Tatu
JF-Expert Member
- Oct 6, 2006
- 1,100
- 313
Claud Mshana
RAIS Jakaya Kikwete amesema kuwa, maandalizi ya zoezi la upigaji kura za maoni za kung'amua wauaji wa albino na vikongwe, limekamilika na litazinduliwa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda.
Akizungumza jana kwenye hotuba yake ya mwisho wa mwezi wa Februari, Rais Kikwete alisema kuwa maandalizi ya kutekeleza zoezi hilo yamekamilika na kwamba, waziri mkuu atafanya uzinduzi rasmi wa zoezi hilo mwishoni mwa wiki ya kwanza ya mwezi huu.
Alisema kuwa alitoa maagizo ya kufanyika kwa zoezi hilo mwezi Desemba mwaka jana kwamba wananchi wapige kura kutaja majina ya waovu hao, akiwa na dhamira ya kuwapa nafasi wananchi kushiriki kikamilifu.
"Maandalizi ya kutekeleza uamuzi wangu huo yanaelekea kukamilika, mheshimiwa waziri mkuu atafanya uzinduzi rasmi wa zoezi hilo mwishoni mwa wiki ya kwanza ya mwezi Machi, 2009 na zoezi lenyewe la kupiga kura kufanyika kuanzia wiki ya pili ya Machi, 2009."
Alifafanua kuwa katika zoezi hilo pia wauaji wa vikongwe, majambazi wa kutumia silaha na wauzaji wa dawa za kulevya nao watahusishwa.
Alitaja utaratibu wa kuendesha zoezi hilo utakuwa ni kufuata kanda na kwamba mikoa imegawanywa katika kanda saba ambazo ni Kanda ya Ziwa inayojumuisha mikoa ya Kagera, Mara, Mwanza na Shinyanga.
Kanda ya Nyanda za Juu Kusini yenye mikoa ya Iringa, Mbeya, Rukwa na Ruvuma; Kanda ya Kati (Dodoma na Singida), Kanda ya Kusini (Lindi na Mtwara), Kanda ya Magharibi (Kigoma na Tabora), Kanda ya Kaskazini (Arusha, Kilimanjaro, Tanga na Manyara), na Kanda ya Mashariki (Dar es Salaam, Pwani na Morogoro).
Aliongeza kuwa wakuu wa mikoa yote nchini wameshapewa mwongozo wa jinsi ya kutekeleza zoezi hilo na kutaja miongoni mwa mambo watakayotakiwa kuzingatia ni pamoja na kuelimisha na kuhamasisha wananchi kushiriki katika zoezi hilo, upigaji kura ufanyike mwezi Machi kwa tarehe zitakazopangwa kwa kuzingatia kanda hizo.
"Kamati za ulinzi na usalama za mikoa zikiongozwa na wakuu wa mikoa zisimamie zoezi hili kwa makini. Kadhalika, kamati za ulinzi na usalama za wilaya zikiongozwa na wakuu wa wilaya zitaongoza utekelezaji katika wilaya zao na kushirikisha serikali za vijiji na mitaa," alisema Rais Kikwete.
"Napenda kuitumia fursa hii kuwasihi Watanzania; wake kwa waume; vijana na wazee tujitokeze kwa wingi kuwataja watu wanaojihusisha na maovu hayo katika jamii. Kura ni siri, hakuna atakayejua umemtaja nani. Hata msimamizi wa kituo hawezi kujua," alisema.
Katika hatua nyingine Rais Jakaya Kikwete ameagiza viongozi wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, kuwashughulikia watumishi wote wazembe wanaosababisha matatizo ya mlundikano wa madai ya walimu na watumishi wengine wa umma.
Kikwete alisema kuwa mlundikano wa malimbikizo ya madai ya watumishi wa umma husababishwa na uzembe wa wakuu wa kazi wasiojali maslahi ya walio chini yao.
Katika hotuba yake ya mwisho wa mwezi, Rais Kikwete alisema kuwa sehemu kubwa ya madai ya malimbikizo ya walimu yanahusu stahili zao za uhamisho, kupandishwa madaraja na likizo na kuongeza kuwa panapotokea migogoro hiyo, wale waliosababisha malimbikizo hayo hawaonekani kuwa ndiyo wakosaji bali serikali kuu ndio huonekana na huingilia kati kuokoa jahazi.
"Napenda kusema kuwa matatizo wayapatayo walimu ndiyo wayapatayo watumishi wengine wa umma katika wizara, idara na taasisi mbalimbali za serikali, hivyo watumishi wote wa idara za serikali wanaosababisha kero hizo wachukuliwe hatua mara moja," alisema Kikwete.
Rais alisema pia tabia ya watu kukaa katika kituo kimoja kwa muda mrefu, huzaa tabia za kufanya kazi kwa mazoea na hivyo kuagiza watu walioko katika kituo kimoja kwa muda mrefu, wahamishwe.
"Nimeagiza watu walio kituo kimoja kwa muda mrefu wahamishwe, kuwahamisha mara kwa mara kutasaidia kuondoa usultani," alisema bila ya kudokeza jaribio la mgomo wa walimu lililotikisa nchi mwishoni mwa mwaka jana, wakati wakishinikiza kulipwa kwa madai yao ya zaidi ya Sh16 bilioni.
Kwa mujibu wa Rais Kikwete alipofanya ziara na kuongea na viongozi wa kisiasa na kiutendaji wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, walikubaliana kuwa malimbikizo ya madai ya malipo ya stahili mbalimbali yapatiwe ufumbuzi, kwani yamekuwa chanzo cha mivutano kati ya serikali na walimu.
Alisema mivutano hiyo haina lazima wala sababu akisisitiza kuwa, kama wahusika katika idara za utawala na fedha katika Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa, Wizara ya Utumishi na Wizara ya Fedha na Uchumi wangetimiza ipasavyo wajibu wao, kusingekuwa na malimbikizo hayo.
"Nilielekeza kuwa kama halmashauri haina pesa za uhamisho, wasiwahamishe watumishi wao; wamekuwa wanafanya hivyo na kulimbikiza madeni makubwa ambayo yamekuwa yanalipwa na serikali kuu mara nyingi baada ya walimu kuchachamaa. Serikali kuu imekuwa inafanya hivyo kuepusha shari, bahati mbaya hiyo imegeuka kuwa mazoea," alisema Kikwete.
Rais alisema kuwa hali hiyo imejengeka na kuonekana kuwa kumhamisha mtumishi kutoka kituo kimoja kwenda kingine wilayani, ni wajibu wa serikali kuu kugharamia uhamisho huo na matokeo yake ni malimbikizo na madai yasiyokwisha yanayozua migogoro ya mara kwa mara.
"Niliagiza mtindo wa kuhamisha walimu bila ya kuwa na fedha za uhamisho ukomeshwe mara moja... ni marufuku kufanya hivyo na agizo langu hilo haliwahusu walimu tu, bali watumishi wote wa umma. Kiongozi au mhusika yeyote atakayekiuka agizo hili, alipishwe yeye gharama za kumhamisha mtumishi huyo," alisema rais.
Kuhusu madai ya likizo, Kikwete alisema hali ni ileile kwani fedha ambazo zilipaswa kugharamia likizo kama hazikutengwa, madeni yatazidi kuongezeka siku hadi siku na kusisitiza kutengwa fedha za kutosha za likizo kwani mapumziko ni muhimu kwa wafanyakazi.
Kikwete pia alizungumzia suala la kuwapandisha watumishi vyeo bila kuwarekebishia mishahara yao, kuwa ni upungufu wa kiutendaji ambao alisema ni lazima ukomeshwe mara moja.
Source: Mwananchi.
This is very disturbing coming from the president. I think this is playing with people's lives. We have different police force and state body to carry investigations but the pres. comes with this approach.
Can you convict someone in the court just buy votes?
JK refuses to take some of FISADI's to court like AC and Dr. IR with all the evidance he got but he wants to vote on peoples who kill Albinos, I don't get it all. Not sure where we are heading as a country.
RAIS Jakaya Kikwete amesema kuwa, maandalizi ya zoezi la upigaji kura za maoni za kung'amua wauaji wa albino na vikongwe, limekamilika na litazinduliwa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda.
Akizungumza jana kwenye hotuba yake ya mwisho wa mwezi wa Februari, Rais Kikwete alisema kuwa maandalizi ya kutekeleza zoezi hilo yamekamilika na kwamba, waziri mkuu atafanya uzinduzi rasmi wa zoezi hilo mwishoni mwa wiki ya kwanza ya mwezi huu.
Alisema kuwa alitoa maagizo ya kufanyika kwa zoezi hilo mwezi Desemba mwaka jana kwamba wananchi wapige kura kutaja majina ya waovu hao, akiwa na dhamira ya kuwapa nafasi wananchi kushiriki kikamilifu.
"Maandalizi ya kutekeleza uamuzi wangu huo yanaelekea kukamilika, mheshimiwa waziri mkuu atafanya uzinduzi rasmi wa zoezi hilo mwishoni mwa wiki ya kwanza ya mwezi Machi, 2009 na zoezi lenyewe la kupiga kura kufanyika kuanzia wiki ya pili ya Machi, 2009."
Alifafanua kuwa katika zoezi hilo pia wauaji wa vikongwe, majambazi wa kutumia silaha na wauzaji wa dawa za kulevya nao watahusishwa.
Alitaja utaratibu wa kuendesha zoezi hilo utakuwa ni kufuata kanda na kwamba mikoa imegawanywa katika kanda saba ambazo ni Kanda ya Ziwa inayojumuisha mikoa ya Kagera, Mara, Mwanza na Shinyanga.
Kanda ya Nyanda za Juu Kusini yenye mikoa ya Iringa, Mbeya, Rukwa na Ruvuma; Kanda ya Kati (Dodoma na Singida), Kanda ya Kusini (Lindi na Mtwara), Kanda ya Magharibi (Kigoma na Tabora), Kanda ya Kaskazini (Arusha, Kilimanjaro, Tanga na Manyara), na Kanda ya Mashariki (Dar es Salaam, Pwani na Morogoro).
Aliongeza kuwa wakuu wa mikoa yote nchini wameshapewa mwongozo wa jinsi ya kutekeleza zoezi hilo na kutaja miongoni mwa mambo watakayotakiwa kuzingatia ni pamoja na kuelimisha na kuhamasisha wananchi kushiriki katika zoezi hilo, upigaji kura ufanyike mwezi Machi kwa tarehe zitakazopangwa kwa kuzingatia kanda hizo.
"Kamati za ulinzi na usalama za mikoa zikiongozwa na wakuu wa mikoa zisimamie zoezi hili kwa makini. Kadhalika, kamati za ulinzi na usalama za wilaya zikiongozwa na wakuu wa wilaya zitaongoza utekelezaji katika wilaya zao na kushirikisha serikali za vijiji na mitaa," alisema Rais Kikwete.
"Napenda kuitumia fursa hii kuwasihi Watanzania; wake kwa waume; vijana na wazee tujitokeze kwa wingi kuwataja watu wanaojihusisha na maovu hayo katika jamii. Kura ni siri, hakuna atakayejua umemtaja nani. Hata msimamizi wa kituo hawezi kujua," alisema.
Katika hatua nyingine Rais Jakaya Kikwete ameagiza viongozi wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, kuwashughulikia watumishi wote wazembe wanaosababisha matatizo ya mlundikano wa madai ya walimu na watumishi wengine wa umma.
Kikwete alisema kuwa mlundikano wa malimbikizo ya madai ya watumishi wa umma husababishwa na uzembe wa wakuu wa kazi wasiojali maslahi ya walio chini yao.
Katika hotuba yake ya mwisho wa mwezi, Rais Kikwete alisema kuwa sehemu kubwa ya madai ya malimbikizo ya walimu yanahusu stahili zao za uhamisho, kupandishwa madaraja na likizo na kuongeza kuwa panapotokea migogoro hiyo, wale waliosababisha malimbikizo hayo hawaonekani kuwa ndiyo wakosaji bali serikali kuu ndio huonekana na huingilia kati kuokoa jahazi.
"Napenda kusema kuwa matatizo wayapatayo walimu ndiyo wayapatayo watumishi wengine wa umma katika wizara, idara na taasisi mbalimbali za serikali, hivyo watumishi wote wa idara za serikali wanaosababisha kero hizo wachukuliwe hatua mara moja," alisema Kikwete.
Rais alisema pia tabia ya watu kukaa katika kituo kimoja kwa muda mrefu, huzaa tabia za kufanya kazi kwa mazoea na hivyo kuagiza watu walioko katika kituo kimoja kwa muda mrefu, wahamishwe.
"Nimeagiza watu walio kituo kimoja kwa muda mrefu wahamishwe, kuwahamisha mara kwa mara kutasaidia kuondoa usultani," alisema bila ya kudokeza jaribio la mgomo wa walimu lililotikisa nchi mwishoni mwa mwaka jana, wakati wakishinikiza kulipwa kwa madai yao ya zaidi ya Sh16 bilioni.
Kwa mujibu wa Rais Kikwete alipofanya ziara na kuongea na viongozi wa kisiasa na kiutendaji wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, walikubaliana kuwa malimbikizo ya madai ya malipo ya stahili mbalimbali yapatiwe ufumbuzi, kwani yamekuwa chanzo cha mivutano kati ya serikali na walimu.
Alisema mivutano hiyo haina lazima wala sababu akisisitiza kuwa, kama wahusika katika idara za utawala na fedha katika Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa, Wizara ya Utumishi na Wizara ya Fedha na Uchumi wangetimiza ipasavyo wajibu wao, kusingekuwa na malimbikizo hayo.
"Nilielekeza kuwa kama halmashauri haina pesa za uhamisho, wasiwahamishe watumishi wao; wamekuwa wanafanya hivyo na kulimbikiza madeni makubwa ambayo yamekuwa yanalipwa na serikali kuu mara nyingi baada ya walimu kuchachamaa. Serikali kuu imekuwa inafanya hivyo kuepusha shari, bahati mbaya hiyo imegeuka kuwa mazoea," alisema Kikwete.
Rais alisema kuwa hali hiyo imejengeka na kuonekana kuwa kumhamisha mtumishi kutoka kituo kimoja kwenda kingine wilayani, ni wajibu wa serikali kuu kugharamia uhamisho huo na matokeo yake ni malimbikizo na madai yasiyokwisha yanayozua migogoro ya mara kwa mara.
"Niliagiza mtindo wa kuhamisha walimu bila ya kuwa na fedha za uhamisho ukomeshwe mara moja... ni marufuku kufanya hivyo na agizo langu hilo haliwahusu walimu tu, bali watumishi wote wa umma. Kiongozi au mhusika yeyote atakayekiuka agizo hili, alipishwe yeye gharama za kumhamisha mtumishi huyo," alisema rais.
Kuhusu madai ya likizo, Kikwete alisema hali ni ileile kwani fedha ambazo zilipaswa kugharamia likizo kama hazikutengwa, madeni yatazidi kuongezeka siku hadi siku na kusisitiza kutengwa fedha za kutosha za likizo kwani mapumziko ni muhimu kwa wafanyakazi.
Kikwete pia alizungumzia suala la kuwapandisha watumishi vyeo bila kuwarekebishia mishahara yao, kuwa ni upungufu wa kiutendaji ambao alisema ni lazima ukomeshwe mara moja.
Source: Mwananchi.
This is very disturbing coming from the president. I think this is playing with people's lives. We have different police force and state body to carry investigations but the pres. comes with this approach.
Can you convict someone in the court just buy votes?
JK refuses to take some of FISADI's to court like AC and Dr. IR with all the evidance he got but he wants to vote on peoples who kill Albinos, I don't get it all. Not sure where we are heading as a country.