Kila mtu anaushambulia mshahara wa mwezi

mdesi

JF-Expert Member
Jul 18, 2013
1,347
2,081
Habari za humu ndani wanajamii,

Mimi ni mfanyakazi kwa muda wa miaka kadhaa, nimetafakari sana nimeona kuwa kuwa mfanyakazi na kusubiri mshahara, ni wazi kuwa huwezi kuwa tajiri hata siku moja.

Zaidi mshahara utakufanya tu ule, yaani uhakika wa watoto kupata mlo unakuwepo, haka kauhakika ndo kanapelekea watu kukimbilia kuajiriwa badala ya kujiajiri.

Ukweli ni kwamba, ukipata mshahara kila mtu anaupangia matumizi; TRA watatoa chao, Mifuko ya jamii itatoa chao, Bodi ya mikopo itatoa chao, vyama mbalimbali km CWT,TUICO, Bima za afya hasa kwa wafanyakazi wa serikali wanakata chao, kunatangazo huwa nalisikia sijui nao wanataka uchangie asilimia moja inaitwa Workers Fund sijui, vinaanzishwa tu ilimradi waukate mshahara.

Hapo hujakopa mkopo wakate rejesho lenye riba.

Hadi hapo huja involve personal expenses za Umeme, pango, chakula, mavazi ya watoto (wewe unaweza kuwa hata na kiatu kimoja tu).

Bado ndugu nao watataka support (kumbuka ukiwakatalia wataona unawabania maksudi).

Jamani jamani usione tunatembea tunastress nyingi mno...na hii hali ya uchumi ya sasa ndo balaa zaidi. Life is becoming harder and harder!
 
Tulivyowaambia msikipigie kura chama cha kijani mlituona wajinga. Sasa namba tunaisoma wote,mpaka miaka 10 iishe tutakua tumenyooka.
 
Jiajili kama huko hakufai.kama ni mwalim anzisha sehem ya tution mtaan mwako na uwape watoto vitu adimu utanyanyuka tuu.au kuwa mkulima.
 
Tatizo watu wamekariri maisha.
Wapo waliojiajiri ila wananidham kubwa sana ye pesa,na wamewekeza kwenye biashara nyingine na hali hii haiwaathiri kivile na maisha yanasonga.

Wapo walioajiriwa,wao starehe tuu,magari,madem,kupombeka,michango ya ajabu,Sasa lazima utafeli tu,maana age haikusubiri,na maisha hayapangwi kwa kiinua mgongo.
Kuajiriwa ni kuzuri sana kama ukijipanga na kujitambua na kuwa mzuri kwenye ku save,basi utatoboa tu
 
Duh kweli mkuu yani mshahara unashambuliwa na kila mtu kama mpira wa kona vile au kibaka wa Kariakoo.
 
Bado na michango ya harusi n.k, Mkuu hiyo ni real life ya maisha yetu sisi waajiriwa daah
Kwenye kuchangia changia harusi mimi nishatoka huko,tukiitisha michango kwa mayatima nj wajane hawachangi lakini raha na starehe za halusi kutwa kucha elfu hamsini hamsini,siku hzi mimi sichangi
 
Mshahara hautoshi aisee.Wakwe,madogo,shangazi,baba,mama wote macho mwisho wa mwezi.Viongozi wa dini nao wanasubiri sadaka yako.Bado michepuko yako na kazi zinakusubiri.
 
Hata biashara nazo zimekuwa mbaya Sana, sasa kama mfanyakazi hapati hela ya kumtosha na bado anakatwa makato chungu mzima unategemea hela kwenye biashara itoke wap???
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom