Kila nikijaribu kumsamehe/kuwasamehe nashindwa

Mkuu huu ujumbe Wako ni Mkubwa sana sana and I wish mwenzangu angekutana na mtu kama wewe baada ya ile ishu maana hii thread isingekuwa Kwenye server ya JF. Nimeelewa 100% ulichoandika na nakubaliana na wewe 110%

Mkuu Nina madhaifu yangu kama binadamu mwingine yoyote yule Ila Nina ubinadamu Wangu pia, mkuu unamsaidia mtu ambaye anahitaji msaada Wako au hata anaonyesha basi kuhitaji msaada Wako. Mwenzangu baada ya hii ishu Kutoka aliangukia Kwenye mikono mibaya na mpaka Sasa yupo Kwenye mikono mibaya sana.

Mwenzangu hajawai kujutia alichokifanya (inawezekana labda yeye anaona hana cha kujutia, sijui). Kwa hyo hata msamaha aliokuwa anaomba au wanaomba walikuwa wanaomba kwa sababu fulani, trust me I know what I am talking about. Sio kuwa nilikuwa tu na vile niliongelea Kwenye thread, nilikuwa na assets nyingine pia ambazo mwenzangu alikuwa anazijua ila alinikuta Nazo pia.

Baada ya kutokea yaliyotokea bado alikuwa Anataka na sehemu ya zile assets ila alipoenda polisi wakamwambia alifanya kosa kuuza vile vitu kwa hyo hata akifungua kesi haitakuwa na uzito wowote, na haya yote alikuwa anafanya chini ya muongozo wa watu fulani fulani. Kwa hyo she was determined to finish me for good. Hvi mkuu mtu amefanya haya yote (Sawa nilikuwa chanzo) mimi nimepata ajali nimeumia sana, nimelala ndani karibia miezi sita, huyu mtu ananiandikia sms "Nitaendelea kulia na Mungu yakukute zaidi ya hilo". Hivi mkuu hata kama mimi ni malaika huyu mtu nitamwelewa kweli? Ngoja ebu nikae kimya aisee.
Ujue nini mpendwa nilitaka tu uelewe ni wapi umejikwaa na umuelewe mwenzio pia ni wapi alijikwaa. Wewe ndo ulianza lakini wakati mwingine reaction ya mtu unayemkosea inaweza ikasolve tatizo au ndo ikakuza tatizo. Unfortunately reaction ya mkeo ilichochea moto. Lakini hatupaswi kumlaumu sana pia; kwa sababu sio kila mtu ana uwezo wa kuhimili dhoruba kali inapokuja.

Usishangae kwa nini mkeo bado anakuchukia na bado anazidi kuharibikiwa; ni kwa sababu bado hajasamehe; bado amekubeba moyoni mwake. Ule uchungu alioubeba ndo unafanya akufanyie vituko vyote hivyo akifikiri anakukomesha kumbe anajikomesha mwenyewe zaidi. Na kadri maisha yake yanavyozidi kuharibika ndivyo uchungu unavyomuongezeka. Possibly kila muda anawaza "bila mume wangu kuchepuka; leo hii tungekuwa tunaishi kwa amani na watoto wetu". Kila baya analokutana nalo, anakuona wewe ndo kisababishi. So usitegemee yeye kukutakia mema. Siku akipata neema ya kusamehe atajuta sana kwa kuharibu maisha yake mwenyewe. Afu anaweza akasema "bora ufe" ila siku ndo umekufa (God forbid); yeye ndo anaweza akawa analia kwa uchungu kuliko unavyodhani; akatamani uamke ili mmalize tofauti zenu (nimelishuhudia hili sana tu).

So wewe usiumizwe sana na vituko vyake; muombee siku moja Mungu amguse akaweze kusamehe na kutoa uchungu moyoni mwake. Ni kwa faida yenu wote na watoto wenu hata kama kila mmoja ataendelea na maisha yake; amani ni ya muhimu sana
 
Nimesoma kitabu hicho chote naomba urudie maneno haya "Utusamehe makosa yetu kama tunavyowasamehe wale waliotukosea" Naomba nikuambie kumsamehe sio kurudiana naye ila nikumtangazia amani. Na vilevile moja ya haki za watoto nikuwajua wazazi wake. Kwanza kuikuwa na tatizo kwako na kwake ingawa wewe umeeleza upande wa matokeo ila nawe unamakosa kwenye hili nalo utubu urekebishe. Maana kuzini wote mlizini sema yeye amepata tunda. Na msingi wa jambo lenyewe ulikuwa mbaya lazima nyumba ianguke. So wewe mtangazie msamaha halafu songa mbele kama unaoa oa endelea na maisha ila watangazie msamaha. Narudia kuwa haimaanishi kuwa anarudi kwenye nafasi yake ila wewe unaondoa kinyongo na unamweleza kuwa nimekusamehe ila utakuwa karibu yangu utakaa kwenye nafasi ulioichagua na unapanga katika hizo wiki mbili za likizo ukitoka huko mgodini wakati watoto wako likizo wanakuwa na muda na mama yao. Ni ngumu ila ukitaka kupona na kuihisha familia yaani watotot wako hilo halina short cut.
 
Nimesoma kitabu hicho chote naomba urudie maneno haya "Utusamehe makosa yetu kama tunavyowasamehe wale waliotukosea" Naomba nikuambie kumsamehe sio kurudiana naye ila nikumtangazia amani. Na vilevile moja ya haki za watoto nikuwajua wazazi wake. Kwanza kuikuwa na tatizo kwako na kwake ingawa wewe umeeleza upande wa matokeo ila nawe unamakosa kwenye hili nalo utubu urekebishe. Maana kuzini wote mlizini sema yeye amepata tunda. Na msingi wa jambo lenyewe ulikuwa mbaya lazima nyumba ianguke. So wewe mtangazie msamaha halafu songa mbele kama unaoa oa endelea na maisha ila watangazie msamaha. Narudia kuwa haimaanishi kuwa anarudi kwenye nafasi yake ila wewe unaondoa kinyongo na unamweleza kuwa nimekusamehe ila utakuwa karibu yangu utakaa kwenye nafasi ulioichagua na unapanga katika hizo wiki mbili za likizo ukitoka huko mgodini wakati watoto wako likizo wanakuwa na muda na mama yao. Ni ngumu ila ukitaka kupona na kuihisha familia yaani watotot wako hilo halina short cut.


Sawa mkuu nitajaribu kuzingatia Ushauri Wako.

Hahahaaa...mbona migodi yote imefungwa mkuu.
 
Ujue nini mpendwa nilitaka tu uelewe ni wapi umejikwaa na umuelewe mwenzio pia ni wapi alijikwaa. Wewe ndo ulianza lakini wakati mwingine reaction ya mtu unayemkosea inaweza ikasolve tatizo au ndo ikakuza tatizo. Unfortunately reaction ya mkeo ilichochea moto. Lakini hatupaswi kumlaumu sana pia; kwa sababu sio kila mtu ana uwezo wa kuhimili dhoruba kali inapokuja.

Usishangae kwa nini mkeo bado anakuchukia na bado anazidi kuharibikiwa; ni kwa sababu bado hajasamehe; bado amekubeba moyoni mwake. Ule uchungu alioubeba ndo unafanya akufanyie vituko vyote hivyo akifikiri anakukomesha kumbe anajikomesha mwenyewe zaidi. Na kadri maisha yake yanavyozidi kuharibika ndivyo uchungu unavyomuongezeka. Possibly kila muda anawaza "bila mume wangu kuchepuka; leo hii tungekuwa tunaishi kwa amani na watoto wetu". Kila baya analokutana nalo, anakuona wewe ndo kisababishi. So usitegemee yeye kukutakia mema. Siku akipata neema ya kusamehe atajuta sana kwa kuharibu maisha yake mwenyewe. Afu anaweza akasema "bora ufe" ila siku ndo umekufa (God forbid); yeye ndo anaweza akawa analia kwa uchungu kuliko unavyodhani; akatamani uamke ili mmalize tofauti zenu (nimelishuhudia hili sana tu).

So wewe usiumizwe sana na vituko vyake; muombee siku moja Mungu amguse akaweze kusamehe na kutoa uchungu moyoni mwake. Ni kwa faida yenu wote na watoto wenu hata kama kila mmoja ataendelea na maisha yake; amani ni ya muhimu sana

Sawa mkuu....nimekusikia
 
mi nikushaur umsamehe tu. ila ucmrudie kabisa. nenda mjin mtafute na kama Mungu amekujalia kidogo mfungulie biashara hata ndogo ndogo. hawa viumbe unaweza kukuta ni dada yake alimdanganya na sasa hib ndio anajutia we msamehe ila ucmkaribie kabisa mfungulie biashara kama unaweza. coz umesema mwenyewe amekuzalia watoto wazur mkumbuke tu hata kwa hilo.
kwa upande wangu mke wangu anajua na kwao wanajua ikitokea tumekosana yeye aondoke tu au niondoke mimi nimuachie nyumba ila cwez kumuachia watoto hilo haijalish sheria zinasemaje. ukitaka kufa zungumzia watoto. mi nikiwa Dar tena nyumban kila iitwapo leo lazima nikae hata lisaa limoja na watoto so ukitaka kifo niambie sijui kisheria hilo mzee naahirisha kwenda mbinguni.


Sawa mkuu nitajaribu kuzingatia Ushauri Wako.

Ila mkuu una maneno,
 
Nilishuhudia Mwanamke aliekwenda kuazima shoka kwa jirani kisha akapasua vyombo na thamani za nyumba nzima aliposikia mumewe ana mpango tu wa kuongeza mke wa pili. Jamaa alikuwa ni mfanyabiashara mkubwa sasa imagine thamani za ndani, kitu Sony Bravia 50 inch curve mpya kabisa ilipigwa shoka chali kifo cha mende...…..Pale ndio niliposema kweli mwanamke ni jalala.

Duuu, mkuu na wewe unajua kutia chumvi, eti kitu Sony bravia 50 inchi curve Mpya kabisa ilipigwa shoka chali kifo cha mende. Hahahahaaaa

We kweli chumvi Namba 2
 
Ila jamani kweli tuseme baadhi ya wanawake nadhan huwa ni pyscho!yaan mtu unaomba hela ua chkula unatumiwa laki 3 alafu unamzengua mwanaume wa hvo??hivi huyu Mungu kwann huwa anakiletea mwenza magimashi?kwann Mungu asikutanishe smart kwa smart?????Mungu tumechoka na haya maisha!..
1.mkeo ana shida 1 tu hajitambui.na vile elimu haipend bas ndo kbs!usimrudie..familia ilikudhalilisha sana!pole mzee baba!
 
Sasa tutajuaje kipi ni kipi labda tupate story upande wa pili.


#NEVER JUDGE ISSUE BY ONE SIDE


Sasa wewe unakuwa Kiazi Sasa, we unatuandikia hapa tupate story upande wa pili titaitoa Wapi sisi???

Hii ndo tuliyoletewa kwa hyo kama una chochote cha kucomment comment kulingana na story iliyoletwa huo upande wa pili kama unautaka labda uende mahakamani.
 
Umeona mbali, mwanamke kama hachepuki siku akukamata tena na ushahidi juu, uwii hasamehi kamwe!

Sana sana anakutafutia tukio tu ili akukomeshe japo anaweza kuzuga kukusamehe!
 
Mwanamke huwa hasamei akikubamba na sms/whatsapp au akikufumania live. Niliwahi kukutwa na kondomu 2004 mfuko wa suruali tukiwa wachumba mpaka leo (November 2019) anakumbushia.
NB:
Usimuombe mwanamke msamaha maana hutasemehewa asilani japo wakat wa tukio atajidai kakusamehe.
We unawajua wanawake vizuri
 
Bro pole sana, msamehe amekuzalia wana....ila usimrudie,,,, namaanisha muinue hata kwa ka biashara......yaani mkopo ili asichezee....uliyowafanyia yanatosha......wala usimsogelee.....ila usimwache aelendee kuteseka....inatosha...
 
Back
Top Bottom