Kilichotokea ANC, hakiwezi kutokea CCM - Msekwa

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,474
39,987
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (Bara) Bw. Pius Msekwa amesema kuwa mgongano na hatimaye kumeguka kwa chama cha ANC kabla ya uchaguzi wao Mkuu wa Rais na Wabunge hakiwezi kutokea kwenye Chama cha Mapinduzi.

Ameyasema hayo akiwa Afrika Kusini kusherekehea kuapishwa kwa Rais mpya wa nchi hiyo Bw. Jacob Zuma. Vyama vya ANC na CCM vina historia ya muda mrefu ya ushirikiano na urafiki kwa miongo mingi sasa.

Wakati huo huo; Mbunge wa Igunga Mhe. Rostam Aziz naye alikuwa Afrika ya Kusini siku ya Jumamosi katika kile kilichoelezewa kuwa ni shughuli zake binafsi. Hata hivyo vinzi vinavyoruka ruka vimeelezea pia ilikuwa ni nafasi kwa RA kukutana na Rais Kikwete ambaye naye alikuwa SA katika sherehe ya kuapishwa kwa Bw. Zuma.

Baada ya sakata lake na mfanyabiashara Mengi na hasa mwelekeo wa kisheria ambao sakata hilo limechukua kuna mambo ambayo Bw. RA alitaka kuhakikisha mkuu wa nchi anayasikia na kuyafahamu na vile vile kufahamu msimamo wake.

Rais Kikwete inadokezwa kuwa alifanya safari toka Uskandinavia kuelekea Afrika Kusini kwenye sherehe ya Zuma na anatarajiwa kuelekea Marekani ambako kuna uwezeekano pia wa kukutana na Rais mpya wa Marekani Bw. Barack Obama..
 
Rais Kikwete inadokezwa kuwa alifanya safari toka Uskandinavia kuelekea Afrika Kusini kwenye sherehe ya Zuma na anatarajiwa kuelekea Marekani ambako kuna uwezeekano pia wa kukutana na Rais mpya wa Marekani Bw. Barack Obama..

Duh! Kama ni kweli sasa huyu bwana itabidi afokewe ili akae nyumbani kwa angalau siku 120 bila kusafiri. Yaani yeye kila kukicha safari safari tu...anaenda kufanya nini kwenye hizo safari? Gotdamnit
 
ana watendaji kibao, wacha atembee tu!

Kwa nchi zilizo makini hicho cheo kinaitwa Roving Ambassador lakini hapa bongo anajulikana kama President of the United Republic of Tanzania. Tatizo la akina Kibunango ni kuwa hamwezi kutofautisha which is which. This is really sad.
 
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (Bara) Bw. Pius Msekwa amesema kuwa mgongano na hatimaye kumeguka kwa chama cha ANC kabla ya uchaguzi wao Mkuu wa Rais na Wabunge hakiwezi kutokea kwenye Chama cha Mapinduzi.

Ameyasema hayo akiwa Afrika Kusini kusherekehea kuapishwa kwa Rais mpya wa nchi hiyo Bw. Jacob Zuma. Vyama vya ANC na CCM vina historia ya muda mrefu ya ushirikiano na urafiki kwa miongo mingi sasa.

Wakati huo huo; Mbunge wa Igunga Mhe. Rostam Aziz naye alikuwa Afrika ya Kusini siku ya Jumamosi katika kile kilichoelezewa kuwa ni shughuli zake binafsi. Hata hivyo vinzi vinavyoruka ruka vimeelezea pia ilikuwa ni nafasi kwa RA kukutana na Rais Kikwete ambaye naye alikuwa SA katika sherehe ya kuapishwa kwa Bw. Zuma.

Baada ya sakata lake na mfanyabiashara Mengi na hasa mwelekeo wa kisheria ambao sakata hilo limechukua kuna mambo ambayo Bw. RA alitaka kuhakikisha mkuu wa nchi anayasikia na kuyafahamu na vile vile kufahamu msimamo wake.

Rais Kikwete inadokezwa kuwa alifanya safari toka Uskandinavia kuelekea Afrika Kusini kwenye sherehe ya Zuma na anatarajiwa kuelekea Marekani ambako kuna uwezeekano pia wa kukutana na Rais mpya wa Marekani Bw. Barack Obama..

Kwanini wasikutane oceanroad/kivukoni, kulikoni-TISS wana vyombo vya kunasa ufisadi?:D
 
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (Bara) Bw. Pius Msekwa amesema kuwa mgongano na hatimaye kumeguka kwa chama cha ANC kabla ya uchaguzi wao Mkuu wa Rais na Wabunge hakiwezi kutokea kwenye Chama cha Mapinduzi.

Ameyasema hayo akiwa Afrika Kusini kusherekehea kuapishwa kwa Rais mpya wa nchi hiyo Bw. Jacob Zuma. Vyama vya ANC na CCM vina historia ya muda mrefu ya ushirikiano na urafiki kwa miongo mingi sasa.

Wakati huo huo; Mbunge wa Igunga Mhe. Rostam Aziz naye alikuwa Afrika ya Kusini siku ya Jumamosi katika kile kilichoelezewa kuwa ni shughuli zake binafsi. Hata hivyo vinzi vinavyoruka ruka vimeelezea pia ilikuwa ni nafasi kwa RA kukutana na Rais Kikwete ambaye naye alikuwa SA katika sherehe ya kuapishwa kwa Bw. Zuma.

Baada ya sakata lake na mfanyabiashara Mengi na hasa mwelekeo wa kisheria ambao sakata hilo limechukua kuna mambo ambayo Bw. RA alitaka kuhakikisha mkuu wa nchi anayasikia na kuyafahamu na vile vile kufahamu msimamo wake.

Rais Kikwete inadokezwa kuwa alifanya safari toka Uskandinavia kuelekea Afrika Kusini kwenye sherehe ya Zuma na anatarajiwa kuelekea Marekani ambako kuna uwezeekano pia wa kukutana na Rais mpya wa Marekani Bw. Barack Obama..

Duh! Kumbe ni kweli RA hakupata nafasi ya kuwasiliana na JK? No wonder ushahidi na nyaraka za siri vinaibiwa huko kwa kina IGP Mwema na mkemia mkuu!
JK kaoa ndugu ya RA na Said Mwema naye kaoa kwakina JK kama sijakosea,sasa haya ni mambo kifamilia ama?
Kama kweli RA kaamua kumfungia safari JK hadi SA...Basi mambo si mambo kwa mafisadi.
Tusubiri tuone huu mkorogo matokeo yake ni nini,lakini kuna watu hawataki kuachia utamu kwani umenoga.
Tulishauri tume ya ukweli na maridhiano hapa JF,na Zitto na yeye aliiwakilisha huko,hawakusikiliza,sasa naona kama imefikia stage ambayo ni irreversible kwasababu ya kiburi.
Ama kweli hakuna marefu yasiyokuwa na ncha na hakuna mwanzo usiokuwa na mwisho....Kelele za mlango hatimaye zimemkosesha usingizi mpangaji. lol!
Kwa anayedhani kupanga ikulu=usingizi mnono amekosea!
 
Kwa nchi zilizo makini hicho cheo kinaitwa Roving Ambassador lakini hapa bongo anajulikana kama President of the United Republic of Tanzania. Tatizo la akina Kibunango ni kuwa hamwezi kutofautisha which is which. This is really sad.
Kwa nchi kama hii, yenye wasifa wa umatonya unategemea nini?
 
Duh! Kumbe ni kweli RA hakupata nafasi ya kuwasiliana na JK? No wonder ushahidi na nyaraka za siri vinaibiwa huko kwa kina IGP Mwema na mkemia mkuu!
JK kaoa ndugu ya RA na Said Mwema naye kaoa kwakina JK kama sijakosea,sasa haya ni mambo kifamilia ama?
Kama kweli RA kaamua kumfungia safari JK hadi SA...Basi mambo si mambo kwa mafisadi.
Tusubiri tuone huu mkorogo matokeo yake ni nini,lakini kuna watu hawataki kuachia utamu kwani umenoga.
Tulishauri tume ya ukweli na maridhiano hapa JF,na Zitto na yeye aliiwakilisha huko,hawakusikiliza,sasa naona kama imefikia stage ambayo ni irreversible kwasababu ya kiburi.
Ama kweli hakuna marefu yasiyokuwa na ncha na hakuna mwanzo usiokuwa na mwisho....Kelele za mlango hatimaye zimemkosesha usingizi mpangaji. lol!
Kwa anayedhani kupanga ikulu=usingizi mnono amekosea!

- Saafi sana Mkulu Mushi, tupo pamoja sana hapa.

FMEs!
 
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (Bara) Bw. Pius Msekwa amesema kuwa mgongano na hatimaye kumeguka kwa chama cha ANC kabla ya uchaguzi wao Mkuu wa Rais na Wabunge hakiwezi kutokea kwenye Chama cha Mapinduzi.

Ameyasema hayo akiwa Afrika Kusini

Msekwa akiwa ndani ya S. Africa, katika ujumbe wa Rais wa TZ, mgeni wa ANC, hakutakiwa kuongea hivyo. Ki-diplomasia hilo ni sawa na kujigamba au kukosoa siasa za ndani za wengine. ANC bado wana hasira, hawakupenda huo mpasuko, umesababisha Zuma akose super majority bungeni aliyoitegemea kusaidia agenda zake, kama kufumua mfumo wa judiciary. Msekwa anafyatua tu bila clue ya state of affairs ugenini. Viongozi wetu kidiplomasia ni taabani vilaza. Ambacho kinasishangaza sana, huyu Msekwa alianza kuwa Katibu Mkuu Mtendaji wa chama toka mwaka 1967, mpaka leo hapati clue?

Au ni hawa waleta habari wetu ni watupu choka hawasemi mazingira, mada, context, ya maongezi ilikuwa nini.
 
Rais Kikwete inadokezwa kuwa alifanya safari toka Uskandinavia kuelekea Afrika Kusini kwenye sherehe ya Zuma na anatarajiwa kuelekea Marekani ambako kuna uwezeekano pia wa kukutana na Rais mpya wa Marekani Bw. Barack Obama..
tehe tehe hilo wese toka uskandi mpaka bondeni kisaha pipa hiloo linakata wingu mpaka majuu kudadadeki na akitoka huko atapitia UK kukagua matangazo ya juma pinto kwa siku 3.......

.....sijawahi kuona taifa ambalo kiongozi wake mkuu anaongoza nchi akiwa ndani ya ndege.....zaidi ya tanzania..
 
hamna marefu yasiyo na ncha.

Rashidi alisema,yanamwisho(kitabu cha Kuli)

Kama kazomewa busanda,tena na Tingatinga,basi asiwe na imani mgando,abadilike.Lolote laweza kutokea na kumeguka ni uwezekano mmojawapo
 
Msekwa akiwa ndani ya S. Africa, katika ujumbe wa Rais wa TZ, mgeni wa ANC, hakutakiwa kuongea hivyo. Ki-diplomasia hilo ni sawa na kujigamba au kukosoa siasa za ndani za wengine. ANC bado wana hasira, hawakupenda huo mpasuko, umesababisha Zuma akose super majority bungeni aliyoitegemea kusaidia agenda zake, kama kufumua mfumo wa judiciary. Msekwa anafyatua tu bila clue ya state of affairs ugenini. Viongozi wetu kidiplomasia ni taabani vilaza. Ambacho kinasishangaza sana, huyu Msekwa alianza kuwa Katibu Mkuu Mtendaji wa chama toka mwaka 1967, mpaka leo hapati clue?

Au ni hawa waleta habari wetu ni watupu choka hawasemi mazingira, mada, context, ya maongezi ilikuwa nini.

- Ulipaswa kujua kwanza Msekwa ameongelea katika mazingara gani kabla hujakurupuka na uncalled accusations ambazo huna uhakika aliposemea ni wapi, haiwezekani Msekwa amesema hayo mbele ya public, ni lazima alikuwa anaongea na waandishi wa bongo akaulizwa kuhusu the ishu, lakini mtu hahitaji kuwa Professor ku-figure that out!

Resepct.

FMEs!
 
tehe tehe hilo wese toka uskandi mpaka bondeni kisaha pipa hiloo linakata wingu mpaka majuu kudadadeki na akitoka huko atapitia UK kukagua matangazo ya juma pinto kwa siku 3.......

.....sijawahi kuona taifa ambalo kiongozi wake mkuu anaongoza nchi akiwa ndani ya ndege.....zaidi ya tanzania..

Hivi ni nchi gani huyu Kikwete ambayo hajafika?
 
Ulipaswa kujua kwanza Msekwa ameongelea katika mazingara gani kabla hujakurupuka na uncalled accusations ambazo huna uhakika aliposemea ni wapi, haiwezekani Msekwa amesema hayo mbele ya public, ni lazima alikuwa anaongea na waandishi wa bongo akaulizwa kuhusu the ishu, lakini mtu hahitaji kuwa Professor ku-figure that out!

Hata kama Msekwa anaongea na waandishi wa Bongo, chochote kile unachokitoa mdomoni mwako kwa waandishi kinakuwa ni public declaration, hakuna siri kwenye siasa na waandishi. Sio lazima uongee jukwaani ndio iwe gaffe. Sasa hivi Balozi wa South Afrika Tanzania akisoma press ya Bongo akaona hii na ikamsumbua, Msekwa hawezi kudai oooh, ilikuwa ni siri yangu na waandishi wa Kibongo. Hizi ni a-be-che za diplomasia.

Aidha waandishi wetu taabani wanapotosha context au ni gaffe la Msekwa kuingilia ya ANC ndani ya S.Africa
 
Hivi ni nchi gani huyu Kikwete ambayo hajafika?
huwa naona viongozi kadhaa wanaongea au kuajdiliana na viongozi wenzao kwa simu badala ya kufunga safari kwenda kuongea nae huko.....kwanini muungwana asimpandie heani obama wakalonga wamalizane kwenye simu?
 
Hivi ni nchi gani huyu Kikwete ambayo hajafika?

Kikwete hajafika Tanzania huru isiyo na ufisadi, inayoendelea kiuchumi bila porojo, inayojari generation inaykkuja, yenye rais anayejua hali halisi ya maendeleo nchini kwa macho yake na si kaumbiwa, yenye rais anayekaa ofini kwake na kufanya maamuzi ya mambo magumu ya kimaenddeleo, ninakuhakikishia Kikwete hajafika hiyo Tanzania
 
Kikwete hajafika Tanzania huru isiyo na ufisadi, inayoendelea kiuchumi bila porojo, inayojari generation inaykkuja, yenye rais anayejua hali halisi ya maendeleo nchini kwa macho yake na si kaumbiwa, yenye rais anayekaa ofini kwake na kufanya maamuzi ya mambo magumu ya kimaenddeleo, ninakuhakikishia Kikwete hajafika hiyo Tanzania

Anyway mdau hapo juu kasema JK ni Roving Ambassador, wacha atalii
 
Back
Top Bottom