Kikwete tangaza hali ya hatari - Kiula

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,005
Kikwete tangaza hali ya hatari - Kiula

na Kulwa Karedia
Tanzania Daima~Sauti ya Watu

WAZIRI wa zamani wa Ujenzi, Nalaila Kiula, amemtaka Rais Jakaya Kikwete kutangaza hali ya hatari ili kulinusuru taifa na wimbi la ufisadi.

Akizungumza jana na Tanzania Daima Jumapili nyumbani kwake Mikocheni, Dar es Salaam, Kiula alisema kutangaza hali ya hatari ndiyo njia pekee itakayomsaidia Rais Kikwete kuanza kuwashughulikia watu ambao sasa wanaonekana kuwa matajiri wa kupindukia.

“Napenda kumshauri Rais Kikwete kutangaza hali ya hatari kwa kipindi hiki ikiwa ana lengo dhidi ya viongozi wote wanaotuhumiwa kujihusisha na vitendo vya kifisaidi… hii itamsaidia kuelewa mbaya ni yupi,” alisema Kiula.

Alisema kama Rais Kikwete hatachukua hatua za makusudi, taifa linaweza kuingia kwenye machafuko yasiyotarajiwa kwa vile kumekuwa na matabaka mawili ya matajiri na maskini.

“Tusipoangalia tutajikuta taifa linaingia kwenye machafuko, hivi sasa tayari kuna matabaki ya matajiri na maskini, jambo hili ni baya na linapaswa kuchukuliwa hatua haraka. Siku wananchi wakikasirika matokeo yake yataonekana,” alisema Kiula.

Alisema vita ya kupamba na mafisadi itafinikiwa iwapo Rais Kikwete atakubali mtangulizi wake, Rais mstaafu Benjamin Mkapa kuhojiwa na vyombo vya dola kwa kuwa anatuhumiwa sana kuhusika na kuwepo kwa vitendo vya ufisadi miongoni mwa watumishi wa umma wakati wa utawala wake.

“Tutakuwa tunajidanganya kama Rais mstaafu Mkapa asipofukuliwa maovu yake… yeye ndiye aliyetufikisha hapo tulipo mpaka sasa, tunaandamwa na mafisadi kwa sababu yake, kwa vile kuna mikataba mingi yenye utata iliyosainiwa wakati wa utawala wake,” alisisitiza Kiula.

Alisema kama Rais Kikwete anataka kujiweka katika hali nzuri ya utawala anatakiwa kutoa haraka orodha ya majina ya watu wanaohusishwa na upoteaji wa fedha Benki Kuu (BoT) kupitia akaunti ya malipo ya madeni ya Nje (EPA).

“Sasa hivi hali inatia kinyaa, kila kona mafisadi, hapa njia pekee ni Rais Kikwete kutoa kibali cha kukamatwa wale wote wanaotajwa majina yao katika kashfa hii ili liwe fundisho kwa wengine,” alisema Kiula.

Katika hatua nyingine, Kiula aliwataka Watanzania kwa imani zao kumwombea Rais Kikwete kila siku ili aweze kupambana na hali ngumu inayomkabili kuhusu wasaidizi wake.
 
Tulisema tangu zamani rais amepewa madaraka ayatumie lakini kwa njia moja ama nyingine ameamua kuyafumbia macho mafisadi na kauli ambayo aliitoa ni kwamba WAUZA UNGA WAJIREKEBISHE hivi kweli tulichagua rais ambaye hana meno?

Tumia madaraka yako JK utaingia kwenye historia ya kuwashughulikia MAFISADI. Ikumbukwe Ali Hassan Mwinyi alipewa fagio la chuma hata lilikoishia kule magogoni hatuelewi sasa na wewe sijui tukupe nini?
 
Ninyi wote wezi wa Tz, Mungu atakuja awachome kwa moto na kiberiti. lakini, kabla ya hapo, sisi wenyewe watz itabidi tuwachome kwa moto hapahapa kwanza.
 
naona anaanza kujirudisha kwenye system ya siasa taratibu.....ale kona ndio walewale kama uzalendo angeuonyesha wakati akiwa kwenye kiti
 
Matatizo ya viongozi wa Tanzania ni kutaka kusikika wakiongea kwenye vyombo vya habari na kuhutubia kwenye mikutano ya kisiasa. Ukija kwenye utendaji ni ziro kabisa.

Afadhari ditto amejifia kuepusha shari. Mungu ailaze pema roho ya Marehemu Ameen.
 
Alicho kisema kina make sense ? Kama nina make sense then let us join him .
 
Ndugu wana jf;
Ni wazi kuwa tumeshalipigia kelele sana hili suala la Ufisadi hapa jf!Tulishawahi kuweka wazi kwenye thread kadhaa..nyingine ambayo pia niliianzisha..kwamba Mh Rais alitakiwa atangaze "state of alertness"kwani issue ni ya kushtua mno!Lakini kumbe wenzetu wako kwenye dunia ya tofauti mpaka watoke madarakani ndio wana uwezo wa kuona kuwa hali ni ya hatari!Kwa taarifa yao sisi hapa jf,tanzania pamoja na wengine wote waliopo around the world tulishaweka wazi kuwa hii issue lazima iende na watu.Kiula tunamkaribisha licha ya kwamba tunajua ana bifu na Mkapa!Wananchi hawana haja ya kuanza kufikiria ni nani wa kumpa madaraka!BALI WANANTAKA UWAJIBIKAJI ILI NEXT TIME YEYOTE ATAKAYEPEWA MADARAKA AJUE CONSEQUENCES ZA UFISADI!Wana jf sisi sasa hivi hatutaki ushabiki wa vyama uchangaywe na issue ya ufisadi..Hii ni kwasababu hata wapinzani wenyewe wakipewa madaraka kabla ya mafisadi kuwajibishwa then hata wao hawataogopa kuitumia system mbovu na sheria tata zilizoachwa na mkoloni kuendelea kumyonya mtanzania mwenzake!Accountability first...then watakaopewa madaraka later watajifunza kutokana na historia!Wananchi wajue kuwa tuko vitani!Vita dhidi ya UFISADI!Vita ambavyo ni lazima either wananchi ama mafisadi mshindi ni lazima apatikane!Na kama mafisadi wakishinda..then historia itakisuta kizazi hiki mbele ya vizazi vyetu vijavyo kwani havitaamini kwamba tulikuwa na akili timamu kama ufisadi ukiprevail!On the other side kama tukishinda then tutakuja hapa jf tena kwa niaba ya wananchi kujipongeza na kujijengea historia madhubuti na ushujaa wa kushinda vita hivi dhidi ya ufisadi!Long live Tanzania..LONG LIVE ITS PATRIOTIC PEOPLE!
 
kutangazwa hali ya hatari pasipo dhamira ya makusudi kupiga vita ufisadi kunaweza pia kutumika kuwalinda mafisadi.
 
kutangazwa hali ya hatari pasipo dhamira ya makusudi kupiga vita ufisadi kunaweza pia kutumika kuwalinda mafisadi.
Hapa jf wengi wetu tuko against na mafisadi na si for mafisadi fo sure!Hivyo ni wazi tuwe pamoja kwenye hili bila spin ya upotoshaji wa namna moja ama nyingine..either kwa bahati mbaya ama makusudi..its obvious we're not here to judge..but time will reveal and eventually be the measurement as to who we really are!
 
Alichofanyiwa Kiula na Mkapa ndicho anataka na viongozi wengine wafanyiwe ni vema maana yeye alifikishwa kizimbani pamoja wasaidizi wake baada ya kujenga barabara nyingi mbovu akiwa waziri wa Ujenzi.Alipelekeshwa mpaka mkewe akafa kwa kind of BP .

Sasa anachodai ni sahihi kuwa watuhumiwa wafikiswe mahakamani ila yeye pia hakuwa msafi.Ila hiyo hali ya hatari sijui inahusu nini hapo somebody break it down for me maana mm najua kukiwa na machafuko ndio inatangazwa ama operation itakayo tumia nguvu ya kijeshi.

Ila hapa kinachotakiwa ni wanainchi kuishinikiza serikali kuwa hawa watu wenye tuhuma wafikishwe kwenye mikono ya sheria maana utamshauri nini huyu hambiliki kwani yeye hajui kinatakiwa nini si atakwambia kelele za mlango tu hizo.Yeye mwenyewe yumo kwenye baadhi ya ufisadi ndio maana mzito.Au tunasahau uchaguzi ulivisha nguo ,kofia Tz nzima ni pesa ile.
 
Inaonyesha jinsi gani Kiula alivyo na usongo na hasa baada ya kutemwa ktk FAMILY...........Kiula you are not genuine
 
hivi anajua maana ya kutangazwa ka hali ya hatari? Au anadhani rais atasema "hey guys, nimetangaza hali ya hatari!"
 
naona anaanza kujirudisha kwenye system ya siasa taratibu.....ale kona ndio walewale kama uzalendo angeuonyesha wakati akiwa kwenye kiti


Inawezekana kuwa alikuwa FISADI, lakini ikumbukwe kua Kiula yeye naye alishughulikiwa na mkapa. Hivyo anayodai ni haki tupu, yaani nao wenzake wenye VIJISENTI vyetu washughulikiwe, tena haraka sana.
 
Natumani ataclarify his position kabla ya Jumanne, vinginevyo tutamuonesha kuwa pendekezo analotoa siyo zuri na ni hatari kama nini.
 
Mimi namuunga mkono Kiula kimsingi kwamba Tanzania inahitaji "Emergence Laws" kushughulikia mafisadi. Watu kama wakina Chenge na wale wote waliohusika na EPA, Richmond, Buzwagi etc walitakiwa washughulikiwe na hizo emergence laws kwa kuwekwa kwanza kizuini huku uchunguzi unaendelea. Mkapa naye angeshughulikiwa na hizi hizi emergence laws mpaka ataporudisha mali za Taifa na yeye mwenyewe kutumikia adhabu jela.

Kinyume na hapo tutaendelea kusoma hadithi magazetini tu jinsi watu walivyoiba fedha zetu; yote ni kwa sababu Katiba yetu kama ilivyo ina mianya mingi ya kuponea hawa mafisadi.
 
Mimi namuunga mkono Kiula kimsingi kwamba Tanzania inahitaji "Emergence Laws" kushughulikia mafisadi. Watu kama wakina Chenge na wale wote waliohusika na EPA, Richmond, Buzwagi etc walitakiwa washughulikiwe na hizo emergence laws kwa kuwekwa kwanza kizuini huku uchunguzi unaendelea. Mkapa naye angeshughulikiwa na hizi hizi emergence laws mpaka ataporudisha mali za Taifa na yeye mwenyewe kutumikia adhabu jela.

Kinyume na hapo tutaendelea kusoma hadithi magazetini tu jinsi watu walivyoiba fedha zetu; yote ni kwa sababu Katiba yetu kama ilivyo ina mianya mingi ya kuponea hawa mafisadi.

Tatizo la hali ya hatari na hizo unazosema imergence laws, zinaweza kukosa macho na kuwakumba hata wasiohusika (inaweza kutumika kulipa visasi). Unaweza kushangaa hata wewe, JF ndani kwani inategemea utashi wa wanaoendesha operation. Ni rahisi kutamka ila shughuli yake ni hatari.
 
Back
Top Bottom