ndio, tumeona hata kwa jirani zetu wa Kenya. Kwamba Tume ya Uchaguzi, Jeshi la Polisi na Vyombo vya habari vilichangia vurugu, mauaji na hasara kubwa kuafuatia matokeo ya uchaguzi mkuu wa Kenya uliopita.
Leo WaKenya wamepata Katiba mpya na kuanza kusonga mbele, lakini, wakiwa na makovu na hata machungu yaliyobaki kwa yaliyotokea huko nyuma. WaKenya walikuwa na uwezo wa kuzuia kilichotokea. Lakini, nao pia, walikuwa na viongozi wa hovyo hovyo waliodhani WaKenya wote ni watu wa hovyo hovyo. Na matokeo ya dhania hiyo dunia nzima imeyaona.
Hivyo basi, kule Igunga WaTanzania tumeshaziona ishara, kuwa kama nchi yetu itakwenda kwenye Uchaguzi Mkuu wa 2015 bila kuufanyia mabadiliko ya kimsingi mfumo wetu wa uchaguzi ikiwamo uwepo wa Tume Huru ya Uchaguzi, bila kuwa na Katiba itakayolifanya Jeshi la Polisi kutenda haki kwa raia na vyama vyote vya siasa kwa wakati wote na bila kuwa na vyombo huru vya habari , basi , sihitaji kuwa na maarifa ya elimu ya nyota kuweza kutabiri machafuko ya kisiasa yakayopelekea madhara makubwa ya kijamii na kiuchumi kwa nchi yetu.
Maana, WaTanzania kwa asili ni watu watulivu na wenye kupenda amani. WaTanzania hawa kwa kawaida watakwenda kwenye mikutano ya siasa na watawasikiliza wanasiasa. Na siku ya kupiga kura watakwenda kupiga kura kwa amani.
Ni vyama vya siasa na baadhi ya wanasiasa ndio wenye kutumia hila , ghilba na hata , kwa kutumia fedha, hutokea wakagharamia vurugu ili baadae kwa kuvilipa vyombo vya habari na hata baadhi ya wana habari, watajenga taswira ya uongo juu ya uwepo wa vurugu na hata kusukuma lawama kwa wapinzani wao wa kisiasa.
Kisha , jeshi la polisi nalo, kwa ama kutojiamini kwa baadhi ya viongozi wa jeshi hilo au kusukumwa kisiasa, nao wataingia kwenye mapambano na wafuasi wa vyama na hata viongozi wa vyama. Na hapo ndipo chuki inapozaa chuki na silaha inapozaa silaha. Ni balaa.
Na uwepo wa Tume ya Uchaguzi isiyo huru unapelekea Tume kuwa na viongozi wasiojiamini, hivyo basi, kuendesha shughuli za uchaguzi katika hali ya mashaka na hata kuegemea upande mmoja. Na katika nchi zetu hizi, siku zote, tabu inakuja kwenye shughuli ya kuhesabu kura na kutangaza matokeo. Joseph Stalin wa Urusi ya zamani alipata kutamka; Katika uchaguzi wowote ule, mpiga kura si anayeamua matokeo, bali mhesabu kura!
Tunachojifunza kwenye kauli hiyo ya Jeseph Stalini ni ukweli, kuwa kikubwa katika mchakato wa uchaguzi ni uwepo wa imani kwa wanaondesha mchakato huo. Kama vyama vya siasa na hata wapiga kura watakosa imani na aliyeteuliwa kuendesha mchakato na hata kuhesabu kura zao, basi, matokeo ya chaguzi yanaweza kuwa chanzo cha vurugu za kisiasa.
Na si tuliona? Kuwa nchi nzima ilihamia Igunga. Kuna wengi tuliopumua kwamba ya Igunga yamepita bila madhara makubwa. Turudi sasa kwenye mengine ya kila siku. Maana, hata msomaji wangu, mchuuzi wa samaki pale Soko Kuu Igunga naye amepumua. Ni baada ya kukoswakoswa panga alipokuwa akipita nje ya Hotel ya Peak pale Igunga siku ile vurugu zilipoanza.
Na hapo ndipo tulipofikia WaTanzania, kwamba chaguzi zetu zimekuwa chanzo cha mashaka badala ya kutupa matumaini ya kwenda mbele. Na sasa ni kuanzia ngazi ya udiwani. Haya ndio mambo ya hovyo hovyo yanayotufanya tuonekane kuwa ni watu wa hovyo hovyo. Tuna uwezo na kila sababu ya kuandaa taratibu za kuendesha mambo yetu kistaarabu. Nahitimisha.
MJENGWA - Picha, Habari & Matangazo