Kilicho nyuma ya madaktari kuomba radhi ni maagizo toka juu

Humu humu ndani mlisema na kutoa orodha ya madaktari eti wamepata kazi nje ya nchi na mambo kibao oohoo mara sijui nini kumbe bado wapo hapa hapa bongo mmmh.Na anae sema JK ni mbabe huyo ni mzushi na muongo mkubwa kama angekuwa hivyo sidhani hata wewe ungejua kusema hayo unayo yasema na kuropoka ovyo kwa kutumia mitandao ukudhani huonekani kwa taarifa yako hata ungetumia njia gani serikari ikikuhitaji utapatikana sana,Hakuna rais aliyeruhusu uhuru wa watu kutoa maoni mpaka wengine wanatukana ovyo na kuhujumu nchi lakini bado wapo tuu,kila lenye mwanzo linamwisho.


Aisee ni kweli kabisa aliyemteka na kumdhuru Dr Ulimboka ni Ramadhani Inghondu Mfanyakazi wa Ikulu
 
mi nafikiri watanzani wenyewe namaanisha wananchi tuchukue hatua,maana tukisubiri tutakosa majibu baadae....
 
Hapo ndio mwisho wa professional yenu, itawachukua tena miaka mingine 50 kuweza kufanya mliyokuwa mnakaribia kuyafikia. Kwani wakati mnaanza hamkujua hii ni vita, kwa nini mlitaka kumuua mtoto wa watu? Kama hawa ndio wasomi ambao tunafikiri wanajua right zao sha wanaongea kama vile hawajawahi kuingia darasani. je hawa raia wengine mawazo yao yapoje?
 
Habari toka Ikulu zinasema kuwa mara baada ya tume ya usuluhishi kwenda kutafuta muafaka wa mgomo wa madaktari na namna ya kutekeleza kama ilivyo amuliwa na mahakama ya kazi. Mh Jk alitoa dukuduku lake la moyoni na akawaambia yafuatayo kama wanaipenda kazi na nchi kwa ujumla.

1. Warudi kwa namna ileile walivyotangaza mgomo warudi na waombe radhi kwa kutumia njia ile ile waliotumia kutangaza mgomo.

2. Katika kutangaza kutojihusisha na mgomo wawataje walio watuma kufanya mgomo. ( Mpaka leo CHADEMA ndo wanajulikana ndio walio sababisha mgomo.

3. Wakiri kuwa wao ndo wakosefu na sio serikali kama walivyokuwa wanadai

Kila mwananchi kwa akili zake changanya na tukio zima la mgomo na tafakari

Hii kamati iliundwa lini? anyway majukumu yake yalikuwa yapi? anyway suluhisho limepatikana? anyway sielewi kitu kabisaaaaaaaaa!
 
mimi nilikuwa siku za karibuni najaribu kuamini kuwa Watanzania tunaweza kujikomboa kifikra katika angalau miaka 10 ijayo lakini kwa matukio kama haya nathubutu kusogeza huo muda kwa miaka 30 mbele hivyo inaweza kufika hata miaka 40 ijayo! Sijui Wakenya watakuwa wapi wakati huo Mungu wangu!!!!


Hapa umesema uhalisia wa mambo. Kama mtu unaweza kujiuliza au kama unaamini katika ushirikina unaweza kuamini kuwa watanzania tumelogwa akili zetu zisifanye kazi au tuna laana fulani hivi. Nashindwa kuamini mambo yanayoendelea katika nchi hii. Aliyekwenda shule hajulikani wala yule ambaye hakusoma hajulikani. Kibaya zaidi hata wale wanaoitwa "Professionals" ni ma-professionals katika makaratasi lakini matendo yao ni sawa na wale ambao hawakulionja darasa. Badala yake kuna kundi la watu walioko madarakani ambao wanaona ndiyo wenye haki ya kuishi vizuri, kuishi katika majumba mazuri, kuendesha magari ya kifahari, kusomesha watoto wao nje ya nchi, na mengine mengi. Kundi hilo linajumlisha viongozi wa serikali, wabunge, majaji, na wengineo. Hawa wako wote chini ya utawala wa ccm ambayo iko pale kuhakikisha kuwa inatumia njia zozote kuhodhi madaraka hata kwa mtutu wa bunduki na kwa kutumia unyonge na ufinyu wa kifikra wa watanganyika. Kwa jinzi watanganyika walivyo katika akili zao kweli kweli we have a long way to go kupata ukombozi wa nchi hii vinginevyo tutaendelea kuona mengi zaidi ya haya yanayotokea ambayo kwa akili za kawaida huwezi kuamini kuwa yanatokea. Mungu peke yake anaweza kutuepusha na janga hili la ccm na serikali yake.
 
Hapo ndio mwisho wa professional yenu, itawachukua tena miaka mingine 50 kuweza kufanya mliyokuwa mnakaribia kuyafikia. Kwani wakati mnaanza hamkujua hii ni vita, kwa nini mlitaka kumuua mtoto wa watu? Kama hawa ndio wasomi ambao tunafikiri wanajua right zao sha wanaongea kama vile hawajawahi kuingia darasani. je hawa raia wengine mawazo yao yapoje?

Mkuu Karim Wade, you are absolutely right, "the thing is people don't know who close they were to the determined goal when they decide to give up".. This was divide and rule, as you know if you cant convice them you simply confuse them, which is exactly what is happening..all valid, logical claims, now are seen as idiotic, and worse hapa itabidi kushtakiwa kwa Mauaji, since wamekiri wamefanya kosa...

and wao kujidanganya kwamba wakimaliza "internship" yaani miezi mitatu iliyobaki" waondoke nchini, wajue HAIWEZEKANI, wajue watarudi kazini under Government's terms(condition).. but all these will happen kama kesi "ikifutwa", but then kuna ndugu wa wafiwa wakiamua tena kuwashtaki?? tena mmoja mmoja?
 
Anaye wasema vibaya madaktari ni kilaza, tena anafikiri kwa kutumia masabuli ya chadem. Daktari yeyote ni mtu msomi, anaona mbali, sio vilaza wanaoona mwisho wa vidole vyao vya miguu. Hakika madaktari walilofaoya ndio uungwana.
Kuhusu chadema kuwa nyuma ya mgomo ule wa madaktari, ilikuwa wazi hata ktk shughuri za bunge, wabunge wa chadema walitokwa mishipa kusapoti mgomo.
 
Utu ni dhamani kuliko kitu chochote pia nafasi yko ni muhimu kuliko mnavyojitazama plz madaktari mnajidhalisha sana hasa intership matatizo ya kuwahudumia watazania ni magumu sana vifaa hakuna.
 
Usijipe moyo kumbukuka nafsi zao zimejaa fedheha na hudhuni kutokana na jinsi serikali yao inavyowatesa.

Kilichopo moyoni mwao kitajidhihirisha 2015.Wananyenyekea si kwa kupenda wala kutumwa na dhamira zao bali ni kwa kuwa hawana jinsi kwani Jk kashika mpini na wao wameshika kwenye makali.Hata hivyo,ubabe wa Jk ni wa muda tu kwani 2015 sio mbali.

Mwisho ukumbuke kuwa CCM ikitoka madarakani hata Jk nae hatakuwa salama
.

Kumbuka orodha ya waliotajwa kuficha mabilioni uswisi.
[/QUOTE]

Ushakuwa mungu?
 
Jambo usilolijua ni kama usiku wa giza...

linalojulikana ni kwamba Katibu Mkuu wa Wizara alisimamishwa na
Waziri wa Afya na Naibu wake waliondolewa ktk Baraza la Mawaziri

hii nayo bado ni kuonyesha serikali ndiyo iliyokuwa na matatizo
 
Tunawaita wasaliti wa watanzania, je walipokua wamegoma na tukaona madai yao ni ya msingi kwa afya za watanzania, wangapi tuliwapa support? au tuliishia kutoa comments tu ktk mitandao ya kijamii? tuliposikia wamesimamishwa kazi kwa kutetea afya bora kwa watanzania,tulifanya nini? "wanaharakati" mlifanya nini kuwasupport? hawana mishahara, hawajui hatma yao ya taaluma waliyoisomea na investment yote waliyoifanya! Nahisi kabla yakuwalaumu,tujilaumu kwanza. Tumewatelekeza kwa ubinafsi wetu,tukihisi hilo linawahusu wao peke yao. Nao wamekata tamaa, na roho ya kupigania utaifa sasa imewatoka wameiga roho zetu tunaojiita "wanaharakati" roho ya ubinafsi.wameamua kujiangalia wao na maisha yao kama watanzania wote wanavyofanya.
Puuzia mbali madai yao, je vifaa vya kazi na dawa zimeshaletwa? kwani hivyo vinatuhusu Watanzania tusio na uwezo wa kupeleka wagöjwa India.

Vinginevyo hata madaktari ni wasaliti kwa Watanzania kwa maana wameungana na watawala kutowajali Watanzania ila maslahi yao kwanza.
 
Back
Top Bottom