Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,474
- 39,987
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (Bara) Bw. Pius Msekwa amesema kuwa mgongano na hatimaye kumeguka kwa chama cha ANC kabla ya uchaguzi wao Mkuu wa Rais na Wabunge hakiwezi kutokea kwenye Chama cha Mapinduzi.
Ameyasema hayo akiwa Afrika Kusini kusherekehea kuapishwa kwa Rais mpya wa nchi hiyo Bw. Jacob Zuma. Vyama vya ANC na CCM vina historia ya muda mrefu ya ushirikiano na urafiki kwa miongo mingi sasa.
Wakati huo huo; Mbunge wa Igunga Mhe. Rostam Aziz naye alikuwa Afrika ya Kusini siku ya Jumamosi katika kile kilichoelezewa kuwa ni shughuli zake binafsi. Hata hivyo vinzi vinavyoruka ruka vimeelezea pia ilikuwa ni nafasi kwa RA kukutana na Rais Kikwete ambaye naye alikuwa SA katika sherehe ya kuapishwa kwa Bw. Zuma.
Baada ya sakata lake na mfanyabiashara Mengi na hasa mwelekeo wa kisheria ambao sakata hilo limechukua kuna mambo ambayo Bw. RA alitaka kuhakikisha mkuu wa nchi anayasikia na kuyafahamu na vile vile kufahamu msimamo wake.
Rais Kikwete inadokezwa kuwa alifanya safari toka Uskandinavia kuelekea Afrika Kusini kwenye sherehe ya Zuma na anatarajiwa kuelekea Marekani ambako kuna uwezeekano pia wa kukutana na Rais mpya wa Marekani Bw. Barack Obama..
Ameyasema hayo akiwa Afrika Kusini kusherekehea kuapishwa kwa Rais mpya wa nchi hiyo Bw. Jacob Zuma. Vyama vya ANC na CCM vina historia ya muda mrefu ya ushirikiano na urafiki kwa miongo mingi sasa.
Wakati huo huo; Mbunge wa Igunga Mhe. Rostam Aziz naye alikuwa Afrika ya Kusini siku ya Jumamosi katika kile kilichoelezewa kuwa ni shughuli zake binafsi. Hata hivyo vinzi vinavyoruka ruka vimeelezea pia ilikuwa ni nafasi kwa RA kukutana na Rais Kikwete ambaye naye alikuwa SA katika sherehe ya kuapishwa kwa Bw. Zuma.
Baada ya sakata lake na mfanyabiashara Mengi na hasa mwelekeo wa kisheria ambao sakata hilo limechukua kuna mambo ambayo Bw. RA alitaka kuhakikisha mkuu wa nchi anayasikia na kuyafahamu na vile vile kufahamu msimamo wake.
Rais Kikwete inadokezwa kuwa alifanya safari toka Uskandinavia kuelekea Afrika Kusini kwenye sherehe ya Zuma na anatarajiwa kuelekea Marekani ambako kuna uwezeekano pia wa kukutana na Rais mpya wa Marekani Bw. Barack Obama..