Kilichojiri bungeni Tarehe 13 April (Muswada wa mafao)

Ni mwendelezo tu wa sera beberu na kandamizi za serikali ya chama cha magamba. Sera kama hii hailengi kumsaidia mwananchi hata kidogo bali kulinda maslahi binafsi ya watawala. Ni wazi fedha nyingi za mifuko ya jamii kama NSSF zimetumika kufanikisha masilahi ya kisiasa ya watawala bila kujali zitarejeshwa vipi! Ni wazi mifuko hii haiwezi kuendelea kuwa hai, hivyo njia ya kuinusuru ni kwa kupitisha sheria kama hizi. Poleni sana wadau waadhirika wa sheria kandamizi. Saa ya ukombozi inakaribia, GET READY.
 
" Muswada
umeandaliwa kwa kuwashirikisha Wadau wote wa Sekta ya
Hifadhi ya Jamii, wakiwemo Wafanyakazi, Waajiri na Serikali,
ikiwemo Mifuko yenyewe kupitia Vikao vya Wadau na pia
Baraza la Ushauri wa Masuala ya Kazi Jamii na Uchumi, yaani
RESCO. Kimsingi, wadau wote waliunga mkono mapendekezo
yaliyomo katika Muswada huu."

Huyu Waziri ni muongo. Hivi lini tulishirikishwa wafanyakazi??

This is very bad indeed! mimi ni mfanyakazi wa serikali lakini kwa kweli sijawahi hata kuwaona hawa "mifuko" wakija mahali petu pa kazi, na hatujawahi kujadili jambo kama hili hata siku moja! Naapa kwa Jina la Bwana.
 
Nimejaribu kupita kwa haraka haraka lakini sijaona ukurasa unaozuia kuchukua hela yetu kabla ya kustaafu. Please alieona huo ukurasa naomba aniambie ili nijaribu kuupitia manake bado siamini ninachoendelea kukisikia!!

Hata mimi sijaona.
 
Ngoja mimi niulize kama nikiacha kazi na miaka 35, Je mwajiri wangu ataendelea kunichangia michango yangu ya NSSF/PPF mpaka nitapofikisha miaka 55 au 60 ya kuchukua mafao yangu?

Kama mwajiri hatanichangia na pesa yangu ikaendelea kuwa ile ile, Je thamani yake itakuwaje baada ya miaka 20 nitakapofikisha miaka 55 ya kustaafu?. Taking into consideration inflation rate ya Tanzania ina stand 20% kwasasa.

Je kwa miaka hiyo 20 ambayo NSSF/PPF watakuwa na pesa yangu, mind you nitakuwa sichangii wala mwajiri hanichangii, Je nitalipwa na RIBA nitakapokwenda kuchukua mafao yangu.
 
Mkurugenzi wa SSRA ndani ya jahazi leo sijui kama kiu na hoja zetu zitapata majibu.
 
Nawapa benefit of doubt wabunge wa vyama vya upinzani kwa maana jinsi sheria zinavyopitishwa ("wanaoafiki waseme ndiyoo" etc) huwezi kutegemea wapinzani wasilkilizwe. Issue ni kuwang'oa magamba 2015 ili sheria za kipuuzi kama hii zibadilishwe
Katika hili wametusaliti. Hii issue inaathiri wengi sana. Kuna watu watalazimishwa kusubiri hadi umri wa kustaafu ambao hata hivyo hawa-qualify kwa mfano kwa kutotimiza miezi 180 ya kuchangia. How do you treat these people? Kwa umuhimu wa hili suala, hata kama wangezidiwa kwa uwingi wa wabunge wa CCM, walikuwa na wajibu wa kuujulisha umma kwenye mikutano yao kwamba walijitahidi kuzuia lakini wakazidiwa na magamba, kitu ambacho hawakufanya. Katika hili nao ni wasaliti.

Kuna mtu kaachishwa kazi leo baada ya kampuni iliyomuajiri kufilisika. Ukimwambia mtu huyu asubiri hadi 2015 atakapoing'oa CCM ndipo apewe hela yake sijui kama utaeleweka ikizingatiwa ukweli kuwa kwa uhaba wa ajira tulionao hana uhakika kama atapata kazi tena, na lini ataipata. Sheria hii ni ya kinyama.
 
" Muswada
umeandaliwa kwa kuwashirikisha Wadau wote wa Sekta ya
Hifadhi ya Jamii, wakiwemo Wafanyakazi, Waajiri na Serikali,
ikiwemo Mifuko yenyewe kupitia Vikao vya Wadau na pia
Baraza la Ushauri wa Masuala ya Kazi Jamii na Uchumi, yaani
RESCO. Kimsingi, wadau wote waliunga mkono mapendekezo
yaliyomo katika Muswada huu."

Huyu Waziri ni muongo. Hivi lini tulishirikishwa wafanyakazi??

mkuu mimi cjawahi hata cku moja kuhudhuria kikao kujadili khs mabadiliko ya hii sheria. hata ceo wangu anashangaa wapi walikaa na kuamua hivyo.
 
Hivi huo mkopo wa nyumba wanaozungumzia utawezekana vipi kwa mtu ambaye kapoteza ajira na ameshindwa kupata nyingine? Nasema hivyo kwa sababu mkopo unahitaji marejesho, itakuwaje kwa ambaye atakuwa hana kipato, atarejesha vipi? Nahisi changa la macho tu hilo!!
 
Hii ni dhuluma ya wazi. Wanajua kwamba si rahisi kwa <60% ya Watanzania kufikia umri huo wengi watakuwa wamekufa kutokana na maisha duni wanayoishi, kwa hiyo pesa yao itafia ndani.

Kama nimeacha/kuachishwakazi leo ambapo nina umri wa miaka 35, na mafao yangu ya NSSF ni milioni 15. Je baada ya miaka ishirini bila ajira, hayo mafao yatakuwa yameongezeka?

Kama hayatakuwa yameongezeka, kwanini msinipe sasa ili nihangaikie kwenye biashara ambapo kiwango mtakachonipa ni kile kile hata kama ingekaa baada ya miaka mia?

Zaidi sana hiyo pesa itakuwa imeshuka thamani sana tu.
 
kabla hujalaumu, soma ukurasa wa 142, uone mnyika alisema nini na wewe unataka nini huku ukiuelewa mfumo wa bunge lako chini ya MAGAMBA

wewe hiyo page umeona nini ambacho mnyika alitetea ukilinganisha na mkanganyiko huu wa miaka ya kustaafu?
mimi sijaona hilo nionyeshe kiongozi
 
Soma hapa wanatuchezea hawa
Aidha, marekebisho hayo yameweka wazi umri wa kustaafu kwa hiari kwa mwanachama kuwa ni kuanzia miaka 55, isipokuwa uanachama wake utakoma pale ambapo mwanachama huyo atatimiza umri wa miaka 60.

Inapendekezwa pia kwamba, mwanachama ambaye hajatimiza muda wa kuchangia, yaani qualified period, anapostaafu apewe michango yake na ya mwajiri pamoja na riba. (Makofi)
 
Hii ni dhuluma ya wazi. Wanajua kwamba si rahisi kwa <60% ya Watanzania kufikia umri huo wengi watakuwa wamekufa kutokana na maisha duni wanayoishi, kwa hiyo pesa yao itafia ndani. Kama nimeacha/kuachishwakazi leo ambapo nina umri wa miaka 35, na mafao yangu ya NSSF ni milioni 15. Je baada ya miaka ishirini bila ajira, hayo mafao yatakuwa yameongezeka? Kama hayatakuwa yameongezeka, kwanini msinipe sasa ili nihangaikie kwenye biashara ambapo kiwango mtakachonipa ni kile kile hata kama ingekaa baada ya miaka mia? Zaidi sana hiyo pesa itakuwa imeshuka thamani sana tu.
Kwa interest rate ya NSSF ya 1.8%, hiyo 15m baada ya miaka 25, taking into consideration the sky rocketing inflation rate, itakuwa na thamani sawa na 5k.
 
Wadau nimesoma hii document na nafikiri wapinzani walifanya sehemu yao!

Nami nimepitia lakini kwa harak haraka nimekutana na zuio hili hapa katika ukurasa wa 68 kifungu cha ix na kifungu cha x katika ukurasa wa 76. Naendelea kusoma kwani nilikuwa na mpango wa kuachana na mwajiri wangu ili nichukue changu nijiwekee akiba (kuwekeza somewhere).

Uk. 68
(ix) Kifungu cha 31 cha Sheria ya Mfuko wa Pensheni wa Serikali za Mitaa, kinachozungumzia kuhusu maslahi ya mwanachama kujitoa kwenye Mfuko kwa sababu ya ndoa au uzazi, hakijafanyiwa marekebisho. Kamati inapendekeza kifanyiwe marekebisho ili kutoruhusu wanachama wanawake kujitoa kwenye uanachama kwa sababu ya ndoa au uzazi ili kwenda sambamba na dhana nzima ya hifadhi ya jamii.

Uk.76:
(x) Utaratibu wa sasa ambapo watumishi waliopo kwenye Mkataba mara wamalizapo muda wao kulipwa pensheni na wakati huo huo kuongezewa Mkataba mwingine. Kamati inaona utaratibu huu unaliingizia Taifa hasara na inapendekeza mtumishi akiongezewa Mkataba asilipwe kiinua mgongo mpaka pale atakapomaliza muda wa Mkataba alioongezewa.

Walioshiriki ktk kamati:

Ninapenda kuwatambua Wajumbe wa Kamati hii kwa majina:- Mheshimiwa Jenista Joakim Mhagama - Mwenyekiti,
Mheshimiwa Juma Selemani Nkamia - Makamu Mwenyekiti, Mheshimiwa John Damian Komba, Mheshimiwa Mch. Dkt. Getrude P. Rwakatare, Mheshimiwa Agnes Elias Hokororo, Mheshimiwa Fatuma Abdallah Mikidadi, Mheshimiwa Mary Pius Chatanda, Mheshimiwa Moza Abedi Saidy, Mheshimiwa Donald Kelvin Max, Mheshimiwa Joseph Osmund Mbilinyi na Mheshimiwa Hamad Ali Hamadi, Mheshimiwa Abdallah Sharia Ameir, Mheshimiwa Salum Khalfan Barwany, Mheshimiwa Mariam Salum Msabaha, Mheshimiwa Assumpter Nshunju Mshama, Mheshimiwa Asha Mohamed Omari, Mheshimiwa Ramadhani Haji Salehe, Mheshimiwa Rebecca Michael
Mngodo, Mheshimiwa Said Mohamed Mtanda, Mheshimiwa Abdallah Haji Ally, Mheshimiwa Hussein Mussa Mzee na
Mheshimiwa Livingstone Joseph Lusinde.
 
Haya ndo mojawapo ya vijimambo ambayo tunatakiwa kuvitumia kuwapiga ban hawa Magamba CCM, asilimia kubwa wameishastaafu na wameishavuta chao, wamekula future yao, wanakula ya kwetu na pia wanakula ya watoto wetu. Hatutaweza kuwavumilia! Walete kwanza hiyo formula ya kukokotoa ndo tujue mwanachama atanufaika kivipi kuliko kuanza kuzuia pesa zetu pasipo kuleta faida zake.
 
I argue wafanyakazi wote tuamke sasa,tuungane katika kuitoa hii serikali dhalimu,nssf hamna hela,wamepeleka wapi?
 
Ngoja mimi niulize kama nikiacha kazi na miaka 35, Je mwajiri wangu ataendelea kunichangia michango yangu ya NSSF/PPF mpaka nitapofikisha miaka 55 au 60 ya kuchukua mafao yangu?

Kama mwajiri hatanichangia na pesa yangu ikaendelea kuwa ile ile, Je thamani yake itakuwaje baada ya miaka 20 nitakapofikisha miaka 55 ya kustaafu?. Taking into consideration inflation rate ya Tanzania ina stand 20% kwasasa.

Je kwa miaka hiyo 20 ambayo NSSF/PPF watakuwa na pesa yangu, mind you nitakuwa sichangii wala mwajiri hanichangii, Je nitalipwa na RIBA nitakapokwenda kuchukua mafao yangu.
Ndiyo. Utalipwa riba ya 1.8%.
 
Nimeona thread moja ya haya mashirika kuwa na uwezekano wa kufilisika. Labda hii ni mbinu mojawapo kuyaokoa. Pia, baada ya jamaa kuchota fedha kwa miaka mingi katika haya mashirika sasa lazima tuyaokoe ili tujilinde.
 
Back
Top Bottom