Kila kitu unachopaswa kujua kuhusu Cryptocurrency na Bitcoin na kwanini siyo uwekezaji mzuri kwako kwa sasa

Kuna Mods misukule ya time warp watafuta huu uzi si muda
aaah au Mama kaongelea wataaamka....
 
Kuna interview Moja kali sana tulifanya na Fredrick Bundala "Sky Walker" wa SNS...
Ni vema mkapata muda wa kuisikiliza then turudi hapa tutatemeana madini Mwanzo Mwisho!!! Nadrop link hapo chini

Screenshot_20210619-021259.jpg
 
Habari kubwa katika kipindi hichi kwa upande wa fedha na uwekezaji ni cryptocurrency au kama inavyofahamika kwa Kiswahili fedha za kidijitali. Aina hii ya fedha imewavutia wengi siyo kwa sababu ya matumizi yake, bali kwa jinsi thamani yake inavyokua kwa kasi na hivyo wengi kuona ni sehemu rahisi ya kupata fedha nyingi bila ya kufanya kazi.

Lakini wengi ninaowaona wanakimbizana na fedha hizi za kidijitali, hawana uelewa wa kutosha. Wengi wanadanganywa na kushawishiwa kuingia kwenye kitu ambacho hawakielewi kwa matumaini kwamba watapata fedha nyingi. Ni kweli wapo watakaopata fedha nyingi, na pia wapo ambao watapoteza fedha nyingi kwenye aina hii ya uwekezaji.

Hivyo leo nimechukua muda, kukuandikia wewe rafiki yangu makala hii yenye kila unachopaswa kujua kuhusu cryptocurrency kwa ujumla, na tukiangalia kwa kina zaidi bitcoin ambayo ndiyo currency ya kwanza na yenye thamani kubwa zaidi. Nitachambua hili kwa lugha rahisi ambayo hata kama huna elimu kubwa utaweza kuelewa na kuweza kuchukua hatua.

Lakini kabla sijaingia kwenye kueleza kwa kina fedha hizi za kidijitali, naomba nikushirikishe hadithi tatu muhimu ambazo zitatupa mwanga wa nini kinaendelea.

Moja; TULIP MANIA 1630 – 1637.

Mnamo karne ya 17, kwenye Jamhuri ya Udachi (Dutch Republic), kulitokea hali ambayo haikuwa ya kawaida. Maua yanayojulikana kwa jina la Tulip yalianza kupata umaarufu ghafla. Maua haya yalikuwa na mwonekano mzuri na pia yalikuwa yana changamoto kwenye ulimwaji wake. Hivyo hili lilifanya watu wayathamini sana, na hili likapelekea bei yake kuwa juu. Kadiri bei ilivyokuwa inapanda, ndivyo wengi zaidi waliyataka maua hayo na bei kuzidi kupanda zaidi.

Ilifika wakati, thamani ya ua moja ikawa zaidi ya mara kumi ya kipato cha mwaka cha mfanyakazi wa kawaida kwenye nchi hiyo. Kutokana na kupanda huku thamani kwa maua aina ya Tulip, jamii nzima ilianza kuhamia kwenye maua hayo, ikafika wakati maua haya yakawa yanatumiwa kama fedha, badala ya dhahabu ambayo imekuwa inatumika wakati wote.

Ilifika hatua, watu wakawa wanalipia maua hayo hata kabla hayajakomaa, yaani yakiwa bado shambani. Kufikia Februari mwaka 1637 maua haya ya Tulip yalifikia bei ya juu kabisa na ghafla bei ikaanza kuporomoka. Bei iliporomoka kwa kasi kiasi cha kuyumbisha uchumi wa nchi nzima na watu wengi kupata hasara kubwa. Hii inasemekana kuwa anguko la kwanza la kiuchumi duniani.

tulip-mania-dot-com-bitcoin.png


Mbili; DOTCOM MANIA 1997 – 2001.

Mwishoni mwa miaka ya 1980 jambo kubwa lilitokea duniani ambalo ni matumizi ya mtandao wa intaneti kwa watu wa kawaida. Mwanzoni mwa miaka ya 1990 matumizi ya mtandao wa intaneti yalishika kasi na biashara nyingi zinazohusisha intaneti zilianzishwa.

Kwa kuwa intaneti ilikuwa kitu kipya, na ambacho kilionesha kuwa na nguvu kubwa, watu wengi walivutiwa na biashara zinazohusisha mtandao wa intaneti. Hivyo watu wengi walikimbilia kuanzisha biashara zinazohusisha intaneti. Inasemekana kwamba mwishoni mwa miaka ya 1990 na kuelekea mwaka 2000 watu wengi walikuwa wakiahidi kuanzisha kampuni zitakazokuwa kubwa na watu wakashawishika kuwekeza fedha zao bila hata ya kuwepo kwa ushahidi au uhakika wowote kwamba biashara inayokwenda kuanzishwa itakuwa imara kweli.

Watu waliingiwa na tamaa ya kufaidika haraka kupitia intaneti, kitu ambacho kilipelekea makampuni mengi kuwa na thamani kubwa kuliko uhalisia. Kilichotokea ni uchumi mzima unaohusisha mtandao wa intaneti kuanguka, makampuni mengi kutangaza hasara na watu wengi kupoteza fedha zao.

Tatu; CRYPTO MANIA 2009 - .......

Mwaka 2009, Satoshi Nakamoto, haijulikani kama ni mtu, kikundi cha watu au taasisi, alikuja na wazo la tofauti kwenye mfumo wa fedha. Kama ambavyo wote tunajua, mzunguko wa fedha umekuwa unadhibitiwa na benki kuu ya nchi husika. Kwa mfano mzunguko wa shilingi ya Tanzania, unadhibitiwa na Benki Kuu ya Tanzania. Hivyo miamala yoyote ya kifedha lazima iweze kufuatiliwa na benki kuu. Satoshi ali/walipendekeza mfumo wa kuondoa udhibiti huo. Badala ya mzunguko wa fedha kudhibitiwa na mtu mwingine, udhibitiwe na watu wawili tu, anayelipa na anayelipwa.

Mfumo huu ulionekana ni mkombozi kwa matatizo mengi ya kifedha, ambayo yapo wazi, mfano nchi kuchapa fedha na hivyo mfumuko wa bei kuwa mkubwa, gharama za kufanya miamala na hata usalama kuwa mdogo, kama ambavyo tumekuwa tunasikia fedha feki kuwepo kwenye mzunguko. Mfumo wa Satoshi ulionekana ni bora kabisa, lakini wengi wakawa na wasiwasi kwamba ni mgumu kueleweka na kutumika.

Hivyo mwaka 2009 Satoshi ali/walikuja na mfumo wa fedha ya kidijitali uliokwenda kwa jina la Bitcoin. Hii ilikuwa sarafu ya kwanza kabisa ya kidijitali, ambayo ilikuwa na lengo la kurudisha udhibiti na usalama wa fedha kwa watumiaji.

Kwa kipindi cha mwaka 2009 thamani ya bitcoin moja ilikuwa dola 0.0001 ambayo kwa kipindi hicho, dola moja ilikuwa tsh 1330, hivyo bitcoin moja ilikuwa sawa na tsh 1 na senti 33. Mpaka kufika mwaka 2010, bado thamani ya bitcoin moja ilikuwa chini ya dola moja. Kuanzia mwaka 2011 bei ya bitcoin imekuwa inaongezeka kidogo kidogo, kutoka dola mia na kuendelea. Mpaka kufika januari 2017, bei ya bitcoin moja ilikuwa chini ya dola elfu moja. Lakini baada ya hapo bei ilianza kuongezeka kwa kasi, kufika oktoba 2017, bei ya bitcoin moja ilikuwa dola elfu 5.

bitcoin-june-2009.png


Tarehe 17 mwezi disemba 2017 ndiyo ilikuwa siku ambayo thamani ya bitcoin ilikuwa juu sana, ambapo bitcoin moja ilikuwa sawa na dola elfu 19. Yaani sawa na zaidi ya shilingi milioni 40. Hebu fikiria hapo, kwamba kama mwaka 2009, ungepata nafasi ya kununua bitcoin moja kwa shilingi moja, mwaka 2017 ungekuwa na zaidi ya milioni 40!

Kwa nini hadithi hizi tatu?

Hadithi hizi tatu zinatufundisha kitu kimoja muhimu sana kwenye fedha na uwekezaji, kwamba mara nyingi tamaa ya watu ikishaingia kwenye kitu, thamani inapanda kuliko uhalisia, kitu ambacho kinatengeneza anguko baadaye. Ilitokea kwa maua ya Tulip, ilitokea kwa biashara za Dotcom na itatokea kwenye cryptocurrency kama ambavyo nitakueleza hapo chini.

Ili tuweze kuweza kuelewana vizuri, na kwa kuwa yapo mengi ya kujifunza kuhusu fedha hizi za kidijitali, tutakwenda kwa mfumo wa maswali na majibu.

Swali; bitcoin ni nini?

Jibu; bitcoin ni mfumo wa malipo wa kielektroniki ambao ni wa moja kwa moja kati ya mlipwaji na mlipaji bila ya kuhusisha upande wa tatu kama benki serikali na taasisi nyingine za kifedha.

Swali; mfumo huu unafanyaje kazi?

Jibu; kunakuwa na sarafu za kidijitali, ambazo zina idadi yanye ukomo. Sarafu hizi ndiyo zinazotumika kama thamani ya malipo. mfumo mzima ni wa kielektroniki na hivyo hakuna sarafu yoyote ya kawaida inayohusika. Badala yake mfumo wa kompyuta unaotoa na kudhibiti sarafu hizi ndiyo unaotumika.

Swali; zipi faida na ubora wa mfumo huu mpya wa malipo?

Mfumo wa kawaida wa fedha una changamoto nyingi ambazo tumekuwa tunaziona kila wakati. Sehemu kubwa ya changamoto hizo inaweza kutatiliwa na mfumo huu wa fedha za kidijitali.

Changamoto ya mfumuko wa bei ambayo imekuwa inasababishwa na serikali kuchapa fedha na hivyo kushusha thamani, unadhibitiwa na uwepo wa kiwango kamili cha sarafu za kidijitali. Kwa mfano kwa Bitcoin kuna sarafu 21,000,000 pekee, zikiisha hizo hakuna nyingine zinazoweza kuzalishwa na hivyo mfumuko wa bei hauwezi kutokea.

Changamoto ya usiri imetatuliwa na mfumo huu mpya kwa kufanya muamala kuwa baina ya watu wawili pekee. Katika mfumo wa kawaida, utamlipa mtu kwa njia ya benki, fedha taslimu au njia za mitandao, ambazo zote hazina usiri.

Changamoto ya gharama za miamala imeondolewa sana na mfumo huu, kwa mfumo wa kawaida, kila unapohamisha fedha eneo moja kwenda eneo jingine unakatwa malipo, na hii ni kwa sababu taasisi nyingi zinahusika. Lakini kwenye mfumo huu, hakuna uhusishaji wa taasisi nyingi, hivyo makato hakuna.

Changamoto ya usalama, tunajua namna ambavyo kuwa na kiasi kikubwa cha fedha ni hatari, pia hata benki siyo salama sana kuweka fedha. Kwa mfumo huu wa fedha wa kidijitali, usalama ni mkubwa, program ya kompyuta inayotumika kudhibiti mfumo huu ni dhabiti sana na haiwezi kuchezewa.

Changamoto ya fedha feki imedhibitiwa na mfumo huu. Kwa kila aina ya sarafu, kwenye mzunguko huwa kunakuwa na fedha feki nyingi. Lakini kwa mfumo huu wa fedha za kidijitali, hakuna namna ya kutengeneza sarafu feki.

Swali; je kuna sarafu za aina ngapi kwenye fedha hizi za kidijitali?

Jibu; Watu wengi wanajua zile sarafu kubwa za kidijitali kama Bitcoin, Ethereum, Ripple, Bitcoin Cash, Cardano, na Litecoin. Lakini mpaka kufika mwezi february 2018 kulikuwa na sarafu za kidijitali zaidi ya 1400, na orodha inaendelea kukua kila siku, kwa sababu yeyote anaweza kuja na sarafu mpya.

Swali; je cryptocurrency utakuwa mfumo kamili wa malipo?

Jibu ni ndiyo, lakini siyo sasa ni kwa baadaye. Lakini pia kama utakuwa mfumo mkuu wa malipo, basi kila serikali itatengeneza mfumo wake wa malipo kwa njia hiyo ya kidijitali. Hakuna serikali inayoweza kukubali kupoteza udhibiti wa fedha, kitu pekee kinafanya serikali ziwepo, tangu enzi za utawala wa roma, ni udhibiti wa fedha, na enzi hizo, dhahabu.

Swali; je Bitcoin itakuja kuwa sarafu ya dunia na kutumiwa na kila mtu?

Jibu ni hapana, Bitcoin imekosa sifa zote za sarafu ya kutumiwa na uma, kwa sababu thamani yake haijatulia, inapanda na kushuka kwa kasi mno. Pia watu wengi wameshaihodhi na hivyo uwezekano wa kutumiwa na kila mtu ni mdogo.

Swali; je soko zima la fedha hizi za kidijitali litaanguka?

Hapa ndipo muhimu sana unapaswa kuelewa. Kwa hizi sarafu nyingi, ukiangalia zilianza na thamani kidogo sana. mfano bitcoin kwa mwaka 2009 na 2010 thamani yake ilikuwa chini ya dola moja. Lakini baada ya watu kuisikia ilianza kupanda thamani na kufikia disemba 2017 ilifikia thamani ya juu kabisa ya sarafu moja kuwa dola elfu 19. Lakini baada ya hapo imekuwa unashuka na kupanda.

Ukuaji huu wa thamani ya sarafu hizi za kidijitali siyo wa kawaida, na unachochewa na tamaa ya watu kuona ni njia ya haraka ya kutengeneza utajiri. Tamaa hii itapelekea sarafu nyingi kuanguka na baada ya hapo zitasimama sarafu imara na ambazo thamani yake inaendana na hali ya uchumi.

Kama ambavyo TULIP ilianguka, na kama DOTCOM ilivyoanguka, CRYPTOCURRENCY pia itaanguka, lakini baada ya hapo zitaibuka sarafu ambazo ni imara na zenye thamani inayoendana na uchumi. Anguko la CRYPTOCURRENCY litawaumiza wengi sana na kuwanufaisha wachache.

[caption id="attachment_4407" align="alignnone" width="800"]
coindesk-bpi-chart1.jpeg
Kwa kipindi cha mwaka mmoja kati ya machi 2017 mpaka mashi 2018, thamani ya bitcoin imeongezeka kutoka chini ya dola elfu moja mpaka dila elfu kumi na tisa. Ni ongezeko ambalo haliwezi kuelezewa vyovyote vile kiuchumi.[/caption]

Swali; je kuna matumizi mengine ya teknolojia hii ukiacha malipo?


Teknolojia iliyopo nyuma ya sarafu hizi za kidijitali, ambayo ni BLOCKCHAIN ina matumizi mengine mengi na makubwa. Mfano inatumika kwenye kuandaa mikataba ya kidijitali, inatumika kwenye kutunza kumbukumbu za siri na kwenye usimamizi na udhibiti wa uwekezaji. Teknolojia ya blockchain inaweza kutumika kwenye kila eneo linalohitaji ufuatiliaji na udhibiti wa hali ya juu, kama kwenye afya, benki, makusanyo ya mapato na kadhalika.

Kwa nini BITCOIN siyo uwekezaji sahihi kwako kufanya kwa sasa?

Mpaka kufika hapa nina imani umeanza kupata picha ya hichi kitu kinachoitwa CRYPTOCURRENCY ni nini, kwamba ni mfumo wa malipo wa kidijitali ambao ni wa moja kwa moja na unaepuka changamoto nyingi za mfumo wa kawaida wa fedha. Pia utakuwa umejua BITCOIN ni moja kati ya sarafu zaidi ya elfu moja ambazo zinatumia mfumo huu. Kwa kipindi hichi BITCOIN ndiyo sarafu yenye thamani kubwa.

Sasa nimalize kwa kukuambia kwa nini BITCOIN siyo uwekezaji sahihi kwako kufanya kwa sasa.

Watu wengi wanahamasishwa sana kuwekeza kwa kununua bitcoin hasa pale ambapo thamani yake ilikuwa inapanda kwa kasi ya ajabu. Lakini wengi ambao wamekuwa wanatamani kuwekeza kwenye mfumo huu, hawapo tayari. Hapa nitataja makundi matano na kama upo kwenye moja ya makundi hayo usiwekeze kwenye cryptocurrency na bitcoin, badala yake endelea na uwekezaji wa kawaida ambao ni salama kidogo ukilinganisha na huu kwa sasa.

1. Kama ndiyo umeielewa cryptocurrency na bitcoin leo, jipe muda wa kujifunza.
Nilichokushirikisha hapa kuhusu cryptocurrency na bitcoin ni kama tone tu la bahari ambayo unapaswa kuelewa kuhusu mfumo huu wa fedha na malipo. Hivyo kama umekuwa unasikia sikia kuhusu hizo bitcoin lakini leo ndiyo umeanza kupata picha basi huu siyo uwekezaji mzuri kwako kwa sasa.

Pendekezo langu ni chukua muda kusoma na kuelewa kwa kina, soma vitabu na siyo makala au kuwasikiliza watu wanaokuambia kwa nini ujiunge au usijiunge. Isome teknolojia hii uielewe kwa undani, kisha soma fedha, uchumi na uwekezaji ili kujua namna vitu hivi vinakwenda. Hapo utakuwa umepata mwanga wa kukusaidia kufanya maamuzi sahihi.

2. Kama huwezi kumudu kupoteza fedha.

Pamoja na hatari ya cryptocurrency na bitcoin kwa sasa, bado ni kitu kizuri kujaribu, ila tu, ni rudie, ila tu unamudu kupoteza fedha. Yaani kama una fedha za ziada, ambazo hata ukizipoteza maisha yako hayatayumba, basi unaweza kujaribu aina hii ya uwekezaji.

Lakini kama bado hujafikia hatua ya kuwa na fedha za ziada, kama upo kwenye madeni na unafikiria aina hii ya uwekezaji itakutoa kimaisha, kaa mbali nayo, ni hatari kwako.

Na kama unawaza kwenda kukopa fedha uwekeze kwenye mfumo huu, huna tofauti na mtu anayevuta sigara huku anaweka petroli kwenye gari, siyo hatari kwako tu, bali na kwa wengine pia.

3. Kama umri wako wa kuzalisha fedha umesogea.

Katika kila anguko la uchumi linalotokea duniani, watu wanaoathirika zaidi ni wale ambao umri wao umeenda na hawawezi tena kujitumikisha. Yaani kama umri umeenda, unakaribia kustaafu au umeshastaafu na una fedha zako za mafao, usiziweke kwenye mfumo huu wa fedha za kidijitali. Hata kama unaona kuna nafasi kubwa ya kuongeza kipato hicho, hatari unayochukua ni kubwa sana kwako, na nguvu za kupambana zimeshapungua.

4. Kama elimu pekee uliyonayo ni ya kuambiwa.

Wapo watu ambao wanatoa elimu hizi za cryptocurrency na bitcoin, ila elimu wanayoitoa ni ya kuwaambia watu kwa nini wajiunge na kuwashawishi kwamba ni uwekezaji ambao hawapaswi kuukosa. Kama hii ndiyo elimu ambayo umekuwa unaipata pekee, hujawa tayari kuwekeza. Unahitaji kujifunza kwa kina, faida na hasara, usalama na hatari kwenye uwekezaji huu kabla hujachukua hatua.

5. Kama sababu pekee ya kuwekeza ni kwa sababu wengine wamekuambia ‘wanapiga hela’

Ipo sababu nyingine ambayo naona watu wanaitumia vibaya kuwekeza kwenye mfumo huu mpya wa fedha na malipo. Na sababu hiyo ni kwamba ona wengine wanapata hela. Na watu wanaonesha kweli wanapata fedha, na ni kweli siyo utani. Kama nilivyoeleza, hata pale sarafu hizi zitakapoanguka, wapo watakaonufaika na wapo watakaopoteza.

Sasa unapofikiria kupata tu, jua kwamba kuna kukosa pia. Hivyo ukiangalia wanaonufaika, usiache kuangalia uwezekano wa kukosa.

Rafiki, nimejaribu kukuelezea kwa lugha rahisi na inayoeleweka kuhusu mfumo huu mpya wa fedha za kidijitali, kama nilivyoeleza hii ni sehemu ndogo sana ya elimu kubwa unayopaswa kuwa nayo kama unataka kuwekeza kwenye mfumo huu. Wito wangu kwako ni uendelee kujifunza zaidi na kama una kiasi cha fedha unachoweza kupoteza, unaweza kujaribu kwenye aina hii ya uwekezaji, ukijua kwamba nafasi ya kupoteza ni kubwa kama ilivyo ya kunufaika.

Kila la Kheri Rafiki Yangu.

Rafiki na Kocha wako,

Dr. Makirita Amani,

www.kisimachamaarifa.co.tz/kocha
Asante nakushukuru kwa moyo wako wakutaka wengine wajifunze
 
Ahsante sana kiongozi..., Natumaini kàtika yale mengi uliyonayo kuhusu cryptocurrency umejaribu kushare nasí yale machaçhe ambayó ni ya muhimu zaidii

Ikikupendeza tumaomba uendelee kutupa elimu na mwongozo juu ya uwekezaji huu wa kidigitali ili tuweze kunufaika nao na kuenenda na kasi ya mabadiliko na ukuaji wa uchumi duniani kiujumla.

Naomba kuwasilishaà✍️✍️
 
I have been wondering there has been coinbase and local bitcoin all tradding bitcoins and with extra cryptos in coinbase, Coinbase have their app but I have never heard of local bitcoin app. Is there an app for this site or not.
Provide the link below if you know they have an app or lets discuss on why they don't have an app so far!
3
 
Kuhusu Forex na Bitcoin nk

Nitajaribu kuelezea kidogo kwa kadri ya ufahamu wangu na uzoefu nilionao juu ya hizi biashara.

Kinyume na watu wengi wadhaniavyo ama walivyoaminishwa Forex au Bitcoin sio utapeli na wala sio biashara ya Pyramid Scheme kama DECI,QNet na zinginezo.

Forex:

Kama jina lilivyo hii ni biashara halali ya kuuza na kununua fedha(Foreign Currency Exchange) ili kupata faida ndogo kutokana na utofauti wa thamani ya fedha hizo.

Biashara hii tunaweza kuifananisha na Bureau de Change iliyokuwa simplified na kuweza kufanyika kidijitali kwa kutumia Computer ama simu ya mkononi.

Mfano mwingine mzuri ni soko la hisa ambalo pia mfumo ni ule ule wa kuuza au kununua hisa za makampuni mbalimbali ambazo pia hupanda au kushuka kutegemeana na hali ya kibiashara ya kampuni husika.

Ikumbukwe pia hizi ni biashara kama zilivyo biashara zingine hivyo kuna pande mbili za matokeo,kupata faida ama kupata hasara japo lengo na jitihada huelekezwa kupata faida zaidi na ku-minimize hasara.

Forex hulenga kuwahi kununua fedha inayoonekana kupanda thamani mapema kwa bei ndogo na pale inapokuwa imepanda thamani kuiuza kwa bei ya juu na hivyo kutengeneza faida kwa utofauti uliotokana na bei ndogo ya kuinunua na bei kubwa ya kuiuza.

Thamani ya fedha hubadilika kupanda au kushuka kutokana na mambo mengi kama kukua au kuanguka uchumi wa nchi kutokana na uzalishaji bidhaa,uuzaji au ununuaji nje(Import/Export)Vita,Migogoro,Majanga kama hili la Corona nk.

Kujua taarifa hizi mshiriki wa biashara hizi ni lazima awe mfuatiliaji wa habari za kiuchumi kwa karibu kwani ndio hasa dira ya biashara yake kujua ni wakati upi sahihi kuuza fedha aliyohodhi kwa kuwa ipo kwenye demand kubwa ama kununua fedha inayopanda ili aiuze baadae.

Formula ni ile ile ya kiuchumi kuwa demand ikizidi bei huongezeka na soko likifurika ama demand kupungua na bei hushuka.

Mfano mzuri ni wa wafanyabiashara wa mazao huyanunua wakati wa mavuno wakati yako mengi na bei ni ndogo na kuja kuyauza baadae wakati kuna uhaba na bei ikiwa imepanda maradufu.

Tatizo la Forex Tanzania ni kuvamiwa yaani watu wametaka kuifanya kama ni get rich quick scheme kwa haraka bila jasho ili mradi wana mitaji.

Forex yahitaji kuisoma kiundani,kufanyia mazoezi makali (demo accounts) na kujifunza saikolojia ya uvumilivu na kutosheka na faida yaani kuwa na trading plan ya kufuata na sio kuyumba kwa kuendeshwa na tamaa.

Wengi wamepata shida kwa kutaka kufanyiwa trading na wengine waliowaaminisha ni wataalamu kumbe nao labda wana ufahamu wa kijuu juu tu na labda walishaanguka kimitaji kwa kutofuata principles sasa wanatafuta fursa za kupata mitaji kupitia kwa watu wengine ambao nao hawafanyi utafiti wa kina kabla ya kuamua kushirikiana na hao wataalamu.

Kiukweli inashauriwa kama mtu hajajifunza hii biashara asiifanye kwani sio Upatu wa kuweka fedha na kusubiri mzunguko ufike alipwe.

Forex yataka elimu,yataka ufuatiliaji na yataka dedication ya full time na sio part time.

Ikibidi kutumia mtu basi yapaswa kuwa na hakika ya uwezo wake na njia rahisi ni kumuomba akupe investor password ya akaunti anayoendesha(iwe ya mfano/demo ama iwe ya ukweli/real) na uifuatilie kwa minimum period ya wiki tatu na hasa vizuri kwa mwezi kuona uhodari wa mtaalamu katika biashara, consistency yake na asilimia ya kufanikiwa faida against asilimia ya losses kabla ya kuamua kushirikiana.

Ni muhimu pia kuwa na mikataba ya kisheria baina ya mtoa fedha na mtaalamu.Hii humpa adabu ya kutrade mtaji wa mtu kwa umakini-responsibly!

Hii ipo duniani kote kuwapo watu wenye mitaji ila hawana knowledge na skills ama muda wa kufanya forex tradings na hivyo kutumia watu wenye skills na muda kwa makubaliano fulani baina yao.

Shida hapa kwetu ilikuja kama wimbi la mafanikio fulani kwamba fulani kapata fedha kwa kuimba basi kila mtu anataka awe mwanamuziki na kusahau kuwa kuna vipaji,elimu,mazoezi ubunifu na determination ya kufanya jambo husika na sio kuingia studio tu na kurekodi.

Kuna mahali nimeona DSE(Dar es salaam Stock Exchange) au soko la hisa wamefungua App ya watu kuweza kushiriki kununua na kuuza hisa viganjani mwao kwa kutumia simu ama computer lengo in ikiwa ni kuwafikia watu wengi na kwa urahisi zaidi.(ni kama platforms za Forex na MT4 au MT5)

Bitcoin:

Hii ni sarafu ya kidijitali iliyoanzishwa na Mjapan aitwaye Satoshi Nakamoto mwaka 2009.

Ni sarafu iliyoendelea kukua na kupanda thamani na huenda hapo baadae ikachukua nafasi ya sarafu nyingi kutokana na uimara wake na umataifa wake(Kuna sarafu za nchi nyingine hazijana nguvu na umaarufu katika masoko ya kimataifa hivyo kutothaminjwa) Kuzigeuza cheap currencies kuwa Bitcoin huzipa thaman na kuzitambua thamani.

Mfano rahisi ni kama Dhahabu inavyowekwa katika mabenki na watu wanaweza kununua au kuwekesha kama amana zinazokubalika duniani kote

Sarafu ya Bitcoin imeanza kutumika kama mfumo wa malipo kwa huduma mbalimbali na mabenki mengi makubwa ya nchi zilizoendelea kiuchumi na kiteknolojia kuzipokea ba kuzitumia
Nachokiona kwa Tanzania na Watanzania ni uoga wa mabadiliko na uelewa mdogo.

Nakumbuka yalipoingia magari yenye mfumo wa Automatic Gear Box watu waliaminishwa kuwa si imara,hamna spare wala mafundi na ilikuwa ngumu sana hata kuyauza.i

Sasa hivi ndio magari mengi na maarufu na wengi hawataki kusikia magari ya manual na wengi wamesahau hata namna ya kuyaendesha au hawajui kabisa.

Dunia sasa inaenda kidijitali na mifumo inabadilika.. Hapa kwetu tumeanza na mifumo ya simu kama M-Pesa.tiGo Pesa,Airtel Money,Z Pesa,T Pesa na Halopesa..

Mwanzoni pia watu walikuwa wagumu sana kuiamini na kuitumia,walipenda zaidi mifumo ya hard cash kwenye kulipa bidhaa,kulipana,kuuza na kununua huduma mbalimbali kama umeme,maji,vocha na muda wa Televisheni.
Wengi wabakumbuka kutuma pesa kwa njia za Telegram Posra,EMS,Kutumia mabasi kama Scandnavia,Kupanga foleni kulipia au kununua umeme,Vocha za kukwangua,Kupanga foleni Mobitel kulipia Airtime nk

Lakini sasa mengi hayo unaweza kuyafanya kirahisi kwa simu na kuokoa muda au gharama za mafuta/ usafiri kwenda benki au vituo vya huduma husika.
Sass hivi kuna Lipa Namba,Masterpass nk unalipa bill za,Hotel,Bar,Maduka unalipia Petrol nk
Ni rahisi kulipa ada za Shule nk.

Ni rahisi kutuma fedha na hata kudeposit na kuwithdraw kweda Benki au kutoka Benki na hii ni kwa muda wowote hata usiku wa manane.

Hizi pia ni e-money(Digital) sio hard cash sasa Bitcoin ni Advanced Digital Currency ambako ndio muelekeo wa dunia yote kwa sasa.
Bitcon moja kwa sassa nadhani ni sawa na Milioni 43 za kitanzania- unaweza ku-google kupata thamani halisi.

Ukiangalia Benki nyingi zinahamasisha kufungua online accounts kwa kutumia Apps zao,kitendo cha dk 5 hadi 10 mtu anafungua akaunti na anaweza kudeposit
Au anacreate debit card kama Master Card au Visa na kuanza kuitumia instantly. Ikiexpire kama ilikuwa na balance inarudishwa kwenye akaunti yako ya simu.

Makampuni ya simu yanahimiza kutumia Apps zaidi kufikia huduma zao na hadi wanatoa ofa kama kutoa bonus ya fedha unapofanya miamala kati yao na mabenki.
Kununua huduma kwa Apps ni rahisi na bafuu kuliko ukitumia USSD codes yaani zile Menu za kubonyeza *150*XX#
Mfano ukinunua bundle la data la wiki la voda kwa USSD code kwa TZS 5,000 utapata GB 2 lakini ukitumi App utapata GB 4 au ukinunua Data bundle la mwezi tiGo kwa USSD utapata GB 21 wakati kwa App pesa hiyohiyo utapata GB 34 (tofauti ya GB 13!)

Dunia inabadilika kuwa Cashless tunaenda Dijitali hivyo si kweli kusema Forex au Bitcoin ni Scams.

Udanganyifu upo kila mahala na wapigaji wapo kote na hupenda kujipenyeza mahali kwenye jambo jipya au lenye uelewa mdogo kwa watu.

Wapo scammers wa makusudi kabisa na wapo makanjanja wa hizi biashara na matokeo huwaingiza hasara sponsors waliowashawishi,ukute hata mtu anasema amepoteza zake alizotoa kuwekeza kuwa katapeliwa isi kwelo ukute ni ameingia loss kwenye real & legal trades na hata huyo mtaalamu wake hajaambulia hata mia na mtaji umenufaisha soko na dalali(Broker)

Tuwe tunajifunza vitu kabla ya kukurupuka kuvivamia na pia tusipende kuita vitu vya ukweli kuwa ni hoax au scams bila kuwa na uelewa navyo(kuvijua) au kuchukulia vile experience mtu aliipata binafsi.

Amini Forex ni real business na watu wanaishi kwa biashara hiyo tena kwa mafanikio makubwa tu.

Tatizo la kuita FX scam ni pale unapotaka kufanyiwa ukiwa huna study kwa uwezo wa anayekufanyia na haraka ya Return of Investment jambo ambalo mara nyingi ni faulo kubwa kwenye hiyo biashara.

Kuhusu Kuku Farm ni farming nzuri kama umeifuatilia mfumo wake ni Cloud farming ambao upo na efficiency nzuri nachokiona ulikwama kutokana na sheria zetu na uelewa(Remember sometimes kuna sheria mbovu) au zisizoenda na wakati.

Ufugaji au Ukulima jumuishi(kutumia washiriki wengi) hukuza mtaji na kupata access ya huduma nyingi na kurahisisha zoezi kuliko kwa individuals wenye mitaji midogo,hawana skills na hawama facilities.

Tunaona hata Mabenki yakiungana ili kukuza mitaji kama mfano wa hivi karibuni tumeona Bank ya CBA ikiungana na Bank ya NIC na hivyo kukuza mtaji na kujipanua kuhuduma na biashara.

Kwa wanaojua mabasi kama ya Super Feo au New Force) yanayoenda mikoani hasa Songea,Mbeya nk ni muunganiko wa wamiliki wengi tofauti (unaweza kuthibitisha hilo kwa kusoma anuani za wamiliki zilizoandikwa chini ya mlango wa dereva) Hivyo biashara za kuinvest mtaji zipo nyingi za ukweli na sio Upatu.
Hata gari nyingi za Uber wanatumia lesseni za tours za kuchangia kupunguza makali na tozo kwa mtu mmoja mmoja.

Sasa DSE imekuja na hiyo program ya kununua na kuuza hisa Online je utaita ni Scam?

Hisa wapo waliobenefit kwa kampuni xa hisa walizonunua kupaa kama CRDB na TBL na wapo waliopata loss kwa hisa walizonunua kudepreciate values mfano kama hisa za TOL(Tanzania Oxygen Limited).

Wanaoinvest kiukweli kwenye Forex au Bitcoin hawana hata time kushawishi watu.Wao wanafanya kwa maslahi yao au ya Investors wanaotafuta ubia kwao.

Ukiona mtu anakushawishi basi huyo bado ni small scale trader anatafuta njia ya kupata kipato kupitia mtaji wako au commission kwa broker kwa kila profit utakayopata(wanaitwa IB au Introducing Broker)
Na hilo unaweza kulikwepa kwa kujisajili binafsi bila kupitia kwa refering person.

Nimeona mtu akisema unafungua akaunti kama Facebook.Hizo zote ni operations za Online huhitaji kuvisit ofisi ya mtoa huduma au kuwakilisha makaratasi.Utatakiwa kuwakilisha nakala za vitambulisho kama cha NIDA,Pasi ya kusafiria,Leseni ya udereva au utility bills kama za umeme au maji zenye jina lako au bank statement kwa aiili ya usalama wa akaunti yako.
Mungu atupe baraka na uhai ili huko mbeleni tushuhudie mabadiliko ya hizi digital business ambazo kwa sasa tunaziona kama gari za automatic.

Kwenye You Tubes na Instagram watu wanaingiza mamilioni kwa kuwa na viewes wengi wa post au musicd na pia followers wengi.Ukimuulizs mtu kama Millard Ayo au Kansiime Anne wa Uganda wanaweza kuthibitisha pay check wanazolipwa kwa activities zao You Tube.

Ujanja upo kila sekta.Counterfeit note zipo,viwanja hewa vipo nk hivyo ni kuwa makini tu huwezi kusema kuwa kuagiza gari Japan ni utapeli labda uliagiza kwa fake agent ukapoteza pesa zako.

Jisomee zaidi hizi links chini na pakua Apps za kujifunza zaidi




View attachment 1646740View attachment 1646741View attachment 1646742View attachment 1646743View attachment 1646744View attachment 1646745
Uzi mzuri huu,ngoja nitulie halafu nisome haya madini...
 
Habari kubwa katika kipindi hichi kwa upande wa fedha na uwekezaji ni cryptocurrency au kama inavyofahamika kwa Kiswahili fedha za kidijitali. Aina hii ya fedha imewavutia wengi siyo kwa sababu ya matumizi yake, bali kwa jinsi thamani yake inavyokua kwa kasi na hivyo wengi kuona ni sehemu rahisi ya kupata fedha nyingi bila ya kufanya kazi.

Lakini wengi ninaowaona wanakimbizana na fedha hizi za kidijitali, hawana uelewa wa kutosha. Wengi wanadanganywa na kushawishiwa kuingia kwenye kitu ambacho hawakielewi kwa matumaini kwamba watapata fedha nyingi. Ni kweli wapo watakaopata fedha nyingi, na pia wapo ambao watapoteza fedha nyingi kwenye aina hii ya uwekezaji.

Hivyo leo nimechukua muda, kukuandikia wewe rafiki yangu makala hii yenye kila unachopaswa kujua kuhusu cryptocurrency kwa ujumla, na tukiangalia kwa kina zaidi bitcoin ambayo ndiyo currency ya kwanza na yenye thamani kubwa zaidi. Nitachambua hili kwa lugha rahisi ambayo hata kama huna elimu kubwa utaweza kuelewa na kuweza kuchukua hatua.

Lakini kabla sijaingia kwenye kueleza kwa kina fedha hizi za kidijitali, naomba nikushirikishe hadithi tatu muhimu ambazo zitatupa mwanga wa nini kinaendelea.

Moja; TULIP MANIA 1630 – 1637.

Mnamo karne ya 17, kwenye Jamhuri ya Udachi (Dutch Republic), kulitokea hali ambayo haikuwa ya kawaida. Maua yanayojulikana kwa jina la Tulip yalianza kupata umaarufu ghafla. Maua haya yalikuwa na mwonekano mzuri na pia yalikuwa yana changamoto kwenye ulimwaji wake. Hivyo hili lilifanya watu wayathamini sana, na hili likapelekea bei yake kuwa juu. Kadiri bei ilivyokuwa inapanda, ndivyo wengi zaidi waliyataka maua hayo na bei kuzidi kupanda zaidi.

Ilifika wakati, thamani ya ua moja ikawa zaidi ya mara kumi ya kipato cha mwaka cha mfanyakazi wa kawaida kwenye nchi hiyo. Kutokana na kupanda huku thamani kwa maua aina ya Tulip, jamii nzima ilianza kuhamia kwenye maua hayo, ikafika wakati maua haya yakawa yanatumiwa kama fedha, badala ya dhahabu ambayo imekuwa inatumika wakati wote.

Ilifika hatua, watu wakawa wanalipia maua hayo hata kabla hayajakomaa, yaani yakiwa bado shambani. Kufikia Februari mwaka 1637 maua haya ya Tulip yalifikia bei ya juu kabisa na ghafla bei ikaanza kuporomoka. Bei iliporomoka kwa kasi kiasi cha kuyumbisha uchumi wa nchi nzima na watu wengi kupata hasara kubwa. Hii inasemekana kuwa anguko la kwanza la kiuchumi duniani.

tulip-mania-dot-com-bitcoin.png


Mbili; DOTCOM MANIA 1997 – 2001.

Mwishoni mwa miaka ya 1980 jambo kubwa lilitokea duniani ambalo ni matumizi ya mtandao wa intaneti kwa watu wa kawaida. Mwanzoni mwa miaka ya 1990 matumizi ya mtandao wa intaneti yalishika kasi na biashara nyingi zinazohusisha intaneti zilianzishwa.

Kwa kuwa intaneti ilikuwa kitu kipya, na ambacho kilionesha kuwa na nguvu kubwa, watu wengi walivutiwa na biashara zinazohusisha mtandao wa intaneti. Hivyo watu wengi walikimbilia kuanzisha biashara zinazohusisha intaneti. Inasemekana kwamba mwishoni mwa miaka ya 1990 na kuelekea mwaka 2000 watu wengi walikuwa wakiahidi kuanzisha kampuni zitakazokuwa kubwa na watu wakashawishika kuwekeza fedha zao bila hata ya kuwepo kwa ushahidi au uhakika wowote kwamba biashara inayokwenda kuanzishwa itakuwa imara kweli.

Watu waliingiwa na tamaa ya kufaidika haraka kupitia intaneti, kitu ambacho kilipelekea makampuni mengi kuwa na thamani kubwa kuliko uhalisia. Kilichotokea ni uchumi mzima unaohusisha mtandao wa intaneti kuanguka, makampuni mengi kutangaza hasara na watu wengi kupoteza fedha zao.

Tatu; CRYPTO MANIA 2009 - .......

Mwaka 2009, Satoshi Nakamoto, haijulikani kama ni mtu, kikundi cha watu au taasisi, alikuja na wazo la tofauti kwenye mfumo wa fedha. Kama ambavyo wote tunajua, mzunguko wa fedha umekuwa unadhibitiwa na benki kuu ya nchi husika. Kwa mfano mzunguko wa shilingi ya Tanzania, unadhibitiwa na Benki Kuu ya Tanzania. Hivyo miamala yoyote ya kifedha lazima iweze kufuatiliwa na benki kuu. Satoshi ali/walipendekeza mfumo wa kuondoa udhibiti huo. Badala ya mzunguko wa fedha kudhibitiwa na mtu mwingine, udhibitiwe na watu wawili tu, anayelipa na anayelipwa.

Mfumo huu ulionekana ni mkombozi kwa matatizo mengi ya kifedha, ambayo yapo wazi, mfano nchi kuchapa fedha na hivyo mfumuko wa bei kuwa mkubwa, gharama za kufanya miamala na hata usalama kuwa mdogo, kama ambavyo tumekuwa tunasikia fedha feki kuwepo kwenye mzunguko. Mfumo wa Satoshi ulionekana ni bora kabisa, lakini wengi wakawa na wasiwasi kwamba ni mgumu kueleweka na kutumika.

Hivyo mwaka 2009 Satoshi ali/walikuja na mfumo wa fedha ya kidijitali uliokwenda kwa jina la Bitcoin. Hii ilikuwa sarafu ya kwanza kabisa ya kidijitali, ambayo ilikuwa na lengo la kurudisha udhibiti na usalama wa fedha kwa watumiaji.

Kwa kipindi cha mwaka 2009 thamani ya bitcoin moja ilikuwa dola 0.0001 ambayo kwa kipindi hicho, dola moja ilikuwa tsh 1330, hivyo bitcoin moja ilikuwa sawa na tsh 1 na senti 33. Mpaka kufika mwaka 2010, bado thamani ya bitcoin moja ilikuwa chini ya dola moja. Kuanzia mwaka 2011 bei ya bitcoin imekuwa inaongezeka kidogo kidogo, kutoka dola mia na kuendelea. Mpaka kufika januari 2017, bei ya bitcoin moja ilikuwa chini ya dola elfu moja. Lakini baada ya hapo bei ilianza kuongezeka kwa kasi, kufika oktoba 2017, bei ya bitcoin moja ilikuwa dola elfu 5.

bitcoin-june-2009.png


Tarehe 17 mwezi disemba 2017 ndiyo ilikuwa siku ambayo thamani ya bitcoin ilikuwa juu sana, ambapo bitcoin moja ilikuwa sawa na dola elfu 19. Yaani sawa na zaidi ya shilingi milioni 40. Hebu fikiria hapo, kwamba kama mwaka 2009, ungepata nafasi ya kununua bitcoin moja kwa shilingi moja, mwaka 2017 ungekuwa na zaidi ya milioni 40!

Kwa nini hadithi hizi tatu?

Hadithi hizi tatu zinatufundisha kitu kimoja muhimu sana kwenye fedha na uwekezaji, kwamba mara nyingi tamaa ya watu ikishaingia kwenye kitu, thamani inapanda kuliko uhalisia, kitu ambacho kinatengeneza anguko baadaye. Ilitokea kwa maua ya Tulip, ilitokea kwa biashara za Dotcom na itatokea kwenye cryptocurrency kama ambavyo nitakueleza hapo chini.

Ili tuweze kuweza kuelewana vizuri, na kwa kuwa yapo mengi ya kujifunza kuhusu fedha hizi za kidijitali, tutakwenda kwa mfumo wa maswali na majibu.

Swali; bitcoin ni nini?

Jibu; bitcoin ni mfumo wa malipo wa kielektroniki ambao ni wa moja kwa moja kati ya mlipwaji na mlipaji bila ya kuhusisha upande wa tatu kama benki serikali na taasisi nyingine za kifedha.

Swali; mfumo huu unafanyaje kazi?

Jibu; kunakuwa na sarafu za kidijitali, ambazo zina idadi yanye ukomo. Sarafu hizi ndiyo zinazotumika kama thamani ya malipo. mfumo mzima ni wa kielektroniki na hivyo hakuna sarafu yoyote ya kawaida inayohusika. Badala yake mfumo wa kompyuta unaotoa na kudhibiti sarafu hizi ndiyo unaotumika.

Swali; zipi faida na ubora wa mfumo huu mpya wa malipo?

Mfumo wa kawaida wa fedha una changamoto nyingi ambazo tumekuwa tunaziona kila wakati. Sehemu kubwa ya changamoto hizo inaweza kutatiliwa na mfumo huu wa fedha za kidijitali.

Changamoto ya mfumuko wa bei ambayo imekuwa inasababishwa na serikali kuchapa fedha na hivyo kushusha thamani, unadhibitiwa na uwepo wa kiwango kamili cha sarafu za kidijitali. Kwa mfano kwa Bitcoin kuna sarafu 21,000,000 pekee, zikiisha hizo hakuna nyingine zinazoweza kuzalishwa na hivyo mfumuko wa bei hauwezi kutokea.

Changamoto ya usiri imetatuliwa na mfumo huu mpya kwa kufanya muamala kuwa baina ya watu wawili pekee. Katika mfumo wa kawaida, utamlipa mtu kwa njia ya benki, fedha taslimu au njia za mitandao, ambazo zote hazina usiri.

Changamoto ya gharama za miamala imeondolewa sana na mfumo huu, kwa mfumo wa kawaida, kila unapohamisha fedha eneo moja kwenda eneo jingine unakatwa malipo, na hii ni kwa sababu taasisi nyingi zinahusika. Lakini kwenye mfumo huu, hakuna uhusishaji wa taasisi nyingi, hivyo makato hakuna.

Changamoto ya usalama, tunajua namna ambavyo kuwa na kiasi kikubwa cha fedha ni hatari, pia hata benki siyo salama sana kuweka fedha. Kwa mfumo huu wa fedha wa kidijitali, usalama ni mkubwa, program ya kompyuta inayotumika kudhibiti mfumo huu ni dhabiti sana na haiwezi kuchezewa.

Changamoto ya fedha feki imedhibitiwa na mfumo huu. Kwa kila aina ya sarafu, kwenye mzunguko huwa kunakuwa na fedha feki nyingi. Lakini kwa mfumo huu wa fedha za kidijitali, hakuna namna ya kutengeneza sarafu feki.

Swali; je kuna sarafu za aina ngapi kwenye fedha hizi za kidijitali?

Jibu; Watu wengi wanajua zile sarafu kubwa za kidijitali kama Bitcoin, Ethereum, Ripple, Bitcoin Cash, Cardano, na Litecoin. Lakini mpaka kufika mwezi february 2018 kulikuwa na sarafu za kidijitali zaidi ya 1400, na orodha inaendelea kukua kila siku, kwa sababu yeyote anaweza kuja na sarafu mpya.

Swali; je cryptocurrency utakuwa mfumo kamili wa malipo?

Jibu ni ndiyo, lakini siyo sasa ni kwa baadaye. Lakini pia kama utakuwa mfumo mkuu wa malipo, basi kila serikali itatengeneza mfumo wake wa malipo kwa njia hiyo ya kidijitali. Hakuna serikali inayoweza kukubali kupoteza udhibiti wa fedha, kitu pekee kinafanya serikali ziwepo, tangu enzi za utawala wa roma, ni udhibiti wa fedha, na enzi hizo, dhahabu.

Swali; je Bitcoin itakuja kuwa sarafu ya dunia na kutumiwa na kila mtu?

Jibu ni hapana, Bitcoin imekosa sifa zote za sarafu ya kutumiwa na uma, kwa sababu thamani yake haijatulia, inapanda na kushuka kwa kasi mno. Pia watu wengi wameshaihodhi na hivyo uwezekano wa kutumiwa na kila mtu ni mdogo.

Swali; je soko zima la fedha hizi za kidijitali litaanguka?

Hapa ndipo muhimu sana unapaswa kuelewa. Kwa hizi sarafu nyingi, ukiangalia zilianza na thamani kidogo sana. mfano bitcoin kwa mwaka 2009 na 2010 thamani yake ilikuwa chini ya dola moja. Lakini baada ya watu kuisikia ilianza kupanda thamani na kufikia disemba 2017 ilifikia thamani ya juu kabisa ya sarafu moja kuwa dola elfu 19. Lakini baada ya hapo imekuwa unashuka na kupanda.

Ukuaji huu wa thamani ya sarafu hizi za kidijitali siyo wa kawaida, na unachochewa na tamaa ya watu kuona ni njia ya haraka ya kutengeneza utajiri. Tamaa hii itapelekea sarafu nyingi kuanguka na baada ya hapo zitasimama sarafu imara na ambazo thamani yake inaendana na hali ya uchumi.

Kama ambavyo TULIP ilianguka, na kama DOTCOM ilivyoanguka, CRYPTOCURRENCY pia itaanguka, lakini baada ya hapo zitaibuka sarafu ambazo ni imara na zenye thamani inayoendana na uchumi. Anguko la CRYPTOCURRENCY litawaumiza wengi sana na kuwanufaisha wachache.

[caption id="attachment_4407" align="alignnone" width="800"]
coindesk-bpi-chart1.jpeg
Kwa kipindi cha mwaka mmoja kati ya machi 2017 mpaka mashi 2018, thamani ya bitcoin imeongezeka kutoka chini ya dola elfu moja mpaka dila elfu kumi na tisa. Ni ongezeko ambalo haliwezi kuelezewa vyovyote vile kiuchumi.[/caption]

Swali; je kuna matumizi mengine ya teknolojia hii ukiacha malipo?


Teknolojia iliyopo nyuma ya sarafu hizi za kidijitali, ambayo ni BLOCKCHAIN ina matumizi mengine mengi na makubwa. Mfano inatumika kwenye kuandaa mikataba ya kidijitali, inatumika kwenye kutunza kumbukumbu za siri na kwenye usimamizi na udhibiti wa uwekezaji. Teknolojia ya blockchain inaweza kutumika kwenye kila eneo linalohitaji ufuatiliaji na udhibiti wa hali ya juu, kama kwenye afya, benki, makusanyo ya mapato na kadhalika.

Kwa nini BITCOIN siyo uwekezaji sahihi kwako kufanya kwa sasa?

Mpaka kufika hapa nina imani umeanza kupata picha ya hichi kitu kinachoitwa CRYPTOCURRENCY ni nini, kwamba ni mfumo wa malipo wa kidijitali ambao ni wa moja kwa moja na unaepuka changamoto nyingi za mfumo wa kawaida wa fedha. Pia utakuwa umejua BITCOIN ni moja kati ya sarafu zaidi ya elfu moja ambazo zinatumia mfumo huu. Kwa kipindi hichi BITCOIN ndiyo sarafu yenye thamani kubwa.

Sasa nimalize kwa kukuambia kwa nini BITCOIN siyo uwekezaji sahihi kwako kufanya kwa sasa.

Watu wengi wanahamasishwa sana kuwekeza kwa kununua bitcoin hasa pale ambapo thamani yake ilikuwa inapanda kwa kasi ya ajabu. Lakini wengi ambao wamekuwa wanatamani kuwekeza kwenye mfumo huu, hawapo tayari. Hapa nitataja makundi matano na kama upo kwenye moja ya makundi hayo usiwekeze kwenye cryptocurrency na bitcoin, badala yake endelea na uwekezaji wa kawaida ambao ni salama kidogo ukilinganisha na huu kwa sasa.

1. Kama ndiyo umeielewa cryptocurrency na bitcoin leo, jipe muda wa kujifunza.
Nilichokushirikisha hapa kuhusu cryptocurrency na bitcoin ni kama tone tu la bahari ambayo unapaswa kuelewa kuhusu mfumo huu wa fedha na malipo. Hivyo kama umekuwa unasikia sikia kuhusu hizo bitcoin lakini leo ndiyo umeanza kupata picha basi huu siyo uwekezaji mzuri kwako kwa sasa.

Pendekezo langu ni chukua muda kusoma na kuelewa kwa kina, soma vitabu na siyo makala au kuwasikiliza watu wanaokuambia kwa nini ujiunge au usijiunge. Isome teknolojia hii uielewe kwa undani, kisha soma fedha, uchumi na uwekezaji ili kujua namna vitu hivi vinakwenda. Hapo utakuwa umepata mwanga wa kukusaidia kufanya maamuzi sahihi.

2. Kama huwezi kumudu kupoteza fedha.

Pamoja na hatari ya cryptocurrency na bitcoin kwa sasa, bado ni kitu kizuri kujaribu, ila tu, ni rudie, ila tu unamudu kupoteza fedha. Yaani kama una fedha za ziada, ambazo hata ukizipoteza maisha yako hayatayumba, basi unaweza kujaribu aina hii ya uwekezaji.

Lakini kama bado hujafikia hatua ya kuwa na fedha za ziada, kama upo kwenye madeni na unafikiria aina hii ya uwekezaji itakutoa kimaisha, kaa mbali nayo, ni hatari kwako.

Na kama unawaza kwenda kukopa fedha uwekeze kwenye mfumo huu, huna tofauti na mtu anayevuta sigara huku anaweka petroli kwenye gari, siyo hatari kwako tu, bali na kwa wengine pia.

3. Kama umri wako wa kuzalisha fedha umesogea.

Katika kila anguko la uchumi linalotokea duniani, watu wanaoathirika zaidi ni wale ambao umri wao umeenda na hawawezi tena kujitumikisha. Yaani kama umri umeenda, unakaribia kustaafu au umeshastaafu na una fedha zako za mafao, usiziweke kwenye mfumo huu wa fedha za kidijitali. Hata kama unaona kuna nafasi kubwa ya kuongeza kipato hicho, hatari unayochukua ni kubwa sana kwako, na nguvu za kupambana zimeshapungua.

4. Kama elimu pekee uliyonayo ni ya kuambiwa.

Wapo watu ambao wanatoa elimu hizi za cryptocurrency na bitcoin, ila elimu wanayoitoa ni ya kuwaambia watu kwa nini wajiunge na kuwashawishi kwamba ni uwekezaji ambao hawapaswi kuukosa. Kama hii ndiyo elimu ambayo umekuwa unaipata pekee, hujawa tayari kuwekeza. Unahitaji kujifunza kwa kina, faida na hasara, usalama na hatari kwenye uwekezaji huu kabla hujachukua hatua.

5. Kama sababu pekee ya kuwekeza ni kwa sababu wengine wamekuambia ‘wanapiga hela’

Ipo sababu nyingine ambayo naona watu wanaitumia vibaya kuwekeza kwenye mfumo huu mpya wa fedha na malipo. Na sababu hiyo ni kwamba ona wengine wanapata hela. Na watu wanaonesha kweli wanapata fedha, na ni kweli siyo utani. Kama nilivyoeleza, hata pale sarafu hizi zitakapoanguka, wapo watakaonufaika na wapo watakaopoteza.

Sasa unapofikiria kupata tu, jua kwamba kuna kukosa pia. Hivyo ukiangalia wanaonufaika, usiache kuangalia uwezekano wa kukosa.

Rafiki, nimejaribu kukuelezea kwa lugha rahisi na inayoeleweka kuhusu mfumo huu mpya wa fedha za kidijitali, kama nilivyoeleza hii ni sehemu ndogo sana ya elimu kubwa unayopaswa kuwa nayo kama unataka kuwekeza kwenye mfumo huu. Wito wangu kwako ni uendelee kujifunza zaidi na kama una kiasi cha fedha unachoweza kupoteza, unaweza kujaribu kwenye aina hii ya uwekezaji, ukijua kwamba nafasi ya kupoteza ni kubwa kama ilivyo ya kunufaika.

Kila la Kheri Rafiki Yangu.

Rafiki na Kocha wako,

Dr. Makirita Amani,

www.kisimachamaarifa.co.tz/kocha
Nimependa uzi wako huu,ni mzuri sana mi nimeipenda biashara hii hila nilishajipa kipindi cha miezi sita kuisoma na kuifatilia umri wangu bado unanieuhusu kujaribu na kurisk hila tafadhali naichukua na wewe umeniongezea kitu.nitakutafuta unielimishe mengi cha msingi naomba contact zako muhimu.

Sent from my TECNO B1g using JamiiForums mobile app
 
Bitcoin, hii ilinifanya nikawa nime data, na niliweza kupungua kilo nying San kwa mawazo ya kupoteza pesa yang ambay nilikuwa na malengo nayo ya kimaendeleo
Kwa kwel niliyumba baada ya kumining kwa scamer.
Sema nilipata kuona crip ya jack ma ndo iliyo niamsha kweny ngazi ya bitcoin na mpka leo nimekuwa risk taker tena wa hatari Sana, siwazi tena kupoteza na nipo mbion kurud kweny hii GAMES Maan bad ninazo bitcoin 0.0789 kweny localbiticoin
 
Wivu utakuua Makirita sio level yako.. Ulitaka asummarize kwa kitu muhimu kama hiki? Hapo ameshawaharibia soko matapeli wa bit oin kama wewe..Kama sio tapeli kinachokufanya upanic na kuanza kuandika utumbo wa kuku ni nini? Kama uzi haukuhusu siupite tu!! Watu kama nyie ndio mkapa anawaitaga wapumbavu na malofa.

Dah leo nimekumbuka hii comment niliisoma 3 years ago na nikawa lofa nikaweka $5000 kununua bitcoin basi leo nimeisoma tena najikuta nacheka tu kuna mipumbav ilitaka tuamini ujinga wao pesa itupite kushoto hahahahahahahahahahaha
 
Bitcoin, hii ilinifanya nikawa nime data, na niliweza kupungua kilo nying San kwa mawazo ya kupoteza pesa yang ambay nilikuwa na malengo nayo ya kimaendeleo
Kwa kwel niliyumba baada ya kumining kwa scamer.
Sema nilipata kuona crip ya jack ma ndo iliyo niamsha kweny ngazi ya bitcoin na mpka leo nimekuwa risk taker tena wa hatari Sana, siwazi tena kupoteza na nipo mbion kurud kweny hii GAMES Maan bad ninazo bitcoin 0.0789 kweny localbiticoin
Hapa ukiuza unapata IST

Sent from my SM-A125F using JamiiForums mobile app
 
Dah leo nimekumbuka hii comment niliisoma 3 years ago na nikawa lofa nikaweka $5000 kununua bitcoin basi leo nimeisoma tena najikuta nacheka tu kuna mipumbav ilitaka tuamini ujinga wao pesa itupite kushoto hahahahahahahahahahaha
kuna watu hawapendi kuona wenzao wakifanikiwa, wanapenda wawe pekeyao hawataki kuwaambia wenzao siri za mafanikio yan
 
Hahaha kwanini hawa watu wa ma cryptocurrency wanatupenda sanaaa?! Bhakhresa na Mengi nao wangetupenda hivi dunia ingekuwa tambarare.
Eti wanataka sisi masikini tuwe matajiri?! Yani watu wa ma cryptocurrency wamekua matajiri wazuri sana wanatupenda masikini.

Siku nikiona Bitcoin imeanza kununua wali kwa mamantilie sitouliza nitajiunga, au nikiona ATM inayotoa Bitcoin, ama bank zetu zikianza kutoa change nitajiunga, lakini huu utajiri wa mitandaoni kama Dr.Shika mimi siutaki.
bro ushajiunga na Bitcoin maana kuna ATM zinatoa Bitcoin huko duniani na hapa nchini mpaka akina mpoki wamekula shavu kuitangaza Bitcoin
 
Back
Top Bottom