Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 233
Kauli aliyotoa Rais Kikwete akiwa katika mkutano wa kampeni wilayani Tarime, kuwa watu wanaoambukizwa virusi vya ukimwi inatokana na kiherehere chao, imezua utata.
Umoja wa mashirika yanayoshughulikia na waathirika wa VVU Kanda ya Ziwa wamemtaka awaombe radhi kwa madai kuwa kauli hiyo inawanyanyapaa waathirika wa ukimwi.
Mwenyekiti wa mashirika yanayotetea waathirika wa VVU Kanda ya Ziwa (LAZONEFA), James Lumumba, alisema mgombea huyo akiwa kama kiongozi wan chi ameonyesha njia ya kuanzisha unyanyapaa dhidi ya waathirika wa ukimwi, kinyume cha kampeni yake alioanzisha ya kupima kwa hiari.
Alisema mara kwa mara kiongozi huyo wan chi amekuwa akitoa kauli tata kuhusu masuala ya kitaifa, akitolea mfano kauli ya hivi karibunium aliyotoa dhidi ya vyama vya wafanyakazi kuwa hahitaji kura zao ikiwa watashinikiza kulipwa mishahara waliyopendekeza kupitia vyama vyao.
"Rais Kikwete alianzisha kampeni ya kupima kwa hiari kama ishara ya kupambana na maambukizi mapya ya VVU nchini, sasa iweje leo hii atupakazie kuwa tulkioambukizwa tulikuwa na kiherehere, au ndiyo kusema nasi hataki kura zetu kama wafanyakazi?" alihoji Lumumba ambaye pia alijitangaza hadharani kuwa mmoja wa watru wanaoishi na VVU…..
Chanzo: Tanzania Daima.
Umoja wa mashirika yanayoshughulikia na waathirika wa VVU Kanda ya Ziwa wamemtaka awaombe radhi kwa madai kuwa kauli hiyo inawanyanyapaa waathirika wa ukimwi.
Mwenyekiti wa mashirika yanayotetea waathirika wa VVU Kanda ya Ziwa (LAZONEFA), James Lumumba, alisema mgombea huyo akiwa kama kiongozi wan chi ameonyesha njia ya kuanzisha unyanyapaa dhidi ya waathirika wa ukimwi, kinyume cha kampeni yake alioanzisha ya kupima kwa hiari.
Alisema mara kwa mara kiongozi huyo wan chi amekuwa akitoa kauli tata kuhusu masuala ya kitaifa, akitolea mfano kauli ya hivi karibunium aliyotoa dhidi ya vyama vya wafanyakazi kuwa hahitaji kura zao ikiwa watashinikiza kulipwa mishahara waliyopendekeza kupitia vyama vyao.
"Rais Kikwete alianzisha kampeni ya kupima kwa hiari kama ishara ya kupambana na maambukizi mapya ya VVU nchini, sasa iweje leo hii atupakazie kuwa tulkioambukizwa tulikuwa na kiherehere, au ndiyo kusema nasi hataki kura zetu kama wafanyakazi?" alihoji Lumumba ambaye pia alijitangaza hadharani kuwa mmoja wa watru wanaoishi na VVU…..
Chanzo: Tanzania Daima.