Kila nikipata rafiki JF ananikimbia

housegirl

JF-Expert Member
Jan 16, 2014
3,125
2,189
Naandika kwa masikitiko makubwa! Wote ni wa ID ya zamani.

Wa KWANZA, Tulikuwa wapinzani lakini alinifwata PM. Ni kama MAXSHIMBA amfwate Faiza Foxy.

( Hivi MAXSHIMBA yuko hai jamani? Ana sauti flani amazing nilikuwa nasubiri aanzishe kanisa lake nihame kanisa mie)

Tulikuwa tunaongea sana PM, aliniambia anauza duka. baadae nikawa busy nikampa number yangu. Aka promise kupiga but he never called. Nilivyorudi JF akataka aone picha yangu. Nikampa my FB name nikamuuliza kwanini hunipigii? Akasema anaogopa kufwatiliwa na usalama wa taifa :D na urafiki ukaisha.

WA PILI anajua na hii ID ya sasa. Alikuwa type ya MshanaJr (ushirikina) Nikaona anajua mambo mengi nikamMP.

Tulikuwa marafiki wazuri, the type of people you could talk to all day. sikuwahi kukutana naye. Jamani sijawahi kupigwa fix na mtu kama huyu jamaa. He took advantage of my curiosity. Hapo ilikuwa tusafiri anipeleke Morogoro kunithibitishia uchawi :D . hapo nipo kwetu nawaza ntaondokaje nikaone uchawi mie!

Unfortunately urafiki wetu ulikufa kwasababu ilishindikana kuwa tu "marafiki". Wakati tunaagana akaniambia hatonifanyia madawa kama alimvyomfanyia cousin wake hadi akafa akaoza juu yake. Sijui kama anajua sikulala week nzima, nilihisi nikilala tu nageuka panya. I would like to talk to him again tho. Nimepoteza contacts zake na Naona ID yake kaikacha.

WA MWISHO ndo kaniacha hoi. Naye anajua hii ID.

Nilivyogundua JF nilikuwa namfwatilia, very intelligent, very interesting. Nilifikiri ni mbabu ana watoto na wajukuu, nikataka urafiki kama mjukuu wake, u know nilikuwa napenda kukaa na wazee ujifunze maisha. Lakini sio siku hizi, wazee wa siku hizi vilaza halafu Hawana adabu. Hata mke wake ukimwangalia unawaza "me mke mwenzio ooh".

Anyways, kumbe hata sio mzee ni kijana tu (kwa umri alionitajia) na kipaji chake. Nilikuwaga naibuka PM nikikwama kwenye mabishano ani boost point lol. Huyu ndo alinifundisha kuacha kuandika vifupi vya "u knw". Aliniambiaga Mara moja kuwa hapendi hadi Leo naandika vizuri.

baadaye I officially asked for friendship. Akakubali akasema alitaka urafiki toka zamani. Nikamwabia Nipe email yako nikutumie na picha. Nikamtumia. Na urafiki ukaisha hajawahi kunijibu tena :D .

Kwahiyo natangaza kususa urafiki na watu wa JF :(

On a serious note, nimetembelea account yangu ya zamani nashangaa is this really me?? Yani ni kama namsoma mtu tofauti. Nimebadilika sana. naona kama nimekuwa kilaza, lakini Kiswahili changu kimekuwa kizuri sijui nilikuwa naongeaje!!

So nimeamua niondoke humu Nikatembee huko duniani halafu nirudi kivingine. Baadae nichungulie hii account nione kama nimebadilika.

IMG_20161220_171328_089.JPG
 
Mkuu huenda una lijisura libaya na ambaye hakuna atakayehitaji kujumuika nawe.

Yaani kati ya hao wote hawajakuomba papuchi?
Aisee,utakuja libaya Nakuapia.
Duh? Hivi kwani sura inahitajika kwenye vigezo vya urafiki ama mapenzi?

Housegirl: Kama hujali jinsia basi mie naweza kuwa rafiki yako!
 
Wakongwe WA jf mnapotea jukwaa Lina watu wapya wengi. Vitu kama hivo ni vyako binafsi tunapenda kuwasikia Wakongwe. Housegirl nakukubali Sana tuwe marafiki hasa uwe Dada yangu
 
Nipe namba yako nikupigie, nikupe yangu ya moyoni kwanza kabla ya kukutongoza nikuchore tatoo usoni....:p
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom