Kila aliyetenda uovu awajibishwe na waliotendewa waende kushtaki na si kulalamika tu

Chizi Maarifa

JF-Expert Member
Jul 29, 2013
10,272
23,046
Huu ni wendawazimu. Ingekuwa hivi kule Magerezani kusingekuwa na wafungwa hata mmoja. Wote wangekuwa wameomba msamaha na wakasamehewa.

Wanasiasa wezi huwa wanaamini wao si Watanzania wa kawaida. Huamini wao ni watu special so wanahitaji special treatment. Huku ni kuwatusi Watanzania.

Kauli za kusema wasamehewe, Rais aanze upya si kauli za waliotendwa. Ni kauli za waliotenda Uovu. Na kila aliyeishi kwa upanga basi afe kwa Upanga.

Wananchi wameteseka sana na baadhi ya wahuni wa kisiasa. Hawa wamenyanyasa sana wananchi, wamewatesa, wameiba mali ya umma, wamejinufaisha wao binafsi. Kwa kutumia mwamvuli wa Chama au Serikali.

Mimi nasema wakutwe na kitu. Sabaya awe ni mmoja wao si mfano wao. Kila mmoja awajibishwe. Waliotendewa hayo waende kushtaki na si kulalamika tu kwenye mitaa. Waende kushtaki.
 
Hakuna kusamehe mtu. Wahuni hawa lazima walipe waliyo wafanyia watu.

Watu wamekatwa mikono wamipigwa misumari miguuni wameingiziwa chupa sehem za siri

HAPANA KWA KWELI SHERIA ITACHUKUA MKONDO WAKE

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Ni lzm walipe Ili iwe fundisho kwa vizazi vijavyo kwamba hakuna kiongozi yeyeto aliyewahi chezea nchi na akabaki salama
 
Wasiojulikana file is loading kaeni mkao wa kula chakula tayari,mtaeleza tu alipo Azory na ben Ili tuwazike kwa heshima.
 
Unaongea kama huna kichwa. Mkuu siasa za visasi hazijamuacha mtu salama. Sabaya alimuua nani mtaje? Mama samia hawezi kujitenga na uovu wa chama. Kama mnataka hivyo basi kila mtu apambane kivyake tuone nani atapona.
 
Unaongea kama huna kichwa. Mkuu siasa za visasi hazijamuacha mtu salama. Sabaya alimuua nani mtaje? Mama samia hawezi kujitenga na uovu wa chama. Kama mnataka hivyo basi kila mtu apambane kivyake tuone nani atapona.
Mpuuzi wewe ule ulikuwa uovu wa Chama au wa Magufuli na nyie wajinga na mafedhuli wenzake.
 
liwepo dawati maalum kila mkoa kupokea malalamiko kwa wote waliotendewa uovu na baada ya hapo hatua zichukuliwe (hatua kweli sio za kisiasa kuziga watu)....

Tukichukua hatua kweli kwa kila mhusika na wale wote waliogusw wakapata haki zao basi itakuwa tumetoa funzo juu ya ujinga huu kujirudia huko baadaye....
 
Huu ni wendawazimu. Ingekuwa hivi kule Magerezani kusingekuwa na wafungwa hata mmoja. Wote wangekuwa wameomba msamaha na wakasamehewa.

Wanasiasa wezi huwa wanaamini wao si Watanzania wa kawaida. Huamini wao ni watu special so wanahitaji special treatment. Huku ni kuwatusi Watanzania.

Kauli za kusema wasamehewe, Rais aanze upya si kauli za waliotendwa. Ni kauli za waliotenda Uovu. Na kila aliyeishi kwa upanga basi afe kwa Upanga.

Wananchi wameteseka sana na baadhi ya wahuni wa kisiasa. Hawa wamenyanyasa sana wananchi, wamewatesa, wameiba mali ya umma, wamejinufaisha wao binafsi. Kwa kutumia mwamvuli wa Chama au Serikali.

Mimi nasema wakutwe na kitu. Sabaya awe ni mmoja wao si mfano wao. Kila mmoja awajibishwe. Waliotendewa hayo waende kushtaki na si kulalamika tu kwenye mitaa. Waende kushtaki.
Palikuwa na uoga mwingi miongoni mwa wananchi. Waliogopa hata kuwaeleza walio karibu nao.
Kama kuna kitu Mwendazake alifanikiwa ni kulijazia hofu TAIFA.
Bila msaada wa kisheria na kisaikolojia, kuna wananchi wengi ambao watachukua muda kupona na kuwa wawazi.
 
14 Reactions
Reply
Back
Top Bottom