Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,475
- 39,988
Kila fani ina zana, nyingine zaitwa nyenzo,
Iwe kazi ya kitwana, yenye malipo ya dezo,
Au kazi ya kibwana, yenye mapochi ujazo,
Jembe lisilo mpini, halifai kwa kilimo!!
Jembe lisilo mpini, halifai kwa kilimo,
Halikiti ardhini, halifai chimba shimo,
Bila mpini la nini, au kichwani hazimo?
Nyavu hizo zisonasa, za nini hizo botini!!
Nyavu hizo zisonasa, za nini hizo botini,
Wataka kuleta visa, samaki hatuwaoni,
Utaja pata mkasa, upigwe ngumi puani,
Msumari usonyoka, hauingii mbaoni!!
Msumari usonyoka, Hauingii mbaoni,
Usije kukupochoka, ukaijeruhi mboni,
Watu wakaja kucheka, utadhani limbukeni,
Chanuo lisilochana, halifai kwa ususi!!
Chanuo lisilochana, halifai kwa ususi,
Usikazane kuchana, utajeruhi utosi,
Tafuta chako kitana, situmie bisibisi,
Moyo ule usopenda, haufai kwa mapenzi!
Moyo ule usopenda, haufai kwa mapenzi,
Wajikuta umekonda, kumkosa wa azizi,
Pale wewe umependa, mpaka wakosa pumzi,
Moyo kama vile zana, isofaa iachie!!
Na. M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Kijiji)
Iwe kazi ya kitwana, yenye malipo ya dezo,
Au kazi ya kibwana, yenye mapochi ujazo,
Jembe lisilo mpini, halifai kwa kilimo!!
Jembe lisilo mpini, halifai kwa kilimo,
Halikiti ardhini, halifai chimba shimo,
Bila mpini la nini, au kichwani hazimo?
Nyavu hizo zisonasa, za nini hizo botini!!
Nyavu hizo zisonasa, za nini hizo botini,
Wataka kuleta visa, samaki hatuwaoni,
Utaja pata mkasa, upigwe ngumi puani,
Msumari usonyoka, hauingii mbaoni!!
Msumari usonyoka, Hauingii mbaoni,
Usije kukupochoka, ukaijeruhi mboni,
Watu wakaja kucheka, utadhani limbukeni,
Chanuo lisilochana, halifai kwa ususi!!
Chanuo lisilochana, halifai kwa ususi,
Usikazane kuchana, utajeruhi utosi,
Tafuta chako kitana, situmie bisibisi,
Moyo ule usopenda, haufai kwa mapenzi!
Moyo ule usopenda, haufai kwa mapenzi,
Wajikuta umekonda, kumkosa wa azizi,
Pale wewe umependa, mpaka wakosa pumzi,
Moyo kama vile zana, isofaa iachie!!
Na. M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Kijiji)