Kila kitu bei ipo juu: Je, Rais Magufuli anapambana na umasikini au anapambana na watu masikini?

juvenile davis

JF-Expert Member
Apr 13, 2015
4,752
4,449
Binafsi namheshimu sana raisi wangu Magufuli japo sikumpa kura yangu(huo ndio ukweli) lakini tunapaswa kuzitii mamlaka tulizonazo.

Wakati anaingia madarakani aliapa wazi kwamba anataka kila mtanzania aifaidi keki ya taifa... Zile ziara zake za kushtukiza hazikunishtua sana. Na hata tumbua tumbua yake haikunishtua kabisa. Maana shida yangu ni kuona unafuu wa sisi walala hoi. Nikashangaa sana kwanza kwa jinsi ishu ya sukari alivoipotezea juu kwa juu na sukari bei haijashuka wala nini!!

Unga/sembe nao bei juu, na sasa umeme unapanda bei. Hivi rais anayajua haya au hajui? Najiuliza, hivi kwa namna ambavyo vitu vinapaa juu bei je raisi anapambana na umasikini au anapambana na sisi masikini? Au haya hayaoni?

Mara nyingi anasema tunaolalamika ni wale tuliozoea pesa za dilidili, jambo ambalo huwa napingana nalo sana kwa kuwa wengine hata kuajiliwa hatujawahi na tunapata pesa ya uhalali na kwa jasho letu, hata dili dili hizo hatuelewi ni kitu gani?!!

Watu tunafanya kazi sana, wengine tunalala saa saba za usiku na kuamka saa 12 au 11 kwenda makazini tena.

Huu msemo wa hapa kazi tu inabidi uendane na maisha jamani.
 
1483121311943.jpg

Hakuna kitu kinaniuma kama watanzania kuwalipa matapeli ya IPTL kupitia Tanesco.

This is unfair na Rais akijipambanua nimchukia ufisadi..........
 
Unavyopandisha bei ya umeme humkomoi mwenye kiwanda mana na yeye atapandisha bei ya bidhaaa yake kufidia ongezeko la operational cost na mwananchi anaathirika direct.

Tuliambiwa kodi kwenye vocha,mobile money transactions,banks transactions hazitamgusa mwananchi lakini leo zigo lote lipo kwa mwananchi. Maisha yanazidi kuwa magumu siku hadi siku.

Serikali badala ya kudeal na haya wanamkomalia faru john. Tuna safari ndefu sana.
 
Lengo nikuwafanya wadanganyika wazidi kuwa masikini na wanyonge mtawaliwe vizuri.

Mkuu hebu shauri wapi pa kuanzia kuhusu hili maana ni dhahiri wananchi hawakubaliani na hili hasa ukizingatia waziri aliapa kwamba bei ya umeme haitapanda na serekali ilisema gas ikianza kutumika tu umeme utashuka bei. Nadhani mchana ulisema petition inafaa. Hebu toa mwongozo tuanzie wapi.
 
nahivi mvua zimegoma bei ya vyakula inawezaongezeka maradufu! lkn itakuwa ni aibu tukilia njaa wkt nikiangalia ramani yetu naona maziwa na makubwa na bahari kwa pembeni
Usinikumbushe sakata la sukari! Bei ilikuwa 1800/= Tukaambiwa bei elekezi ambayo iligoma kuelekezeka! Sasa hivi ni 2400/= plus! Halafu kimyaaaa! Afadhali wangetoa tamko la kutengua bei elekezi!
"Kuna watu wanaficha sukari" inaonekana hizi ni zama za kufichaficha tu, mara sukari mara fedha
 
Back
Top Bottom