Allen Kilewella
JF-Expert Member
- Sep 30, 2011
- 18,292
- 33,903
Ukiangalia sasa hivi kwenye kila taarifa watoa taarifa wanasema kuwa kama si Rais Magufuli kufanya hiki na kile jambo fulani lisingefanyika.
Shirika la umma likipata faida, mradi ukijengwa, Helkopta ikinunuliwa na mambo kadha wa kadha lazima isemwe kwamba bila ya Rais Magufuli jambo hilo lisingefanyika. Picha ninayoipata inawezekana huko serikalini hakuna mipango zaidi ya kusubiri maelekezo toka kwa Rais.
Nimegundua pia kwamba tuna lundo la watu wasiohitajika kwani mambo mengi yanafanywa na Rais Mwenyewe. Kumbe Tanesco hawakuwa na mpango wa kupata faida mpaka Rais ndiye amesababisha wao wapate faida.
Inakera kuona kwamba kumbe inawezekana kodi yetu ingefanya mambo mengi sana ya maana kama hao wangoja maagizo wangepunguzwa serikalini na kwenye mashirika ya umma. Huu mzigo ambao watumishi wa umma wanamtwisha Rais Magufuli ndiyo maaana inafika mahali anawaza yeye akiondoka kama haya yanayofanyika sasa yataendelezwa.
Rais asingesema hivyo kama wengi wa walio chini yake wangekuwa wanatoa mchango kwa yale anayoyafanya. Hata CCM hivi sasa kila kitu ni Magufuli. Kwa maoni yangu tupunguze watu serikalini na kwenye mashirika ya umma ili kuongeza tija kwani wengi wao kazi zao zinafanywa na Rais Magufuli mwenyewe.
Viongozi wa CCM nao wakae pembeni maana chama chao hakuna kinachofanya bali ni kutegemea nguvu ya Magufuli kujiendesha!!
Shirika la umma likipata faida, mradi ukijengwa, Helkopta ikinunuliwa na mambo kadha wa kadha lazima isemwe kwamba bila ya Rais Magufuli jambo hilo lisingefanyika. Picha ninayoipata inawezekana huko serikalini hakuna mipango zaidi ya kusubiri maelekezo toka kwa Rais.
Nimegundua pia kwamba tuna lundo la watu wasiohitajika kwani mambo mengi yanafanywa na Rais Mwenyewe. Kumbe Tanesco hawakuwa na mpango wa kupata faida mpaka Rais ndiye amesababisha wao wapate faida.
Inakera kuona kwamba kumbe inawezekana kodi yetu ingefanya mambo mengi sana ya maana kama hao wangoja maagizo wangepunguzwa serikalini na kwenye mashirika ya umma. Huu mzigo ambao watumishi wa umma wanamtwisha Rais Magufuli ndiyo maaana inafika mahali anawaza yeye akiondoka kama haya yanayofanyika sasa yataendelezwa.
Rais asingesema hivyo kama wengi wa walio chini yake wangekuwa wanatoa mchango kwa yale anayoyafanya. Hata CCM hivi sasa kila kitu ni Magufuli. Kwa maoni yangu tupunguze watu serikalini na kwenye mashirika ya umma ili kuongeza tija kwani wengi wao kazi zao zinafanywa na Rais Magufuli mwenyewe.
Viongozi wa CCM nao wakae pembeni maana chama chao hakuna kinachofanya bali ni kutegemea nguvu ya Magufuli kujiendesha!!