habari ya hapa
JF-Expert Member
- Dec 20, 2012
- 12,791
- 8,739
Heshima kwenu wanajamvi,
Leo katika pilikapilika zangu za hapa na pale, nikiwa na biashara zangu za kukopesha madera, vyupi, sidiria nk.
Nalipata kukutana na bwana mmoja hivi mitaa fulani hapa jijini, twafahamiana kidogo, isipokuwa hatujapata kuonana kitambo, bwana yule alifurahi aliponiona hali kadhalika bibi mie nilifurahika pia.
Bwana yule hakutaka tusimame sana tulipokutania, badala yake alitaka niingie ofisini kwake kutoka tuliposimama jengo lapili yake ili nipafahamu, basi nalifanya hivyo bila hiana.
Tulipoingia alinitambulisha kwa watu wake, baadae tukaingia ndani ofisini kwake sasa, bwana yule alitaka nikae kwa kiti, nalifanya hivyo pasi na shaka, tuliongea mawili matatu nikataka kuondoka, nikamwambia bwana yule, wacha niende nishapafahamu tena nitakuja wakati mwingine, akasema sawa.
Ile nainuka toka kwa kiti na yeye anainuka alipoketi, kumwangalia vizuri bwana yule tayari suruali yake hapa mbele palivimba sana, ile nasogelea mlango akanambia bibi wewe, nikamwitika bwana wewe! Akasema inamaana hujaona? Nikamuuliza, sijaona nini?
Akasema huoni bwana huyu anataka kuchana suruali, nikaguna kidogo, nikamwambia bwana wewe sijui nini wasema, Mara paap! Akanisogelea, nilistuka kidogo, nikamwambia bwana wewe samahani nachelewa kukusanya madeni yangu, nitakujia wakati mwingine, akaniambia sasa waniachaje na hali hii? Hakyanani niliishiwa pozi.
Bahati nzuri wakati natafakari nimtulize kwa jibu gani, secretary wake akagonga mlango, ndo ikawa njia ya bibi mie kutoka mbio kwenye hilo tundu la sindano.
Sijamuelewa bwana yule, zile ni nyege gani? Maana yake nini kunivimbishia mdude wake tena ofisini kwake? Ni mtu ambaye twaheshimiana sana kanishangaza mno.
Yule secretary nimemshukuru sana, maana nyege mshindo alizonionyesha bosi wake si za sayari hii.
Leo katika pilikapilika zangu za hapa na pale, nikiwa na biashara zangu za kukopesha madera, vyupi, sidiria nk.
Nalipata kukutana na bwana mmoja hivi mitaa fulani hapa jijini, twafahamiana kidogo, isipokuwa hatujapata kuonana kitambo, bwana yule alifurahi aliponiona hali kadhalika bibi mie nilifurahika pia.
Bwana yule hakutaka tusimame sana tulipokutania, badala yake alitaka niingie ofisini kwake kutoka tuliposimama jengo lapili yake ili nipafahamu, basi nalifanya hivyo bila hiana.
Tulipoingia alinitambulisha kwa watu wake, baadae tukaingia ndani ofisini kwake sasa, bwana yule alitaka nikae kwa kiti, nalifanya hivyo pasi na shaka, tuliongea mawili matatu nikataka kuondoka, nikamwambia bwana yule, wacha niende nishapafahamu tena nitakuja wakati mwingine, akasema sawa.
Ile nainuka toka kwa kiti na yeye anainuka alipoketi, kumwangalia vizuri bwana yule tayari suruali yake hapa mbele palivimba sana, ile nasogelea mlango akanambia bibi wewe, nikamwitika bwana wewe! Akasema inamaana hujaona? Nikamuuliza, sijaona nini?
Akasema huoni bwana huyu anataka kuchana suruali, nikaguna kidogo, nikamwambia bwana wewe sijui nini wasema, Mara paap! Akanisogelea, nilistuka kidogo, nikamwambia bwana wewe samahani nachelewa kukusanya madeni yangu, nitakujia wakati mwingine, akaniambia sasa waniachaje na hali hii? Hakyanani niliishiwa pozi.
Bahati nzuri wakati natafakari nimtulize kwa jibu gani, secretary wake akagonga mlango, ndo ikawa njia ya bibi mie kutoka mbio kwenye hilo tundu la sindano.
Sijamuelewa bwana yule, zile ni nyege gani? Maana yake nini kunivimbishia mdude wake tena ofisini kwake? Ni mtu ambaye twaheshimiana sana kanishangaza mno.
Yule secretary nimemshukuru sana, maana nyege mshindo alizonionyesha bosi wake si za sayari hii.