Kikwete - Tuhuma nzito dhidi ya CHADEMA

Dah wakuu Kj choka mbya.

Kwanza ni mwongo ..hakuna mgombea Uraisi yoyote aliyehubiri udini. Labda yeye

Pili Messeji za Shamte anataka kuzikanusha wakati tunazo na zimetoka CCM . Mbona Shamte anajulikana namna hii ? Aibu tupu.
 
Hawana jipya, sasa wanapayuka tu. Lolote linalokuja anapayuka...

Asubiri 31/10/2010!!!
 
Bila kujali kwamba unachosema ni cha kweli au hapana, tukirudi kwenye kauli yake ya kukemea udini ni ya kuungwa mkono na sisi wana JF bila kisingizio chochote kwani bila kufanya hivyo tutakuwa hatujashiriki kuukemea udini ndani na nje ya JF

Tatizo ni kwamba mheshimiwa rais amekuwa akisema kuna watu wanachochea umwagaji wa damu lakini hakuna hatua zozote zinazochukuliwa dhidi ya watu hao. Sasa hii inatufanya tuanze kutilia mashaka kauli zake kuwa inawezekana ni yeye ndiye mchochezi wa umwagaji wa damu na udini.

Kama rais na amiri jeshi mkuu ana mamlaka yote ya kumchukulia hatua mtu yoyote ambaye anatishia kumwaga damu. Sasa na yeye anapolalamika na kugeuza hii kuwa ni sehemu ya kampeni yake ya kuomba kura bila kuwachukulia watu hao hatua tunapata mashaka kama kweli watu hao wapo.

Mtu wa kwanza kuingiza masuala ya udini kwenye kampeni ni Makamba ambaye mara tu baada ya Dr. Slaa kutangazwa kuwa mgombea wa Chadema alitangaza kuwa wananchi wasimwamini kwa sababu amekiuka mkataba wake wa upadre. Aliyasema haya wakati akijua wazi kuwa Dr. Slaa alishaacha upadre kwa muda wa zaidi ya miaka kumi na mitano kabla ya kugombea urais na kuwa upadre wake huo ambao haupo tena hauna uhusiano wowote na kugombea kwake urais.

Ni Makamba huyohuyo aliyeanza kuhoji mahusiano binafsi ya Dr. Slaa na Mushumbuzi na aliacha kuhoji mahusiano hayo baada ya kutakiwa aeleze kwanza kilichomfukuzisha ualimu kwa aibu.

Hatutaki damu imwagike na kama kweli kuna mtu anatishia kumwaga damu basi hatua stahiki zichukuliwe na vyombo vya dola ili kumdhibiti. Lakini mheshimiwa rais anapopita kila mahali na kufanya suala la watu kutaka kumwaga damu kama sehemu ya kampeni yake basi kuna matatizo makubwa sana. Kwa kufanya hivyo rais anageuza suala hili la kijinai kuwa ni ajenda yake ya kwenda ikulu.



 
kama nimemwelewa vizuri ndugu kikwete alipokemea udini alikuwa ametoa mfano, lakini ametoa angalizo kwa watanzania wa dini zote kwa maana na vyombo vya habari kama hivyo vya kiislamu au na kikiristo pia.

Kazi ya rais siyo kutoa maangalizo na kuacha uvunjifu wa amani (kama upo) ukiendelea. Kama kuna mtu anavunja sheria kwa kutangaza kuwa atamwaga damu achukuliwe hatua na huo uwezo upo. Kwa nini rais na vyombo vya dola havichukui hatua basi kwa watu hao? Hatutaki umwagikaji wa damu na hatutaki wanasiasa waumbe kitisho cha umwagikaji wa damu ambacho hakipo halafu wakifanye kuwa ajenga ya msingi ya kampeni zao.
 
Mkuu hapo kwa "MY TAKE" ndipo kulIkonifanya nikakutwangia senksi. Sasa kama amemaliza kampeni, aanze kutekeleza ahadi sasa!

Kikwete anatabia ya uongo tena muongo aliye kubuu,mroho wa madaraka anatapatapa akihofia serikali ya ilikuwa ikishikiliwa na ccm sasa wakati umewadia wa kukabidhi serikali kwa chama cha upinzani.

Yeye alihusudu safari za nge kupaa angani sasa anaanza kusingizia vyama kuhusu umwagaji damu yeye sasa ndiye anayepanda mbegu ya chuki anawasingizia waislamu wenzake iliwamunusuru kikwete amekuwa kama mtu anayezama baharini hushika maji akitegemea ataokoka.

Safari hii haponi, nchi tuna chukua sisi hatumpini kwa imani yake wala sura yake sisi kipimo chetu na uchapakazi ameshindwa hafai hawezi kutugsisi tuko tayari kufa lakini nilazima uang'oke
 
Nilisema hapa zamani sana kuwa hawa ccm hawana aibu, wao wanacheza sana hii michezo ya kuchafua vyama vingine. Ona sasa Kikwete mwenyewe kaingia kwenye game.

Chadema na vyama vingine vya upinzani, wajibuni ccm accordingly. Wao ndio wadini wakubwa kabisa.
 
Wanachokifanya ni propaganda. Bahati mbaya wanawatukana viongozi wa dini. They are muflisi, majitaka.
HATUDANGANYIKI. Aliyekuwa akiuliza mchango wa Kingunge ndio huo wa kumlisha majitaka maskini Kikwete!
 
Nilitamani sana angesema kwa confidende kama slaa anavoanikaga ujinga wao live na kutoa ushaidi wa kutosha ili tumuelewe!! angesema kwenye mkutano wa slaa uliofanyka tarehe flani siku flani mahali flani alisema hv na hv na hv tungeleewa coz naapa cjawahi kuckia hata cku moja hata kwenye taarifa ya habari wakati wakionesha mikutano baadhi ya kikwete na slaa ckuckia mahali slaa akiongea kubagua dini wala kabila wamtake radhi kwanza na wamuombe mwenyeenzi mungu awasamehe kwa kumnenea dr.slaa maneno kama hayo!!! hyo ni kashfa na matusi humo humo.. sisiem ina maisha mafupi kama umeme wa LUKU
 
hivi nauliza. Kushtukia dili kwamba wazee wa zamani wanajipanga kuiba kura ndo kuhubiri kumwaga damu . kwahiyo mzee wa zamani alitaka watu wakae kimya tu wakati wao wanajipanga kuchakachua hizo kura..ndo kudumisha amani huku.DAMU HAIMWAGWI ILA WATU WATAKUWA MAKINI NA HAIBI MTU KURA MWAKA HUU
 
Naona na membe naye anaongelea Udini, naona hii agenda ya Udini ni ya CCM, na zaidi ya hapo anadai jk ana uzoefu wa uongozi miaka 30, 10 waziri wa mambo ya nje, 5 uraisi 4 mwenyekiti wa ccm, pia amekuwa mwenyikiti wa au, sasa mwenyekiti wa eac, na kwamba anapendwa dunia nzima, na ukitaka maendeleo ushike dunia, sasa huo uwenyekiti wa au/oau ni wakupewa sio kwamba mtu awe makini ndio anapewa, mfano hata amini aliwahi kuwa mwenyekiti wa oau/au, na huo wa afrika mashariki ni wa kuzunguka kat ya nchi za afrika mashariki, hivyo raisi hata awe lipumba/slaa nk ikifika zamu ya tanzania watakuwa wenyekiti wa hiyo jumuiya, kuhusu mendeleo mbona museveni au kibaki au kagame hawasafiri kama kikwete ili kuishika dunia na uchumi wao unakuwa kwa haraka zaidi ya wa tanzania??? kweli tunaongozwa na vilaza wengi kweli kweli, sasa waziri wa mambo ya nje akiwa hivyo anaweza kutetea kweli maslahi ya nchi dhidi ya uganda, rwanda, kenya au burundi, au zambia, malawi nk? kuishika dunia unatakiwa uishike si kwa kujipendekeza au kuomba misaada bali kwa kuhudi na maarifa, chini imepiga hatua si kwa kujipendekeza kwa amerika au uingereza.
 
CCM ndio Wanaohubiri udini ,kuna waraka nimepata kutoka kwa rafiki yangu unasema "tusimchague kafir" unaenezwa na baadhi ya waislamu kwa ufadhiri wa CCM. CCM wapo hoi na wameona nyia ya kuwarudisha ikulu ni kuhubiri udini na ukabila



Chagua SLAA elimu bure afya bure.
 
Luteni Makamba mbona huwa ana-quote mistari ya Biblia na Quran kila uchao na amewahi kutunga kitabu kwa kutumia misahafu hiyo miwili, pia alipokuwa Mbeya Vijijini kwenye kampeni za uchaguzi mdogo ambapo Mch Lakson Mwanjala alichaguliwa kuwa mbunge wa Jimbo hilo Luteni Makamba alisikika akisema kuwa Jimbo hilo linastahili kuongozwa na Msafwa kama lilivyo Jimbo lake kuongozwa na Msambaa!
Anyway, JK ajiulize ni kwa nini udini anaodai upo umeongezeka katika kipindi chake kuliko wakati mwingine wowote uwao! Kama ana akili atagundua kwamba ni yeye aliyeivalisha Ilani ya Uchaguzi ya CCM, 2005 kibaraghashia kwa kujumuisha mambo ya Kadhi, na hapo ndipo mambo yalipoanza kuharibika!
 
Kwa lugha hiyo aliyoizungumza hapo juu, huyu mzee atatuletea machafuko. Kaishiwa hoja sasa anataka kutoka madarakani akiacha nyuma moto unawaka. Ni mbinu ya ki-kamikaze hii!
 
ndio maana nawaomba saaana saana wazeee wa CCm hususana waliowahi kuwa Maraisi Alhaji Ali Hassan Mwinyi na Che Nkapa infwakt, mkapa aende kwa Mzee Mwinyi wajadili ili suala sasa sijui nani ataanza kumpigia simu mwenzake ili wakaliongele hili suala , halafu waombe ushauri wa usalama wa taifa wa hali ilivyo , baada ya hapo wamwite Mwenzao Jakaya Mrisho Kikwete
na kumuomba ajitoe kwa faida ya nchi, baada uchaguzi tuanze kutibu ili tatizo kwa kuwapa wananchi maendeleo ya kweli. na kuondoa hii dhana ya fulani kaonewa nk
 
Ahadi sijui zimeisha sasa amehamia kuwapaka matope wapinzani wake, lakini licha ya juhudi zao zote lakini wapiga kura bado wapo makini na wanachuja kila wanaloambiwa. Huyu jamaa asipoangalia atakufa kwa presha!![/QUOTE]

Imeshapand sana, ndiyo maana akili sasa inayeyuka!
Alienda Mafia , akasahau kwamba amerudia ahadi zile zile za mwaka 2005, na akawaambia kwamba pesa alizotoa za maendeleo TZS 200M zimeliwa na wajanja. Bahati mbaya mmoja wa wajanja aliokuwa anawasema ndo mgombea ubunge kwa tiketi ya CCM, amabaye pia ndiye mbunge aliyemaliza kipindi kilichopita.
Sasa mafia almost wote ni waisilamu, na wamemshitukia kwamba kawafanya mabwege...hivyo hawampi kura! Nawashauri Slaa na Lipumba wakaziombe hizo kura za Mafia Island, JK hazipati hata iweje.........
 
Kumaliza hii sumu ya Lindi, Mtwara, Pwani; basi Dr. Slaa ende huko mara moja kuondoa hii takataka ya Jk kwa watu mara moja, mtu ukishindwa kubali yaishe siyo kuleta habari ya udini ( Wakristo na waisalamu wanakaa pamoja). kama kuna vitu halisahau Ikulu ende achukue mara moja na siyo kueneza sumu ya udini na kutuharibia nchi yetu. Mafisidi na uongozi mbaya haoni ndio unamkula sasa sio kitu kingine. Iluku sio mahali ya kukimbilia na sasa kutoka unashindwa - Marekani utaenda kwa pensheni yako!
 
Mpeni pole jamani, anaonyesha rangi yake halisi.
Mie nasikiliza siku zote Radio imani ili nipate mawaidha ya Kiislamu hususani kwenye mahusiano na maisha.
Lakini tangu Slaa aingie kwenye kinyanyang'anyiro cha uraisi , mambo yamebadiklika kabisa! Wale watu wanahubiri mabo hatari sana, na wanasoma magazeti ya Rostam na Habari leo tu! Na siku wakisoma mwananchi, basi hukwepa kabisa kusoma habari za Dk Slaa.
Siku moja asunuhi ya Radio Imani na Magazeti, yule msomaji alisoma habari ya matokeo ya kura za maoni yaliyoonyesha kwamba Slaa anongoza...Mtume! alipiga astaghafirtuah, akajilaumu akasema " Ah, habari zingine zinatia hata kinyaa kuzitamka" , na hapo hakuendelea kusoma gazeti la Mwananchi! Hapo ndipo alipotufikisha Rostam na Waarabu wenziwwe wa Morogoro, huku wakipata baraka zote za uongozi wa juu wa CCM akiwepo Kapten Gerge Mkuchika, ambaye ametishaia kuyafungia magazeti ya Mwanahalisi na Mwananchi!
Siamini kwamba huyu ndiye JK tuliyekuwa tunasimama barabarani kushangilia misafara yake tukidhani tumepata mkombozi!
Ee Mungu, u wapi hata haya yaendelee Tanzania zama hizi za Sayansi!
 
huyu wa kushoto naye anataka ubunge kwa ticket ya chadema

SUGU.jpg
 
Nimekuwa nikifuatilia kwa muda mrefu kauli na matamko mbali mbali ya mheshimiwa rais. Lakini kinachotia shaka ni kuwa inaonesha hali ndani ya CCM si nzuri na sitaki kuamini kuwa mheshimiwa rais wa nchi ameshindwa kabisa kupata waendeshaji wazuri wa Kampeni. Mambo yanayofanywa na kampeni machinery ya Kikwete sometimes yanaonesha tatizo kubwa sana alilo nalo rais mwenyewe.... Uwezo mdogo. Uwezo mdogo wa kuchambua mambo na uwezo mdogo wa kuongoza.

Mheshimiwa rais amekuwa akitembea na furushi la ahadi, ahadi zingine zikiwa zile zile alizoahidi mwaka 2005. Huku akiziboresha kidogo tu kwa maneno. Mheshimiwa rais amenyanganywa ajenda ya kupambana na ufisadi na amekubali kushindwa. Yaani amekubali kuwa ufisadi hauoni .... au haupo, huku katika baadhi ya kampeni zake akilalamika kuwa mambo hayakufanyika kwa sababu ya watu walioko huko. Niliwahi kumsikia akilalamika huko Tunduru kuwa kuna fedha ilishatolewa ila imekwamia pale wilayani. Hili jambo linatia aibu, rais anakili kuwa watu wa wilayani hawawezi? Au anadanganya watu?

Nawaheshimu washauri wake kama Kina January Makamba. Naamini January ni msomi kijana tena mwenye exposure ya kutosha. Ila wasi wasi wangu ni kuwa je January kweli ana influence katika yale anayoongea Mheshimiwa Rais? Inaelekea kazi yake inaishia kuandika tu hotuba!! Tena kwa viongozi wa nchi ya dunia ya Tatu wasiojali sana wananchi wanawaonaje provided wana vyombo vya dola chini yao, hizo hotuba mara nyingi rais mwenyewe huzichakachua kwa kuongeza maneno kibao ya kwake mwenyewe.

Sasa nije kwenye hii hoja ya udini. Ni kuwa CCM wameamua kuingia kwenye strategy ya kutisha watu. Mwalimu Nyerere aliwahi kusema ukimsikia mtu analalamikia sana udini, mwangalie vizuri sana, utakuta udini anao yeye mwenyewe. Sidhani kuwa PR strategist wa Mheshimiwa Kikwete wanamshauri atumie udini kama sera yake ya kuingilia ikulu. Inawezekana ni fear zake tu anazojazwa na washauri wengi alionao. Lakini lililo wazi kabisa ni kuwa kampeni hzi za kutisha watu na udini hazimjengi yeye!! Akumbuke kuwa yeye anagombea akiwa ni mkuu wa nchi vile vile. Kuna faida zake na hasara zake vile vile. Hasara zake ni kuwa haya anayoyalalamikia ni mambo ya jinai. Sheria zetu za uchaguzi zimeharamisha kampeni za kutumia dini na kabila na mheshimiwa Rais Kikwete ndo mtekelezaji mkuu wa sheria zetu. Ina maana watu wanapita majukwaani wakivunja sheria za nchi kwa kisingizio cha uchaguzi halafu mheshimiwa rais anawaachia tu ili aje walalamikie wananchi? Ndo kama yale ya kusema serikali yake imetoa hela ila zimenasa wilani? Hao waliozikwamisha fedha zilizotolewa na serikali amewachukulia hatua gani? Au anataka awaambie watu kuwa mfumo wa serikali haufanyi kazi?

Na hili la kampeni za udini, anataka kutuambia kuwa mfumo wa serikali anaoungoza umeshindwa kudhibiti uvunjwaji wa sheria, halafu anataka bado tumuamini kwa kumpigia kura?? Hawa wanaomshauri mheshimiwa Rais Kikwete wamkalishe chini! Asiwe anaongea hearsay anazozisikia zikisemwa na watu jamani, yeye ni rais. Awe anasema kile kilichoandikwa tu!! Hawa kina Slaa wakimgeuzia kibao (nashangaa slaa hajalibebea bango vizuri suala hili) rais hana pa kujificha. Kampeni ya mheshimiwa Kikwete ni Mbofu mbofu sana. Sasa labda tusema Mheshimiwa rais mwenyewe ndo si makini hivyo?? Kampeni yake imejaa gaffe tupu. Kuwabeba mikono kina Mramba wenye kesi za ufisadi zilizoanzishwa na vyombo vya dola anavyovisimamia mheshimiwa Kikwete si ni uingiliaji wa wazi wa mwenendo wa uchunguzi? Hivi ni mtendaji gani aliyeko chini ya rais ambaye ataendelea kumchunguza mtu ambaye rais mwenyewe ametamka mbele ya hadhara kuwa ni mtu safi??

Hawa kina Lowasa na Kina Chenge ni liability kubwa kwa rais, lakini amekubali kufa nao! Sasa mbona hakukataa kujiuzuru kwa Lowassa kama anaamini Lowassa ni mtu safi. Mkapa aliwahi kumuondoa uwaziri Mheshimiwa Juma Ngasongwa, Baadaye akamrudisha tena katika baraza la mawaziri baada ya kuona kuwa hakuwa na makosa.

Amekuwa akimtetea Lowassa wazi wazi mbele ya umma, lakini haijawahi kutamkwa kuwa hii Richmond ilikuwa mali ya nani!! Au Richmond haikuwahi kuwepo? Watu waamini hivyo? Mambo contraversial kama hayo mheshimiwa rais ilitakiwa ajitenge nayo. Lakini ameshindwa kukubali kuwa kuna jinai, na ameshindwa kukubali kuwa hawa watu wana makosa. Sasa mambo kama haya yanamfanya aonekane hana msimamo, anasimamia nini? Kama unajua na ana uhakika kuwa Lowassa hakuwahi kuwa na kosa, anashindwa nini kumrejesha madarakani??

Rais, kwa kukemea wanaotumia udini bila kuwachukulia hatua za kisheria tu; hata CCM kupeleka malalamiko dhidi ya watu hao kwenye tume ya uchaguzi, ni ishara wazi kuwa udini ni yeye anayeutumia. Na hatutashindwa kusema Mheshimiwa Rais amefirisika kisiasa!! Sasa anakimbilia udini ili iwe ndo gamba lake!! Mediocrity!!
 
Back
Top Bottom