Kilichoisambaratisha NCCR-Mageuzi ile ya 1995 ni nini?

Naipendatz

JF-Expert Member
Jul 27, 2011
5,080
8,217
Wazee kwa wale waliokuwa wafuatiliaji wa siasa zetu kipindi cha between 95 to 2000 naomba mnisaidie kwa hili! Ni sababu zipi zilisababisha kuanguka kwa lile chama ambalo lilikuwa tishio hadi kwa mkuu Nyerere? Is it unafiki? ulafi wa madaraka? uroho wa fedha? ukabila? ukanda? uzushi?......?

pls wazee naomba mnisaidia all the details and stories behind anguko la nccr ya enzi hizo?

CAN HISTORY REPEAT ITSELF TO CHADEMA?

TOFAUTI KUBWA NI NINI KATI YA CHADEMA YA SASA NA THAT NCCR???
 
Umetumwa lakini tutakusaidia usiwe na wasi

Kwanza hapakuwepo na matatizo makubwa sana ya kuwafanya watu waichukie ccm kama ilivyo sasa,pesa ilikuwa na thamani na ufisadi haukuwa mkubwa kama sahivi

Pili elimu ilikuwa bado ndogo kwa wananchi hvyo walikuwa hawana uwezo mkubwa wa kuchambua mambo tofauti na sasa wasomi ni wengi karibu kila familia kuna mtu kapita ama anasoma sec n,k

Tatu kuwepo kwa uhuru wa vyombo vya habari kumewafanya wananchi kuelewa mambo mengi waliyokuwa hawayajuhi yaliyokuwa yakiwafanya kuwa maskini k.v. rushwa,dili feki,ufisadi,kuuzwa kwa nchi yao n.k

Nategemea wenzangu wataelezea na mapungufu mengi ya nccr na kufa kwake
 
Watanzania walikuwa waoga wakati huo,sasa sivyo.Mabadiliko ya Kisiasa duniani ni tofauti kwa sasa na wakati huo.
 
Umetumwa lakini tutakusaidia usiwe na wasi

Kwanza hapakuwepo na matatizo makubwa sana ya kuwafanya watu waichukie ccm kama ilivyo sasa,pesa ilikuwa na thamani na ufisadi haukuwa mkubwa kama sahivi

Pili elimu ilikuwa bado ndogo kwa wananchi hvyo walikuwa hawana uwezo mkubwa wa kuchambua mambo tofauti na sasa wasomi ni wengi karibu kila familia kuna mtu kapita ama anasoma sec n,k

Tatu kuwepo kwa uhuru wa vyombo vya habari kumewafanya wananchi kuelewa mambo mengi waliyokuwa hawayajuhi yaliyokuwa yakiwafanya kuwa maskini k.v. rushwa,dili feki,ufisadi,kuuzwa kwa nchi yao n.k

Nategemea wenzangu wataelezea na mapungufu mengi ya nccr na kufa kwake

Mkuu mwaka 1995 Watanzania walikuwa na hamasa kubwa sana ila tu tatizo ilikuwa ni kwamba walikuwa wakimpenda mtu na si sera. Watanzania walimpenda Mrema. Nakumbuka siku alipojiunga na NCCR mageuzi mtaa wa Aggrey siku hiyo kadi za NCCR ziliuzwa kama karanga.

Vyombo vya habari hasa magazeti yalikuwepo mengi tu: Tazama, Motomoto, Majira, Cheche, n.k. Kuhusu suala la elimu ni kweli walikuwepo wachache ukilinganisha na sasa.

Watu wanasema Marando alichangia anguko kubwa la NCCR baada ya varangati kule Tanga na Mrema kutupwa nje kupitia dirishani. Ila mimi naamini NCCR ilikufa kwa sababu ya kugombea Ruzuku. Ruzuku kwenye Chama ni sumu kubwa na inawagombanisha watu.

Nakumbuka wakati huo NCCR kulikuwa na watu kama Anthony Komu (yupo CDM kwa sasa) na Mabere Marando na hawa walikuwa na nafasi yao kubwa tu katika kuanguka kwa NCCR Mageuzi.

Mkuu CHADEMA pia kuna fukuto kuhusu Ruzuku: Wangwe (mwenyezi mungu amrehemu) aliipigia kelele kwamba iende kuimarisha Chama mikoani badala ya kubaki makao makuu na kulipana madeni ya helcopita; bahati mbaya hatunaye. Kuna mambo yanenda chinichini kwamba ruzuku inaliwa na wakubwa kwa njia ya posho. Wakubwa wanalipwa posho kubwa wakati wakitekeleza majukumu ya chama lakini wa chini wanatakiwa wajitolee!!

Watu wameichoka CCM lakini CHADEMA wasipoangalia masuala ya posho na ruzuku yatawafarakanisha.
 
Labda ukisoma kitabu cha Ndimala Tegambwage, cha Mtafaruku na Hatima ya Mageuzi Tanzania utafahamu kwa undani zaidi. Pamoja na hayo yote, nikuhakikishie NCCR-Mageuzi itaendelea kuwepo.
 
Labda ukisoma kitabu cha Ndimala Tegambwage, cha Mtafaruku na Hatima ya Mageuzi Tanzania utafahamu kwa undani zaidi. Pamoja na hayo yote, nikuhakikishie NCCR-Mageuzi itaendelea kuwepo.

George weka hicho kitabu hapa kama unacho!
 
Wazee kwa wale waliokuwa wafuatiliaji wa siasa zetu kipindi cha between 95 to 2000 naomba mnisaidie kwa hili! Ni sababu zipi zilisababisha kuanguka kwa lile chama ambalo lilikuwa tishio hadi kwa mkuu Nyerere? Is it unafiki?ulafi wa madaraka?uroho wa fedha?ukabila?ukanda?uzushi?......?pls wazee naomba mnisaidia all the details and stories behind anguko la nccr ya enzi hizo? CAN HISTORY REPEAT ITSELF TO CHADEMA? TOFAUTI KUBWA NI NINI KATI YA CHADEMA YA SASA NA THAT NCCR???

NCCR imesambaratika lini wewe au unaharisha maneno! NCCR ipo labda CCJ ndio imesambaratika.
 
Mkuu mwaka 1995 Watanzania walikuwa na hamasa kubwa sana ila tu tatizo ilikuwa ni kwamba walikuwa wakimpenda mtu na si sera. Watanzania walimpenda Mrema. Nakumbuka siku alipojiunga na NCCR mageuzi mtaa wa Aggrey siku hiyo kadi za NCCR ziliuzwa kama karanga.

Vyombo vya habari hasa magazeti yalikuwepo mengi tu: Tazama, Motomoto, Majira, Cheche, n.k. Kuhusu suala la elimu ni kweli walikuwepo wachache ukilinganisha na sasa.

Watu wanasema Marando alichangia anguko kubwa la NCCR baada ya varangati kule Tanga na Mrema kutupwa nje kupitia dirishani. Ila mimi naamini NCCR ilikufa kwa sababu ya kugombea Ruzuku. Ruzuku kwenye Chama ni sumu kubwa na inawagombanisha watu.

Nakumbuka wakati huo NCCR kulikuwa na watu kama Anthony Komu (yupo CDM kwa sasa) na Mabere Marando na hawa walikuwa na nafasi yao kubwa tu katika kuanguka kwa NCCR Mageuzi.

Mkuu CHADEMA pia kuna fukuto kuhusu Ruzuku: Wangwe (mwenyezi mungu amrehemu) aliipigia kelele kwamba iende kuimarisha Chama mikoani badala ya kubaki makao makuu na kulipana madeni ya helcopita; bahati mbaya hatunaye. Kuna mambo yanenda chinichini kwamba ruzuku inaliwa na wakubwa kwa njia ya posho. Wakubwa wanalipwa posho kubwa wakati wakitekeleza majukumu ya chama lakini wa chini wanatakiwa wajitolee!!

Watu wameichoka CCM lakini CHADEMA wasipoangalia masuala ya posho na ruzuku yatawafarakanisha.

Wangwe Bangi zilikuwa zinamsumbua na alidanganywa na UWT kupitia wastaafu wa Jeshi kutoka Tarime kuikengeuka CDM. Baada wao kuona wamemshirikisha mambo mengi ambayo yote hayakuzaa matunda walikuwa hawana jinsi maana siri zao bado walitaka ziendelee kuwa siri.
 
walifitiniwa, na kwa cdm nawasihi wawe makini na wanachama wahamiaji toka ccm!
 
Umetumwa lakini tutakusaidia usiwe na wasi<br />
<br />
Kwanza hapakuwepo na matatizo makubwa sana ya kuwafanya watu waichukie ccm kama ilivyo sasa,pesa ilikuwa na thamani na ufisadi haukuwa mkubwa kama sahivi<br />
<br />
Pili elimu ilikuwa bado ndogo kwa wananchi hvyo walikuwa hawana uwezo mkubwa wa kuchambua mambo tofauti na sasa wasomi ni wengi karibu kila familia kuna mtu kapita ama anasoma sec n,k<br />
<br />
Tatu kuwepo kwa uhuru wa vyombo vya habari kumewafanya wananchi kuelewa mambo mengi waliyokuwa hawayajuhi yaliyokuwa yakiwafanya kuwa maskini k.v. rushwa,dili feki,ufisadi,kuuzwa kwa nchi yao n.k<br />
<br />
Nategemea wenzangu wataelezea na mapungufu mengi ya nccr na kufa kwake
<br />
<br />
Asante mkuu kwa maelezo yako
 
<font size="3"><br />
NCCR imesambaratika lini wewe au unaharisha maneno! NCCR ipo labda CCJ ndio imesambaratika.</font>
<br />
<br />
Mkuu mi naona neno kusambaratika limekuwa gumu kuelewa, jamaa ametumia kusambaratika akimaanisha kukosa nguvu kama awali na sio kufa kama chama cha ccj
 
Labda ukisoma kitabu cha Ndimala Tegambwage, cha Mtafaruku na Hatima ya Mageuzi Tanzania utafahamu kwa undani zaidi. Pamoja na hayo yote, nikuhakikishie NCCR-Mageuzi itaendelea kuwepo.

Ukweli ni kwamba NCCR ilianzishwa na maofisa wa usalama ili ku-contain opposition, na kuchafua image yote ya upinzani. Baadaye ikajulikana kuwa wananchi wenye nia ya mageuzi wanaburuzwa na wahuni wanaojidai wanamageuzi. kwa sasa inaonekana kuwa baada ya kumaliza kazi yao NCCR wameanza kuingia CHADEMA, the fact is NCCR imekufa, kilichopo ni kuwa ipo kwenye makaratasi na kuthibitisha uwepo hewa wake kwa wabunge wawili watatu iliyo nao.
 
watu ambao awaaminiki ni marando huyu ni kama mbegu ya gamba lakini viongozi wa cdm ni makini akistukiwa wakwanza kujitoa nae muhanga ni yeye
 
Mkuu mwaka 1995 Watanzania walikuwa na hamasa kubwa sana ila tu tatizo ilikuwa ni kwamba walikuwa wakimpenda mtu na si sera. Watanzania walimpenda Mrema. Nakumbuka siku alipojiunga na NCCR mageuzi mtaa wa Aggrey siku hiyo kadi za NCCR ziliuzwa kama karanga.

Nakumbuka wakati huo NCCR kulikuwa na watu kama Anthony Komu (yupo CDM kwa sasa) na Mabere Marando na hawa walikuwa na nafasi yao kubwa tu katika kuanguka kwa NCCR Mageuzi.

Mkuu CHADEMA pia kuna fukuto kuhusu Ruzuku: Wangwe (mwenyezi mungu amrehemu) aliipigia kelele kwamba iende kuimarisha Chama mikoani badala ya kubaki makao makuu na kulipana madeni ya helcopita; bahati mbaya hatunaye. Kuna mambo yanenda chinichini kwamba ruzuku inaliwa na wakubwa kwa njia ya posho. Wakubwa wanalipwa posho kubwa wakati wakitekeleza majukumu ya chama lakini wa chini wanatakiwa wajitolee!!

Watu wameichoka CCM lakini CHADEMA wasipoangalia masuala ya posho na ruzuku yatawafarakanisha.

Kuna kosa kubwa sana la kimkakati ambalo vyama vyetu vimekuwa vikilifanya kila siku. Utakuta ma-opportunist kama huyu Komu kila wanapokwenda wanapewa nafasi za haja, hivi hakuna wanachama waaminifu wakuweza kushika nafasi hizo kuliko hawa wapima upepo? Hata hivyo kilichoiua NCCR ni ile tabia ya Mrema kuamini kwamba yeye ndiye alikuwa kila kitu. Hata hiyo ruzuku alitaka yote iwe mikononi mwake kwa kuamini kuwa ilipatikana kwa ubavu wake. Kumbuka kauli yake wakati akienda TLP kuwa alikuwa na mtaji (wanachama wa kuhama nao). Leo hii yuko wapi na mtaji wake huo? Hili laweza kuwa funzo kwa makamanda wetu wa leo.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom