Kila la heri Msanii - JamiiForums Community

Status
Not open for further replies.

Steve Dii

JF-Expert Member
Jun 25, 2007
6,402
1,254
Wana JF,
Hii ni kumwombea mema ndugu yetu Msanii kwenye siku yake ya ndoa.
Tukiwa kama jamii yenye kupenda muungano kwenye matukio yanayo tuzingira kama Wanadamu, kwenye raha na kwenye majonzi, napenda kumtakia kheri na faraja Msanii kwenye siku yake aliyo itaja hapa chini:
mkuu invisible, ingawa ninaweza kujiprintia ya kwangu lakini nitapenda kununua mbili, yangu moja na my wife (naoa desemba 23), medium moja na large moja tena ziwe polo shirts. Ninashauri pia kuwepo na aina tatu au nne za messages ktk tshrts halafu ukizipost hapa iwe rahisi members kuchagua. ujue ktk forums yako kuna wana ccm, chadema, tlp nk, pia na sisi wengie tusioamini ktk siasa. naona nimeongea sana (tatizo nilimeza kasuku utotoni).
Maandishi hayo yanapatikana kwenye thread Hii Hapa Ya JF Tshirt.

Nimatumaini yangu hapo juu kuwa Msanii ametaja hiyo siku akimaanisha 23-12-2007, na siyo 23-12-2008.

Ni hayo tu, Kila la Kheri Msanii.

SteveD.
 
Ujumbe mfupi kutoka kwa ndugu Msanii:

Mkuu
thats is what i wanted from you guys.
wengine wanadhani kusupport haruc ni kuchangia mifwedha ila naamini kuwa jamii ikikubariki basi hata ndoa hudumu. cha msingi kuunga mkono kwa namna yeyote...
nilikuwa outline muda sasa thus sijatembelea threads lakini sasa nakenda huko
(unaweza kuipost hii comment ktk thread)

Thanx sana Steve D

SteveD.
 
mbona hatukualikana wakati anatongoza?

mkuu brazameni,
nilisita kuwaalika wakati natongoza ndito yangu kwa kuwa mngekuwa mnanipigia makelele wakati naconcentrate.

ninasubiri pongezi kutoka kwa invisible, ole, worm, shy, mwanakijiji, mwafrika wa kike, bubu mtamka ovyo, zitto, mtu (alikuwepo ktk jopo la mshenga) pamoja na ninyi nyooote....

mniombee tu nisije nikakosea njia wakti wa honeymoon nikaingia mlango wa no entry....

Thanx Steve D
Mungu Akubariki kwa kuanzisha thread hii kwa ajili ya haruc yangu
 
duh, kuoa tena?? haya bwana hongera zako nyingi sikufikie ktk siku hiyo spesheli na ndoa yako idumu, iwe yenye neema nyingi, furaha na faraja, mpate watoto weeeengiiiiiiiiii ili nyumba yenu ipate kuwa na furaha zaidi.......nakusihi, uwache "mechi za ugenini" tena uzisahau kabisaaa!!!!.
 
Wana JF,
Hii ni kumwombea mema ndugu yetu Msanii kwenye siku yake ya ndoa.
Tukiwa kama jamii yenye kupenda muungano kwenye matukio yanayo tuzingira kama Wanadamu, kwenye raha na kwenye majonzi, napenda kumtakia kheri na faraja Msanii kwenye siku yake aliyo itaja hapa chini:

Maandishi hayo yanapatikana kwenye thread Hii Hapa Ya JF Tshirt.

Nimatumaini yangu hapo juu kuwa Msanii ametaja hiyo siku akimaanisha 23-12-2007, na siyo 23-12-2008.

Ni hayo tu, Kila la Kheri Msanii.

SteveD.

aleeleleeleeeleeleeeee alelleeeleeelleeeeeelleeeeeee


kimaso maso weee msani msimuone kimaso maso weee msanii

kimaso maso weee na wabaya wasimuone.



na zawadi nyengine kwako msanii


tun ao mti tunao twende nao pole pole

tukaupasue mbao mashina hadi vilele


kwa hgio msumeno wako usiwe butu ukapasue mbao vyema tu huko
 
msanii, mungu akupe baraka na maisha mema katika ndoa yako,akuepushe na wenye vijicho. na mwisho wa yote nakuusia kaka yangu uwe mwenye subira kwani maisha ya ndani ya ndoa yanahitaji uvumilivu sana.na pia mtunze sana shemegi yetu.kule kwetu kuna msemo unasemwa kwa bwana harusi "mwanamke hapigwi kofi,anapigwa kwa kununuliwa mvao wa kanga". mwisho wa yote mabrukk aruusanaa
 
mtu wa pwani huo wimbo wa wapi???

Msanii. Umefanya jambo jema kuamua kuoa. If you play your cards rite, Ndoa ni kama paradiso. Trust me.
Mungu akupe nguvu, akubariki wewe na mamaaa. Amen.
 
Msanii,

Hongera sana... Kila la kheri mkuu! Sisi wengine hatuoi wala kuolewa. Labda tuunganishwe na robots nyingine. :)

Kwa niaba ya JF Administration crew, nakupa pongezi na kukuomba uwe mvumilivu katika ndoa yako. Upendo utawale daima na furaha iifunike familia yenu.

Majaribu ni mtaji, tumia kila fursa ipatikanayo kuwaelimisha wanenu (mkijaaliwa) pamoja na mkeo na wewe usijisahau kujiendeleza kimasomo.

Epuka ugomvi usio na msingi baina yako na mkeo. Mke ni mkeo, mheshimu, elewa ni ubavu wako. Ndoa ni tamu wawili mkiamua kuifanya iwe hivyo. Inaweza kuwa chungu mkiamua pia.

Hakuna upendo unaokwisha, huchuja na hatimaye hujengwa na wahusika (wawili bila kuwaingiza majirani ama ndugu). Mapenzi ni hisia, hujengwa kwa wawili kufanyiana matendo ya upendo ambayo ndiyo huyajenga mapenzi ya dhati. Epuka kuwaingiza ndugu katika mahusiano yenu. Washirikishe mengine lakini si maamuzi ya nini umfanyie mkeo na nini usimfanyie. Huyo ni wewe na wewe ni yeye!

Penye nia pana njia, huyo ni malaika wako, ubavu wako, damu yako, chaguo lako (wengine si mali kitu kwa sasa). Mfanye aone faida ya kuwa na wewe.

Kila la kheri katika ndoa yako na Mwenyezi Mungu awajaalie mpate watoto wenye afya njema na busara katika jamii.

Invisible
 
Msanii,

Hongera sana... Kila la kheri mkuu! Sisi wengine hatuoi wala kuolewa. Labda tuunganishwe na robots nyingine. :)

Kwa niaba ya JF Administration crew, nakupa pongezi na kukuomba uwe mvumilivu katika ndoa yako. Upendo utawale daima na furaha iifunike familia yenu.

Majaribu ni mtaji, tumia kila fursa ipatikanayo kuwaelimisha wanenu (mkijaaliwa) pamoja na mkeo na wewe usijisahau kujiendeleza kimasomo.

Epuka ugomvi usio na msingi baina yako na mkeo. Mke ni mkeo, mheshimu, elewa ni ubavu wako. Ndoa ni tamu wawili mkiamua kuifanya iwe hivyo. Inaweza kuwa chungu mkiamua pia.

Hakuna upendo unaokwisha, huchuja na hatimaye hujengwa na wahusika (wawili bila kuwaingiza majirani ama ndugu). Mapenzi ni hisia, hujengwa kwa wawili kufanyiana matendo ya upendo ambayo ndiyo huyajenga mapenzi ya dhati. Epuka kuwaingiza ndugu katika mahusiano yenu. Washirikishe mengine lakini si maamuzi ya nini umfanyie mkeo na nini usimfanyie. Huyo ni wewe na wewe ni yeye!

Penye nia pana njia, huyo ni malaika wako, ubavu wako, damu yako, chaguo lako (wengine si mali kitu kwa sasa). Mfanye aone faida ya kuwa na wewe.

Kila la kheri katika ndoa yako na Mwenyezi Mungu awajaalie mpate watoto wenye afya njema na busara katika jamii.

Invisible

Duuuh, wewe ROBOT haya yote umejifunzia wapi... kwenye production line huko Japan nini?! Au wame upgrade chip yako ya mahusiano na ku-upload program ya mapenzi?... haya yetu macho tu iROBOT... usije ukatufanyizia bure kwa kuingiwa na jazba na kuanza kuji-program kuteketeza wanadamu... lol

SteveD.
 
Kama unapata maziwa rejareja ya nini kununua ng'ombe mzima na kupata taabu za kuasafisha banda, kutafuta majani, madawa nk.

Mambo ya kujitafutia uzee hayo....
 
Mimi naomba Anuani yako nikutumie CD ya muziki ya mizuri ya kiswahili

zaidi ya yote nakutakia mafanikio na maisha mema ya ndoa wengine tuko njiani .

lakini siwezi kukupongeza kwa asilimia moja kwa sababu ndoa haijafungwa huyo mwanadada anaweza kugauza sura wakati wa kula kiapo

sijui nanihii atanikubali
 
mkuu brazameni,
nilisita kuwaalika wakati natongoza ndito yangu kwa kuwa mngekuwa mnanipigia makelele wakati naconcentrate.

ninasubiri pongezi kutoka kwa invisible, ole, worm, shy, mwanakijiji, mwafrika wa kike, bubu mtamka ovyo, zitto, mtu (alikuwepo ktk jopo la mshenga) pamoja na ninyi nyooote....

mniombee tu nisije nikakosea njia wakti wa honeymoon nikaingia mlango wa no entry....

Thanx Steve D
Mungu Akubariki kwa kuanzisha thread hii kwa ajili ya haruc yangu

atiiii??!!!!sijakuelewa vizuri umemaanisha nini lango wa no entry??laaaahaulaaa
 
si nikasahau jambo la msingi nililotaka kusema...nakutakia maisha mema ya Ndoa ndugu yangu na ujue kuanzia siku hiyo sio wewe tena hata katika yote ufanyayo juwa watakiwa ujali na mawazo na uwepo wa mwenzio!!
 
Kama unapata maziwa rejareja ya nini kununua ng'ombe mzima na kupata taabu za kuasafisha banda, kutafuta majani, madawa nk.

Mambo ya kujitafutia uzee hayo....

Nakataa kata kata
pole kwa mawazo hayo ilaa
UKITAKA KUJUA UHONDO WA NGOMA INGIA UCHEZE.
 
Status
Not open for further replies.
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom