Kila kitu unachopaswa kujua kuhusu Cryptocurrency na Bitcoin na kwanini siyo uwekezaji mzuri kwako kwa sasa

Dear Client,

We are pleased to inform you that Vodacom’s M-Pesa mobile option for deposits and withdrawals has been reenabled. Be sure to use this payment solution to conveniently make fast and convenient transactions in a just few steps.



Enjoy the benefits:

Instant deposits
Withdrawals within 24 hours
No commission or transfer fees from our side

Multiple transactions per day
Advanced security and safety



Terms and Conditions:
Minimum amount of deposit: 200 000 TZS.

Maximum deposit amount per transaction: 500 000 TZS.

Minimum withdrawal amount: 25 USD.
Mobile number to use in the transaction must be Vodacom M-Pesa and the one that client provided upon registration with Tickmill.


To change the mobile number in his/her Client Area, must send email to support@tickmill.com or contact Account Manager, requesting to change phone number by stating the reason (e.g. to deposit via Vodacom M-Pesa).

Should you have any questions, please do not hesitate to contact our dedicated Support Team via email, phone or Live Chat.

Kind Regards,

The Tickmill Team.
 
Crypto haina maana tufanye vitu halisia
Braza nakuhakikishia IMF na powerful world banks wakishakubali kuachana na Fiat currencies na kupromote crypto currency ndio tutajua hii kitu inamake sense sana, tukiwa ndani ya JF hatijui trend ya hiz cryptos na jins zinavyorun marketing systems ila huko duniani economists and investors are dancing a crazy trend ya crypto, cryptos zipo catchy sana na zinatrend moto sana!
Let's adjust to the inevitable future, get into crypto, let's meet there!
 
Habari kubwa katika kipindi hichi kwa upande wa fedha na uwekezaji ni cryptocurrency au kama inavyofahamika kwa Kiswahili fedha za kidijitali. Aina hii ya fedha imewavutia wengi siyo kwa sababu ya matumizi yake, bali kwa jinsi thamani yake inavyokua kwa kasi na hivyo wengi kuona ni sehemu rahisi ya kupata fedha nyingi bila ya kufanya kazi.

Lakini wengi ninaowaona wanakimbizana na fedha hizi za kidijitali, hawana uelewa wa kutosha. Wengi wanadanganywa na kushawishiwa kuingia kwenye kitu ambacho hawakielewi kwa matumaini kwamba watapata fedha nyingi. Ni kweli wapo watakaopata fedha nyingi, na pia wapo ambao watapoteza fedha nyingi kwenye aina hii ya uwekezaji.

Hivyo leo nimechukua muda, kukuandikia wewe rafiki yangu makala hii yenye kila unachopaswa kujua kuhusu cryptocurrency kwa ujumla, na tukiangalia kwa kina zaidi bitcoin ambayo ndiyo currency ya kwanza na yenye thamani kubwa zaidi. Nitachambua hili kwa lugha rahisi ambayo hata kama huna elimu kubwa utaweza kuelewa na kuweza kuchukua hatua.

Lakini kabla sijaingia kwenye kueleza kwa kina fedha hizi za kidijitali, naomba nikushirikishe hadithi tatu muhimu ambazo zitatupa mwanga wa nini kinaendelea.

Moja; TULIP MANIA 1630 – 1637.

Mnamo karne ya 17, kwenye Jamhuri ya Udachi (Dutch Republic), kulitokea hali ambayo haikuwa ya kawaida. Maua yanayojulikana kwa jina la Tulip yalianza kupata umaarufu ghafla. Maua haya yalikuwa na mwonekano mzuri na pia yalikuwa yana changamoto kwenye ulimwaji wake. Hivyo hili lilifanya watu wayathamini sana, na hili likapelekea bei yake kuwa juu. Kadiri bei ilivyokuwa inapanda, ndivyo wengi zaidi waliyataka maua hayo na bei kuzidi kupanda zaidi.

Ilifika wakati, thamani ya ua moja ikawa zaidi ya mara kumi ya kipato cha mwaka cha mfanyakazi wa kawaida kwenye nchi hiyo. Kutokana na kupanda huku thamani kwa maua aina ya Tulip, jamii nzima ilianza kuhamia kwenye maua hayo, ikafika wakati maua haya yakawa yanatumiwa kama fedha, badala ya dhahabu ambayo imekuwa inatumika wakati wote.

Ilifika hatua, watu wakawa wanalipia maua hayo hata kabla hayajakomaa, yaani yakiwa bado shambani. Kufikia Februari mwaka 1637 maua haya ya Tulip yalifikia bei ya juu kabisa na ghafla bei ikaanza kuporomoka. Bei iliporomoka kwa kasi kiasi cha kuyumbisha uchumi wa nchi nzima na watu wengi kupata hasara kubwa. Hii inasemekana kuwa anguko la kwanza la kiuchumi duniani.

tulip-mania-dot-com-bitcoin.png


Mbili; DOTCOM MANIA 1997 – 2001.

Mwishoni mwa miaka ya 1980 jambo kubwa lilitokea duniani ambalo ni matumizi ya mtandao wa intaneti kwa watu wa kawaida. Mwanzoni mwa miaka ya 1990 matumizi ya mtandao wa intaneti yalishika kasi na biashara nyingi zinazohusisha intaneti zilianzishwa.

Kwa kuwa intaneti ilikuwa kitu kipya, na ambacho kilionesha kuwa na nguvu kubwa, watu wengi walivutiwa na biashara zinazohusisha mtandao wa intaneti. Hivyo watu wengi walikimbilia kuanzisha biashara zinazohusisha intaneti. Inasemekana kwamba mwishoni mwa miaka ya 1990 na kuelekea mwaka 2000 watu wengi walikuwa wakiahidi kuanzisha kampuni zitakazokuwa kubwa na watu wakashawishika kuwekeza fedha zao bila hata ya kuwepo kwa ushahidi au uhakika wowote kwamba biashara inayokwenda kuanzishwa itakuwa imara kweli.

Watu waliingiwa na tamaa ya kufaidika haraka kupitia intaneti, kitu ambacho kilipelekea makampuni mengi kuwa na thamani kubwa kuliko uhalisia. Kilichotokea ni uchumi mzima unaohusisha mtandao wa intaneti kuanguka, makampuni mengi kutangaza hasara na watu wengi kupoteza fedha zao.

Tatu; CRYPTO MANIA 2009 - .......

Mwaka 2009, Satoshi Nakamoto, haijulikani kama ni mtu, kikundi cha watu au taasisi, alikuja na wazo la tofauti kwenye mfumo wa fedha. Kama ambavyo wote tunajua, mzunguko wa fedha umekuwa unadhibitiwa na benki kuu ya nchi husika. Kwa mfano mzunguko wa shilingi ya Tanzania, unadhibitiwa na Benki Kuu ya Tanzania. Hivyo miamala yoyote ya kifedha lazima iweze kufuatiliwa na benki kuu. Satoshi ali/walipendekeza mfumo wa kuondoa udhibiti huo. Badala ya mzunguko wa fedha kudhibitiwa na mtu mwingine, udhibitiwe na watu wawili tu, anayelipa na anayelipwa.

Mfumo huu ulionekana ni mkombozi kwa matatizo mengi ya kifedha, ambayo yapo wazi, mfano nchi kuchapa fedha na hivyo mfumuko wa bei kuwa mkubwa, gharama za kufanya miamala na hata usalama kuwa mdogo, kama ambavyo tumekuwa tunasikia fedha feki kuwepo kwenye mzunguko. Mfumo wa Satoshi ulionekana ni bora kabisa, lakini wengi wakawa na wasiwasi kwamba ni mgumu kueleweka na kutumika.

Hivyo mwaka 2009 Satoshi ali/walikuja na mfumo wa fedha ya kidijitali uliokwenda kwa jina la Bitcoin. Hii ilikuwa sarafu ya kwanza kabisa ya kidijitali, ambayo ilikuwa na lengo la kurudisha udhibiti na usalama wa fedha kwa watumiaji.

Kwa kipindi cha mwaka 2009 thamani ya bitcoin moja ilikuwa dola 0.0001 ambayo kwa kipindi hicho, dola moja ilikuwa tsh 1330, hivyo bitcoin moja ilikuwa sawa na tsh 1 na senti 33. Mpaka kufika mwaka 2010, bado thamani ya bitcoin moja ilikuwa chini ya dola moja. Kuanzia mwaka 2011 bei ya bitcoin imekuwa inaongezeka kidogo kidogo, kutoka dola mia na kuendelea. Mpaka kufika januari 2017, bei ya bitcoin moja ilikuwa chini ya dola elfu moja. Lakini baada ya hapo bei ilianza kuongezeka kwa kasi, kufika oktoba 2017, bei ya bitcoin moja ilikuwa dola elfu 5.

bitcoin-june-2009.png


Tarehe 17 mwezi disemba 2017 ndiyo ilikuwa siku ambayo thamani ya bitcoin ilikuwa juu sana, ambapo bitcoin moja ilikuwa sawa na dola elfu 19. Yaani sawa na zaidi ya shilingi milioni 40. Hebu fikiria hapo, kwamba kama mwaka 2009, ungepata nafasi ya kununua bitcoin moja kwa shilingi moja, mwaka 2017 ungekuwa na zaidi ya milioni 40!

Kwa nini hadithi hizi tatu?

Hadithi hizi tatu zinatufundisha kitu kimoja muhimu sana kwenye fedha na uwekezaji, kwamba mara nyingi tamaa ya watu ikishaingia kwenye kitu, thamani inapanda kuliko uhalisia, kitu ambacho kinatengeneza anguko baadaye. Ilitokea kwa maua ya Tulip, ilitokea kwa biashara za Dotcom na itatokea kwenye cryptocurrency kama ambavyo nitakueleza hapo chini.

Ili tuweze kuweza kuelewana vizuri, na kwa kuwa yapo mengi ya kujifunza kuhusu fedha hizi za kidijitali, tutakwenda kwa mfumo wa maswali na majibu.

Swali; bitcoin ni nini?

Jibu; bitcoin ni mfumo wa malipo wa kielektroniki ambao ni wa moja kwa moja kati ya mlipwaji na mlipaji bila ya kuhusisha upande wa tatu kama benki serikali na taasisi nyingine za kifedha.

Swali; mfumo huu unafanyaje kazi?

Jibu; kunakuwa na sarafu za kidijitali, ambazo zina idadi yanye ukomo. Sarafu hizi ndiyo zinazotumika kama thamani ya malipo. mfumo mzima ni wa kielektroniki na hivyo hakuna sarafu yoyote ya kawaida inayohusika. Badala yake mfumo wa kompyuta unaotoa na kudhibiti sarafu hizi ndiyo unaotumika.

Swali; zipi faida na ubora wa mfumo huu mpya wa malipo?

Mfumo wa kawaida wa fedha una changamoto nyingi ambazo tumekuwa tunaziona kila wakati. Sehemu kubwa ya changamoto hizo inaweza kutatiliwa na mfumo huu wa fedha za kidijitali.

Changamoto ya mfumuko wa bei ambayo imekuwa inasababishwa na serikali kuchapa fedha na hivyo kushusha thamani, unadhibitiwa na uwepo wa kiwango kamili cha sarafu za kidijitali. Kwa mfano kwa Bitcoin kuna sarafu 21,000,000 pekee, zikiisha hizo hakuna nyingine zinazoweza kuzalishwa na hivyo mfumuko wa bei hauwezi kutokea.

Changamoto ya usiri imetatuliwa na mfumo huu mpya kwa kufanya muamala kuwa baina ya watu wawili pekee. Katika mfumo wa kawaida, utamlipa mtu kwa njia ya benki, fedha taslimu au njia za mitandao, ambazo zote hazina usiri.

Changamoto ya gharama za miamala imeondolewa sana na mfumo huu, kwa mfumo wa kawaida, kila unapohamisha fedha eneo moja kwenda eneo jingine unakatwa malipo, na hii ni kwa sababu taasisi nyingi zinahusika. Lakini kwenye mfumo huu, hakuna uhusishaji wa taasisi nyingi, hivyo makato hakuna.

Changamoto ya usalama, tunajua namna ambavyo kuwa na kiasi kikubwa cha fedha ni hatari, pia hata benki siyo salama sana kuweka fedha. Kwa mfumo huu wa fedha wa kidijitali, usalama ni mkubwa, program ya kompyuta inayotumika kudhibiti mfumo huu ni dhabiti sana na haiwezi kuchezewa.

Changamoto ya fedha feki imedhibitiwa na mfumo huu. Kwa kila aina ya sarafu, kwenye mzunguko huwa kunakuwa na fedha feki nyingi. Lakini kwa mfumo huu wa fedha za kidijitali, hakuna namna ya kutengeneza sarafu feki.

Swali; je kuna sarafu za aina ngapi kwenye fedha hizi za kidijitali?

Jibu; Watu wengi wanajua zile sarafu kubwa za kidijitali kama Bitcoin, Ethereum, Ripple, Bitcoin Cash, Cardano, na Litecoin. Lakini mpaka kufika mwezi february 2018 kulikuwa na sarafu za kidijitali zaidi ya 1400, na orodha inaendelea kukua kila siku, kwa sababu yeyote anaweza kuja na sarafu mpya.

Swali; je cryptocurrency utakuwa mfumo kamili wa malipo?

Jibu ni ndiyo, lakini siyo sasa ni kwa baadaye. Lakini pia kama utakuwa mfumo mkuu wa malipo, basi kila serikali itatengeneza mfumo wake wa malipo kwa njia hiyo ya kidijitali. Hakuna serikali inayoweza kukubali kupoteza udhibiti wa fedha, kitu pekee kinafanya serikali ziwepo, tangu enzi za utawala wa roma, ni udhibiti wa fedha, na enzi hizo, dhahabu.

Swali; je Bitcoin itakuja kuwa sarafu ya dunia na kutumiwa na kila mtu?

Jibu ni hapana, Bitcoin imekosa sifa zote za sarafu ya kutumiwa na uma, kwa sababu thamani yake haijatulia, inapanda na kushuka kwa kasi mno. Pia watu wengi wameshaihodhi na hivyo uwezekano wa kutumiwa na kila mtu ni mdogo.

Swali; je soko zima la fedha hizi za kidijitali litaanguka?

Hapa ndipo muhimu sana unapaswa kuelewa. Kwa hizi sarafu nyingi, ukiangalia zilianza na thamani kidogo sana. mfano bitcoin kwa mwaka 2009 na 2010 thamani yake ilikuwa chini ya dola moja. Lakini baada ya watu kuisikia ilianza kupanda thamani na kufikia disemba 2017 ilifikia thamani ya juu kabisa ya sarafu moja kuwa dola elfu 19. Lakini baada ya hapo imekuwa unashuka na kupanda.

Ukuaji huu wa thamani ya sarafu hizi za kidijitali siyo wa kawaida, na unachochewa na tamaa ya watu kuona ni njia ya haraka ya kutengeneza utajiri. Tamaa hii itapelekea sarafu nyingi kuanguka na baada ya hapo zitasimama sarafu imara na ambazo thamani yake inaendana na hali ya uchumi.

Kama ambavyo TULIP ilianguka, na kama DOTCOM ilivyoanguka, CRYPTOCURRENCY pia itaanguka, lakini baada ya hapo zitaibuka sarafu ambazo ni imara na zenye thamani inayoendana na uchumi. Anguko la CRYPTOCURRENCY litawaumiza wengi sana na kuwanufaisha wachache.

[caption id="attachment_4407" align="alignnone" width="800"]
coindesk-bpi-chart1.jpeg
Kwa kipindi cha mwaka mmoja kati ya machi 2017 mpaka mashi 2018, thamani ya bitcoin imeongezeka kutoka chini ya dola elfu moja mpaka dila elfu kumi na tisa. Ni ongezeko ambalo haliwezi kuelezewa vyovyote vile kiuchumi.[/caption]

Swali; je kuna matumizi mengine ya teknolojia hii ukiacha malipo?

Teknolojia iliyopo nyuma ya sarafu hizi za kidijitali, ambayo ni BLOCKCHAIN ina matumizi mengine mengi na makubwa. Mfano inatumika kwenye kuandaa mikataba ya kidijitali, inatumika kwenye kutunza kumbukumbu za siri na kwenye usimamizi na udhibiti wa uwekezaji. Teknolojia ya blockchain inaweza kutumika kwenye kila eneo linalohitaji ufuatiliaji na udhibiti wa hali ya juu, kama kwenye afya, benki, makusanyo ya mapato na kadhalika.

Kwa nini BITCOIN siyo uwekezaji sahihi kwako kufanya kwa sasa?

Mpaka kufika hapa nina imani umeanza kupata picha ya hichi kitu kinachoitwa CRYPTOCURRENCY ni nini, kwamba ni mfumo wa malipo wa kidijitali ambao ni wa moja kwa moja na unaepuka changamoto nyingi za mfumo wa kawaida wa fedha. Pia utakuwa umejua BITCOIN ni moja kati ya sarafu zaidi ya elfu moja ambazo zinatumia mfumo huu. Kwa kipindi hichi BITCOIN ndiyo sarafu yenye thamani kubwa.

Sasa nimalize kwa kukuambia kwa nini BITCOIN siyo uwekezaji sahihi kwako kufanya kwa sasa.

Watu wengi wanahamasishwa sana kuwekeza kwa kununua bitcoin hasa pale ambapo thamani yake ilikuwa inapanda kwa kasi ya ajabu. Lakini wengi ambao wamekuwa wanatamani kuwekeza kwenye mfumo huu, hawapo tayari. Hapa nitataja makundi matano na kama upo kwenye moja ya makundi hayo usiwekeze kwenye cryptocurrency na bitcoin, badala yake endelea na uwekezaji wa kawaida ambao ni salama kidogo ukilinganisha na huu kwa sasa.

1. Kama ndiyo umeielewa cryptocurrency na bitcoin leo, jipe muda wa kujifunza.
Nilichokushirikisha hapa kuhusu cryptocurrency na bitcoin ni kama tone tu la bahari ambayo unapaswa kuelewa kuhusu mfumo huu wa fedha na malipo. Hivyo kama umekuwa unasikia sikia kuhusu hizo bitcoin lakini leo ndiyo umeanza kupata picha basi huu siyo uwekezaji mzuri kwako kwa sasa.

Pendekezo langu ni chukua muda kusoma na kuelewa kwa kina, soma vitabu na siyo makala au kuwasikiliza watu wanaokuambia kwa nini ujiunge au usijiunge. Isome teknolojia hii uielewe kwa undani, kisha soma fedha, uchumi na uwekezaji ili kujua namna vitu hivi vinakwenda. Hapo utakuwa umepata mwanga wa kukusaidia kufanya maamuzi sahihi.

2. Kama huwezi kumudu kupoteza fedha.
Pamoja na hatari ya cryptocurrency na bitcoin kwa sasa, bado ni kitu kizuri kujaribu, ila tu, ni rudie, ila tu unamudu kupoteza fedha. Yaani kama una fedha za ziada, ambazo hata ukizipoteza maisha yako hayatayumba, basi unaweza kujaribu aina hii ya uwekezaji.

Lakini kama bado hujafikia hatua ya kuwa na fedha za ziada, kama upo kwenye madeni na unafikiria aina hii ya uwekezaji itakutoa kimaisha, kaa mbali nayo, ni hatari kwako.

Na kama unawaza kwenda kukopa fedha uwekeze kwenye mfumo huu, huna tofauti na mtu anayevuta sigara huku anaweka petroli kwenye gari, siyo hatari kwako tu, bali na kwa wengine pia.

3. Kama umri wako wa kuzalisha fedha umesogea.
Katika kila anguko la uchumi linalotokea duniani, watu wanaoathirika zaidi ni wale ambao umri wao umeenda na hawawezi tena kujitumikisha. Yaani kama umri umeenda, unakaribia kustaafu au umeshastaafu na una fedha zako za mafao, usiziweke kwenye mfumo huu wa fedha za kidijitali. Hata kama unaona kuna nafasi kubwa ya kuongeza kipato hicho, hatari unayochukua ni kubwa sana kwako, na nguvu za kupambana zimeshapungua.

4. Kama elimu pekee uliyonayo ni ya kuambiwa.
Wapo watu ambao wanatoa elimu hizi za cryptocurrency na bitcoin, ila elimu wanayoitoa ni ya kuwaambia watu kwa nini wajiunge na kuwashawishi kwamba ni uwekezaji ambao hawapaswi kuukosa. Kama hii ndiyo elimu ambayo umekuwa unaipata pekee, hujawa tayari kuwekeza. Unahitaji kujifunza kwa kina, faida na hasara, usalama na hatari kwenye uwekezaji huu kabla hujachukua hatua.

5. Kama sababu pekee ya kuwekeza ni kwa sababu wengine wamekuambia ‘wanapiga hela’
Ipo sababu nyingine ambayo naona watu wanaitumia vibaya kuwekeza kwenye mfumo huu mpya wa fedha na malipo. Na sababu hiyo ni kwamba ona wengine wanapata hela. Na watu wanaonesha kweli wanapata fedha, na ni kweli siyo utani. Kama nilivyoeleza, hata pale sarafu hizi zitakapoanguka, wapo watakaonufaika na wapo watakaopoteza.

Sasa unapofikiria kupata tu, jua kwamba kuna kukosa pia. Hivyo ukiangalia wanaonufaika, usiache kuangalia uwezekano wa kukosa.

Rafiki, nimejaribu kukuelezea kwa lugha rahisi na inayoeleweka kuhusu mfumo huu mpya wa fedha za kidijitali, kama nilivyoeleza hii ni sehemu ndogo sana ya elimu kubwa unayopaswa kuwa nayo kama unataka kuwekeza kwenye mfumo huu. Wito wangu kwako ni uendelee kujifunza zaidi na kama una kiasi cha fedha unachoweza kupoteza, unaweza kujaribu kwenye aina hii ya uwekezaji, ukijua kwamba nafasi ya kupoteza ni kubwa kama ilivyo ya kunufaika.

Kila la Kheri Rafiki Yangu.

Rafiki na Kocha wako,

Dr. Makirita Amani,

www.kisimachamaarifa.co.tz/kocha
I have been wondering there has been coinbase and local bitcoin all tradding bitcoins and with extra cryptos in coinbase, Coinbase have their app but I have never heard of local bitcoin app. Is there an app for this site or not.
Provide the link below if you know they have an app or lets discuss on why they don't have an app so far!
 
Braza nakuhakikishia IMF na powerful world banks wakishakubali kuachana na Fiat currencies na kupromote crypto currency ndio tutajua hii kitu inamake sense sana, tukiwa ndani ya JF hatijui trend ya hiz cryptos na jins zinavyorun marketing systems ila huko duniani economists and investors are dancing a crazy trend ya crypto, cryptos zipo catchy sana na zinatrend moto sana!
Let's adjust to the inevitable future, get into crypto, let's meet there!

Sasa mkuu kama watu wanasema ni scam tufanyaje
 
Sasa mkuu kama watu wanasema ni scam tufanyaje
Braza watu hawana elimu (correct information & knowledge) kuhusu e-marketing watu tunataka post/ad ije tusign up tuanze kulipwa bila kujua in detail hicho kitu kinamaanisha nini, kwasababu scammers are everywhere we fall into them due to e-marketing ignorance kumbe tukipunguza papara na kuquestion kila kitu on the way tunaweza kujikuta mbali sana. Unashangaa mtu kaingia kwenye Forex kichwa kichwa bila knowledge ya kutosha anapunwa hela anakuja hapa JF anaanza ooh forex is a scam, mara ohh usipende hela za kudownload, like for real my nigga.?

Bottom line: ukisikia kitu just get yourself satisfied of its ins and outs (truth) , I believe there is a thin line between the rich and the poor, excellence and mediocrity nayo ni principles/routines za kawaida sana ambazo tunazipuuzia kila siku
Kwa mfano: time management, curiousity, passion, endurance, discipline, focus, flexibility and so so so many
 
Habari kubwa katika kipindi hichi kwa upande wa fedha na uwekezaji ni cryptocurrency au kama inavyofahamika kwa Kiswahili fedha za kidijitali. Aina hii ya fedha imewavutia wengi siyo kwa sababu ya matumizi yake, bali kwa jinsi thamani yake inavyokua kwa kasi na hivyo wengi kuona ni sehemu rahisi ya kupata fedha nyingi bila ya kufanya kazi.

Lakini wengi ninaowaona wanakimbizana na fedha hizi za kidijitali, hawana uelewa wa kutosha. Wengi wanadanganywa na kushawishiwa kuingia kwenye kitu ambacho hawakielewi kwa matumaini kwamba watapata fedha nyingi. Ni kweli wapo watakaopata fedha nyingi, na pia wapo ambao watapoteza fedha nyingi kwenye aina hii ya uwekezaji.

Hivyo leo nimechukua muda, kukuandikia wewe rafiki yangu makala hii yenye kila unachopaswa kujua kuhusu cryptocurrency kwa ujumla, na tukiangalia kwa kina zaidi bitcoin ambayo ndiyo currency ya kwanza na yenye thamani kubwa zaidi. Nitachambua hili kwa lugha rahisi ambayo hata kama huna elimu kubwa utaweza kuelewa na kuweza kuchukua hatua.

Lakini kabla sijaingia kwenye kueleza kwa kina fedha hizi za kidijitali, naomba nikushirikishe hadithi tatu muhimu ambazo zitatupa mwanga wa nini kinaendelea.

Moja; TULIP MANIA 1630 – 1637.

Mnamo karne ya 17, kwenye Jamhuri ya Udachi (Dutch Republic), kulitokea hali ambayo haikuwa ya kawaida. Maua yanayojulikana kwa jina la Tulip yalianza kupata umaarufu ghafla. Maua haya yalikuwa na mwonekano mzuri na pia yalikuwa yana changamoto kwenye ulimwaji wake. Hivyo hili lilifanya watu wayathamini sana, na hili likapelekea bei yake kuwa juu. Kadiri bei ilivyokuwa inapanda, ndivyo wengi zaidi waliyataka maua hayo na bei kuzidi kupanda zaidi.

Ilifika wakati, thamani ya ua moja ikawa zaidi ya mara kumi ya kipato cha mwaka cha mfanyakazi wa kawaida kwenye nchi hiyo. Kutokana na kupanda huku thamani kwa maua aina ya Tulip, jamii nzima ilianza kuhamia kwenye maua hayo, ikafika wakati maua haya yakawa yanatumiwa kama fedha, badala ya dhahabu ambayo imekuwa inatumika wakati wote.

Ilifika hatua, watu wakawa wanalipia maua hayo hata kabla hayajakomaa, yaani yakiwa bado shambani. Kufikia Februari mwaka 1637 maua haya ya Tulip yalifikia bei ya juu kabisa na ghafla bei ikaanza kuporomoka. Bei iliporomoka kwa kasi kiasi cha kuyumbisha uchumi wa nchi nzima na watu wengi kupata hasara kubwa. Hii inasemekana kuwa anguko la kwanza la kiuchumi duniani.

tulip-mania-dot-com-bitcoin.png


Mbili; DOTCOM MANIA 1997 – 2001.

Mwishoni mwa miaka ya 1980 jambo kubwa lilitokea duniani ambalo ni matumizi ya mtandao wa intaneti kwa watu wa kawaida. Mwanzoni mwa miaka ya 1990 matumizi ya mtandao wa intaneti yalishika kasi na biashara nyingi zinazohusisha intaneti zilianzishwa.

Kwa kuwa intaneti ilikuwa kitu kipya, na ambacho kilionesha kuwa na nguvu kubwa, watu wengi walivutiwa na biashara zinazohusisha mtandao wa intaneti. Hivyo watu wengi walikimbilia kuanzisha biashara zinazohusisha intaneti. Inasemekana kwamba mwishoni mwa miaka ya 1990 na kuelekea mwaka 2000 watu wengi walikuwa wakiahidi kuanzisha kampuni zitakazokuwa kubwa na watu wakashawishika kuwekeza fedha zao bila hata ya kuwepo kwa ushahidi au uhakika wowote kwamba biashara inayokwenda kuanzishwa itakuwa imara kweli.

Watu waliingiwa na tamaa ya kufaidika haraka kupitia intaneti, kitu ambacho kilipelekea makampuni mengi kuwa na thamani kubwa kuliko uhalisia. Kilichotokea ni uchumi mzima unaohusisha mtandao wa intaneti kuanguka, makampuni mengi kutangaza hasara na watu wengi kupoteza fedha zao.

Tatu; CRYPTO MANIA 2009 - .......

Mwaka 2009, Satoshi Nakamoto, haijulikani kama ni mtu, kikundi cha watu au taasisi, alikuja na wazo la tofauti kwenye mfumo wa fedha. Kama ambavyo wote tunajua, mzunguko wa fedha umekuwa unadhibitiwa na benki kuu ya nchi husika. Kwa mfano mzunguko wa shilingi ya Tanzania, unadhibitiwa na Benki Kuu ya Tanzania. Hivyo miamala yoyote ya kifedha lazima iweze kufuatiliwa na benki kuu. Satoshi ali/walipendekeza mfumo wa kuondoa udhibiti huo. Badala ya mzunguko wa fedha kudhibitiwa na mtu mwingine, udhibitiwe na watu wawili tu, anayelipa na anayelipwa.

Mfumo huu ulionekana ni mkombozi kwa matatizo mengi ya kifedha, ambayo yapo wazi, mfano nchi kuchapa fedha na hivyo mfumuko wa bei kuwa mkubwa, gharama za kufanya miamala na hata usalama kuwa mdogo, kama ambavyo tumekuwa tunasikia fedha feki kuwepo kwenye mzunguko. Mfumo wa Satoshi ulionekana ni bora kabisa, lakini wengi wakawa na wasiwasi kwamba ni mgumu kueleweka na kutumika.

Hivyo mwaka 2009 Satoshi ali/walikuja na mfumo wa fedha ya kidijitali uliokwenda kwa jina la Bitcoin. Hii ilikuwa sarafu ya kwanza kabisa ya kidijitali, ambayo ilikuwa na lengo la kurudisha udhibiti na usalama wa fedha kwa watumiaji.

Kwa kipindi cha mwaka 2009 thamani ya bitcoin moja ilikuwa dola 0.0001 ambayo kwa kipindi hicho, dola moja ilikuwa tsh 1330, hivyo bitcoin moja ilikuwa sawa na tsh 1 na senti 33. Mpaka kufika mwaka 2010, bado thamani ya bitcoin moja ilikuwa chini ya dola moja. Kuanzia mwaka 2011 bei ya bitcoin imekuwa inaongezeka kidogo kidogo, kutoka dola mia na kuendelea. Mpaka kufika januari 2017, bei ya bitcoin moja ilikuwa chini ya dola elfu moja. Lakini baada ya hapo bei ilianza kuongezeka kwa kasi, kufika oktoba 2017, bei ya bitcoin moja ilikuwa dola elfu 5.

bitcoin-june-2009.png


Tarehe 17 mwezi disemba 2017 ndiyo ilikuwa siku ambayo thamani ya bitcoin ilikuwa juu sana, ambapo bitcoin moja ilikuwa sawa na dola elfu 19. Yaani sawa na zaidi ya shilingi milioni 40. Hebu fikiria hapo, kwamba kama mwaka 2009, ungepata nafasi ya kununua bitcoin moja kwa shilingi moja, mwaka 2017 ungekuwa na zaidi ya milioni 40!

Kwa nini hadithi hizi tatu?

Hadithi hizi tatu zinatufundisha kitu kimoja muhimu sana kwenye fedha na uwekezaji, kwamba mara nyingi tamaa ya watu ikishaingia kwenye kitu, thamani inapanda kuliko uhalisia, kitu ambacho kinatengeneza anguko baadaye. Ilitokea kwa maua ya Tulip, ilitokea kwa biashara za Dotcom na itatokea kwenye cryptocurrency kama ambavyo nitakueleza hapo chini.

Ili tuweze kuweza kuelewana vizuri, na kwa kuwa yapo mengi ya kujifunza kuhusu fedha hizi za kidijitali, tutakwenda kwa mfumo wa maswali na majibu.

Swali; bitcoin ni nini?

Jibu; bitcoin ni mfumo wa malipo wa kielektroniki ambao ni wa moja kwa moja kati ya mlipwaji na mlipaji bila ya kuhusisha upande wa tatu kama benki serikali na taasisi nyingine za kifedha.

Swali; mfumo huu unafanyaje kazi?

Jibu; kunakuwa na sarafu za kidijitali, ambazo zina idadi yanye ukomo. Sarafu hizi ndiyo zinazotumika kama thamani ya malipo. mfumo mzima ni wa kielektroniki na hivyo hakuna sarafu yoyote ya kawaida inayohusika. Badala yake mfumo wa kompyuta unaotoa na kudhibiti sarafu hizi ndiyo unaotumika.

Swali; zipi faida na ubora wa mfumo huu mpya wa malipo?

Mfumo wa kawaida wa fedha una changamoto nyingi ambazo tumekuwa tunaziona kila wakati. Sehemu kubwa ya changamoto hizo inaweza kutatiliwa na mfumo huu wa fedha za kidijitali.

Changamoto ya mfumuko wa bei ambayo imekuwa inasababishwa na serikali kuchapa fedha na hivyo kushusha thamani, unadhibitiwa na uwepo wa kiwango kamili cha sarafu za kidijitali. Kwa mfano kwa Bitcoin kuna sarafu 21,000,000 pekee, zikiisha hizo hakuna nyingine zinazoweza kuzalishwa na hivyo mfumuko wa bei hauwezi kutokea.

Changamoto ya usiri imetatuliwa na mfumo huu mpya kwa kufanya muamala kuwa baina ya watu wawili pekee. Katika mfumo wa kawaida, utamlipa mtu kwa njia ya benki, fedha taslimu au njia za mitandao, ambazo zote hazina usiri.

Changamoto ya gharama za miamala imeondolewa sana na mfumo huu, kwa mfumo wa kawaida, kila unapohamisha fedha eneo moja kwenda eneo jingine unakatwa malipo, na hii ni kwa sababu taasisi nyingi zinahusika. Lakini kwenye mfumo huu, hakuna uhusishaji wa taasisi nyingi, hivyo makato hakuna.

Changamoto ya usalama, tunajua namna ambavyo kuwa na kiasi kikubwa cha fedha ni hatari, pia hata benki siyo salama sana kuweka fedha. Kwa mfumo huu wa fedha wa kidijitali, usalama ni mkubwa, program ya kompyuta inayotumika kudhibiti mfumo huu ni dhabiti sana na haiwezi kuchezewa.

Changamoto ya fedha feki imedhibitiwa na mfumo huu. Kwa kila aina ya sarafu, kwenye mzunguko huwa kunakuwa na fedha feki nyingi. Lakini kwa mfumo huu wa fedha za kidijitali, hakuna namna ya kutengeneza sarafu feki.

Swali; je kuna sarafu za aina ngapi kwenye fedha hizi za kidijitali?

Jibu; Watu wengi wanajua zile sarafu kubwa za kidijitali kama Bitcoin, Ethereum, Ripple, Bitcoin Cash, Cardano, na Litecoin. Lakini mpaka kufika mwezi february 2018 kulikuwa na sarafu za kidijitali zaidi ya 1400, na orodha inaendelea kukua kila siku, kwa sababu yeyote anaweza kuja na sarafu mpya.

Swali; je cryptocurrency utakuwa mfumo kamili wa malipo?

Jibu ni ndiyo, lakini siyo sasa ni kwa baadaye. Lakini pia kama utakuwa mfumo mkuu wa malipo, basi kila serikali itatengeneza mfumo wake wa malipo kwa njia hiyo ya kidijitali. Hakuna serikali inayoweza kukubali kupoteza udhibiti wa fedha, kitu pekee kinafanya serikali ziwepo, tangu enzi za utawala wa roma, ni udhibiti wa fedha, na enzi hizo, dhahabu.

Swali; je Bitcoin itakuja kuwa sarafu ya dunia na kutumiwa na kila mtu?

Jibu ni hapana, Bitcoin imekosa sifa zote za sarafu ya kutumiwa na uma, kwa sababu thamani yake haijatulia, inapanda na kushuka kwa kasi mno. Pia watu wengi wameshaihodhi na hivyo uwezekano wa kutumiwa na kila mtu ni mdogo.

Swali; je soko zima la fedha hizi za kidijitali litaanguka?

Hapa ndipo muhimu sana unapaswa kuelewa. Kwa hizi sarafu nyingi, ukiangalia zilianza na thamani kidogo sana. mfano bitcoin kwa mwaka 2009 na 2010 thamani yake ilikuwa chini ya dola moja. Lakini baada ya watu kuisikia ilianza kupanda thamani na kufikia disemba 2017 ilifikia thamani ya juu kabisa ya sarafu moja kuwa dola elfu 19. Lakini baada ya hapo imekuwa unashuka na kupanda.

Ukuaji huu wa thamani ya sarafu hizi za kidijitali siyo wa kawaida, na unachochewa na tamaa ya watu kuona ni njia ya haraka ya kutengeneza utajiri. Tamaa hii itapelekea sarafu nyingi kuanguka na baada ya hapo zitasimama sarafu imara na ambazo thamani yake inaendana na hali ya uchumi.

Kama ambavyo TULIP ilianguka, na kama DOTCOM ilivyoanguka, CRYPTOCURRENCY pia itaanguka, lakini baada ya hapo zitaibuka sarafu ambazo ni imara na zenye thamani inayoendana na uchumi. Anguko la CRYPTOCURRENCY litawaumiza wengi sana na kuwanufaisha wachache.

[caption id="attachment_4407" align="alignnone" width="800"]
coindesk-bpi-chart1.jpeg
Kwa kipindi cha mwaka mmoja kati ya machi 2017 mpaka mashi 2018, thamani ya bitcoin imeongezeka kutoka chini ya dola elfu moja mpaka dila elfu kumi na tisa. Ni ongezeko ambalo haliwezi kuelezewa vyovyote vile kiuchumi.[/caption]

Swali; je kuna matumizi mengine ya teknolojia hii ukiacha malipo?

Teknolojia iliyopo nyuma ya sarafu hizi za kidijitali, ambayo ni BLOCKCHAIN ina matumizi mengine mengi na makubwa. Mfano inatumika kwenye kuandaa mikataba ya kidijitali, inatumika kwenye kutunza kumbukumbu za siri na kwenye usimamizi na udhibiti wa uwekezaji. Teknolojia ya blockchain inaweza kutumika kwenye kila eneo linalohitaji ufuatiliaji na udhibiti wa hali ya juu, kama kwenye afya, benki, makusanyo ya mapato na kadhalika.

Kwa nini BITCOIN siyo uwekezaji sahihi kwako kufanya kwa sasa?

Mpaka kufika hapa nina imani umeanza kupata picha ya hichi kitu kinachoitwa CRYPTOCURRENCY ni nini, kwamba ni mfumo wa malipo wa kidijitali ambao ni wa moja kwa moja na unaepuka changamoto nyingi za mfumo wa kawaida wa fedha. Pia utakuwa umejua BITCOIN ni moja kati ya sarafu zaidi ya elfu moja ambazo zinatumia mfumo huu. Kwa kipindi hichi BITCOIN ndiyo sarafu yenye thamani kubwa.

Sasa nimalize kwa kukuambia kwa nini BITCOIN siyo uwekezaji sahihi kwako kufanya kwa sasa.

Watu wengi wanahamasishwa sana kuwekeza kwa kununua bitcoin hasa pale ambapo thamani yake ilikuwa inapanda kwa kasi ya ajabu. Lakini wengi ambao wamekuwa wanatamani kuwekeza kwenye mfumo huu, hawapo tayari. Hapa nitataja makundi matano na kama upo kwenye moja ya makundi hayo usiwekeze kwenye cryptocurrency na bitcoin, badala yake endelea na uwekezaji wa kawaida ambao ni salama kidogo ukilinganisha na huu kwa sasa.

1. Kama ndiyo umeielewa cryptocurrency na bitcoin leo, jipe muda wa kujifunza.
Nilichokushirikisha hapa kuhusu cryptocurrency na bitcoin ni kama tone tu la bahari ambayo unapaswa kuelewa kuhusu mfumo huu wa fedha na malipo. Hivyo kama umekuwa unasikia sikia kuhusu hizo bitcoin lakini leo ndiyo umeanza kupata picha basi huu siyo uwekezaji mzuri kwako kwa sasa.

Pendekezo langu ni chukua muda kusoma na kuelewa kwa kina, soma vitabu na siyo makala au kuwasikiliza watu wanaokuambia kwa nini ujiunge au usijiunge. Isome teknolojia hii uielewe kwa undani, kisha soma fedha, uchumi na uwekezaji ili kujua namna vitu hivi vinakwenda. Hapo utakuwa umepata mwanga wa kukusaidia kufanya maamuzi sahihi.

2. Kama huwezi kumudu kupoteza fedha.
Pamoja na hatari ya cryptocurrency na bitcoin kwa sasa, bado ni kitu kizuri kujaribu, ila tu, ni rudie, ila tu unamudu kupoteza fedha. Yaani kama una fedha za ziada, ambazo hata ukizipoteza maisha yako hayatayumba, basi unaweza kujaribu aina hii ya uwekezaji.

Lakini kama bado hujafikia hatua ya kuwa na fedha za ziada, kama upo kwenye madeni na unafikiria aina hii ya uwekezaji itakutoa kimaisha, kaa mbali nayo, ni hatari kwako.

Na kama unawaza kwenda kukopa fedha uwekeze kwenye mfumo huu, huna tofauti na mtu anayevuta sigara huku anaweka petroli kwenye gari, siyo hatari kwako tu, bali na kwa wengine pia.

3. Kama umri wako wa kuzalisha fedha umesogea.
Katika kila anguko la uchumi linalotokea duniani, watu wanaoathirika zaidi ni wale ambao umri wao umeenda na hawawezi tena kujitumikisha. Yaani kama umri umeenda, unakaribia kustaafu au umeshastaafu na una fedha zako za mafao, usiziweke kwenye mfumo huu wa fedha za kidijitali. Hata kama unaona kuna nafasi kubwa ya kuongeza kipato hicho, hatari unayochukua ni kubwa sana kwako, na nguvu za kupambana zimeshapungua.

4. Kama elimu pekee uliyonayo ni ya kuambiwa.
Wapo watu ambao wanatoa elimu hizi za cryptocurrency na bitcoin, ila elimu wanayoitoa ni ya kuwaambia watu kwa nini wajiunge na kuwashawishi kwamba ni uwekezaji ambao hawapaswi kuukosa. Kama hii ndiyo elimu ambayo umekuwa unaipata pekee, hujawa tayari kuwekeza. Unahitaji kujifunza kwa kina, faida na hasara, usalama na hatari kwenye uwekezaji huu kabla hujachukua hatua.

5. Kama sababu pekee ya kuwekeza ni kwa sababu wengine wamekuambia ‘wanapiga hela’
Ipo sababu nyingine ambayo naona watu wanaitumia vibaya kuwekeza kwenye mfumo huu mpya wa fedha na malipo. Na sababu hiyo ni kwamba ona wengine wanapata hela. Na watu wanaonesha kweli wanapata fedha, na ni kweli siyo utani. Kama nilivyoeleza, hata pale sarafu hizi zitakapoanguka, wapo watakaonufaika na wapo watakaopoteza.

Sasa unapofikiria kupata tu, jua kwamba kuna kukosa pia. Hivyo ukiangalia wanaonufaika, usiache kuangalia uwezekano wa kukosa.

Rafiki, nimejaribu kukuelezea kwa lugha rahisi na inayoeleweka kuhusu mfumo huu mpya wa fedha za kidijitali, kama nilivyoeleza hii ni sehemu ndogo sana ya elimu kubwa unayopaswa kuwa nayo kama unataka kuwekeza kwenye mfumo huu. Wito wangu kwako ni uendelee kujifunza zaidi na kama una kiasi cha fedha unachoweza kupoteza, unaweza kujaribu kwenye aina hii ya uwekezaji, ukijua kwamba nafasi ya kupoteza ni kubwa kama ilivyo ya kunufaika.

Kila la Kheri Rafiki Yangu.

Rafiki na Kocha wako,

Dr. Makirita Amani,

www.kisimachamaarifa.co.tz/kocha
Hii story yako is obsele today
Laiti kama ningelijua zamani, nigekuwa naongea lugha nyingine
Lakini hujachelewa kama ukianza sasa, dunia inaenda kasi mno...........
 
Braza nakuhakikishia IMF na powerful world banks wakishakubali kuachana na Fiat currencies na kupromote crypto currency ndio tutajua hii kitu inamake sense sana, tukiwa ndani ya JF hatijui trend ya hiz cryptos na jins zinavyorun marketing systems ila huko duniani economists and investors are dancing a crazy trend ya crypto, cryptos zipo catchy sana na zinatrend moto sana!
Let's adjust to the inevitable future, get into crypto, let's meet there!
Mkuu hii crypto haitaweza kuja kuwa major means of exchange sababu ni limited
 
Mkuu hii crypto haitaweza kuja kuwa major means of exchange sababu ni limited
Ipo limited kivipi, wewe ndio umeshikilia future na akili za watu, kuna masterminds duniani hapa science has never had. future is very unpredictable, people can flip things in very unpredictable ways. Hapa nimeongelea generally tu kwamba what you believe or percieve right now on some aspects can be modified or just naturally change in astonishing ways in few decades to come.
 
Mkuu hii crypto haitaweza kuja kuwa major means of exchange sababu ni limited
By the way adoption ya cryptocurrency haiwezi kuchukua muda mfupi though, mega revolutions kama hiz zinapitia turbulent periods before they stabilize and totally get embodied in human lives.
 
Acha majibu ya ngebe kijana..nilidhani una kitu utaelewa kumbe unamangangamanga tu juu ya hii technology adhimu. Unadhani unaijua Cryptocurrency vizuri kuzidi team ya financial advisor wa bill gate? Iliyomshauri awekeze mamilion kwenye Bitcoin? Na other altcoins?

Punde nitaandika hapa kidogo simple but informative kuihusu Bitcoin achana na maessay yako ya kizamani marefu kama tamthilia ya isidingo.

Nimepitia makala zako nyingi yenye replies nyingi ni 69 zingine zote hazifiki reply 20. Kwanini unaandika kizamani wewe kocha sijui kocha wa timu gani? Ukitaka kuandika makala ndefu jifunze skills and techniques za modern writings zenye kuvutia na kuchochea hamu ya kuendelea kusoma article kuna watu kibao hapa bongo wanaondika makala simple zenye namna ya kukufanya uendelee kusoma andishi husika hadi mwisho bila kujalisha content ikoje. Kocha ukiendelea kuandika kama mwandishi wa Rai au Mzalendo ya mwaka 47 utajikuta unasoma na kujijibu mwenyewe thread zako hapa JF maana you don't fit in this Era readers world.
Una wivu Boss
 
Msaada wenu wadau nataka ninunue coin, wallet ipi inafaa kutunzia, pia niomba maelekezo ya jinsi ya kununua coin.
 
Acha majibu ya ngebe kijana..nilidhani una kitu utaelewa kumbe unamangangamanga tu juu ya hii technology adhimu. Unadhani unaijua Cryptocurrency vizuri kuzidi team ya financial advisor wa bill gate? Iliyomshauri awekeze mamilion kwenye Bitcoin? Na other altcoins?

Punde nitaandika hapa kidogo simple but informative kuihusu Bitcoin achana na maessay yako ya kizamani marefu kama tamthilia ya isidingo.

Nimepitia makala zako nyingi yenye replies nyingi ni 69 zingine zote hazifiki reply 20. Kwanini unaandika kizamani wewe kocha sijui kocha wa timu gani? Ukitaka kuandika makala ndefu jifunze skills and techniques za modern writings zenye kuvutia na kuchochea hamu ya kuendelea kusoma article kuna watu kibao hapa bongo wanaondika makala simple zenye namna ya kukufanya uendelee kusoma andishi husika hadi mwisho bila kujalisha content ikoje. Kocha ukiendelea kuandika kama mwandishi wa Rai au Mzalendo ya mwaka 47 utajikuta unasoma na kujijibu mwenyewe thread zako hapa JF maana you don't fit in this Era readers world.
Mie nikujibu hapo kuwa wewe ni Bora kuliko team ya Bill gate iliyomshauri awekeze huko.
Iko hivi hii game hakuna mwamba ama Mungu wa hili game la financial instruments.
Unawajua Lehman Brothers walipoteza Billions ngapi wakafilisika mkuu.
Unaijua stocks ya Northern Rocks ikitokea Nini.
All in all is ol about probabilities and managing risk. Reward and risk are two sides of coin.
 
Back
Top Bottom