Kili Music Awards 2007/08

Invisible

Robot
Feb 11, 2006
9,075
7,873
Binafsi nimeona michemsho mingi sana. Kuna wenye mitizamo tofauti?

Yani wameboa ile mbaya!

Stage - ZERO

Burudani - ZERO

MC - 49%

Judgment ya nani anashinda na kwanini - 26%

Maandalizi kwa ujumla 37%

Mmechemka mwaka huu. Yani ma - MC wameshindwa hata kupata mawasiliano na waandaaji inavyoelekea. Imeudhi sana... msirudie makosa kama haya
 
Binafsi nilikuwa na imani kubwa na uwezo wa MCs (Masoud na Fina) kwani kwa uzoefu wao sikutarajia wanaweza kuangushwa hivi. Mchemsho mkubwa ulikuja pale wakati wa kumpa zawadi ya wimbo bora wa Mwaka kijana MarLaw...

Pole Fina na Masoud, mlijitahidi. Mi nlidhani kwakuwa yanafanyiwa Kempiski basi mambo ingekuwa swafi! Hapana, haikukaa sawa. Ngoja tuone wadau wengine wanasemaje
 
kwani nini kimetokea, kwangu hii ni breaking news in a piece.
Mama, nikiendelea kuandika mimi tu nitakuwa nahukumu bure. Najua walio Bongo ni usiku wa manane lakini kukicha na haswa kuanzia J3 watakufahamisheni nini kilijiri.

Kifupi ni michemsho mitupu
 
Kweli Ilikua Mchemsho Mtupu,maandalizi Yalikua Shaghalabagala Msanii Kama Bushoke Kupata Tuzo Kwa Wimbo Usio Wake Tena Wa Mwaka 2008 Kiasi Kwamba Mpaka T.i.d Akafanya Vurugu.walichemka Waandaaji,waliwatenga Viburudisho Vya Mioyo Yetu Fm Na Acudo Je Walishindwa Hata Kufikiria Tuzo (aidha Bendi Bora Ya Kutoka Nje Ifanyayo Kazi Tz) Ili Kutowatenga Hwa Wakongo?
Mi Nliona Ubovu Mkubwa
 
Mama, nikiendelea kuandika mimi tu nitakuwa nahukumu bure. Najua walio Bongo ni usiku wa manane lakini kukicha na haswa kuanzia J3 watakufahamisheni nini kilijiri.

Kifupi ni michemsho mitupu

peacock= ilikuwa mchemsho nadhani mcs hajazoez stage, sababu ni watangazaji wa radio, ingekuwa labda wa t.v ingesaidia kuwa na presentation nzuri, shughuli yaweza kuwa nzuri au mbaya zaidi yategemea na how mcs are
 
peacock= Ilikuwa Mchemsho Nadhani Mcs Hajazoez Stage, Sababu Ni Watangazaji Wa Radio, Ingekuwa Labda Wa T.v Ingesaidia Kuwa Na Presentation Nzuri, Shughuli Yaweza Kuwa Nzuri Au Mbaya Zaidi Yategemea Na How Mcs Are

Peacock Mcs Wako Fiti Wamezoea Kazi Yao Kili Music Awards Walichemka Sana Tu Tena Niaibu Halafu Wakarusha Live Tbc1 Sehemu Mbalimbali Ulimwenguni Waliona Huo Mchemsho.

Fina Na Masoud Walijitahidi Sana Kufukia Mashimo Lakini Walishindwa, Hata Mimi Nilifikiri Kill Ya Mwa Ka Huu Ingekuwa Funika Bovu Kumbe Ovyooooooooo
 
Kweli Ilikua Mchemsho Mtupu,maandalizi Yalikua Shaghalabagala Msanii Kama Bushoke Kupata Tuzo Kwa Wimbo Usio Wake Tena Wa Mwaka 2008 Kiasi Kwamba Mpaka T.i.d Akafanya Vurugu.walichemka Waandaaji,waliwatenga Viburudisho Vya Mioyo Yetu Fm Na Acudo Je Walishindwa Hata Kufikiria Tuzo (aidha Bendi Bora Ya Kutoka Nje Ifanyayo Kazi Tz) Ili Kutowatenga Hwa Wakongo?
Mi Nliona Ubovu Mkubwa
Next time mnawasusia hakuna kwenda hao waandaji ni wachemfu sana.....Kwanza walimkumbuka james Dandu muanzilishi wa awards hizi?
 
Hawa jamaa hamna kitu hasa kwenye kuamua nani abebe tuzo
 
Oh,

Maoni yote kumbe yanaonesha WAMECHEMKA sio? Then kuna haja ya watu hawa kurekebisha mambo kadha wa kadha!
 
Hawa jamaa walianza vizuri ila miaka inavyozidi kwenda wanazidi kuchemka
Yani Bushoke kapewa tuzo ya wimbo ambao sio wake na wimbo wenyewe hauna hata miezi minnne tangu utoke
Hivi ni kweli MARLOW alimfunika ALI KIBA?
Ombi langu kwa wasanii ni bora MSUSIE hizo tuzo but itakuwa ngumu kwani kuna wale ambao wanapata tuzo wasizostahili hawatasusa
 
Wanaumwa hawa na wamegubikwa na tamaa zisizoelweka ambazo zinachangia wao kupeana tuzo kwa sababu tu wanajuana...

inakera!
 
ilitia aibu sana sana!!
mimi niliwaonea sana huruma ma mc, wangekuwa nao si wakakamavu, watu wote wangelitoka ukumbini.
Kuna wakati wimbo wa taarabu unaimbwa mhhh nashindwa hata kuhadithia, manake ilikuwa AIBU KUBWA.
muziki ulikatika yeye akabaki naimba peke yake, alipotaka kushuka jukwaani, ukaanza, akataka kurudi kuendelea, ukakatika tena najua kijasho kilimtoka, anaemjua ampe pole na hongera kwa ukakamavu wa kushuka stejini.
Aibu tupu, ilifanya nimkumbuke mke wa Mtoto wa Dandu alipokuwa anataka kuiendeleza yeye kumuenzi mumewe. Lazima ingekuwa tofauti sana.
Hawa walitakiwa waingie kwenye siasa, wasivuruge fani amabyo inakuwa bila matatizo ya kijinga kama haya. Tanzania utaratibu wa dizaini hii ulipita zamani sasa. Wasiturudishe nyuma.
TBL wafute udhamini mpaka kieleweke, wanajiaibisha na kupoteza hela zao
 
Yaani hizi tuzo kadri siku zinavyoenda wanazidi kuboronga. Hiyo yote ni laana toka kwa Mtoto wa Dandu. kwani wanashindwa hata kumuenzi muasisi wa hizo tuzo. angekuwa hai hadi leo hii najua wasanii wa bongo wangekuwa mbali sana na tuzo zingeboreshwa zaidi.

Nampongeza sana Bushoke kwa ujasiri wake wa kuwarudishia tuzo yao - Kill Music Awards. ile tuzo mtu aliyestahili kupata ni TOP IN DAR.
 
Hawa kili time ni money oriented sote twawafahamu...ndio maana hata mwaliko wa sherehe walikuwa very strategic wakaandaa listi ya watu wao yaani MAFISADI wenzao wakawachangisha wakapata mihela..kibao.Jambo la kusikitisha hii award ilianzisshwa na Marehemu DANDU.sina uhakika kama walimkumbuka mke wake kwenye hafla hiyo..mliokuwepo nisaidieni kama alikuwepo au alishatupwa nje...
 
KIla idala lazima wakubali walichemka sana na kuna hali ya kaupendeleo flani kwani kura watu tulipiga kwa khali na mali washindi wengine.Kwa Bongo hii ni kawaida washindi iwa wanakuwa wameandaliwa tayari.
 
Yaani hizi tuzo kadri siku zinavyoenda wanazidi kuboronga. Hiyo yote ni laana toka kwa Mtoto wa Dandu. kwani wanashindwa hata kumuenzi muasisi wa hizo tuzo. angekuwa hai hadi leo hii najua wasanii wa bongo wangekuwa mbali sana na tuzo zingeboreshwa zaidi.

Nampongeza sana Bushoke kwa ujasiri wake wa kuwarudishia tuzo yao - Kill Music Awards. ile tuzo mtu aliyestahili kupata ni TOP IN DAR.

sorry TID kwa wimbo gani
 
Mpaka leo washindi hawajapewa zawadi zao zaidi ya vyuma vizito vyenye kupakwa rangi vikang'aa kama gold vile.

This' interesting infwakti!
 
Hawa kili time ni money oriented sote twawafahamu...ndio maana hata mwaliko wa sherehe walikuwa very strategic wakaandaa listi ya watu wao yaani MAFISADI wenzao wakawachangisha wakapata mihela..kibao.Jambo la kusikitisha hii award ilianzisshwa na Marehemu DANDU.sina uhakika kama walimkumbuka mke wake kwenye hafla hiyo..mliokuwepo nisaidieni kama alikuwepo au alishatupwa nje...

kufa kufaana...
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom