Kikwete ziarani Zanzibar: Ahadi, vijembe, na maagizo

Kwani ni lazima aende yeye huko anakosema ndipo wapewe misaada?Akienda mtanzania mwingine let say waziri hawezi kupewa hiyo misaada?
 

Alisema tangi hilo litakuwa na uwezo wa kuchukua lita za ujazo 200,000, wakati lile la awali lilikuwa na uwezo wa kuchukua lita 20,000. Alisema Serikali ya Japan imetoa Sh milioni 106.8 wakati SMZ imetoa Sh milioni 30 na nguvu za wananchi ni Sh milioni mbili. Alisema huo ni mojawapo ya miradi 10 iliyoanza kutekelezwa kuanzia mwaka 2000.

kwa hesabu za haraka haraka wahisani wametoa 106.8mil kwa mradi na miradi iko 10 kwahiyo makadilio ya jumla yote ni kati ya (1-2)Bil tokea mwaka 2000. mi nafikili gharama za kuifuatilia hiyo misaada inazidi misaada yenyewe! na rais amesahau kauli ya Mwakyembe kua watanzania sio wajinga tena.
 
Mkwere kuupata urais tu akaanza safari za nje ili kusafisha nyota.....kwi kwi kwi.
 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete amewaambia wapinzani wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) kuwa inaweza kuwachukua muda mrefu mno kupata nafasi ya kuunda Serikali, ama pengine wasiipate kabisa, na hivyo ni muhimu kwao kushirikiana na Serikali ya CCM katika kuwaletea wananchi wa Tanzania Visiwani maendeleo.
Naam, habari ndio hiyo
 
kwa hesabu za haraka haraka wahisani wametoa 106.8mil kwa mradi na miradi iko 10 kwahiyo makadilio ya jumla yote ni kati ya (1-2)Bil tokea mwaka 2000. mi nafikili gharama za kuifuatilia hiyo misaada inazidi misaada yenyewe! na rais amesahau kauli ya Mwakyembe kua watanzania sio wajinga tena.
Hizo milioni 106.8 ni kwa ajili ya mradi mmoja tu wa tanki la maji.
 
mabalozi waliopo nje ya nchi wanafanya kazi ghani?. kama huyo balozi wa japan anashindwa kuwaelekeza wa japan Tanzania ilipo bora mkulu amrudishe bongo
 
Yaani inashangaza sana. Kununua magari ya fahari, wala hawaendi Japan, wanaamua tu. Ila miradi ya maji ndio lazima mkuu aende kuitambulisha Kengeja. Duh, kazi ni kubwa kuliko nilivyodhani. NIlitegemea angetoa sababu kubwa zaidi ya hiyo ya matanki 10. Maana wakazi wa Kengeja hawako interested kujua kuwa waJapan wanawajua. Wanachotaka ni maji na mambo mengine ya maendeleo. Mbona tuna-shift the goal post?
 
Tatizo la viongozi wa Serikali hawafanyi ziara kama viongozi wa Serikali bali wanafanya ziara kama viongozi wa Chama na ndipo hapo mazungumzo yao yanapowaweka pabaya ,utaona ziara ya kiongozi wa serikali imejaa magwanda ya kijani na manjano utafikiri ni uchaguzi wa CCM.
Wacha hotuba zao zijae utumbo zinapowekwa katika kilingo cha serikali.
 
hopeless.gif
 
Kikwete atawadanganya wasiojua historia ya Zanzibar. Huko Kengeja kulikuwa na maji ya bomba, barabara ya lami na simu tokea wakati wa ukoloni. Serikali ya CCM ndio walioacha vitu hivyo kuharibika hadi kuwa havifanyi kazi. Barabara wanazodai kuzijenga zote zilikuwapo na wanachokifanya hadi leo hakijafikia ile hali waliyoirithi kutoka ile serikali wanayoiita ya waarabu.
 
Mradi umegharimu shs 138m, je kweli kuna haja ya kupanda ndege kwenda Japani na msafara mzito kwenda kuomba kiasi hicho cha pesa?. Gari moja la kiongozi linagharimu kiasi gani?, viongozi ambao bado wanaishii mahotelini kwa kukosa nyumba kama wao wanavyodai wanagharimu kiasi gani?, hiyo safari ya kwenda huko Japani imetumia shs ngapi?.

Hapa hapahitaji shule katika kupanga na kupangua mahesabu haya, matatizo yetu ni kwamba hatuna kipaumbele katika mipango yetu ya maendeleo.

Gari moja la kiongozi (shangingi) linaweza kuwa na gharama kama hizo za mradi, na serikali haioni haya kununua magari hayo kwa wingi na kulipa cash kwa faida ya viongozi wakati huohuo miradi muhimu ya maendeleo kwa jamii inakwama. VERY BIG SHAME ON ALL TANZANIANS
 
CUF yajibu hotuba ya JK Pemba

"Hasira za Wapemba kwa CCM Zinatokana na Kufeli kwa Chama Cha Mapinduzi"

Wapendwa Wanahabari,

Kufuatia ziara yake ya hivi majuzi kisiwani Pemba, Rais wa Jamhuri ya Muungano, Mhe. Jakaya Kikwete, amenukuliwa akiwaambia Watanzania wa kisiwa cha Pemba kwamba huenda upinzani usiingie kabisa madarakani, na kwa hivyo ni vyema wakashirikiana na Chama cha Mapinduzi (CCM) ambacho ndicho kilichopo sasa madarakani..

Licha ya kuwa kauli hii ni ya kisiasa ambayo inaweza kutafsiriwa kwa muelekeo huo tu – kwani huyu ni mwenyekiti wa CCM ambaye kwa vyovyote asingetarajiwa kukitabiria chama chake kuondoka madarakani au kukiri kwamba kuna chama chengine ambacho kinaweza kuchukua nafasi ya CCM – sisi Kurugenzi ya Haki za Binaadamu na Mahusiano ya Umma ya The Civic United Front (CUF – Chama cha Wananchi) tunaona kuwa kuna haja ya kuitolea ufafanuzi.

Kwanza, kumekuwa na tabia ya viongozi wa ngazi za juu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano kuyatafsiri matatizo ya kisiwa cha Pemba kisiasa tu bila ya kuzingatia hali halisi ya kiuchumi ambayo wananchi wa kisiwa hicho wamekuwa wakipambana nayo.

CUF tunaposema kwamba hali ya maisha ni ngumu, ni kwa kuwa serikali zilizopo madarakani zimekisusa kisiwa cha Pemba na kukitenga kabisa kimaendeleo.

Serikali hizi, ambao zinaongozwa na CCM, zimekuwa zikifanya hivyo kama ni njia ya kuwakomoa wakaazi wa kisiwa hicho ambao tangu kuanzishwa tena kwa mfumo wa vyama vingi, mwaka 1992, wamekuwa wakionesha wazi msimamo wao wa kuipinga CCM.

Kwa hivyo, wakaazi wa Pemba wataendelea kuzipinga serikali zilizopo si kwa sababu ya chuki wala fitina, bali kwa sababu serikali hizo zimeshindwa kukidhi (have failed to deliver) matashi yao.

Pili, kwa kuwa Rais Kikwete na wenzake wanajuwa hasira walizonazo wakaazi wa kisiwa cha Pemba dhidi ya serikai hizi zilizoshindwa kuinua hali ya maisha ya mkaazi wa kisiwa hicho – kama vile pia zilivyoshindwa kwa wengine – basi wanatafuta kisingizio cha kuzielezea hasira hizo, kwamba eti ni viongozi wa vyama vya upinzani.

Huko ni kuwadhalilisha wananchi hao kwa kuwaona kama kwamba wenyewe hawana uwezo wa kuchanganua na kufahamu hasa lilipo tatizo lao, ambalo ni serikali za CCM zilizofeli, mpaka wachanganuliwe na viongozi wa upinzani. Hasira za wananchi wa Pemba ni muakisiko wa kufeli kwa CCM, na si chenginecho.

Tatu, ni vibaya kwa Rais Kikwete kutumia uzinduzi wa miradi ya maendeleo kuwasimanga wananchi wa kisiwa cha Pemba, kwani kwanza miradi hiyo inajengwa kwa kodi zao au kwa misaada ya wahisani ambayo huko ilikotolewa ilitolewa kwa ajili ya wananchi hao, na si kinyume chake.
Kama alivyosema mwenyewe, Serikali kujenga miundombinu ni jukumu lake na wala Rais Kikwete asijenge picha kwamba anawafanyia hisani wananchi wa huko; na hivyo akapata sababu ya kuwasimanga.

Mwisho, ikiwa kweli Rais Kikwete ana dhamira ya kuisaidia Zanzibar kuondokana na ule aliouita ‘Mpasuko wa Kisiasa’ anapaswa kuliangalia suala hili kwa uadilifu. Kuendelea kwake kupiga mifano ya watu ‘waliogomewa’ kupata huduma za kijamii kutoka kwa wenzao lakini asigusie kabisa sababu halisi zilizopelekea hao waliogomea kugomea, ni kuwabagua watu na ni kuendeleza mpasuko.

Tunakusudia kusema, ikiwa Rais Kikwete anaongelea kisa cha mwanachama wa CCM kususiwa biashara yake na wana-CUF, kwa mfano, basi pia na azungumzie kuwa mwana-CCM huyo aliyesusiwa ndiye aliyeshiriki kuwabaka watoto wa wana – CUF, kuiba mali zao na kuwaletea makundi ya Janjaweed kuwavunjia nyumba zao. Je, Rais Kikwete yuko tayari kuueleza ukweli huu pia?
 
Kikwete amesema "..kazi ya wabunge na wawakilishi wa upinzani ni kufoka tu.." Je mnaelewa hapa ?
Wabunge mpo ? Jamaa anasema kazi zenu ni kufoka tu akimaanisha hamna maana yeyote ile ndani ya Bunge wala hamna faida ambayo itawashughulisha na kuwapa mtihani wao waliopo serikalini na chama chao kitaendelea kutawala milele. Kaazi ipo.
 
Tatizo nnaloliona hapo ni pale ambapo watawala huwa kuna wakati hawaonyeshi tofauti ya ziara za kichama au kiserikali.
 
Tatizo nnaloliona hapo ni pale ambapo watawala huwa kuna wakati hawaonyeshi tofauti ya ziara za kichama au kiserikali.

Ni kweli kabisa ,Raisi anaona kwa vile yeye ni Raisi akitumia ziara za Kiserikali kukisafisha chama chake atafanikiwa kumbe ndio anazidi kukizamisha nafikiri bado ana hasira za Butiama kupelekwa kapa sasa anawazamisha wenziwe kwa kwenda kuhubiri utumbo.
 
Ni kweli kabisa ,Raisi anaona kwa vile yeye ni Raisi akitumia ziara za Kiserikali kukisafisha chama chake atafanikiwa kumbe ndio anazidi kukizamisha nafikiri bado ana hasira za Butiama kupelekwa kapa sasa anawazamisha wenziwe kwa kwenda kuhubiri utumbo.

Nadhni huwa anajisahau kwamba yeye ni raisi wa watu wote hata hao CUF
 
Nadhni huwa anajisahau kwamba yeye ni raisi wa watu wote hata hao CUF

Ajabu ameenda kuisifia misaada wakati alitakiwa atoe tathmini ya serikali imekifanyia nini kisiwa cha Pemba,hivi hashangai nchi ya Pemba haina hata kiwanda wakazi wake wanaokaribia milioni hajui wapi wanapata feza ya kuwaendeshea maisha,wakati matibabu kwa fedha,elimu kwa fedha na kila kitu kwa fedha umeme wa jenereta kama hakuna umeme hakuna maji.Barabara hizo za pemba ambazo hazizidi hata kilomita 40 zinajengwa na serikali za CCM tokea nchi zipate uhuru mpaka leo bado kila Raisi anakwenda kukagua barabara hizo,Waziri nae anakagua barabara hizo hizo.
Ujinga mliokuwa mnadhania wanao Wapemba jueni kwamba umeshawatoka sasa wanapigania utawala wao na Mkapa nae anapelekwa kwenye mahakama ya kimataifa taratibu zipo mbioni. Mpaka kieleweke.
 
The truth will always prevail kuna mzaha kila mahali.Na tatizo hapa ni kwamba Serikali yetu imekosa long lasting solutions to our problems but rather kuongeza tatizo juu ya tatizo!
 
Unajuwa viongozi wa Serikali na CCM wanumizwa kichwa na watu wa Pemba. Inashangaza sana kuwa viongozi hao wafikapo Pemba huwa hawawi makini na wanachokisema. Mara nyingi hudanganywa na viongozi wachache walioko Pemba kuwa wananchi wameamka na kukipenda CCM na waendapo mikutanoni basi ule umati unaojitokeza huwapa hamasa viongozi wetu na kuanza kuropoka ovyo. Kampeni za mwaka wamwanzo wa vyama vingi Dr Salmini kwa mori alifika kubariki mauwaji ya mwanachama wa CUF aliyeuliwa kwa kupachika bendera, kipindi cha Amani pia alikwenda kwa mikogo na baada ya matokeo akawafutukia Wapemba na Kikwete kwa upande wake amedanganyika na kujenga hamsa iasi cha kutamka yasiyofaa lakini kwa Wapemba awabu ataliona 2010.
Wapemba tangu kifo cha Karume na kuondoka kwa Jumbe bado hawajampata kiongozi wa kuwa na imani nae.Kipindi cha kwanza cha Amani Wapemba walimtegemea kuwa atawanusuru lakini haikuwa hivyo na ndio kisassi chao kilionekana 2005 na Kikwete pia walitegemea lakin kwa kauli hizi wataona kuwa tofauti ni sji tu mengine ni yaleyale. Sifikiri kuwa Wapemba watajali kauli hizo.
 
Kamanda taratibu, Prez yupo Pemba na lazima aongee Kipemba ili afahamike...

What do you mean by that? Una maana Wapemba ndio mbumbumbu? wanaohitaji kudharauliwa? au waliozoea kudanganywa? Hapa mzee hukuwatendea haki wenzetu na ipo haja ya kufuta usemi wako.
 
Back
Top Bottom