Ta Muganyizi
R I P
- Oct 19, 2010
- 5,361
- 2,732
Hakuna sehemu nchini humu ambapo wananchi wanafurahia maisha. Leo hii mtu angeangalia channel 10 hadi mda huu zinaoneshwa picha za walioumia kutokana na maji yalichafuliwa na Mgodi wa Mara, wananchi wanaonesha ngozi zao zilivyobabuka lakini hakuna anayewasikiliza hata kidogo . Mwananchi mmoja wa Nyamongo aitwaye Omari Bina anasisitiza kuwa Manager mmoja aliyekuja na kuwa anaongoza mgodi wa Barrick aliyemtaja kwa jina la Mr. Jeff aliwaambia kuwa waache kelele maana yeye anamuhonga Rais sembuse Ofisi ya kijiji.
Wengine kama bwana Mseti anasema hakuna kiongozi yeyote aliyewasaidia. Viongozi wengi sana wameenda pale hadi Rais akaona na ngozi za watu waliochubuka na kama angesogea karibu angesikia harufu za watu wanaumia na vidonda lakini hakuna kilichofanyika. Tume iliundwa na mkemia mkuu alishiriki ambapo damu zao zilichukuliwa na maji vikaenda kupimwa lakini hadi muda wa miaka miwili hakuna majibu. Serikali inajali mgodi kuliko wananchi. Hata kanda maalum iliyopelekwa Tarime kule si kwa wananchi bali ni kulinda mgodi.
Cha ajabu taarifa inaendelea kutolewa na uongozi wa kijiji kuwa watumie tu hayo maji hayana shida wahote na kunywa. Matokeo yake mwananchi mmoja anasema ni lengo la Serikali ya kikwete na wazungu wananchi wafe ili wachukue ardhi kabisa. Wananchi wanaomba walau tamko kuwa yale maji yana nini? Ni vipimo gani vinamaliza miaka miwili bila majibu. Mr Jeff wa Barrick anasema ameshamuhonga Rais Ikulu, sasa diwani na VEO watawafanya nini? Bwana Andrew Thomas wa Tarime anasema hata pale baada ya mgodi kukubali kuwa watawapeleka walioathirika hospitali. Mtanzania mwenzao kiongozi akasema maji ni salama hivyo hakuna kilichofanyika.
Hii inatisha, inasemekana kamati ya bunge ilitoa mapendekezo kuwa waathirika wapatiwe huduma haraka iwezekanavyo, lakini hakuna kilichofanyika tu, bunge nao wakaonekana wasanii tu, wanasubiri 90 milioni wakanunue magari.
Ukienda Babati kwenye nyumba ya wazee nako ufisadi, mwenye dhamana ya kuwatunza anachakachua bajeti na kusema kuwa serikali haitoi chochote na badala yake wazee ambao hawana meno wanalishwa makande na maharage mabichi wamechoka na wanasema serikali haiwajali. Ukiangalia nyumba hizo wanazoishi zinanyufa kibao lakini hakuna matengenezo. Kisingizio ni kuwa eti serikali haina Tsh. 3,000,000/= kwa mwezi kuwasaidia wazee!!! Mie nimeshashangaa vya kutosha.
Wananchi walioweka tiki kwenye picha ya kikwete wakati wa uchaguzi na viongozi wengine wa ccm wanajisikia vibaya sana. Kila tunapoangalia taarifa za habari kupitia chanel mbalimbali hapa nchini na kuona jinsi watanzania wanavyoteseka mmaeneo mablimbali, wanaona aibu wanainama chini, pia utasikia wakisema "kwa kweli kikwete katuangusha", "yaani hii ni aibu". Na hii ndo tujue kwamba JK hawezi fanya kitu maana hata yule Bwana Jeff wa Barrick amesema yeye anahonga Ikulu kwa pesident hicyo matatizo yao wapeleke Ikulu!!!
My Take;
Jamani tufanye lolote tuwezalo basi tu angalau wananchi waelewe, loh!!mie naanza kuona aibu kujitangaza kuwa mie mtanzania.Sijui niende wapi. Nionavyo mimi nafasi ya President Tanzania iko vacant, aliyeko anakaimu, hawezi kusema lolote maana Rais hayupo!!!sijui uchaguzi lini??!!
Anayesema sisi tunaoanika maovu hatuna lolote, tuandamane tuhesabu siku, Mungu kaiona dhamira yake lakini haitachukua muda pasipo wewe usiyeona kuonja uchungu huu kwa vitendo.
Wengine kama bwana Mseti anasema hakuna kiongozi yeyote aliyewasaidia. Viongozi wengi sana wameenda pale hadi Rais akaona na ngozi za watu waliochubuka na kama angesogea karibu angesikia harufu za watu wanaumia na vidonda lakini hakuna kilichofanyika. Tume iliundwa na mkemia mkuu alishiriki ambapo damu zao zilichukuliwa na maji vikaenda kupimwa lakini hadi muda wa miaka miwili hakuna majibu. Serikali inajali mgodi kuliko wananchi. Hata kanda maalum iliyopelekwa Tarime kule si kwa wananchi bali ni kulinda mgodi.
Cha ajabu taarifa inaendelea kutolewa na uongozi wa kijiji kuwa watumie tu hayo maji hayana shida wahote na kunywa. Matokeo yake mwananchi mmoja anasema ni lengo la Serikali ya kikwete na wazungu wananchi wafe ili wachukue ardhi kabisa. Wananchi wanaomba walau tamko kuwa yale maji yana nini? Ni vipimo gani vinamaliza miaka miwili bila majibu. Mr Jeff wa Barrick anasema ameshamuhonga Rais Ikulu, sasa diwani na VEO watawafanya nini? Bwana Andrew Thomas wa Tarime anasema hata pale baada ya mgodi kukubali kuwa watawapeleka walioathirika hospitali. Mtanzania mwenzao kiongozi akasema maji ni salama hivyo hakuna kilichofanyika.
Hii inatisha, inasemekana kamati ya bunge ilitoa mapendekezo kuwa waathirika wapatiwe huduma haraka iwezekanavyo, lakini hakuna kilichofanyika tu, bunge nao wakaonekana wasanii tu, wanasubiri 90 milioni wakanunue magari.
Ukienda Babati kwenye nyumba ya wazee nako ufisadi, mwenye dhamana ya kuwatunza anachakachua bajeti na kusema kuwa serikali haitoi chochote na badala yake wazee ambao hawana meno wanalishwa makande na maharage mabichi wamechoka na wanasema serikali haiwajali. Ukiangalia nyumba hizo wanazoishi zinanyufa kibao lakini hakuna matengenezo. Kisingizio ni kuwa eti serikali haina Tsh. 3,000,000/= kwa mwezi kuwasaidia wazee!!! Mie nimeshashangaa vya kutosha.
Wananchi walioweka tiki kwenye picha ya kikwete wakati wa uchaguzi na viongozi wengine wa ccm wanajisikia vibaya sana. Kila tunapoangalia taarifa za habari kupitia chanel mbalimbali hapa nchini na kuona jinsi watanzania wanavyoteseka mmaeneo mablimbali, wanaona aibu wanainama chini, pia utasikia wakisema "kwa kweli kikwete katuangusha", "yaani hii ni aibu". Na hii ndo tujue kwamba JK hawezi fanya kitu maana hata yule Bwana Jeff wa Barrick amesema yeye anahonga Ikulu kwa pesident hicyo matatizo yao wapeleke Ikulu!!!
My Take;
Jamani tufanye lolote tuwezalo basi tu angalau wananchi waelewe, loh!!mie naanza kuona aibu kujitangaza kuwa mie mtanzania.Sijui niende wapi. Nionavyo mimi nafasi ya President Tanzania iko vacant, aliyeko anakaimu, hawezi kusema lolote maana Rais hayupo!!!sijui uchaguzi lini??!!
Anayesema sisi tunaoanika maovu hatuna lolote, tuandamane tuhesabu siku, Mungu kaiona dhamira yake lakini haitachukua muda pasipo wewe usiyeona kuonja uchungu huu kwa vitendo.