Kilicho nyuma ya madaktari kuomba radhi ni maagizo toka juu

Kumbuka orodha ya waliotajwa kuficha mabilioni uswisi...[/QUOTE]

Hebu tufafanulie hapo penye nyekundu, manake hiyo list hatujawahi kuiona.

Kuhusu kuomba kwa Drs, naona kama wameridhia kuila mikono yao. Sasa watakuwa wanalishwa tu.
 
Kushangilia ni sawa na engineer ku compromise na ratio ya jengo la ghorofa na kujenga kama mwenye jengo atakavyo ili apate pesa yake tu.
 
Mkuu Return of Undertaker, CHADEMA ni chama cha kisiasa, huu ulikuwa mgomo wa Taaluma, ...Tusichanganye vitu,

Kwa akili ya wale walioomba msamaha, ni kwamba watasamehewa na ni "ukweli walikosea" sasa ninachoshindwa kuelewa ni kwa nini makundi haya yahusishwe,
1. CHADEMA
2.MAT(Medical Association of Tanzania)

mgomo haukuwa na SHURUTI, ila HIARI..then if so, iweje leo wajitokeze na kusema "walidanganywa", hoping that you are a great thinker, does it ring a bell anyhow with their reason?..i dont think so...na hapa ndio walipokosea, kuchanganya kati ya SUBIRA na UKIMYA!!




Nadhani;

WIVU na KUTOJIAMINI:
Mkuu, takribani madaktari 400ambao watahitimu mwaka huu wamepangwa katika hospitali tayari, "wakichukua" nafasi yao, sasa nashindwa kuelewa kwanini baada ya kuona jambo hili likitokea ndio wakumbuke "msamaha" unapaswa kutoka...nisingependa kutoa maneno ya kashfa kwa madaktari wenzangu kwa kiwa ni wanafamilia(kitaaluma), lakini nina uhakika msamaha si wa DHATI ila kurudishwa.


SUBIRA:
Kwa daktari wa kitanzania akaaye masaa 30 macho kabla ya kukabidhi shift nyingine akiwa sehemu mbali mbali (wodini,chumba cha upasuaji,kliniki nk) ambaye amekwishazoea "kutingwa" na utitiri wa kazi, kusubiri bila kufanya kazi, ni MATESO, na hasa inapokuja suala la kimahakama...tofauti na hospitali, mahakama hutaja kesi kwa mpango wake, na huitaji SUBIRA ya hali ya juu kupata kusikilizwa kwa kesi yako..hii imetafsiriwa kuwa ni UKIMYA wa MAT hata mara baada ya MAT kutamka "tusubiri jambo hili lipo kisheria" katika mtandao wao kutokana na wengi(madaktari WALIOFUKUZWA kuwa nje ya jiji na hivyo kuwa ngumu katika kuitisha mkutano physically)


KIBURI:
Ilikuwa ni shida kwao(madaktari "WALIOATHIRIWA" na mgomo kuendelea kusubiri mtaani baada ya kushindwa kwenda nje au kuwa katika ajira binafsi but above all nielewavyo mimi...madaktari wa kitanzania "tuna viburi" at times..na ninasema hivi kwasababu ANTICIPATION before war/battle or any crisis for that matter it's not questionable, lakini kwa baadhi ya madaktari wakitambua kuwa mgomo unaweza kuwatoa kazini.

Kuna msemo unasema "usichague nguo ya kujisitiri ikiwa uko uchi" ..kama mtu aliondoshwa kazini, nijuavyo mimi katika kujisitiri angekuwa na vijikazi vidogo vidogo vimtunze kwa muda hadi pale maamuzi ya mahakama yatapotoka...lakini jambo hili lilikuwa next to impossible kwa baadhi ya madaktari..wakijifariji kwa maneno, "utaua fani", lakini ninachoshindwa kuelewa je fani hiyo ilikuwa "haifi" wakati ukiwa idle??!...but this was used as scapegoat, the truth being Kujishusha ili kufanya kazi hata kama ina kipato kidogo kuliko ulichokuwa unapata ni shida!! wengi walitaka kipato sawa au zaidi..na hicho ndio ninachoita KIBURI.

-lakini mtu anaweza kutafsiri ninawahukumu/kulaumu bure na kuwa sasa ndio "wamejishusha"..ofcourse they have, but is it genuine?..
ingekuwa ni jambo rahisi kuomba msamaha kama suala halipo mahakamani, na takribani wiki mbili zilizopita Mh. Hussein Mwinyi(Waziri wa Afya) alipokuwa pale MNH na MOI alisema "serikali haijawafukuza intern doctors, bali MCT itawaita mmoja mmoja kuwahoji".. sasa swali ni kwamba msamaha huu utabatilisha maamuzi ya Serikali? vipi mahakama na MCT?
 
Hebu tufafanulie hapo penye nyekundu, manake hiyo list hatujawahi kuiona.

Kuhusu kuomba kwa Drs, naona kama wameridhia kuila mikono yao. Sasa watakuwa wanalishwa tu.

Mkuu Nono, kuna list ilitoka jumamosi(15092012), ikionesha lmajina ya watu kama mkuu Salary slip alivyosema ila iliondolewa na Mods, na hata baada ya ku-complain kuondolewa kwake(bado complains ziliondolewa pia)..hata hivyo ilinukuliwa(quoted) na wadau wengi wengi na iko mitaani TAYARI!!
 
Hainingii akilini asilani kuwa mpaka leo hii bado kuna watu wanafikiria kujikomba kwa JK? Kutafuta nini? Huyu JK tumjuaye unajikomba kwake anakushiti na huo ndo mwisho wako. Bora usimamie principles zako mbele yake, ya umma na Mungu!
 
JK hoyee! JK Hoyee, safi sana JK, walijaribu madaktari wameshindwa, wamejaribu walimu wameshindwa, nani sasa ataweza? JK hoyee
Waislam na Uamusho
 
Kila mtu anakula kwake. Kila mtu ana mahitaji tofauti kwenye maisha. Migomo isiyofuata taratibu za migomo na ambayo ni ya kudharau waliokuajiri mara nyingi inaishia hapo walipofika.

Kufuata sheria zilizozopo siyo utumwa. Sheria zinaweza kubadilishwa lakini siyo kwa mitulinga kama walivyotaka kufanya hao madaktari.
 
Haya ndio maamuzi magumu lakini sahihi kwa wakati fulani hasa kwa nchi masikini.
Daktari kutangaza mgomo usio na kikomo kwa nchi kama yetu whatever the reason behind, haikubaliki!!!
Wengi waliothirika na masikini ambao hawana hatia.

Lakini la muhimu ni kuwa tuantakiwa tukae chini na kuanza kupanga namna ya kujenga tena uzalendo.
Angalia hawa vijana intern ambao most of them are below 25 years of age wengi wanasombwa na mob psychology lakini wakisimama kama individual hawawezi kutetea hicho wanachokifanya leo.
Tupo pamoja katika madai yenu lakini njia mliyoitumia this time si sahihi.
 
  • Thanks
Reactions: KVM
Acha watu washangilie. Kuna uzuri wake kuwa na akili butu. OK, wameshinikizwa kuomba radhi, na morali wa kuhudumia wagonjwa unarudi automatically?

Kama unadhani naongopa nenda wodi yoyote Muhimbili kaone mlundikano wa wagonjwa na waulize kama wanaonwa kama zamani. Binadamu hashinikizwi, professionalism bwana wewe isikie redioni tu usiichezee.

Retreat is not a surrender. Nawasifu maintern hao kwa sababu vita hupiganwa vizuri unapokuwa uwanja wa vita, Acha warudi uwanjani na vita ni palepale na tena yenye tija.

Atakayeumia sio daktari na sio raisi (anaenda UK tu hata akipata mafua). Watanzania wanaoshangilia kwamba JK kashinda ndio watakaoendelea kufa kama utitiri kwa sababu ya ujinga wao. Kila walichokidai madaktari kilihusu kulenga huduma bora za wananchi haohao ambao wanakenua meno sasa. Wataipata sasa. Tulia usubiri.
 
enhe, ngoja mi niseme hivi;
1. madaktari wameona kuwa ulimboka amewasaliti na wao wakaamua kumsaliti kwa kuomba radhi?
2. madaktari wameamua kufunika kombe mwanaharamu apite?
3. baathi ya madaktari wamejikuta ngoma nzito hawaiwezi kucheza, wakaona bora wajisalimishe?
all in all kuwa na msimamo ni vizuri, kujiamini ni vizuri na kujitolea pia ni vizuri. huwezi vyote hivyo jitayarishe kuwa mtumwa daima. poleni sana ndugu zetu kwa kuwa na double standards
 
Subiri kdg na Padri Slaa naye ataomba radhi kwa watanzania kwa ajili ya UNAFIKI wake sijui naye atakuwa kajishushia HESHIMA?
 
Hao Ma-Dr wanatofauti gani katika maamuzi na umiliki wa matokeo wakilinganishwa na Aunt Ezekile au Mh. ZItto?
 
Ukweli ni kwamba hawa hawana usajili wa kuwa madaktari,wanafanya hivyo ili wawe madaktari wenye usajili,then hawa hawa ukiitishwa mgomo miaka 2 ijayo watakuwepo.
 
Kitendo cha madaktari kuomba msamaha kunafungulia mlango wa kuwashtaki the hegue kwa kusababisha vifo vya ndugu zetu.kuomba msamaha inamaanisha umekubali kosa.
 
Hali itakuwa mbaya sana huko mbeleni, kwa madakitari kwa upande mmoja, na kwa wananchi kwa upande mwingine.. Manake Serikali will never give a damn pale watakapojifanya kutangaza mgomo. Na hata wakigoma bado Serikali haitajali, hence akina sie tutabakia kufa kama kuku wenye kifaduro.... Labda kama hii habari ya wao kuomba radhi si kweli!
 
Back
Top Bottom