Kila la kheri Kamanda LEMA

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Nov 25, 2010
6,135
17,800
Hukumu ya rufaa yako ya kupinga kuvuliwa Ubunge ni kesho pale Mahakama ya Rufani ya Tanzania. Wewe ni Kamanda makini,mjenzi wa hoja,mpambanaji,mpigania chama,huna makundi,huongozi kakikundi cha wasaliti,hukeshi mitandaoni ila mikutanoni kwenye M4C pamoja na Makamanda wengine wa jeshi la ukombozi la CHADEMA.

Kesho utaandika historia.Utaionja ladha ya haki.Kwa lolote liwalo,tupo pamoja nawe. Kesho,utauvaa utu upya. Majaji watatu wa Mahakama ya Rufani watakuwa mboni ya haki yako kesho. Tunaombea waseme kama hivi " In the premises, we allow this appeal with costs...."

Ubarikiwe Kamanda Godbless Lema!

-YAMETIMIA-


Aliyekuwa Mbunge wa Arusha Godbless Lema amerudishiwa ubunge wake baada ya kushinda katika rufaa ya kesi yake ya kupinga matokeo iliyosomwa jijini Dar es Salaam leo.


Hukumu imeangalia haswa swala la "Locus Stand" ya kama "waliofungua kesi walikuwa na haki kisheria ya kufanya hivyo". Kadiri ya pingamizi ya mawakili wa Lema Ndg. Kimomogoro na Tundu Lissu, waliofungua shitaka dhidi ya Lema hawakuwa na "Locus Stand" ya kufanya hivyo. Kwa hiyo mengine yote yanakuwa "null and void". Hukumu haikuchukua hata nusu saa aibu iliyoje hii?.


Hoja moja tu tena ya kwanza kati ya hoja 18 zilizowasilishwa na upande wa rufaa kupinga hukumu hiyo mbele ya majaji Salum Massati, Bernard Luanda na kiongozi wao Nathalia Kimaro imeonesha ukomavu wa mawakili Kimomogoro na Tundu Lissu. Nachukua fursa hii kuwapongeza majaji hawa Salum Massati, Bernard Luanda na Nathalia Kimaro na mawakili Kimomogoro na Tundu Lissu kwa kuonesha ukomavu wao na kuthibitisha kuwa taaluma yao haina mashaka hata chembe. Mungu awajaalie wazidi kuwa na mafanikio makubwa na heri katika kazi zao, tunahitaji wazalendo kama hawa ili nchi iwe na ustawi na kudumisha haki.


Lema alivuliwa ubunge Aprili 5, 2012 katika hukumu iliyotolewa na Jaji Gabriel Rwakibalira, kutokana na kesi iliyofunguliwa na makada watatu wa CCM; Mussa Mkanga, Happy Kivuyo na Agnes Mollel, wakipinga ushindi wake katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010. Serikali inatakiwa kumchunguza kwa makini Jaji Gabriel Rwakibalira. Kwa maoni yangu nadhani huyu ni kada wa CCM na kama sivyo basi taaluma yake ni batili na butu sharti achunguzwe pia alisomea wapi kwani hawa ndiyo akina KIHIYO wanaogushi vyeti na kukalia nyadhifa muhimu huku wajuzi walio makini wakikosa nafasi kwa kuwa hawana ndugu wa kuwapachika katika nafasi hizo. Hivi karibuni kulitokea tuhuma zilizoenea kuwa baadhi ya majaji na mahakimu hawajui Kiingereza hali inayosababisha kushindwa kutoa hukumu sahihi kwa misisngi ya haki bali wanahukumu kwa utashi na matakwa yao hii ni hatari kwa taifa letu. Hakika kuna haja ya uteuzi wa Majaji kuchunguzwa upya hii ni aibu kwa Mheshimiwa Rais na washauri wake kwani huu ni mfano mmoja tu wa majaji uozo, Je, wako wangapi wa sampuli yake?


Swali la msingi la kujiuliza ni: Je, ni raia wema wangapi wameathiriwa na hukumu butu kama hizi hizi za Jaji Gabriel Rwakibalira na wakatumikia adhabu zisizo sahihi kwa kukosa utetezi wa mawakili makini?
 
wana wa arusha wanasubiri kwa hamu!
Vyovyote itakavyokuwa atapokelewa kama shujaa.tumeandaa ndege ya kumrudisha kamanda nyumbani!
 
Nimeanza kusherehekea ushindi wa lema toka leo.

Watakao ungana na mimi,wani inbox,nitalewa zaidi ya daimond
 
Mungu asaidie kwa kweli....inaweza kupunguza hii tension ya vijana vibaka na wenye tamaa wanaoharibu chama
 
From my heart, kwa nia safi ya Lema na Tanzania hii namtakia heri.

Najua atashinda!
 
Da, sijui itakuwaje hiyo kesho, Ila kwa vyoyote vile itakavyo kuwa, poa tu, Mungu awatangulie
 
Itakuwa pigo kwa Zitto coz alimtaget Kamanda lema.hawa wawili hazipandi kwa kuwa zitto hataki kupigwa bao asalie na umaarufu bila mbadala wake kuwepo.
 
Yes, Namuombea Lema ashinde na moyo wangu unaniashiria atashinda kwa jinsi kesi ilivyo kaa. Lema, endelea kujenga chama. Achama na Makundi ya wapumbavu. Sijakuona katika mabaraza ya wenye mizaha. Chama kitajengwa na wenye moyo siyo wenye njaa. Propaganda zote hizi ni upepo zitapita.....................
 
Naamini kwa uweza wa mungu utashinda hii kesi braza.ww ni jembe mkubwa,CDM tunakuhitaji WTZ wanakuhitaji na hata WANA-A TOWN wanakuhitaji.Hakika Lema akishinda hii kesi tutapunguza huu upuuzi unaofanywa na hawa was8****.GODBLESS BRAZA
 
kwa uwezo wake Allah mwingi wa rehema, naamini kamanda lemaa atashinda.
 
Our prayers with him, we are crossing our fingers for his victory tomorrow
 
Baada ya kesho tutajua, tuishi tanzania au Tutafute hifadhi msumbiji!
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom