Kila nikishusha Bei dhidi ya washindani wangu nao hushusha Zaidi yangu, nifanye nini kuongeza mauzo?

Biashara ni sayansi na inataka elimu au uzoefu wa mda mrefu sana
Tatizo kila mmoja anafanya biashara siku hizi na faida ndio hizo mnazopigania za 200
Mtu anafanya biashara ya faida 200 na anakuambia siachi hata 100 basi bora kutafuta kazi nyingine

Mlo wao wanalia hapohapo kwa maji ya kisima yaani maisha ya wengine ni duni sana kiasi unasema hivi huyu ni mfanyabiashara au anaganga njaa tu
Mwisho wa mwaka TRA wakija kudai chao hujawakusanyia kabisa maana wewe ulikuwa unaweka faida yako tu bila kuweka na VAT maana ukiweka na hiyo vat bei lazima iwe juu

Ndio hapo tunarudi na kusema biashara ni Elimu
Angalia Asians wanavyofanya biashara
Kesho akiendesha V8 unasema mwizi kumbe faida ya bidhaa zake ni zaidi ya nusu na VAT kakulima kiaina

Tutakalia kusema wakuja wanaiba sana ila hatujui kuwa biashara ni zaidi ya tunavyoiona
Wengi wanafuata mkumbo tu halafu msimu wa kulima usifika anaenda kulima na kumuacha wife anauza duka

Sasa unajiuliza huyu ni mfanyabiashara au mkulima?
Sifoki ila ukweli ndio huo na wengi wanafeli kwa sababu ya jirani kampiga bao anaenda kuchukua mkopo wa mamilioni ili ajaze duka ila bado anakuja kufeli vibaya na mwisho nyumba inapigwa mnada

Hitimisho naona kiwango cha biashara kwa wengi ni kuuza ubuyu na karanga tu
Kwahio unatuambia nini mkuu?! Ushauri...?
 
Wengi wanatoa ushauri bila kuelewa biashara ya duka la jumla. Ngoja nitoe mwazo yangu kuhusu hii biashara kidogo.

Mosi, hii biashara kama una mtaji mdogo basi inatakiwa utafute sehemu ambayo utakuwa mbali na wenye mtaji mkubwa maana wao wanachukua mzigo mkubwa na huwa wanapata kamisheni wakimaliza ule mzigo. Kwahiyo anakuwa analenga faida ndogo ili auze haraka ili apate kamisheni.

Pili, inatakiwa uwe unafanya delivery bure kwa wateja wako, hii itasaidia sana kwa wale wateja wavivu ambao hawapendi kuzunguka yani wanapiga simu unawapelekea mzigo.

Biashara ya jumla ni biashara kichaa inayoumiza sana kichwa kama upo sehemu yenye ushindani halafu una mtaji mdogo
Excellent.
 
Sidhani kama nina jibu ila sio mbaya nikiweka ushauri wangu pia.
Kwanza kupunguza bei ni jambo jema, pale ambapo bado kuna faida reasonable. Anayepima faida ni reasonable ni wewe! Kwa hiyo nikushauri vitu vichache
1. Panua wigo wa soko lako. Jaribu kuwafikia watu wengine. Unasema ni duka la jumla. Ina maana unaweza ku supply kwa maduka ya reja reja. Badala ya kukaa hapo na kugombea wateja fanya kuwatafuta wateja wa reja reja huko waliko. Tumia mitandao na hata kutembelea maeneo mbalimbali na ujaribu kuwaomba uwe supplier wao. Ukiongeza wigo wa soko, unaongeza uwezo wa kushindana pia. Itakugharimu muda na nguvu, lakini ndio njia ya kuongezeka.

2. Offer Delivery. Wateja wengi huwa wanakuja kwa sababu hawana namna. Ukiwapa ofa ya kuwapelekea kwa gharama kidogo watapenda sana, haswa kama mtajenga uaminifu.

3. Punguza matumizi yasiyo ya lazima. Kama unashusha bei inabidi na matumizi yapungue ili kufidia punguzo.

Sio mtaalam wa hiyo aina ya biashara ila kutoa ushauri sio jambo baya!
 
Nyota naisafisha kwakutoa zaka ktk Mali yangu
Ushawahi kusikia chochote kuhusu ndumba kwenye biashara labda? Au kusikia figisufigusu za biashara maybe? Dawa za kuongeza mvuto? Kalumanzira je...Tawire tawire
Kuna wanaofanya hivyo na wanatusua

Japo nakwambia sio uende huko maana unaweza kukuta wenzio wanakupiga gap kutokana na hizo ishu

Ushauri wangu fuata hizo tips unazopewa na wadau za price, customer care,people,promotion, place n.k
Hakuna Cha nyota kufifia Wala nin....nichangamoto zakibiashara tu mkuu

Sent from my SM-J720F using JamiiForums mobile app
 
Kwahio unatuambia nini mkuu?! Ushauri...?

Ni kupambana tu ingawa unapambana na watu wa aina nyingi sana na wengine wanakuwa na bidhaa nyingi za wizi kwa hiyo hata akiuza cost bado ana faida maana kalipia hela kidogo sana

Mkuu nazijua biashara hizi na faida zake sio kubwa halafu mtu anauza mpaka cost

Ni mapato wanayajua haya kuwa wengi hawana elimu ya ulipaji wa kodi ndio maana wengi wanakadiriwa tu

Ushauri ni kuweka bidhaa zenye faida kubwa au kujitahidi kuwa na miradi mingi
Kuwa na biashara tatu au nne ni nzuri zaidi
 
Pole mkuu kwa changamoto hiyo
Kiukweli wewe unapitia changamoto Kama yangu
Ila Hebujaribu mbinu hizi
1 omba mungu kwa Iman yako Kila siku kabla na baada ya kufungua biashara yako
2 fungua mapema kuliko wenzako na funga kwa kuchelewa kuliko wao
3 kuwa msafi kwenye mwili, mdomo (kauli nzur kwa wateja) pia mpangilio mzuri wa bidhaa zako
Nk usisahau kuwa mcheshi na mchangamfu hasa kwa watoto heshima kwa wakubwa hasa wazee
4 jiongeze kwenye vitu ambavyo kwa namna yyte ile wapinzan wako hawawezi
Mfano
Tafuta maharage mazuri kuliko wao,
Choroko na karanga nzur kuliko wao
Uza Hadi vile vitu ambavyo watu weningine hawana mfano sindano za kushona nguo nk
5 tafuta Bango andika baadhi ya vitu na Bei zake Kisha liweke hapo njiani karibu na duka lako watu wakipita walione

6 tembelea mama ntilie waombe wawe wateja wako ukipata 5 wanaochukua angalau vitu vya 20000 Kila siku una uhakika w mauzo ila uwe nao makin ni warushi wazuri sana

Nakutakia Kila la kheri mdau mwenzangu
 
Baadhi siyo wateja ni watu wanajumua kwako wanapeleka kwa miongoni mwa washindani wako na wanarudi kwako kukupa pressure, uza bei yako utayopata faida wateja wa kweli utawapata tu pia ongeza thamani kwenye biashara yako kama lugha nzuri, kufanya delivery, nyongeza ya ziada.
 
Pole mkuu kwa changamoto hiyo
Kiukweli wewe unapitia changamoto Kama yangu
Ila Hebujaribu mbinu hizi
1 omba mungu kwa Iman yako Kila siku kabla na baada ya kufungua biashara yako
2 fungua mapema kuliko wenzako na funga kwa kuchelewa kuliko wao
3 kuwa msafi kwenye mwili, mdomo (kauli nzur kwa wateja) pia mpangilio mzuri wa bidhaa zako
Nk usisahau kuwa mcheshi na mchangamfu hasa kwa watoto heshima kwa wakubwa hasa wazee
4 jiongeze kwenye vitu ambavyo kwa namna yyte ile wapinzan wako hawawezi
Mfano
Tafuta maharage mazuri kuliko wao,
Choroko na karanga nzur kuliko wao
Uza Hadi vile vitu ambavyo watu weningine hawana mfano sindano za kushona nguo nk
5 tafuta Bango andika baadhi ya vitu na Bei zake Kisha liweke hapo njiani karibu na duka lako watu wakipita walione

6 tembelea mama ntilie waombe wawe wateja wako ukipata 5 wanaochukua angalau vitu vya 20000 Kila siku una uhakika w mauzo ila uwe nao makin ni warushi wazuri sana

Nakutakia Kila la kheri mdau mwenzangu
Umemshauri vizuri sana mkuu.
 
Pole sana mkuu. Ushauri wangu unaweza kuhitaji muda kidogo ila ukisimama utakuletea matokeo ya muda mrefu sana

Wewe shida yako ni wateje na ushindani.

Binafsi naamini katika Nguvu ya Digital Marketing na kujenga uhusiano mzuri na wateja na kuwatumia kama mabalozi wangu.

Digital Marketing ni uwekezaji unaoukujengea brand na kupaisha biashara yako popote muda wowote.

Ila unahitaji muda (Kuanzia miezi 6)ili kupata matokeo mazuri.

Kufanya biashara locally kama zamani kwasasa ni changamoto.
 
Kwa lugha nyingine ibrand biashara yako badala ya kuendelea kupunguza bidhaa

Ktk biashara unachopaswa kufanya ni kucheza na saikolojia ya mteja Tu..

mfano wewe na mshindani wako wote mnauz mchele wa kyela kilo ni TSH 1500/=,mwenzio akapunguza bei akauza 1200/= wewe badala ya kuuza elfu Mia mbili km yeye badala yake pima kilo yako weka kwenye package mzuri kuliko mfuko(kifaa) aliikuja nao.custimer care pia ni kipengere muhimu sn..hapo utamfanya mteja ajiskie vizuri sn
Umewahi kufanya biashara?
 
Habari wakuu,

Nimekuja kwenu kutaka fikra na mawazo.. Niko ktkt biashara ya duka la jumla la vyakula kwa muda Sasa changamoto iliyopo kila mshindani wangu analenga kushika wateja soko kwa kushusha Bei chini Zaid nami nimekua nikishuka nao..

Sasa Basi Hali hii imepelekea kuzid kukupunguza faida ktk kila bidhaa matokeo yake unajikuta ktk bidhaa unayoiuza 56000 unabakiwa na faid200.

Na ukisema ubaki na bei juu tofaut na washindani wako Basi wateja wengi hukimbilia kwa wenye Bei ndogo Zaid maana soko ni dogo wateja niwale wale mnafanya kugawana wateja kwa mbinu ya kushusha Bei.

Wakuu nin nifanye nitoboe maana nawaza mbinu nyingi Zina feli.

Tafuta source ya uhakika na nafuu unapochukulia mzigo huenda wewe unachukua ghali ndomana wanajua wakishusha mpaka sehemu fulan we huwezi Mana itakula kwako.

Tafuta chanzo lingine cha kuchukulia mzigo pengine mpigie supply wako kwa namba nyingine jidai unataka mzigo alafu sema bei ya chini ili uone Mambo inakuaje!

Hyo n akili ya salesman nimekupa sababu tabia zetu tunazijua duka zinatengana kwa ukuta tuu au barabara lakini kila mmoja anabei yake
 
Habari wakuu,

Nimekuja kwenu kutaka fikra na mawazo.. Niko ktkt biashara ya duka la jumla la vyakula kwa muda Sasa changamoto iliyopo kila mshindani wangu analenga kushika wateja soko kwa kushusha Bei chini Zaid nami nimekua nikishuka nao..

Sasa Basi Hali hii imepelekea kuzid kukupunguza faida ktk kila bidhaa matokeo yake unajikuta ktk bidhaa unayoiuza 56000 unabakiwa na faid200.

Na ukisema ubaki na bei juu tofaut na washindani wako Basi wateja wengi hukimbilia kwa wenye Bei ndogo Zaid maana soko ni dogo wateja niwale wale mnafanya kugawana wateja kwa mbinu ya kushusha Bei.

Wakuu nin nifanye nitoboe maana nawaza mbinu nyingi Zina feli.
Huo ubinafsi wako ndo unakuponza, mda wote unawaza vita, wenzako wanataka amani, wewe ukiwasha moto wao wanakuja na maji wanauzima unabaki kupangusa majivu
 
Nina duka la jumla la dawa za binadamu mbinu ninayotumia ni ndogo sana nawapumbaza wateja wangu kwa kushusha bei bidhaa Fulani uku bidhaa nyingine napandisha bei zaidi..ile bidhaa niliyoshusha bei ndio inaficha bidhaa fulani niliyopandisha bei....
Iko hivi naangalia items zinazotoka sana ndio hizo hizo nashusha bei uku items nyingine napandisha bei kubwa sana...yaani wateja hawakauki wanasema nina bei ndogo kumbe nawazuzua kwa baadhi ya items nang'ata na kupuliza
 
Nina duka la jumla la dawa za binadamu mbinu ninayotumia ni ndogo sana nawapumbaza wateja wangu kwa kushusha bei bidhaa Fulani uku bidhaa nyingine napandisha bei zaidi..ile bidhaa niliyoshusha bei ndio inaficha bidhaa fulani niliyopandisha bei....
Iko hivi naangalia items zinazotoka sana ndio hizo hizo nashusha bei uku items nyingine napandisha bei kubwa sana...yaani wateja hawakauki wanasema nina bei ndogo kumbe nawazuzua kwa baadhi ya items nang'ata na kupuliza
Umetishaa
 
Habari wakuu,

Nimekuja kwenu kutaka fikra na mawazo.. Niko ktkt biashara ya duka la jumla la vyakula kwa muda Sasa changamoto iliyopo kila mshindani wangu analenga kushika wateja soko kwa kushusha Bei chini Zaid nami nimekua nikishuka nao..

Sasa Basi Hali hii imepelekea kuzid kukupunguza faida ktk kila bidhaa matokeo yake unajikuta ktk bidhaa unayoiuza 56000 unabakiwa na faid200.

Na ukisema ubaki na bei juu tofaut na washindani wako Basi wateja wengi hukimbilia kwa wenye Bei ndogo Zaid maana soko ni dogo wateja niwale wale mnafanya kugawana wateja kwa mbinu ya kushusha Bei.

Wakuu nin nifanye nitoboe maana nawaza mbinu nyingi Zina feli.
Ongeza muda wa kufungua na kufunga biashara.
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom