Kila mwenye uchungu na nchi ya Tanzania afanye yafutayo mimi nieanza

Joblube

JF-Expert Member
Mar 4, 2011
369
151
Wana JF

Sambamba na maandamano napendekeza kila mwenye uchungu na nchii hii ya Tanzania afanyekazi ya kuwaelewesha watanzania mmojammoja ubaya wa CCM na madhara yake kwa Tanzania nakuhakisha kila wiki unamwelewesha at list mtu mmoja kuhusu ubaya na madhambi ya CCM na mbinu zao zote za Udini,ukabila pamoja nakuwasisitizia umuhimu wa kupiga kura. Mimi sio kiongozi lakini nieanzakufanya kazi hiyo nimeona mafanikio watu wanaelewa sasa japokuwa mwanzoni kunakuwa na kaubishi kidogo baadae wanaelewa. Nimefanya hivyo hasa ninaporudi kijijini na nimewaibua sasa watu watano wanoyoichukia CCM kisawasawa na watano hao mmoja ni ndugu yangu mjumbe wa CCM wa shina. Hii mnaionaje? Hakuna kulala mpaka kieleweke.
 
Mbona umechelewa sana. Mimi nilifanya hivyo tangu mwaka jana wakati tunajiandaa na uchaguzi. Ukiondoa watu fulani fulani (wakubwa na wanaofaidika na sisiem) wengine wote waliopo kwenye phone book yangu ya simu ya mkonoi ni wapenzi na wafurukutwa wa chadema. Hiyo sikutanii!! Hata tunapowasiliana huwa tunahabarishana kinachojili kuhusu masuala ya kisiasa hapa nchini na jukumu letu la kuwaelimisha wananchi ambao bado wapo kwenye usingizi wa kuiota sisiem. Kwa taarifa yako phone book yangu sasa ina majina 311. Kuna ndugu, marafiki mtaani kwangu, wafanyabiashara na wadau mbalimbali ninaofanya nao kazi. Ila nilichogundua wahindi hawapendi vyama vya upinzani. Of course sababu ipo wazi.
 
Ndugu yangu kuna wengine ni masikio ya kufa, hayasikii dawa hata umwelimishe vp.
Lakini nadhani ni mbinu nzuri lakini chalenji wakikuuliza ni chama gani mbadala na kwanini utatoa vigezo vipi?
 
thats good and more constructive kuliko kujadili sana with more energy as to why jk ordered zubery to be given that chairmanship ya kamati anayoongoza. unajua kwenye msafara wa mamba kenge hawakosekani. so ktk jahazi lenu cdm wasaliti kama zubery kabwe hawakosekani. dawa ni kuhamasisha watu wengi zaidi vijijini,mashuleni/vyuoni kuutambua ubazazi wa ccm na haja ya kuibua mabadiliko. ili hata kama cdm haitachukua power 2015 angalau kuwe na viti vingi sana bungeni ikibidi nusu kwa nusu. u see?
 
Back
Top Bottom