GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,544
- 108,864
- Thread starter
- #21
Wamezoea mipasho na ubabe na matamko yasiyokua na tija
Kenya wako vizuri kila sekta ..ni odinga tu anajaribu kutia doa nchi ya kenya lakini kenya they are very smart na educated ...huku kwetu mtu ni educated kwa makaratasi na vyeti tu lakin akili hamna ...
Eti leo hii unaweza kumfananisha museven na nyerere ..? What nonsense!
100% Precisely Mkuu. Hata Mimi nilishtuka sana na kuona aibu kubwa pale niliposikia Mzee Rais Museveni leo hii anafananishwa na Hayati Baba wa Taifa Nyerere. Hivi Mchezaji Nguli wa zamani Pele wa Brazil leo hii anaweza kufananishwa / kulinganishwa na Juma Nyosso wa Tanzania? Hivi ni kwanini tumefikia sasa hatua ya kumdhalilisha Hayati Nyerere hivi?
Najua na nayatambua sana mafanikio makubwa ya Rais Museveni kwa nchi ya Uganda tokea alipoingia madarakani mwaka 1986 ila nikimtathmini na kumchambua Kiuongozi, Kitabia na Kinidhamu hajafikia hata 25% tu ya Hayati Baba wa Taifa Nyerere nikajiuliza huyo aliyesema Museveni ni kama Nyerere alitumia Vigezo gani / vipi kuhalalisha hilo ambavyo labda Mimi GENTAMYCINE sivijui au sivifahamu?
Ungesema kwamba Museveni anaenda kuwa Charles Taylor wa Liberia ningekubaliana nawe kwa 100%. Mkuu vitu vingine vinatia hasira halafu najijua mwenyewe hasira zangu zilivyom jirani hivyo ngoja ninyamaze tu nisije nikamdharau Mtu humu halafu nikajikuta namkufuru bure Mwenyezi Mungu wangu Mungu wa Ibrahim, Isaka na Yakobo.
Na nahisi kuwa Watu ni Watanzania wenzetu humu humu pamoja na Usomi na Uzee / Uhenga wao bado hawamjui vizuri Hayati Baba wa Taifa Nyerere. Yaani leo hii kweli Museveni anafananishwa na Nyerere kweli? Huyu Mtu yupo serious kweli? Mkuu bora hata usingelileta hili kwani umeshanipandisha tayari temper yangu.