Kilango apasua jipu

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,007
Kilango apasua jipu

2008-07-17 12:07:12
Na Victor Kwayu, PST, Same

Mbunge wa Same Mashariki (CCM), Bi. Anna Kilango Malecela, amesema mkakati alionao sasa ni kuendelea kukemea baadhi ya viongozi na watu wachache wanaoonyesha mwelekeo wa kuendelea kumiliki na kuhodhi mapato ya nchi kwa maslahi yao binafsi.

Aliyasema hayo jimboni kwake jana wakati akizungumza na wanahabari katika mahojiano maalum.

``Ni vyema niwaelimishe wananchi kikamilifu kwamba, wabunge wote wanaoendelea kuchachamaa bungeni au majukwaani wanachokitafuta ni kikubwa zaidi kuliko kupambana na mafisadi,`` alisema.

Aliongeza kuwa, uamuzi huo unatokana na ukweli kwamba wapo baadhi ya viongozi wachache pamoja na kikundi kidogo kinachoendelea kuhodhi mapato ya nchi isivyo halali.

Alisema kwa kipindi kifupi, baadhi ya viongozi ndani ya serikali wameonekana kutoridhika na kipato wanachokipata na badala yake wametumia mianya ya madaraka waliyonayo kumiliki fedha na rasilimali za nchi isivyo halali.

``Endapo kwa umoja wetu kama wabunge ndani ya Bunge hatutapambana na hali hii, hatua ya watu wachache wenye uchu na fedha za walalahoi kutalipeleka taifa mahala pabaya`` alionya.

Aliitaka jamii kutambua kuwa wabunge wote wanaochachamaa bungeni au majukwaani wanachokitaka ni kikubwa zaidi kuliko kupambana na mafisadi.

Alisema kinachopiganiwa ni kuwa na mgawanyo sawa wa rasilimali za nchi kwa manufaa ya kila raia na sio kwa kundi la wachache kujilimbikizia utajiri kwa njia zisozo halali.

Bi. Anne alisema ingawa uamuzi wa wabunge hao licha ya kuwa ni mgumu na utakaoleta matokeo baadaye unapaswa kuungwa mkono na kila mwananchi kwakuwa serikali imeonyesha nia ya kukabiliana na vitendo hivyo.

``Rais wa nchi ameonyesha kukerwa na hali hii ya vitendo vya wazi kwa baadhi ya viongozi... hatua hiyo inatupa moyo kwa sisi wabunge kuendelea na mapambano haya kwa ajili ya kuleta maisha bora kwa kila Mtanzania.``

``Kwa msingi huo, tunaomba wananchi watuombee ili pamoja na mambo mengine tuweze kuyafikia malengo hata kama matokeo hayataonekana sasa lakini vizazi vijavyo vishuhudie jitihada zetu``, alisema.

Alisema baadhi ya wananchi wamekuwa na mitazamo tofauti juu ya kuwepo mgawanyiko miongoni mwa wabunge kwa kuona baadhi yetu tukihitaji mabadiliko na wengine wakipuuza.

Alisema wabunge wengi wanataka mabadiliko wakati wachache wanayapinga na kwamba wanaofanya hivyo kuhofia mabadiliko hayo yatagusa maslahi yao binafsi.

``Nasisitiza kwamba ni vyema tukawaacha hata kama wakitubeza...hatutakata tamaa kwa hili kwakuwa ni la maslahi ya wananchi na taifa``, alisema.

Katika hatua nyingine, mbunge huyo aliwataka wabunge wa CCM kuwa mstari wa mbele kukosoa viongozi wanaokiuka wajibu wa kazi kwa maslahi binafsi.

Alisema akiwa mbunge wa CCM na mjumbe wa Halmashauri Kuu hatapenda kuona chama na serikali vikitetereka.

Mbunge huyo alikuwa katika ziara ya siku mbili jimboni mwake iliyokuwa imelenga kuzindua ujenzi wa visima 30 vya maji safi katika tarafa ya Mamba Vunta pamoja na kujionea maendeleo ya ujenzi wa kiwanda cha kisasa cha kusindika tangawizi ya wakulima wa kata za Mamba Miyamba, Bwambo na Mpinji.

SOURCE: Nipashe
 
Bubu nakubaliana na maneno hayo ya Mama Anna kwani ni kama anawa bipu wabunge wenzake wayasimamie maslahi ya TAIFA.

Ila sasa kuhusu HILO JIPU..Kama ni MAJIPU keshapasuwa na wengine walishapasua kwa sana tu..Sasa swali ni moja..Je kuna lililopona?

Ninampongeza sana kwa jitihada zake....Lakini je atapata ushirikiano?

Tunajuwa kuwa walishindwa kwenye ile bajeti ambayo wapinzani wali abstain.

This time hapa ndio kipimo kikubwa kuliko vyote kwenye historia ya TAIFA LETU.

Macho yetu na masikio ni DODOMA.

Hivyo basi..NARUDIA...Kama wabunge hao wenzake wasipokubaliana na mapendekezo ya kamati ya madini basi yeye na wenzake ambao hawana maslahi WAJITOWE ccm NA MAPINDUZI YAANZE!

Naomba kuwasilisha.
 
Kwani kama humo ndani ya chama wabunge hawa na wajumbe hawa wakimsikiliza...Basi kweli iyakuwa ni kama MUUJIZA kwa wengine wetu.

Jana hiyo hiyo pia majina ya wajumbe wapya wa Halmashauri Kuu ya Taifa yalitangazwa na miongoni mwao wapo ambao hawakuwa wana mtandao lakini ni vigogo wenye majina mazito kama vile Bw. Frederick Sumaye, Bw. Jackson Msome, Bi Kate Kamba, Profesa Samuel Wangwe, Anne Kilango Malecela, Zainabu Gama Profesa Juma Kapuya, kitendo kinachodhihirisha kuwa makundi sasa yamekwisha.

Wengine ni Kingunge Ngomable Mwiru, Anna makinda, Zakhia Meghji, John Chiligati na Yusufu Makamba. Mara baada ya majina ya wajumbe wa Halmashauri Kuu kutangazwa, kulilipuka shangwe na kusakata muziki uliokuwa upigipwa na Bendi ya TOT Plus chini ya Kapteni John Komba ambaye pia alichaguliwa kuwa mjumbe wa NEC pamoja na Khadija Kopa.

Mwenyekiti wa jopo la uchaguzi, Spika Samuel Sitta aliyetangaza matokeo alisema uchaguzi ulikuwa huru na haki na kwamba walioshinda wameshinda kihalali.

Nafasi ya ukatibu mkuu iliyokuwa ikishikiliwa na Bw. Yusuf Makamba na wajumbe wa Sekretarieti zitajazwa leo.
 
Kilango apasua jipu

``Rais wa nchi ameonyesha kukerwa na hali hii ya vitendo vya wazi kwa baadhi ya viongozi... hatua hiyo inatupa moyo kwa sisi wabunge kuendelea na mapambano haya kwa ajili ya kuleta maisha bora kwa kila Mtanzania.``


Inawezekana unajibalaguza kwa Kikwete.

Unauma na kupuliza.

Ni msanii wewe Mama Malecela.
 
Kilango apasua jipu

2008-07-17 12:07:12
Na Victor Kwayu, PST, Same

Mbunge wa Same Mashariki (CCM), Bi. Anna Kilango Malecela, amesema mkakati alionao sasa ni kuendelea kukemea baadhi ya viongozi ......

``Rais wa nchi ameonyesha kukerwa na hali hii ya vitendo vya wazi kwa baadhi ya viongozi... hatua hiyo inatupa moyo kwa sisi wabunge kuendelea na mapambano haya kwa ajili ya kuleta maisha bora kwa kila Mtanzania.``

SOURCE: Nipashe

Mhe Kilango pls wacha kumfagilia JK.....una prove gani kuwa anakerwa? mbona hatumjasikia akikemea wala kuwajibisha hawo MAFISADI ambao wko katika harakati ya kujisafisha.

Mhe Kilango ingekuwa bora zaidi, mngeweza kumkumbusha Muungwana wajibu wake, maanake anaonekana tangu akalie kiti amesahau kilichompeleka hapo.
 
Inawezekana unajibalaguza kwa Kikwete.

Unauma na kupuliza.

Ni msanii wewe Mama Malecela.

Kipi alichokifanya kuonyesha kukerwa kwake na ufisadi? Hasa ukitilia maanani mafisadi wote bado hawajaguswa?
 
Inaonekana Mimi na Mkuu Kuhani tulikuwa na jibu sawa kwa wakati mmoja......uzalendo bana
 
Mhe Kilango pls wacha kumfagilia JK.....una prove gani kuwa anakerwa? mbona hatumjasikia akikemea wala kuwajibisha hawo MAFISADI ambao wko katika harakati ya kujisafisha.

Mhe Kilango ingekuwa bora zaidi, mngeweza kumkumbusha Muungwana wajibu wake, maanake anaonekana tangu akalie kiti amesahau kilichompeleka hapo.

Yule Askofu wa KKKT Stephen Munga na Kilango wote wanampa sifa za kushughulikia mafisadi lakini ukweli ni kwamba hajafanya chochote.
 
Mbunge wa Same Mashariki (CCM), Bi. Anna Kilango Malecela, amesema

1. mkakati alionao sasa ni kuendelea kukemea baadhi ya viongozi na watu wachache wanaoonyesha mwelekeo wa kuendelea kumiliki na kuhodhi mapato ya nchi kwa maslahi yao binafsi.

2. ``Ni vyema niwaelimishe wananchi kikamilifu kwamba, wabunge wote wanaoendelea kuchachamaa bungeni au majukwaani wanachokitafuta ni kikubwa zaidi kuliko kupambana na mafisadi,`` alisema.

3. ukweli kwamba wapo baadhi ya viongozi wachache pamoja na kikundi kidogo kinachoendelea kuhodhi mapato ya nchi isivyo halali.

4. Alisema kwa kipindi kifupi, baadhi ya viongozi ndani ya serikali wameonekana kutoridhika na kipato wanachokipata na badala yake wametumia mianya ya madaraka waliyonayo kumiliki fedha na rasilimali za nchi isivyo halali.

5. ``Endapo kwa umoja wetu kama wabunge ndani ya Bunge hatutapambana na hali hii, hatua ya watu wachache wenye uchu na fedha za walalahoi kutalipeleka taifa mahala pabaya`` alionya.

6. Aliitaka jamii kutambua kuwa wabunge wote wanaochachamaa bungeni au majukwaani wanachokitaka ni kikubwa zaidi kuliko kupambana na mafisadi.
Alisema kinachopiganiwa ni kuwa na mgawanyo sawa wa rasilimali za nchi kwa manufaa ya kila raia na sio kwa kundi la wachache kujilimbikizia utajiri kwa njia zisozo halali.

7. ``Rais wa nchi ameonyesha kukerwa na hali hii ya vitendo vya wazi kwa baadhi ya viongozi... hatua hiyo inatupa moyo kwa sisi wabunge kuendelea na mapambano haya kwa ajili ya kuleta maisha bora kwa kila Mtanzania.``

8. ``Kwa msingi huo, tunaomba wananchi watuombee ili pamoja na mambo mengine tuweze kuyafikia malengo hata kama matokeo hayataonekana sasa lakini vizazi vijavyo vishuhudie jitihada zetu``, alisema.

9. Alisema wabunge wengi wanataka mabadiliko wakati wachache wanayapinga na kwamba wanaofanya hivyo kuhofia mabadiliko hayo yatagusa maslahi yao binafsi.

10. ``Nasisitiza kwamba ni vyema tukawaacha hata kama wakitubeza...hatutakata tamaa kwa hili kwakuwa ni la maslahi ya wananchi na taifa``, alisema.

Eti haya maneno yamesemwa na kiongozi msanii kama Mtikila? Unajua sometimes elimu isiyoweza kukusaidia binafsi, kweli haiwezi kutusaidia wananchi wengine tunaokuja hapa JF kuchota elimu ya taifa letu, kwa wale tuliowategemea kuwa wameenda shule, kumbe masikini ya Mungu ni bure tupu,

Maana sasa wanasema hata mtoto wa mungu naye ni msanii, sasa eti tuwashangae au kuwasikiliza hao?
 
Mbunge huyo alikuwa katika ziara ya siku mbili jimboni mwake iliyokuwa imelenga kuzindua ujenzi wa visima 30 vya maji safi katika tarafa ya Mamba Vunta pamoja na kujionea maendeleo ya ujenzi wa kiwanda cha kisasa cha kusindika tangawizi ya wakulima wa kata za Mamba Miyamba, Bwambo na Mpinji.

Eti kuwakumbuka wananchi wa jimbo lako kwa kuwawekea visima vya maji kama mbunge alivyoahidi wakati wa kampeni za uchaguzi, ni kuwa msanii basi huu ni usanii babukubwa tena sana, I am down na this kind of usanii!
 
Mama Malecela acha woga na usanii katika kutafuta ukweli.
Kama umeamua kuipigania nchi na wananchi basi ni bora kuwa mkweli na muwazi.
Hakuna cha maana alichofanya kikwete katika kupambana na wezi na mafisadi ili kuonesha anakerwa na uchafu huo. USIWE MWONGO WALA MWOGA KATIKA UKWELI.

Kikwete anafurahishwa na uchafu unaondelea kwani amekuwa kimya kuukaripia na sanasana anawalinda wezi na mafisadi hao.

Samahani mama Kilango mimi nilikuwa na kadi ya CCM ambayo nimeichana na siitaki tena CCM. Na kwa msingi huo CCM imepoteza kura yangu 2010.

Mwisho naomba tukubaliane kutokukubaliana kwamba CCM inanuka rushwa, wizi na ufisadi. CCM inatakiwa kufutwa kabisa na msajili wa vyama vya siasa Tanzania kwani inaipeleka nchi katika mapigano ya wenyewe kwa wenyewe.

Ni watanzania hawo hawo walipigana na wazungu kwa kutumia mikuki, mawe, marungu nk katika kutetea mipaka na uhuru wao, na bila kuficha ukweli ni kwamba Watanzania hawo hawo wamechoka na uchafu unaoendelea hivyo hawataona shida kurudia vita vya majimaji na vingenevyo si muda mrefu toka sasa.
 
Wote nyie mnaomponda mama Malecela sijui hasa mlitaka afanye nini kama MBUNGE!.. usanii upi haswa ikiwa leo hakuna hata mmoja wenu anadiriki kusimama..
Hivi mmetumwa au?... huyu mama anazungumzia MAFISADI kwa wananchi wa vijijini ambako sote tunaomba kila siku wazipate habari za JF, sasa iwe anatafuta umaarufu ama hapana lakini message imewafikia wananchi na ndilo tunalojaribu hapa JF kila siku.. Hakuna maneno aliyosema Mama Malecela ambayo sisi wenyewe humu hatusemi hali baadhi yetu mnafanya kazi serikalini, wana CCM na wengine washikaji wa hao mnaowasema.. Je, nanyi mpo kundi gani?..
Kuchana kadi sii hoja na hakuna anayeweza kuthibitisha kuchana kadi ndio kujitenga na CCM.. wewe nenda tawi la CCM, tena mchukue Michuzi awakilishe ujumbe wako magazetini - Uirudishe kadi ya CCM, utoka uanachama na sababu uzitaje kama unaweza sema hata nusu ya haya aliyosema mama Malecela!.. thubutu!
Na ukiweza basi hapo mkuu utakuwa umefungua uwanja kwa wananchi kuelewa yanayokukera lakini kuchana kadi haisaidii kitu kwa sababu record za CCM bado zinakutambua, hawaelewi sababu wala kitu gani kinakukera..
Kuchana kadi ni sawa na kupoteza tu!
 
Mama Malecela acha woga na usanii katika kutafuta ukweli.
Kama umeamua kuipigania nchi na wananchi basi ni bora kuwa mkweli na muwazi. Hakuna cha Kikwete anafurahishwa na uchafu unaondelea kwani amekuwa kimya kuukaripia na sanasana anawalinda wezi na mafisadi hao.

Mkuu heshima yako, ninaomba kutofuatiana tena sana na mawazo yako, ninasema hivi manpoamua kumshambulia kiongozi kama Mama Kilango, ambaye wengine tunaamini kuwa ni muadilifu, basi lazima muwe na hoja, kwa sababu so far hamna hoja, as the results inakuwa ni chuki za binafsi na kwa sababu zenu mnazozijua wenyewe ingawa pia zingine tunazifahamu,

Kwa mfano hapa unasema kuwa amesema uongo, hapa ukweli ni kwamba Mama Kilango amesema mtizamo tofauti na wako on rais wetu, kwa sababu kuna valid argument pia kuwa kati ya marais wetu wote waliowahi kututawala huyu peke yake ndiye ameweza kuwaondoa viongozi wanaoshukiwa na ufisadi, badala ya kuwahamishia nafasi nyingine kama ilivyokuwa kawaida huko nyuma kabla hajawa rais, kwa hiyo kama ni uongo nafikiri ukweli hapa uko clear kuwa muongo ni nani kati yako na Mama Kilango,

Yes, rais hafanyi kama ambavyo tungependa hapa JF afanye, lakini ni kiongozi gani Tanzania ya sasa kuanzia upinzani mpaka CCM, anyefanya exactly kama tunavyotaka hapa JF? Au Chadema wanayafanya tunayotaka hapa JF? Imean kumshambulia Mama Kilango, ni haki ya kila mwananchi, lakini hapa JF ni lazima uwe na hojz nzito, maana otherwise itakluwa ni kelele za debe tupu hizi, tunataka kuona hoja, ambao zikiwa nzito atafikishiwa kama tunavyowafikisha viongozi mbali mbali wanaotwangwa hapa, lakini sio hizi nyepesi nyepesi?

Samahani mama Kilango mimi nilikuwa na kadi ya CCM ambayo nimeichana na siitaki tena CCM. Na kwa msingi huo CCM imepoteza kura yangu 2010.

Mkuu mimi bado ninayo kadi ya CCM na mwanchama hai, CCM mepoteza kura yako, lakini haikupoteza kura za wananchi wote wa Tanzania, ambao wengi wao wanaelewa kuwa matatizo yake ni ya baadhi ya viongozi wachache, lakini sio chama kizima, lakini angalia kura yako isije ikaishia baharini!

Mwisho naomba tukubaliane kutokukubaliana kwamba CCM inanuka rushwa, wizi na ufisadi. CCM inatakiwa kufutwa kabisa na msajili wa vyama vya siasa Tanzania kwani inaipeleka nchi katika mapigano ya wenyewe kwa wenyewe.

CCM hainuki anything, ila tuna viongozi wachache wanaonuka, kama vile upinzani pia si kuna viongozi wanaonuka kama kina Mtikila, wengine bado ni siri lakini subiri Rostam akiamua kusema yote, unajua kuna watu hamtarudi humu?

Ni watanzania hawo hawo walipigana na wazungu kwa kutumia mikuki, mawe, marungu nk katika kutetea mipaka na uhuru wao, na bila kuficha ukweli ni kwamba Watanzania hawo hawo wamechoka na uchafu unaoendelea hivyo hawataona shida kurudia vita vya majimaji na vingenevyo si muda mrefu toka sasa.a maana alichofanya kikwete katika kupambana na wezi na mafisadi ili kuonesha anakerwa na uchafu huo. USIWE MWONGO WALA MWOGA KATIKA UKWELI.[/SIZE]

1. Wa-Tanzania waliopigania maji maji hawkuwa na uwezo wa kupiga kura kuamua nani wawe viongozi wao, au chama gani kiwaongoze kama ilivyo sasa, wakiingia kwenye vita vya maji maji badala ya kutowapigia kura viongozi wachafu wachache watakuwa ni wajinga wa akili na wenda wazimu, not worhty kupewa support na wananchi wastaarabu.

2. Kikwete hajafanya mengi na kwa haraka kama tunavyotaka, lakini anayo record ya kuwaondoa kwenye power kuanzia Waziri Mkuu, na mawaziri watatu wa serikali yake in just two years, kwa hiyo ni kweli anakerwa na ufisadi lakini sio kwa speed ambayo tungependa awe nayo, kwa hiyo kwa mtizamo wa mama Kilango ni sawa kabisaa, tusipotoshane hapa!

Sasa hapa labda wananchi ndio wataamua baada ya kusoma facts kama muoga na muongo ni nani hasa!
 
Wote nyie mnaomponda mama Malecela sijui hasa mlitaka afanye nini kama MBUNGE!.. usanii upi haswa ikiwa leo hakuna hata mmoja wenu anadiriki kusimama..

Mkuu Bob,

Heshima mbele, hawa niachie mimi nitakula nao sahani moja, unajua ahadi yetu bado iko pale pale kuwa kiongozi yoyote muadilifu wa taifa letu, hatufikiria mara mbili kumtetea, tena mpaka dakika ya mwisho as long as anasimama kwenye mstari unaotakiwa maana na yeye akianza ufisadi basi tutasema ukweli,

kama vile juzi, kwa kawaida tumekuwa tukimkubali sana Mtikila pamoja na mapungufu yake, lakini baada tu ya kujlikan kuwa ni fisadi basi tumesema ukweli kuwa he is out kwenye hivi vita na mafisadi, lakini Mama Kilango bado yumo katika orodha yetu, ya viongozi waadilifu na walo mstari wa mbele kupinga ufisadi.

Ndio maana hata kabla hajaenda huko jimboni kuweka misigni ya visima vya wananchi, wiki iliyopita tumemsaidia mchango wa hali na mali, na in the process tumewaomba washikaji wetu wengi kusaidia mfuko huo na waka-respond kwa wingi sana, within one day zilipatikana shillingi millioni 10, kutoka kwa washikaji wetu tu, kwa hiyo kuna ambao bado tuna imani na baadhi ya viongozi wetu, na hapa nitoe shukrani kwa wote walisohiriki kunisaidia kuchanga hizo hela Mtalipwa na Mungu tu, lakini wananchi walalahoi huko Same East watakunywa maji safi!

Yaaani bina-adam umejaa chuki hata ukweli huwezi kuuona?
 
Wote nyie mnaomponda mama Malecela sijui hasa mlitaka afanye nini kama MBUNGE!.. usanii upi haswa ikiwa leo hakuna hata mmoja wenu anadiriki kusimama..
Hivi mmetumwa au?... huyu mama anazungumzia MAFISADI kwa wananchi wa vijijini ambako sote tunaomba kila siku wazipate habari za JF, sasa iwe anatafuta umaarufu ama hapana lakini message imewafikia wananchi na ndilo tunalojaribu hapa JF kila siku.. Hakuna maneno aliyosema Mama Malecela ambayo sisi wenyewe humu hatusemi hali baadhi yetu mnafanya kazi serikalini, wana CCM na wengine washikaji wa hao mnaowasema.. Je, nanyi mpo kundi gani?..
Kuchana kadi sii hoja na hakuna anayeweza kuthibitisha kuchana kadi ndio kujitenga na CCM.. wewe nenda tawi la CCM, tena mchukue Michuzi awakilishe ujumbe wako magazetini - Uirudishe kadi ya CCM, utoka uanachama na sababu uzitaje kama unaweza sema hata nusu ya haya aliyosema mama Malecela!.. thubutu!
Na ukiweza basi hapo mkuu utakuwa umefungua uwanja kwa wananchi kuelewa yanayokukera lakini kuchana kadi haisaidii kitu kwa sababu record za CCM bado zinakutambua, hawaelewi sababu wala kitu gani kinakukera..
Kuchana kadi ni sawa na kupoteza tu!

Mbona unazunguka kureeeeefu wakati pointi ya msingi dhidi ya Malecela imesemwa ni kuhusu anavyomnadi, anavyomsafisha a failing president?

Malecela anatembea mitaani na Bungeni akimhubiri Kikwete. ``Rais wa nchi ameonyesha kukerwa na hali hii ya vitendo vya wazi kwa baadhi ya viongozi...``

Hakuna serious observer sasa hivi anae endorse rekodi ya Kikwete katika kupambana na ufisadi.

Na Malecela mwenyewe, jinsi alivyokuwa mjanja kama Sungura, hatamki hata siku moja kwamba Kikwete kafanya kazi nzuri, isipokuwa standard line yake ni kusema "Rais ana nia." Anajua Kikwete anaharibu. Utamtathmini vipi mtu kakaa Ikulu miaka miwili na nusu kwa kuongelea "nia" huku anaongoza Serikali yenye maskendo na yenye teuzi za mara mbili mbili za mafisadi, kina Chenge, na watu questionable, kina Mkullo wa Hazina?

Wengine hatumjui huyu Mama mpaka tuwe na fitina nae. Akiporomoka hatunufaiki. Akifanikiwa ku push back ufisadi wote tutafaidika. Kwa nini tuwe na mzizi nae?

Kuna sababu za kumuita huyu Mama msanii. Kilango Malecela atasaidia re-election ya Kikwete kwa mahubiri yake ya "Rais ana nia nzuri..." Anawaandaa Wananchi kumpa nafasi ya kutimiza hiyo "nia nzuri" siku za mbele. Mbele, Mkandara, maana yake hapa ni 2010!

Anawahadaa.

Inawezekana ni kujikomba komba kuomba cheo.

Sio kila nabii mpya atakaekuja na kusema "mimi ndiye" basi umpokee bila kumchunguza. Hata Kikwete alisema yeye ndiye. Kumbe siye. Malecela anasema ndiye. Akijua sie.

Ni msanii huyu Mama Malecela.
 
Hakuna serious observer sasa hivi anae endorse rekodi ya Kikwete katika kupambana na ufisadi.

Na wala hakuna serious obsever anyeweza kumuita mama Kilango msanii, isipokuwa tu kama huyo serious obsever ni msanii yeye mwenyewe,

Kikwete atashinda tena urais, kwa sababu aliposhinda mara ya kwanza hakutegemea endorsement ya Mama Kilango, kwa hiyo hawezi kuiihitaji next time arround, hayo mengine ni makelele ya mlango hayazuii mama Kilango kulala au kendelea na shughuliz ake z akila siku,

Kila siasa zinafanywa na strategy, sio kukurupuka tu, Kikwete ni rais wa taifa aliyechjaguliwa kwa mujibu wa katiba ya taifa letu, sasa pamoja na mpungufu yake bado ni lazima aheshimiwe kama rais, na pia kuna mazuri na mabaya aliyokwisha yafanya, haiwezekani yakisemwa mauzri yake machache basi iwe filimbi tu kama wajinga hapa JF, hapana sisi ni watu wazima tuna akili za kutosha kuelewa kinachoendelea,

Kila kiongozi hafai, sasa wewe vipi ni bin-adam mwenzetu au spirit? Kumjua kwako au kutomjua haibadili anything kwenye sifa za uongozi wa mama Kilnago au rais wa jamhuri, ila so far huna hoja ya kumuita msanii maana inakuwa sio taabu kujua msanii hasa hapa ni nani!
 
KONA YA KARUGENDO: Mama Socrates wa Tanzania

Padri Privatus Karugendo Julai 2, 2008

ANNE Kilango Malecela, Mbunge wa Same Mashariki, akichangia hotuba ya Bajeti Waziri wa Fedha na Uchumi Mustafa Mkulo, alijifananisha na mwanafalsafa wa zamani Socrates. Alisema yuko tayari kufa akitetea ukweli.
ANNE Kilango Malecela Socrates alikataa kwenda kinyume na yale aliyokuwa akiyaamini na kuyatetea katika jamii ya wakati wake. Wafuasi wake walimbembeleza akubali kukana ukweli, ili apone kifo. Enzi hizo Socrates, alikuwa muhimu sana katika jamii na alikuwa mwalimu wa kutegemewa na watu wengi.

Hivyo wafuasi wake waliona ni bora, akane ukweli, ili aendelee kuwapo kuwafundisha na kuibua mambo mapya katika ulimwengu wa fikra. Lakini Socrates alikataa kukana ukweli, maana hakuna heshima ya mwanadamu kuzidi mtu kufa akitetea ukweli. Hivyo Socrates, alikubali kufa kwa kunywa sumu! Galileo Galilei, mwanasayansi na bingwa wa hisabati wa kale wa Italia, aliyeshutumiwa kwa mawazo yake kwamba dunia ilikuwa mviringo na inalinzuguka jua, alipata kusema kwamba " ukweli mara zote ni rahisi kuuelewa pindi unapougundua; tatizo ni jinsi ya kuugundua." Niongezee hapa kwamba na pindi mtu anapougundua ukweli, na kwa vile mara zote ukweli ni rahisi kuuelewa, ni lazima mtu awe tayari kuufia ukweli huo.

Anayekubali kusaliti ukweli, anausaliti utu wake na heshima yake kama binadamu. Imeandikwa kwenye Biblia, kwamba Musa, alinyosha mikono na jua likasimama.Usiku haukuingia, hiyo ikawasaidia wana wa Israeli kupambana na maadui zao. Uvumbuzi wa ukweli wa Gelileo, ulipingana na dhana hii, maana jua limesimama daima, na kinachozunguka ni dunia. Galileo, alikuwa tayari kufa akitetea ukweli huu. Ameheshimika hadi leo hii, na ukweli umebaki ule ule kwamba dunia ni mviringo na inazunguka jua.

Anne Kilango Malecela au Mama Socrates wa Tanzania, ameugundua ukweli juu ya udhibiti na ulinzi mbovu wa fedha za umma. Na kwamba fedha nyingi ziko mikononi mwa watu wachache. Na kwamba watu wachache hawa wakiendelea kushikilia fedha hizi peke yao, hatuwezi kuendelea. Ametoa mfano wa fedha za EPA, zilizoingia mikononi mwa watu wachache kwa njia za udanganyifu. Ukweli huu unamfanya mama huyu awe tayari kufa, kama alivyosema menyewe, kama watu wengine waliokufa wakiutetea ukweli.

Mwanafalsafa mwingine wa zamani wa Ujerumani, Arthur Schopenhauer, aliyeishi kati ya mwaka 1788 na 1860, alisema hivi ju ya ukweli: " ukweli wowote hupitia ngazi tatu. Kwanza, ngazi ya kukejeliwa. Pili, ngazi ya kupingwa na hata ikibidi damu kumwagika. Na tatu, ni ngazi ya kukubalika; kwa kuwa ukweli hujisimamia wenyewe".Hivyo kwa hoja ya Arthur Schopenhauer, haishangazi kuona akina mama Anna Abdalah, Chitalilo na wengine wanamkejeli Anne Kilango. Wanasema anapayuka, wanasema anazungumza kwa mbwembwe, wanasema lengo lake ni kutaka kugombea kiti cha Mwenyekiti wa Taifa wa UWT, wanafikiri anakisaliti chama chake cha CCM, wengine wanakwenda mbali kusema kwamba ana hasira za kushindwa kuingia Ikulu 2005, kwamba mbio za Mzee Malecela ziliishia sakafuni.

Hizo zote ni hatua za kupita katika kutafuta ukweli. Na jinsi hali inavyokwenda, na labda ndiyo maana Anne Kilango, anasema haogopi- inawezekana hata hatua ya pili ya kumwagika damu tukaipitia, (bila hekima, busara na uzalendo) kabla ya ukweli wenyewe kukubalika na kujisimamia.

Ishara ziko wazi: Wakati Chitalilo, akichangia hotuba ya Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu, mbali na kumtetea rais mstaafu Benjamin Mkapa na kujaribu kuwasafisha Edward Lowasa na wenzake, alisema Andrew Chenge, hakubomoa nyumba ya mtu. Hivyo anashangaa sana watu wanaomtuhumu. Wakati akitoa hoja hii yenye utata, baadhi ya wabunge walikuwa wakimshangilia kwa nguvu zote. Maana yake ni kwamba na wao wanakubaliana na hoja hiyo kwamba kwa vile Chenge, hakuvunja nyumba ya mtu basi ni halali awe na fedha bilioni nje hata kama alizipata kwa njia chafu.

Mtumishi wa serikali ya Tanzania, hawezi kupata mabilioni hayo kwa mshahara wake. Kwa mantinki hii, ni kwamba hata na wale wanaouza madawa ya kulevya kwa vile hawavunji nyumba ya mtu, ni halali yao kuwa na vijisenti vyao, wanaokwepa ushuru kwa vile hawavunji nyumba ya mtu wana haki ya kuwa na vijisenti vyao, wale wanaopokea rushwa na kupitisha mikataba mibovu, kwa vile hawavunji nyumba ya mtu wana haki ya kuwa na vijisenti vyao. Ni wangapi wa kukubaliana na hoja hii ya Chitalilo? Ni lazima hapa yatokee mapambano, kabla ya ukweli kujitokeza.

Ingawa wana CCM, wanaendeleza propaganda kwamba wao ni wamoja, ukweli unaonyesha kinyume. Haiwezekani watu wenye busara tunaowafahamu ndani ya CCM, wakubaliane na mawazo mgando kama ya Chitalilo. Ni lazima yatokee mapambano ndani ya CCM, mapambano baina ya CCM na vyama vingine vya kisiasa na mapambano baina ya wananchi na viongozi wao. Inawezekana mapambano haya yakajitokeza wakati wa Uchaguzi Mkuu wa 2010 au kabla ya hapo, maana dalili zote ziko wazi na kuzipuuza ni kujidanganya.

Ishara nyingine ambayo inafunua uwezekano wa kuweza kutufikisha kwenye hatua ya pili ya ukweli, ambapo ukweli hupingwa hadi kufikia umwagaji damu, ni ushabiki unaoendelea ndani ya Bunge. Inashangaza na kusikitisha kuona jinsi baadhi ya wabunge wa CCM wanavyounga mkono kila hoja bila uchambuzi kwa nia ya kuisifia Serikali na kuwakomoa Wapinzani. Bahati nzuri sasa tuna Waziri Mkuu Mizengo Pinda, anayejibu hoja kwa ustadi, umakini na unyenyekevu.

Mtu anaweza kuhoji ni kwa nini wabunge wote wa CCM, waliisifia Bajeti ya Wizara ya Fedha na Uchumi huku ikiwa na makosa ya kitakwimu? Mbona baada ya wabunge wa Upinzani kubaini kasoro za kitakwimu, wabunge wa CCM hawakuungana na wa Upinzani kuwawajibisha wasaidizi wa Waziri wa Fedha na Uchumi? Kuunga mkono kwa lengo la kuwakomoa wapinzani, bila umakini wa kutosha ni usaliti.




MHESHIMIWA Chitaliloe

Chitalilo anashangaa ni kwa nini watu wanaendelea kuimba EPA na Richmond. Hivi yeye na wanaomuunga mkono hawaoni kwamba bado maeneo hayo yanazua maswali mengi kuliko majibu. Hivi hawajui kwamba umma wanaodai wanauwakilisha bungeni unataka kusikia mwisho halisi wa masuala hayo. Kama mbunge haoni vitu vya wazi kama masuala hayo, lakini jamii nzima inayomzunguka inaona, hii maana yake ni kwamba huyu aliyeko bungeni hastahili, walioko nje ndio wanaostahili.

Umma unajiuliza: Je, ni kweli fedha za EPA zimerudi? Wahusika wamefikishwa kwenye vyombo vya sheria? Je, hadi sasa tunafahamu nani anaimiliki Richmond? Tuliambiwa Richmond ilikuwa kampuni hewa! Lakini kampuni hewa ikakabidhi shughuli zake zote kwa kampuni nyingine ambayo hadi leo inalipwa fedha za Watanzania. Kwa nini watu wasiendelee kuhoji? Kwa nini watu wasiendelelee kuimba EPA na Richmond hadi kikaeleweka?

Tunavyoendelea ni wazi zitatungwa sheria kali za kuzuia kuandika chochote juu ya ufisadi, rushwa na uporaji wa mali ya umma kwenye magazeti. Hoja ya Chrisant Mzindakaya, inatupeleka huko. Anahoji ni kwa nini Benjamin Mkapa anaandikwa vibaya kwenye magazeti. Anataka yaandikwe mazuri ya Mkapa, na mabaya yawekwe pembeni kwa vile Mkapa, alikuwa "mtawala" wetu. Anasema kule nje anasifiwa sana na wanatushangaa ni kwa nini sisi tunamtukana.

Sababu za watu wa nje kumsifia ziko wazi kabisa. Aliwaachia uhuru wa kusomba kila kitu na bado wanaendelea kusomba – ni kwa nini wasimsifie? Nafikiri Mzindakaya, anataka Bunge, litunge sheria ya kutowagusa "watawala" wakitoka madarakani.

Mifano hiyo niliyoitoa na mingine inaonyesha kwamba tunataka tusitake ni lazima tupitie hatua ya pili ya kutafuta ukweli, kama inavyoelezwa na mwanafalsafa Arthur Aschopenhauer.

Hatua ya ukweli kupingwa na hata ikibidi damu kumwagika! Tukumbuke pia kwamba si lazima anayetafuta ukweli kuonja matunda ya ukweli huo. Katika matukio mengi, jitihada za kupigania ukweli zinanufaisha vizazi vinavyofuata.

Nchi nyingi za Afrika zilizomwaga damu baada ya uhuru, ziliukejeli ukweli. Watu walisema na kupiga kelele juu ya rushwa na ufisadi; lakini walinyamazishwa, walifungwa na wengine waliuawa. Kwa vile nchi hizo zilikuwa na watu wa mfano wa Anne Kilango, wa kusimama na kutetea ukweli – ziliingia katika vita ya wenyewe kwa wenyewe.

Vita hiyo imechukua miaka mingi, hadi pale nchi hizo zilipougundua ukweli na kuamua kuacha vita. Kama anavyosema Galileo Galilei, kwamba ukweli mara zote ni rahisi kuuelewa pindi unapougundua; tatizo ni jinsi ya kuugundua.

Nchi hizo za Kiafrika, zimegundua ukweli, baada ya kuharibu mali nyingi na kupoteza maisha ya watu wengi.

Ingawa sifahamu vizuri historia ya mama huyu Socrates wa Tanzania, hoja zake zinashawishi na kuwagusa Watanzania wengi wa kawaida. Uchumi wa Tanzania, uko mikononi mwa wachache. Wakati maisha yanaendelea kuwa magumu, bei ya mafuta inapanda, mfumko wa bei unashika kasi ya kutisha, lakini wachache wetu wanaogelea katika ufahari.

Wanafanya manunuzi na matumizi yao nje, wanasomesha watoto wao nje, wakiugua wanakimbizwa India, Ulaya au Marekani. Wamejenga majumba ya kifahari na wanaendesha magari ya bei mbaya. Ipo mifano mingi ya kuelezea jambo hili na Watanzania wengi sasa wanafahamu.

Mfano mjadala juu ya kampuni ya Meremeta na usiri unaoizunguka. Inaonekana wazi kuna ufisadi pale, lakini Serikali inashikwa kigugumizi kutoa maelezo na kujifunga kwamba Meremeta ni ya Jeshi, na siri za Jeshi hazijadiliwi.

Hii inaweza kuwa mbinu mpya ya kuwakinga mafisadi. Kila matumizi ya fedha yenye utata yatakuwa yanasukumwa jeshini maana hakuna ruhusa ya kujadili matumizi ya kijeshi! Kinachohitajika ni kuwafunulia zaidi wananchi kama anavyofanya mama Socrates.

Panahitajika watu wachache wa kusimama na kutetea ukweli. Utafiti wa haraka unaonyesha kwamba idadi kubwa ya Watanzania inashawishiwa na mawazo ya watu kama kina Anne Kilango, kuliko ya Chitalilo na Mzindakaya.

Nguvu ya umma hujionyesha katika uchaguzi: kura ni silaha ya pekee kwa mwanachi. Lakini uzoefu unatuonyesha jinsi kura zinavyochezewa: Kenya na Zimbabwe ni mifano mizuri. Matokeo ya kuchezea kura si mazuri, yanaishia kwa umwagaji damu.

Hoja yangu ni kwamba kila raia mwema wa Tanzania, hawezi kupuuzia msimamo wa kutafuta na kusema ukweli. Mbegu ya kutafuta na kusema ukweli haiwezi kuoza. Ni hekima kwa viongozi kuanza kusoma alama za nyakati.



Mwandishi wa makala hii anapatikana kwa S. L. P. 114 Magu, Mwanza. Simu: 0754 633122
 
...Kikwete ni rais wa taifa aliyechjaguliwa kwa mujibu wa katiba ya taifa letu, sasa pamoja na mpungufu yake bado ni lazima aheshimiwe kama rais, na pia kuna mazuri na mabaya aliyokwisha yafanya, haiwezekani yakisemwa mauzri yake machache basi iwe filimbi tu kama wajinga hapa JF, hapana sisi ni watu wazima tuna akili za kutosha kuelewa kinachoendelea,

Katika rekodi ya mazuri ya Kikwete, kupambana na ufisadi halimo.

Ukibisha hilo hiyo ni irresponsible punditry.

Kikwete administration imepagawa na skandali za ufisadi.

Maswala ya uhalali wa Kikatiba wa kuchaguliwa kwa Kikwete na heshima kwa Rais yote hayo hayahusiani na kashfa za utawala wake wa rushwa. Ni kama kumsafisha.

Malecela anatembea vijijini akiwaambia unsuspecting peasants kwamba Kikwete ana nia nzuri. Sio mkweli.
 
Katika rekodi ya mazuri ya Kikwete, kupambana na ufisadi halimo.
Ukibisha hilo hiyo ni irresponsible punditry. Kikwete administration imepagawa na skandali za ufisadi. Maswala ya uhalali wa Kikatiba wa kuchaguliwa kwa Kikwete na heshima kwa Rais yote hayo hayahusiani na kashfa za utawala wake wa rushwa. Ni kama kumsafisha.

Mkuu ninachosema ni kwamba ilipofikia sasa inaonekana wewe una beef ya binafsi na mama Kilango, sasa dawa ni umtafute au upewe mawasiliano yake umweleze shida yako maana haiwezekani kuwa kila anlofanya kwako ni tatizo tu, Kikwete ana mazuri na mapungufu pia, lakini in two years bado ana muda wa kutosha kuonnyehsa mapya au kurekebisha mabaya aliyokwisha fanya, sasa kumwita mama Kilango msanii sijui Mtikla unamwitaje?

Majority ya sisi wa-Tanzania tunakubaliana na kazi ya mama Kilango kwa taifa letu so far, ila ni wewe ni mwenzako mmoja ndio mna tatizo, lakini tunasema hivi haiuzii mama Kilango kufanya shughuli zake, ndio maana nikasema ilikuwa a big suprise last week tulipowaomba wananchi kusaidia kuchagia hela za kujenga visima huko Same East, wananchi waliposikia ni mama Kilango, in one day tuliweza kukusanya shillingi millioni 10,

Sasa hivi yupo East Same, atarudi kesho Dodoma, na Jumatatu atakuwa tena ndani ya bunge, kuwakilisha wananchi wa jimbo lake na sisi wa taifa, sasa wewe uendelee na hicho kikorosho! Mambo ya rais hawezi kuyabeba mbunge, yeye kazi yake ni kama hii kujenga visima vya maji kwa wananchi!

Malecela anatembea vijijini akiwaambia unsuspecting peasants kwamba Kikwete ana nia nzuri. Sio mkweli.

Mama yuko jimboni kwake aliposema hayo, na pia ameyasema sio mara moja bungeni, sasa sidhani kama hao peasant walikuwa bungeni pia, mkuu mwache mama afanye kazi, au kwenu hakuna kina mama viongozi nini?
 
FMES,

I wish Mama K would go postal on everybody in CC, NEC and Serikali kuu who is toying with us.

I know sometimes she has to play it safe, but let her know that we are behind her and we will support her if he would go Postal on Kikwete and Mafisadi demanding accountability!

The truth is, Kikwete has never demanded accountability publicly or in private. He is avoiding everything and allowing nature to take its course!\


Mama K inabidi apandishe mashetani na munkari wa Kipare siku moja, watu watafutane, by the time vumbi limetulia maji na mafuta yatatengena kwenye chungu!
 
Back
Top Bottom