Kimbunga
Platinum Member
- Oct 4, 2007
- 14,941
- 9,947
Wana JF hivi karibuni kamati za Bunge zilikuwa zikipitia hesabu za mashirika na idara mbalimbali za serikali ila jambo la kushangaza ni kwamba kila Kamati ilipokuwa ikienda kesho yake nilishuhudia kwenye magazeti vichwa vya habari kama, "Kamati ya Bunge Yanusa Ufisadi TCRA." Kingine "Kamati ya Bunge Yanusa Ufisadi Mamlaka ya Korosho" bado kingine "Kamati ya Bunge Yanusa Ufisadi Halmashauri". "Kamati ya Bunge Yakataa Tena Hesabu za Bodi ya Utalii". n.k, n.k, n.k!!
Nimebaki najiuliza hivi fisadi yuko wapi sasa? Ina maana Tanzania yote imejaa mafisadi? Ina maana wote wanaofanya ufisadi huo ni wana CCM? Mbona CCM inatuambia kuna mafisadi watatu? Kama nchi inanuka ufisadi kiasi hiki nini kinatakiwa kufanyika ili hata serikali yenye viongozi ambao si mafisadi ikiingia madarakani iondoe ufisadi uliotamalaki kila mahala? Mwisho kabisa ukiniondoa mimi, nani si fisadi?
Nimebaki najiuliza hivi fisadi yuko wapi sasa? Ina maana Tanzania yote imejaa mafisadi? Ina maana wote wanaofanya ufisadi huo ni wana CCM? Mbona CCM inatuambia kuna mafisadi watatu? Kama nchi inanuka ufisadi kiasi hiki nini kinatakiwa kufanyika ili hata serikali yenye viongozi ambao si mafisadi ikiingia madarakani iondoe ufisadi uliotamalaki kila mahala? Mwisho kabisa ukiniondoa mimi, nani si fisadi?