Kila kitu bongo kipo tofauti

Kwame Nkrumah

JF-Expert Member
Dec 2, 2008
886
376
Sijazunguka sana dunia hii, lakini katika nchi mbili tatu zilizoendelea nilizobatika kupita nimeona kuna tofauti kubwa katika baadhi ya taratibu na namna nchi hizi zinavyoendeshwa na nyumbani. Kama una tofauti nyingine umeona au mambo yanayofanana tufahamishe pia.

1. Kazi za serikalini katika nchi hizi ni kazi za wito.Watu huenda serikalini kuhudumia jamii. Watu wanalipwa hela ambayo kwa mtu wa sekta binafsi ni some changes in the pocket.
Kwa nyumbani serikalini ndiyo sehemu ya kuibuka na utajiri, dili za kifisadi kila mahali, Polisi, TRA, Mawizarani n.k

2. Nchi zilizoendelea viongozi ni WATUMISHI, wametumwa kutumikia wananchi.Wanakaa ofisini na kufanya kazi.
Sisi viongozi ni semi-gods, wasemalo ndiyo sheria. Hawapo ofisini kila mara ukienda unaambiwa njoo kesho.

3. Asilimia 90 ya magari ya serikali utakayoyaona ni magari ya huduma kwa wananchi kama vile kuzoa taka, magari ya polisi, ujenzi wa barabara,fire brigades au snow cleaning kama ni sehemu ya winter kali.
Sisi asilimia 90 ya magari ya serikali ni magari ya kupeleka viongozi kazini, kupeleka watoto wa boss shule, mke wa mkurugenzi saloon na kubebea majani ya ng'ombe wa meneja.

3. Bunge ni chachu ya maendeleo.
Kazi ya bunge letu ni "kushauri" serikali. Kila mbunge anayesimama anasema "mimi namshauri waziri......" na kupiga mihuri kila kiletwacho na chama tawala.

4. Wageni wanaheshimu sana sheria za nchi husika.
Kwetu wageni ni "superior" kuliko sisi.Watapewa ardhi mara moja, watapewa kazi nzuri na kwa haraka sana, bila hata vibali vya kazi. Wakati huohuo wazalendo wakiitwa bungeni wezi na Waziri wa Kazi. Wageni watapewa madini na kutuachia mashimo, watatesa na hata kuua raia.

5.Benki zinabembeleza wateja kuchukua mikopo.
KwetU tunabembeleza benki kutupa mikopo.

6. Vyombo vya usalama vina nguvu za kisheria kumchunguza kila mtu. Hakuna mtu ambaye hagusiki. Sheria ni msumeno kwa kila mtu.
Nyumbani utaanzia wapi? Akina yakhe ndiyo tumejaa Keko, Isanga na kule Zanzibar kwenye vyuo vya mafunzo.

7.Cabinet ni ndogo na maendeleo yao tunayaona.
Sisi Cabinet ni kubwa. Ufanisi close to zero.

8. Malalamiko na kashfa mbalimbali huchunguzwa kwa kina na kutolewa majibu mara moja.
Sisi licha ya malalamiko chungu mzima, kwa mifano tu ya Bandari, Airport na Ardhi.hamna hatua yoyote inayochukuliwa. Sana sana ni mkuu wa kitengo kinacholalamikiwa kuongezewa madaraka.

9.Watu wanaoongoza vita dhidi ya mafisadi [ yes, wao pia wana mafisadi], kutetea haki na kusimamia sheria ni mashujaa na wanaheshimiwa na nchi na kuenziwa.
Kwetu watu hawa ni maadui wa umoja, wanataka kuvunja amani na kuigawa nchi.

10.Wananchi wanapiga kura kwa kupewa sera na njia mbadala za kutatua changamoto mbalimbali zinazoikabili jamii husika.
Kwetu sisi wananchi tunachagua viongozi kwa kufuata nani alitupa fulana na kanga nyingi na kupika pilau kushinda mgombea mwingine. shame on us wananchi !!!

11. Wananchi kupata habari ni haki ya kikatiba, a very deep, enshrined and cherished aspect of life.
Sisi kupata habari ni kwa kudra tu.

12. Ukiona ajira inatangazwa gazetini ujue nafasi kweli ipo.
Kwetu ukiona hivyo ujue tayari shemeji wa Mkurugenzi ameishaajiriwa toka mwezi uliopita na tayari yupo nje ya nchi kwenye semina.

13.Wanajeshi wanaheshimiwa, kupendwa na kuenziwa kwa mapenzi waliyonayo kwa nchi yao hata kujitoa kujiunga na jeshi.
Wanajeshi wetu ni maarufu kwa kupiga raia.
 
Unashangaa hayo tu?

Mbwa Bongo ana njaa kiasi kwamba bosi akijisaidia mbwa wake "anazoa" kinyesi; majuu mbwa akijisaidia bosi wake anazoa kinyesi.
 
Sijazunguka sana dunia hii, lakini katika nchi mbili tatu zilizoendelea nilizobatika kupita nimeona kuna tofauti kubwa katika baadhi ya taratibu na namna nchi hizi zinavyoendeshwa na nyumbani. Kama una tofauti nyingine umeona au mambo yanayofanana tufahamishe pia.

Ni kweli kabisa kila kitu tofauti bongo, hebu tusaidie tufanye nini??
 
Ni kweli kabisa kila kitu tofauti bongo, hebu tusaidie tufanye nini??

Simple, Kila kitu kinacholalamikiwa do the opposite. Kwa mfano kama wananchi wanalalamika Wakenya wanapewa kazi sana, dawa yake ni kuwapa kazi WaTZ badala ya wageni unless WaTZ hawana ujuzi na kazi hiyo. Kama wananchi wanalalamika Vigogo hawafikishwi mahakamani, dawa yake ni kufikisha vigogo katika mahakama huru na yenye kutenda haki.
 
Simple, Kila kitu kinacholalamikiwa do the opposite. Kwa mfano kama wananchi wanalalamika Wakenya wanapewa kazi sana, dawa yake ni kuwapa kazi WaTZ badala ya wageni unless WaTZ hawana ujuzi na kazi hiyo. Kama wananchi wanalalamika Vigogo hawafikishwi mahakamani, dawa yake ni kufikisha vigogo katika mahakama huru na yenye kutenda haki.

Thanks Kwame, play your part!!!
 
wananchi kweli tumechoka sana tu.....frankly kila nikiona picha ya muungwana nasikia kutapika.....
 
Tatizo kubwa tililonalo sisi Waafrika, ni kwamba hatuwezi kujitawala wenyewe. Kama Mzungu akituongoza; basi tunakuwa na maendeleo zaidi kuliko tukijiongoza wenyewe.
 
Tatizo kubwa tililonalo sisi Waafrika, ni kwamba hatuwezi kujitawala wenyewe. Kama Mzungu akituongoza; basi tunakuwa na maendeleo zaidi kuliko tukijiongoza wenyewe.

Uwezo wa kujitawala na kuleta maendeleo tunao tena mkubwa sana. Kinachofanya nchi zilizoendelea kuendelea kuchupa ni "TRUE DEMOCRACY" katika kupata uongozi wa nchi. Kama Africa na hasa Tanzania ingekuwa na vyombo huru vya kusimamia haki kuanzi ile ya kuchagua, mahakama, polisi et al. Tungeshuhudia yule aliyepo madarakani kufanya kila awezalo kutumikia wananchi kwa kuhofia kuwa voted out pindi uchaguzi unapowadia. Democracy ina "DOMINO" effect kwani Wananchi watamwajibisha rais, rais naye anawawajibisha watendaji wake na watendaji nao watafanya kazi kwa juhudi ili wananchi wasione hawahudumiwi na hivyo kumuwajibisha rais ambaye ni bosi wao.

Mfumo uliopo sasa kwenye nchi nyingi kama Tanzania wa chama kimoja ndiyo unaua maendeleo, kwani uchaguzi huru upo ndani ya CCM katika kupata wagombea, baada ya hapo ni kanyaboya la tume na UWT kupanga matokeo. Maendeleo tuyasahau kwani viongozi pia wamejisahau kwa kuwa kila kitu kipo upande wao, wamuhofie nani?
 
Tatizo letu ni mfumo wa siasa zetu, ulijenga hofu sana kwa wananchi na kuwafanya watawala kuwa miungu.

Mfumo wetu wa utawala uliwafanya watawala wawe na nafasi ya ku manipulate systems kwa maslahi yao, hence a lot of mind games and misuse of powers.

Ujinga, elimu ya siasa ilikuwa na ipo kwa manufaa ya kuwakweza watawala na sio kuwafunua waelimishwaji. Waelimishwaji wanakaririshwa mpaka soli za viatu wanavyovaa watawala. na kwamba watawala ni previleged people, hivyo waliiba na kurundika mali kwao tunawapigia makofi.

Mpaka watanzania watakapo kubali kutake a bit of risk, for a short term, hali haitabadilika. Mie na wewe lazima tubalishe watawala wabovu:

1. kwa kusema ukweli na kukemea maovu tunayoyaona kwa wazi, bila haya wala woga,
2. kwa kuwadhamini kugombea nafasi za uongozi wale tunaoona wanafaa,
3. na pia kwa kugombea sisi wenyewe, pale tunapopima kuwa tunaweza kufanikiwa.

Motive isiwe kutafuta mali au cheo, bali iwe ni corrective measure ya siasa na utawala. Tuanzie mahali kurekebisha, naamini inawezekana.

Kwa mfano: Mpaka sasa katika jimbo au sehemu unayotoka umeshaanza kuangalia nani anafaa kushika hatamu? umefanya nini ili wengine wajue mawazo na sababu za wewe kutaka mtawala au kiongozi aliyepo abadilishwe?

Je watu wanaokuzunguka wanajua msimamo wako wa siasa za bongo? au ndio bendera fuata upepo? Tulifanya makosa sana kujivuta kwenye siasa tukawaachia wajinga watawale, kuanzia serikali za mitaa mpaka taifa!

Correction time is now, play your part!
 
Tatizo kubwa tililonalo sisi Waafrika, ni kwamba hatuwezi kujitawala wenyewe. Kama Mzungu akituongoza; basi tunakuwa na maendeleo zaidi kuliko tukijiongoza wenyewe.

Mimi nafikiri ni viongozi waliopo madarakani sasa hivi, sidhani kama ni waafrika wote wapo hivyo. Kuna mifano hai ya nchi za Kiafrika ambazo zinaongozwa na waafrika na nchi hizi ni mfano wa kuigwa. Rwanda, Botswana ni nchi zinazofaa kuigwa. Mozambique nayo inakuja kwa kasi. Swali ni kwamba kama viongozi waliopo hawafai kwa nini wapo madarakani ?
 
Tatizo letu ni mfumo wa siasa zetu, ulijenga hofu sana kwa wananchi na kuwafanya watawala kuwa miungu.

Mfumo wetu wa utawala uliwafanya watawala wawe na nafasi ya ku manipulate systems kwa maslahi yao, hence a lot of mind games and misuse of powers.

Ujinga, elimu ya siasa ilikuwa na ipo kwa manufaa ya kuwakweza watawala na sio kuwafunua waelimishwaji. Waelimishwaji wanakaririshwa mpaka soli za viatu wanavyovaa watawala. na kwamba watawala ni previleged people, hivyo waliiba na kurundika mali kwao tunawapigia makofi.

Mpaka watanzania watakapo kubali kutake a bit of risk, for a short term, hali haitabadilika. Mie na wewe lazima tubalishe watawala wabovu:

1. kwa kusema ukweli na kukemea maovu tunayoyaona kwa wazi, bila haya wala woga,
2. kwa kuwadhamini kugombea nafasi za uongozi wale tunaoona wanafaa,
3. na pia kwa kugombea sisi wenyewe, pale tunapopima kuwa tunaweza kufanikiwa.

Motive isiwe kutafuta mali au cheo, bali iwe ni corrective measure ya siasa na utawala. Tuanzie mahali kurekebisha, naamini inawezekana.

Kwa mfano: Mpaka sasa katika jimbo au sehemu unayotoka umeshaanza kuangalia nani anafaa kushika hatamu? umefanya nini ili wengine wajue mawazo na sababu za wewe kutaka mtawala au kiongozi aliyepo abadilishwe?

Je watu wanaokuzunguka wanajua msimamo wako wa siasa za bongo? au ndio bendera fuata upepo? Tulifanya makosa sana kujivuta kwenye siasa tukawaachia wajinga watawale, kuanzia serikali za mitaa mpaka taifa!

Correction time is now, play your part!

Kitu kingine ambacho ni kinyume sana nyumbani ni rushwa kwa polisi. Nchi zingine ukimpa polisi rushwa, au hata ukijaribu tu kutoa rushwa utaozea jela.
Sisi usipompa Polisi rushwa utaozea jela !!
Njia moja rahisi for us to play our part, na isiyohitaji resources nyingi ni
Kwa mimi na wewe kukataa kutoa rushwa.
 
Unasema "Kila kitu bongo tofauti". Mi nasema: "Kila kitu Bongo tambarare". They call it "Bongo state of mind". :rolleyes:
 
Mkuu umesema ukweli mtupu.

Katika nchi za wenzetu raia wanajua haki na wajibu wao kwa serikali and vice versa.

Bongo wengi wetu tupotupo tu tunaishi ili mradi sukuma twende hatua malengo wala mwelekeo. Hatuna uzalendo kwa kwa nchi na rasilimali zake ndio maana ufisadi na rushwa vimeota mizizi kila kona.

Bongo wengi wetu tumejibweteka na kusubiri serikali kutufanyia kila kitu (pengine kutujengea hadi vyoo) badala ya sisi kushirikiana na serikali katika kujiletea maendeleo.

Bongo wengi wetu hatufuati sheria za nchi wala taratibu tulizojiwekea hali inayofanya kila mtu atake kuwa juu ya sheria.

Wabongo tumejenga hulka mbaya sana ya kutokujali mstakabali wa nchi, wengi wetu ni wala rushwa, wapindishaji sheria n.k.

Bongo uswahiba mwingi kila mahali ni technical know who na sio technical know how!

Ni hadi pale tutakapobadilika na kuwajibika ipasavyo, kukubali kuwajibishwa, kufuata sheria za nchi, kuacha ubinafsi + uswahiba na kuchagua viongozi kutokana na uwajibikaji wao ndipo tutakapotoka kwenye lindi na umasikini.
 
Unashangaa hayo tu?

Mbwa Bongo ana njaa kiasi kwamba bosi akijisaidia mbwa wake "anazoa" kinyesi; majuu mbwa akijisaidia bosi wake anazoa kinyesi.

Tumeendelea sana Bongo kama mbwa wanaweza kusafisha kinyesi.....nafikiri wanahitaji mafunzo zaidi ili wa-vacuum clean maofisi, aahaha aahaha teh teh teh
 
Sijazunguka sana dunia hii, lakini katika nchi mbili tatu zilizoendelea nilizobatika kupita nimeona kuna tofauti kubwa katika baadhi ya taratibu na namna nchi hizi zinavyoendeshwa na nyumbani. Kama una tofauti nyingine umeona au mambo yanayofanana tufahamishe pia.

1. Kazi za serikalini katika nchi hizi ni kazi za wito.Watu huenda serikalini kuhudumia jamii. Watu wanalipwa hela ambayo kwa mtu wa sekta binafsi ni some changes in the pocket.
Kwa nyumbani serikalini ndiyo sehemu ya kuibuka na utajiri, dili za kifisadi kila mahali, Polisi, TRA, Mawizarani n.k

Sijui nchi hiyo uliyotembelea. Lakini ktk nchi nyingine serikali haiajiri watu bogus. Inaajiri top creams ktk fani mbalimbali na kuwalipa vizuri, na ndio maana wana-deliver na nchi zao zinasonga mbele kwa mbele. Hoja kuwa kazi ktk serikali ya Tz ni wito ni kansa inayosababisha serikali kuajiri watu bogus na kuwalipa mafao finyu, na in return hao wafanyakazi ambao wengi ni bogus kwa kulipwa peanuts wanageuza maeneo yao ya kazi kuwa vilinge vya rushwa ili kulipizia nakisi ya gharama za maisha.

Huu ni muono wangu.
 
Sijui nchi hiyo uliyotembelea. Lakini ktk nchi nyingine serikali haiajiri watu bogus. Inaajiri top creams ktk fani mbalimbali na kuwalipa vizuri, na ndio maana wana-deliver na nchi zao zinasonga mbele kwa mbele. Hoja kuwa kazi ktk serikali ya Tz ni wito ni kansa inayosababisha serikali kuajiri watu bogus na kuwalipa mafao finyu, na in return hao wafanyakazi ambao wengi ni bogus kwa kulipwa peanuts wanageuza maeneo yao ya kazi kuwa vilinge vya rushwa ili kulipizia nakisi ya gharama za maisha.

Huu ni muono wangu.

Hili swali Nyani Ngabu huwa anajibu vizuri sana. Ni kweli kama intention ni money making, serikalini si sehemu ya kufanya kazi. Hivyo ndivyo kwenye nchi za wenye akili wanavyofanya. Kina Bill Gates na Ruppert walikuwa na uwezo mubwa sana wa kufanya kazi serikalini, no one can doubt kuwa wao ni cream kwenye fani zao lakini walichagua kutengeneza hela.

Huku kwetu watu wanaacha taaluma zao wanaingia kwenye siasa au kutafuta kazi zinazwapa opportunity ya kuiba pesa za serikali. Huu ni ukweli usiofichika. Ukiangalia nini wamefanya tangu waingie kwenye ofisi zao hutaona. Lakini angalia magari mangapi wamenunua, angalia akaunti zao za nje, angalia wanavyojirusha utaona kuwa hawakuingia kazini kwa lengo la kufanya kzai ila kuiba.
 
-Nchi za watu huwezi kumtuma mtoto kununua beer au sigara, na mtu mzima ukienda kununua hivyo vitu lazima uonyeshe ID yako ambayo ina picha yako na mwaka wa kuzaliwa.
Kwetu beer na sigara unajinunulia tu hakuna ID wala nini mbaya zaidi watu wazima wanatuma watoto umri wa miaka 7 akamnunulie beer au sigara.
 
-Nchi za watu huwezi kumtuma mtoto kununua beer au sigara, na mtu mzima ukienda kununua hivyo vitu lazima uonyeshe ID yako ambayo ina picha yako na mwaka wa kuzaliwa.
Kwetu beer na sigara unajinunulia tu hakuna ID wala nini mbaya zaidi watu wazima wanatuma watoto umri wa miaka 7 akamnunulie beer au sigara.

Siyo kwenda kununua tu, wako watu wanaenda na watoto wao bar.
 
Hili swali Nyani Ngabu huwa anajibu vizuri sana. Ni kweli kama intention ni money making, serikalini si sehemu ya kufanya kazi. Hivyo ndivyo kwenye nchi za wenye akili wanavyofanya. Kina Bill Gates na Ruppert walikuwa na uwezo mubwa sana wa kufanya kazi serikalini, no one can doubt kuwa wao ni cream kwenye fani zao lakini walichagua kutengeneza hela.

Huku kwetu watu wanaacha taaluma zao wanaingia kwenye siasa au kutafuta kazi zinazwapa opportunity ya kuiba pesa za serikali. Huu ni ukweli usiofichika. Ukiangalia nini wamefanya tangu waingie kwenye ofisi zao hutaona. Lakini angalia magari mangapi wamenunua, angalia akaunti zao za nje, angalia wanavyojirusha utaona kuwa hawakuingia kazini kwa lengo la kufanya kzai ila kuiba.

Mkuu BL,

Nakubaliana na wewe kuwa kuna wanataaluma kwa makusudi mazima wanaacha professions zao na kukimbilia kwenye siasa ili kutafuta upenyo wa kujinufaisha kwa namna moja au nyingine. Kuna baadhi ya wahadhiri mathalan akina Kapuya, Msola et al, hawa ni mfano hai. Wamekimbia ofisi zao kuja kuyatumikia matumbo yao kwenye siasa bila haya wala aibu. Lakini nadhani kwa ujumla wake, waTZ tunapenda sana shortcut na mteremko. Hatupendi kufanya kazi kwa bidii, tunafanya kazi kidogo tu tena kwa kusukwasukwa halafu tunadai maswali ni duni! Wasomi kwa wasio wasomi! Kutokana na kufanya kazi kidogo tunavuna kidogo na tunaishia kupata mafao kidogo!

Kwa upande mwingine ni kuwa system ya serikali, iliyowekwa CCM inalea uzembe. Kila kitu sasa hivi nchini kinategemea siasa. Siasa zinawagawa watu kwenye vyama. Vyama vinawepeleka watu kwenye makundi. Na haya makundi yanakuwa kama magenge ya mafioso. Usimba na Uyanga, bila kutazama mustakabali wa taifa. Watu wanakwiba fedha waziwazi lakini hawafanywi chochote kwa sababu wapo kundi fulani la wenye kushika mpini. Wanakwiba rasilimali za taifa halafu wanagawa. Na haya makundi chanzo chake kinarudi palepale: watu kutotaka kufanya kazi na kutaka kuvuna wasichopanda kwa kutumia mgongo wa siasa. You can imagine hii cycle ya uvivu wa kufanya kazi unaokolezwa na uchu wa mali na ubinafsi, unavyobomoa nchi.

Nikirejea kwenye hoja ya watumishi wa umma, pengine sikutaja kuwa serikali za nchi za watu mtumishi wa serikali ana kipato kinachomwezesha kuishi maisha ya kati bila matatizo, kitu ambacho ni ndoto hapa kwetu. Serikali haibuni njia mpya za kujinasua kimapato, huku wafanyakazi wake wakiwa na morali duni hawajitumi na ni wala rushwa wakubwa na kwa kufanya hivyo wanaikosesha serikali mapato, kandoni wengine wanajipenyeza kwa kutumia gia ya siasa kuiba kidogo tulichonacho kwa kushirikiana na watu wa ngazi za juu kabisa serikalini..and the cycle continues.
 
Back
Top Bottom