Kila nikiifikiria hii kodi nashindwa kuwaelewa TRA, naona kama naibiwa

live on

JF-Expert Member
Dec 30, 2018
790
1,264
Nimefungua biashara mwezi wa tisa nikaona ni bora niende TRA ili nifanye biashara kwa kufuata sheria za nchi na nilipe kodi.

Kutokana na biashara yangu nikakadiriwa kodi laki moja na hamsini kwa mwaka; sikuwa na shida na hilo.

Lakini kitu kilichonishangaza baada ya kuprintiwa makaratasi yangu ya makadirio nikaambiwa hiyo laki na hamsini inatakiwa niilipe kabla ya tarehe 31 December

Nikamwambie yule dada biashara nimeanza mwezi huu wa tisa na hizi kodi naona hapa mmezigawanya katika robo 4 mimi inanihusu hi robo ya mwisho sasa kwa nini nilipie na hizo robo 3 kipindi ambacho biashara haikuwepo?

Yule dada akaniambia system ndio imesetiwa hivyo haijalishi biashara umeanza lini unatakiwa ulipe kodi yote ya mwaka mzima

Naomba TRA mnijibu maswali mzima?

1) Nani aliyeiseti hiyo system ya kuwaibia walipa kodi ni kwamba elimu yake ndogo au alifanya kusudi ili kutukomoa tunaotaka kulipa kodi kwa hiyari?

2) Kwa elimu yangu ndogo niliyo nayo kodi inalipwa baada ya kufanya biashara na kupata income sasa iweje mnadai kodi katika kipindi ambacho biashara haikuwepo?

3) mmenikadiria income yangu ni laki tano kwa mwaka ambayo kodi yake ndiyo hiyo laki na hamsini sasa iweje income nitakayo ipata kwa miezi 4 muichaji kodi ya mwaka mzima?

4) Haya mahesabu ya kodi mnayo yafanya ndivyo mlivyo fundishwa huko chuoni kwenu pale kijitonyama au mnatoa kichwani kwenu ili kuwa vunja moyo walipa kodi?
Screenshot_20191201-135057.jpeg
 
Kwakweli maofisa wa TRA sijui ni rushwa au sijui wamekaaje? Wakija kukukadilia kodi hukubambikia makadirio yasiyokuwa ya uhalisia hata kodi ya pango nayo wanaipigia kodi na ukilalamika wanasema eti system imesettiwa hivyo! Hayo nimekutana nayo saana hila huwa nakomaaa na kutaka kuongea na Meneja mpaka wanaachia! Komaa nao vyinginevyo itakula kwako!
 
Hutakiwi kukadiriwa kodi na TRA; sheria inakuhitaji wewe mwenyewe ndie upeleke makadirio yako. Ndio maana kukawekwa na penalty (adhabu) endapo itabainika kuwa makadirio yako yalikuwa ni madogo kuliko mapato makubwa (inapotokea tofauti kati ya mapato halisi na makisio ni tofauti angalau kwa 20% au zaidi).
Siku nyingine tafuta mhasibu akusaidie.
 
Watanzania huwa tunasoma lakini hatuelimiki
Maana kusoma na kuelimika ni vitu viwili tofauti
Hiyo laki 5 hapo ndio income yako ya mwaka ikishaingia hiyo ndio unalipa kodi sasa iweje income ya miezi 3 ichajiwe kodi ya mwaka hiyo pesa itatoka wapi
Wanataka uchote katika capital yako uwapelekee
Hapo bro umeibiwa na inasikitisha taasisi muhimu ya serikali inawaibia walipa kodi wake
 
Kwakweli maofisa wa TRA sijui ni rushwa au sijui wamekaaje? Wakija kukukadilia kodi hukubambikia makadirio yasiyokuwa ya uhalisia hata kodi ya pango nayo wanaipigia kodi na ukilalamika wanasema eti system imesettiwa hivyo! Hayo nimekutana nayo saana hila huwa nakomaaa na kutaka kuongea na Meneja mpaka wanaachia! Komaa nao vyinginevyo itakula kwako!
Nimegundua kwa nini watanzania wengi hawalipi kodi tatizo ni maofisa wa TRA eidha wana mapungufu kutokana na tatizo la elimu yetu tunayoipata darasani au wanafanya kusudi ili kutengeneza mazingira ya rushuwa
 
Hutakiwi kukadiriwa kodi na TRA; sheria inakuhitaji wewe mwenyewe ndie upeleke makadirio yako. Ndio maana kukawekwa na penalty (adhabu) endapo itabainika kuwa makadirio yako yalikuwa ni madogo kuliko mapato makubwa (inapotokea tofauti kati ya mapato halisi na makisio ni tofauti angalau kwa 20% au zaidi).
Siku nyingine tafuta mhasibu akusaidie.
Mkuu unajua kweli unachokiongea ?, Certified accountant akikufanyia mahesabu mara nyingi bei yake ni kwenye laki tatu sasa mtu kodi yake imekadiriwa na TRA kama ni laki na nusu alipe laki tatu ili akadiliwe laki na nusu ?

TRA wanakadilia accordingly na band za mauzo tofauti tofauti kwa mwaka yana gharama zake elekezi, cha kufanya ili usipunjwe inabidi uwe unatunza mahesabu na risiti ili wakuchaji accordingly bila hayo mahesabu wanakadiria accordingly na watakavyoona kulingana na duka, biashara na sehemu husika (kumbu ni mauzo na sio faida inayopigiwa kodi).., na Kodi inachajiwa kwa mwaka ingawa unaruhusiwa kulipa installments nne (kwahio ukianza kazi hata desemba 1 utachajiwa installment zote kuanzia mwanzo wa mwaka
 
Mkuu unajua kweli unachokiongea ?, Certified accountant akikufanyia mahesabu mara nyingi bei yake ni kwenye laki tatu sasa mtu kodi yake imekadiriwa na TRA kama ni laki na nusu alipe laki tatu ili akadiliwe laki na nusu ?

TRA wanakadilia accordingly na band za mauzo tofauti tofauti kwa mwaka yana gharama zake elekezi, cha kufanya ili usipunjwe inabidi uwe unatunza mahesabu na risiti ili wakuchaji accordingly bila hayo mahesabu wanakadiria accordingly na watakavyoona kulingana na duka, biashara na sehemu husika (kumbu ni mauzo na sio faida inayopigiwa kodi).., na Kodi inachajiwa kwa mwaka ingawa unaruhusiwa kulipa installments nne (kwahio ukianza kazi hata desemba 1 utachajiwa installment zote kuanzia mwanzo wa mwaka
Vp akianza January?
 
Vp akianza January?
watagawa ile kodi mara nne installment ya kwanza by march awe amelipa akianza july hapo installment zimebaki mbili tu, kodi ni ya mwaka unaweza kulipa yote at once ila umepewa installment kupunguza mzigo wa kulipa at once...
 
Hilo ni deni tayari linasoma katika tin namba yangu na natakiwa nililipe kabla ya tarehe 31 December
Nisipo lipa ikifika 2020 nitapigwa penati kwa kweli najuta kwa nini nilienda TRA
hahahahaha pole sana
 
Mkuu unajua kweli unachokiongea ?, Certified accountant akikufanyia mahesabu mara nyingi bei yake ni kwenye laki tatu sasa mtu kodi yake imekadiriwa na TRA kama ni laki na nusu alipe laki tatu ili akadiliwe laki na nusu ?

TRA wanakadilia accordingly na band za mauzo tofauti tofauti kwa mwaka yana gharama zake elekezi, cha kufanya ili usipunjwe inabidi uwe unatunza mahesabu na risiti ili wakuchaji accordingly bila hayo mahesabu wanakadiria accordingly na watakavyoona kulingana na duka, biashara na sehemu husika (kumbu ni mauzo na sio faida inayopigiwa kodi).., na Kodi inachajiwa kwa mwaka ingawa unaruhusiwa kulipa installments nne (kwahio ukianza kazi hata desemba 1 utachajiwa installment zote kuanzia mwanzo wa mwaka

Mtu gani huyo anaetoza laki 3 kwa ajili ya kumuelekeza mtu kufanya provisional income tax assessment? Halafu ni nani aliekuambia lazima huyo mtu awe ni CPA? Umepinga nilichoandika wakati mwenyewe unathibitisha kutokuwa na uhakika kati ya provisional income tax, final return, presumptive income tax na self-assessment.
 
Mtu gani huyo anaetoza laki 3 kwa ajili ya kumuelekeza mtu kufanya provisional assessment? Halafu ni nani aliekuambia lazima huyo mtu awe ni CPA?
hesabu za kawaida na risiti za mauzo na manunuzi unaweza kuwapelekea TRA na wenyewe watakwambia unatakiwa kulipa ngapi.., kwahio huyo muhasibu wako ambae angetoa ushauri angelipwa ngapi na angesave kiasi gani katika hio laki na nusu kwa mwaka ili jamaa alipe ngapi ?
 
hesabu za kawaida na risiti za mauzo na manunuzi unaweza kuwapelekea TRA na wenyewe watakwambia unatakiwa kulipa ngapi.., kwahio huyo muhasibu wako ambae angetoa ushauri angelipwa ngapi na angesave kiasi gani katika hio laki na nusu kwa mwaka ili jamaa alipe ngapi ?

Ndugu, provisional tax assessment ni jukumu la mfanyabiashara husika na si la TRA. Sheria haisemi kuwa TRA ndio wamkadirie mlipa kodi.

Kama hadi leo hujui hivyo basi naomba urudi kujifunza upya.
 
Duu laki tano kwa mwaka bora uchukue kitambulisho cha machinga ulipe 20 kwa mwaka
Maana hapo inaonyesha mtaji wako ni chini ya 4ml
 
Back
Top Bottom