Kikwete siyo safi! - yes I said it!

Tatizo letu weusi nafikiri ni ile ubwana tuliyorithishwa na wakoloni.watu waliyopata unyapara walikura daraja la pili. wazungu walikuwa daraja la kwanza. walipoondoka wazungu watawala wakawa ndo daraja la kwanza.hii hali haijatoweka miongoni mwa watu weusi, bado inatutafuna.watumishi wanadhani wao ni bora kuliko wengine kwaiyo wanahitaji vingi kuliko wengine.Watumishi hawajibiki kwa umma kama ilivyokuwa enzi za ukoloni. Kikwete na watu wake wanajifanya mabwana na si watumishi.Mkuu wa jeshi mwanasheria mkuu, usalama, makatibu wa kuu, mawaziri,wakurugenzi, wabunge, wote ni mabwana.Kwaiyo mwananchi yupoyupo tu kupiga kura basi. Mikataba ya mali ya umma ni siri. Dhana ya mali ya umma iko wapi?Ni mali ya mabwana.Wananchi hatuna chetu. Kama mali ni yetu mikataba isingekuwa siri. Kwaiyo wakina kikwete na mawaziri kwa sababu ni mabwana mikataba kwanza lazima iwafaidi wao basi na si umma. Tuanze upya.Kila mwananchi anakijanawake lazima naye awe na maisha mazuri siyo kijana wako kuwa mtumishi wa kijana wa mwanamke mwingine.Vita vya iddi amini watanzania wote walishiriki kwa kutoa maisha yao na mali yao na siyo mrisho kikwete,RA, lowasa,mramba, peke yao.haitawezekana kamwe. NIMEWAKILISHA
Zhule, umeongea makubwa na yaliyo kweli mtupu. Mi binafsi nakuunga mkono 100%. Sisi waafrika tunahitaji KUJIKOMBOA KIFIKRA. Bado kasumba za kikoloni zinatutafuna, na zitaendelea kututafuna. Tunapenda kuwa mabwana tukipata nafasi, na kupalilia ubinafsi - ufamilia badala ya Utaifa. Huko tutatoka lini? Kazi ipo kwelikweli.
 
Although a couple of months have lapsed withought giving my comments, that cannot stop me from telling the truth.

Mwanakijiji asserts that JK SIYO SAFI" Yes to some extent I can I gree with him as Kikwete being a Humanbeing cannot be perfect by a hundred percent. But the point is that, all evils" ufisadi" available in our country today have their genesis from Mkapa's regime.The issue of Richmond company did not start during Kikwete regime!!!.

After all, Kikwete at that was just a minister who used to receive instruction from his Boss Mkapa. The issue was a collective responsibility of all Government system. From President to the last office messinger of the state.In that situation, what would you expect Kikwete to do? Had he pretended to be Samaritanian and challenged his coleagues, today he would not be a head of state any more.

CCM' PRINCIPLE " If you challnge the, you will be persecuted openly. Do not forget what happened to Kolimba. Although he was CCM Member by blood, he was persecuted because of being honest, and royal to his country.

It seems to me that most complainers do not know exactly what the cause of corruption and why it happens in our country.Today I will not talk more about it as its time is not due and more over is out of the subject of my concerns for today. But most important is that, our great enemy in Tanzania is Benjamin Mkapa. He is the one who reached our country at the place where it is today. He was the one to sell our country to false foreign investors.

From financial, Industrial to Mineral sectors all were sold to his friends. And Kikwete was just a messenger of Mkapa during that time. Hence, if you(M/KIJIJI) were him, would you be ready to be victimised at the expense of other government officials? That is, to be ready to lose your job, as such, you and your family suffer, because you want to appease general public?

Kikwete is not an angle or Prophet. He is just a normal human being like yuo and I.He has alot of commitments to fulfil.Let us first raise our cmmon concers about the arrest of all Fisads- including Mkapa and prosecut them. We should not raise our concers based upon theological extrimism or rather basing on tribalism and forget that we are all passengers who sailing on the same boat.If it snks, not only some specific passengers gonna die but all.

Public interest must be given first priority, not religiously.
 
Jamani, hebu tukumbushane iwapo nitakuwa nimekosea. Taarifa ya Luhanjo ya jana ni taarifa ya kwanza kabisa ya Ikulu (yaani ya JK) kuhusu Richmond?

Tukio la karibu sana na hilo lilikuja wiki chache baada ya EL kuanguka, Jk aliwaambia wazee wa CCm wa Dar kuwa ilikuwa ni ajali ya siasa. Hakugusia kabisa Richmond kwa undani wake. Sikumbuki iwapo Ikulu ilisema chochote kuhusu richmond, hata hayo yaliyosemwa katika taarifa ya jana ya Luhanjo Ikulu haikuwahi kuyasema hapo nyuma.

Ingeyasema huko nyuma, angalau JK angepata kauhalali ka-kusema: 'nilishazungumzia hili: kwamba Richmond ilikuwa ya kitapeli tu.'

Sasa anabwata nini? Kwa kuwa maji yanaanza kufika shingoni? Kama alilikoroga, si bora alinywe tu?

Na uko wapi ule 'ujasiri' wake aliouonyesha mwaka jana Bungeni (tarehe kama hizi) pale alipoligeuza Bunge kuwa mahakama yake na kujipachika u-CID, u-prosecutor na ujaji alipotoa hukumu dhidi ya wezi wa EPA?

Hatujasikia tena mkazo wa hukumu hasa kwa wale “waliorudisha’ hela na pia kutueleza nani alirudisha ngapi.

Au anataka tuamini kuwa mamilioni “yaliyorudishwa” yalishanunuliwa mbolea na wakulima mikoa kadha wameshafaidika, na kwa hiyo “file closed?”

Kwa nini safari hii asiende tena Bungeni na kulifanya tena mahakama na atoe “hukumu” dhidi yake mwenyewe na watu wake kwamba hawahusiki na Richmond na kwa hiyo “case closed?”
 
Although a couple of months have lapsed withought giving my comments, that cannot stop me from telling the truth.

Mwanakijiji asserts that JK SIYO SAFI" Yes to some extent I can I gree with him as Kikwete being a Humanbeing cannot be perfect by a hundred percent. But the point is that, all evils" ufisadi" available in our country today have their genesis from Mkapa's regime.The issue of Richmond company did not start during Kikwete regime!!!.

After all, Kikwete at that was just a minister who used to receive instruction from his Boss Mkapa. The issue was a collective responsibility of all Government system. From President to the last office messinger of the state.In that situation, what would you expect Kikwete to do? Had he pretended to be Samaritanian and challenged his coleagues, today he would not be a head of state any more.

CCM' PRINCIPLE " If you challnge the, you will be persecuted openly. Do not forget what happened to Kolimba. Although he was CCM Member by blood, he was persecuted because of being honest, and royal to his country.

It seems to me that most complainers do not know exactly what the cause of corruption and why it happens in our country.Today I will not talk more about it as its time is not due and more over is out of the subject of my concerns for today. But most important is that, our great enemy in Tanzania is Benjamin Mkapa. He is the one who reached our country at the place where it is today. He was the one to sell our country to false foreign investors.

From financial, Industrial to Mineral sectors all were sold to his friends. And Kikwete was just a messenger of Mkapa during that time. Hence, if you(M/KIJIJI) were him, would you be ready to be victimised at the expense of other government officials? That is, to be ready to lose your job, as such, you and your family suffer, because you want to appease general public?

Kikwete is not an angle or Prophet. He is just a normal human being like yuo and I.He has alot of commitments to fulfil.Let us first raise our cmmon concers about the arrest of all Fisads- including Mkapa and prosecut them. We should not raise our concers based upon theological extrimism or rather basing on tribalism and forget that we are all passengers who sailing on the same boat.If it snks, not only some specific passengers gonna die but all.

Public interest must be given first priority, not religiously.


Mzee wa fungu mbona sijakuelewa ? yaani kwa ujumla JK si msafi ni kuanzia akiwa waziri hadi Rais hata kama alikuwa anapokea amri yeye anatekeleza .The bottom line ni hii kwamba he is not clean na hawezi kusafisha nyumba kwa kuwa amezoea uchafu
 
The issue of Richmond company did not start during Kikwete regime!!!. After all, Kikwete at that was just a minister who used to receive instruction from his Boss Mkapa.

we bwana utamdanganya nani? issue ya Richmond ni ya 2006, ilikuwaje Kikwete apokea amri za Mkapa mwaka 2006? Kumbukumbu tunazo aise,huwezi kutudanganya watu wazima sisi, revise your notes.

unaweza pia kusoma Tamko la Luhanjo hapa: https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/35210-tamko-la-ikulu-juu-ya-richmond.html
 
The issue of Richmond company did not start during Kikwete regime!!!.

After all, Kikwete at that was just a minister who used to receive instruction from his Boss Mkapa.

Let us first raise our cmmon concers about the arrest of all Fisads- including Mkapa and prosecut them.

Kwenya NyekundU:

Suala la Richmond lilianza lini?

Kwenye Blue:

Ikulu inasema Kikwete hausiki coz he was president na wahusika ni mawaziri sasa unapingana na Ikulu?

Kwenye Magenta

Hakuna JIWE Litakalosalia


Asante
 
Ndugu zangu,ni lini tutakoma kuibiwa? kikwete ni dhahili ya kuwa ni kibogoyo hana meno kwa hivyo hawezi kungata au ana meno ambayo hayana makali au ana meno ambayo hayana sumu hivyo hata akingata hayaumizi ila watanzania wanashangaa ya wapi meno aliyopewa na aliyoahidi kuyatumia kwa manufaa ya watz.Nilishawahi kusema ni ndoto kuwachulia hatua watu kama Rostamu na Lowasa kwa kuwa kikwete ni sehemu yao na hawawezi kufanya lolote alafu kikwet asijue.Kwa ujumla hana uwezo wa kuongoza nchi maana anapotakiwa kutoa maamuzi ya kuonyesha kuwa yeye ni Rais wa nchi na si rahisi wa nchi yeye anatulia tuli kama hakuna jambo linaloendelea sijui niseme mangapi huyu bwana antuboa sana pamoja na kwamba atapita kwa kishindo mwakani kama ujuavyo tulivyo watz.Kikwete ni namba moja kwenye ufisadi hawezi kuwachukulia hatua wateule wake maana yu sehemu yao.NINACHO KWENU NDUGU ZANGU WATANZANIA,HATATOKEWA KIONGOZI YEYOTE NDANI YA CCM ANAYEWEZA KUTUFIKISHA TUNAPOTAKA SYSTEM NZIMA IMEOZA HATA AJE NANI LAKINI AKIWA NDANI YA CCM HATAWEZA KUONDOA MISINGI YA KULINDANA.USHAURI WA BURE,TUIONDOE CCM ILI SYSTEM YOTE IBADILIKE
Mwanakijiji,

Hii makala yako ina madai mapya, naomba kama unaweza fafanua juu ya hili suala la Lowassa kukutana na Karamangi London. Mimi sijawahi kulisikia, kama ni kweli basi huenda hapo sio tu kuna moshi mkubwa bali hata moto wenyewe unawaka. Kwanini Lowassa akutane na Karamangi kinyemelea?

Pili hili la Kampuni ya Tanzania Royalty Exploration, je ni kweli Msabaha na JK wana hisa? Kama ni kweli basi pia hapa
patakuwa na moto mkali.

Kama madai yako yote haya Mwanakijiji ni sahihi, basi nchi yetu imekwisha. Huyu JS amefikaje mpaka kuwa karibu na JK?

Manyang'au yanatunyang'anya sisi maskini hata kile kidogo tulichopewa na mungu kwa kuwatumia watu ambao tumewaweka madarakani kwa mbwembwe zote na kuwapa kila tulicho nacho ili waishi vizuri na wasipate tamaa, lakini wao wameamua kutusaliti na kuwa mafisadi.

Kweli inasikitisha sana!
 
Hongera kwa uchambuzi wako ndugu MWANAKIJIJI.

Pamoja na mambo mengi ya busara forum hii inavyo jitahidi kufanya ili kurekebisha maadili, nami ningependa kuchangia kidogo.

Japo wahenga husema kuwa samaki mmoja akiooza basi wote hali moja, kwa upande wa kapu la CCM na serikali yake samaki wote kimsingi wameoza hivyo ni vigumu mmoja kuwa mzima. Maovu mengi ya CCM kila mtu anayajua na mengi furum hii imechangia sana kuyalipua, sasa nini kifanyike?

Nionavyo mimi, JK pamoja na udhaifu wake unaotia kichefuchefu, mi nna machache ya kusema.

Utawala uliopita ndio uliomuandaa kuchukua madaraka, hivyo ilibidi naye anywe damu ya walalahoi ili afikike hapo alipo, inaonyesha kuwa uovu mwingi ambao ulikuwa chini yake na hakufanya kitu kuzuia ni kwasababu ndo ilikuwa gear yake ya kuwaacha wenzake wajichafue ili yeye apite.

Kimsingi yeye hakushiriki bali kosa lake ni hakuzuia maovu hayo alipokuwa Wizara ya madini au Fedha, kwake ilibidi afanye vile ili wenzie wamwone kuwa ni mwenzao, ndo maana wanashindwa kumlipua kwani wanajua kuwa kwasasa ameshika mipini miwili, (uchafu wao na urais).

Nionavyo mimi JK anania ya kuleta mabadiliko, japo yuko karibu kuchanika msamba katika maamuzi ya aidha kuwasaliti wenzie au wananchi walio mchagua. Mambo mengi anayo yafanya yaki maendeleo yanaonekana kimataifa na kitaifa tusipinge tu kwasabubu ya upinzani (ukiangalia uhuru wa bunge kuna transparency na debate za kweli kuliko historia nzima ya bunge la Tanzania).

Nionavyo mimi upande wa biashara na siasa kama sija kosea Tanzania hatuna sheria inayo mkataza waziri kuwa na shares au kumiliki biashara, hivyo JK yuko ndani ya misingi ya haki yake kama mtanzania wa kawaida. Halafu sioni kwanini asijaribu kuwa karibu na mtu aliye wekeza nae, kwani ingekuwa wewe Mwanakijiji ungefanyaje ungejiweka mbali na mwekezaji wako? hizo ni strategies za kibiashara tu.

Nionavyo mimi kwakuwa kapu zima la CCM limeoza je naye akiwa mmoja wao afanye nini? Kwanza na nampongeza kuwafikisha mahakamani baadhi ya mafisadi wakubwa kama Yona, Mramba, Mgonja na akina EPA (ni moja kati ya mambo ambayo asingeweza kufanya). Japo kwa wengi inaonekana ni kiinimacho fulani lakini mi naona kama ni hatua moja mbele.

Nionavyo mimi, ni maswali mengi inabidi tujiulize kama sisi, je tuna institutions za kweli za kusaidia kupambana na ufisadi na kusafisha kapu lilijaa samaki wabovu? mijadala ya hivi karibuni ya Tanesco, Bunge, Bandari, TRA, TAKURURU, Madini na Benki kuu inaonyesha ufisadi mtupu. Je tuna mahama ya kweli ambayo ni safi, FBI yetu je iko safi? DCI?

Kama ulivyosema Mwanakijiji, ukijihusisha na wezi na wewe utaoneka mwizi, lakini issue hapa ni complicated usipojihusisha nao, utajihusisha na nani wakati hakuna msafi hata mmoja?

Nionavyo mimi Tanzania tunakazi kubwa sana ya kubadisha maadili na hulka zetu za kijinga, uchafu wetu haupo kwa viongozi tu upo pia from our grass roots. Tunaishia kuwalaumu viongozi kila dakika wakati sisi ndio tunaowachagua ili walinde maslahi yetu madogo madogo. Tunapata mshahara laki na nusu, familia watoto wa tano, vimada wawili na watoto kadhaa wengine. Kila siku vikao vya kila siku kwenye baa, zungusha kwa saanaaaa. Hizo pesa tunazitoa wapi budget ya karibu mil 2 kila mwezi na sisi ni wafanyakazi wa kawaida? ofcourse lazima tumchague mtu anaye kula matawi ya juu wakati huo huo atuachie na sisi tule matawi ya chini. Culture hii ya mtanzania wa kawaida haijaanza leo, ndo maana wabongo hatuandamani hata tukikandamizwa vipi, what for?

Siku moja nilikula dinner na mkt wa chama Chadema, nikamuuliza maoni yake kuhusu CCM, hakusita kunijibu kuwa "li CCM nikama lidude fulani kubwa sana lililoshikana kwa marefu na mapana, likibiringika linabiringika kwa pamoja, likianguka linaanguka pamoja, uwezo na ufanisi wake unawazidi uwezo hata viongozi wake, ndani yake kuna mifarakano, mitafaruku, matatizo lakini nguzo zake ni imara kuliko unavyofiria"

Nionavyo mimi, ndugu Mwanakijiji CCM siyo ya kuanguka leo au JK kutoukwaa urais tena, please be reasonable, mwangalie RA pamoja na tuhuma zote hizo aliporudi kwa wapiga kura wake walimpokea kama rais, Mcheki Lowasa, Chenge and the list goes on.

Nionavyo mimi inabidi tujaribu kuzikubali juhudi za JK za kuleta utawala bora, elimu, afya na mawasiliano. Ili mkulima apate kuuza mazao yako sokoni, mwanae aende shule na mkewe apate matibabu ya uzazi hospitali. Wakati huo huo tuendelee kufaidi uwazi huu wa vyombo vya habari ambao unatuwezesha kutoa maoni yetu pale tunapo jisikia, japo sio asilimia mia (ulimsikia spika analaumu internet hapo juzi). Halafu tuendelee kushabikia wabunge wetu wakilipuana Bungeni.

Nionavyo mimi, kwa kifupi, siku moja niliposafiri kwenda mwanza kupitia Nairobi , down town Nairobi niliona maandishi makubwa yameandikwa ukutani yasemayo " KUNA MWANGA GIZANI"
 
As. usual you are right on the spot. nakumbuka maneno ya marehemu Sembene Ousmane katika kitabu chake cha God's Bits of Wood, "mother what is it that washes the water'? kwa maana nyingine huwezi hata siku moja mtu ukatumia maji machafu kufulia nguo. In short ni kwmaba JK na watu wake wa karibu wamenufaika na ubadhirifu uliopo tanzania long kabla hajaingia ikulu. JK can not bite the hand that feeds him without implicating himself. Taifa limeingia hasara.

umenikumbusha mbali kweli. nilimuuliza mwalimu aliyetuchambulia hicho kitabu na wala asinipe jibu. inawezekana wengi ni makasuku tu
 
Jamani, hebu tukumbushane iwapo nitakuwa nimekosea. Taarifa ya Luhanjo ya jana ni taarifa ya kwanza kabisa ya Ikulu (yaani ya JK) kuhusu Richmond?

Tukio la karibu sana na hilo lilikuja wiki chache baada ya EL kuanguka, Jk aliwaambia wazee wa CCm wa Dar kuwa ilikuwa ni ajali ya siasa. Hakugusia kabisa Richmond kwa undani wake. Sikumbuki iwapo Ikulu ilisema chochote kuhusu richmond, hata hayo yaliyosemwa katika taarifa ya jana ya Luhanjo Ikulu haikuwahi kuyasema hapo nyuma.

Ingeyasema huko nyuma, angalau JK angepata kauhalali ka-kusema: 'nilishazungumzia hili: kwamba Richmond ilikuwa ya kitapeli tu.'

Sasa anabwata nini? Kwa kuwa maji yanaanza kufika shingoni? Kama alilikoroga, si bora alinywe tu?

Na uko wapi ule 'ujasiri' wake aliouonyesha mwaka jana Bungeni (tarehe kama hizi) pale alipoligeuza Bunge kuwa mahakama yake na kujipachika u-CID, u-prosecutor na ujaji alipotoa hukumu dhidi ya wezi wa EPA?

Hatujasikia tena mkazo wa hukumu hasa kwa wale “waliorudisha’ hela na pia kutueleza nani alirudisha ngapi.

Au anataka tuamini kuwa mamilioni “yaliyorudishwa” yalishanunuliwa mbolea na wakulima mikoa kadha wameshafaidika, na kwa hiyo “file closed?”

Kwa nini safari hii asiende tena Bungeni na kulifanya tena mahakama na atoe “hukumu” dhidi yake mwenyewe na watu wake kwamba hawahusiki na Richmond na kwa hiyo “case closed?”
Hapo juu nilopo highlight kwa mark nyekundu ndipo ulipozungumzia ukweli hasa. Yeye alimsafisha Lowasa wala hakujitetea wala kuitetea serikali. Umegusa penyewe hasa.
 
Jamani, hebu tukumbushane iwapo nitakuwa nimekosea. Taarifa ya Luhanjo ya jana ni taarifa ya kwanza kabisa ya Ikulu (yaani ya JK) kuhusu Richmond?

Tukio la karibu sana na hilo lilikuja wiki chache baada ya EL kuanguka, Jk aliwaambia wazee wa CCm wa Dar kuwa ilikuwa ni ajali ya siasa. Hakugusia kabisa Richmond kwa undani wake. Sikumbuki iwapo Ikulu ilisema chochote kuhusu richmond, hata hayo yaliyosemwa katika taarifa ya jana ya Luhanjo Ikulu haikuwahi kuyasema hapo nyuma.


Hawakusema hapo awali kwa kuwa walikuwa wanatengeneza mpango wa kumsafisha Lowasa na wenzake kwenye hii kashfa,kwa hiyo wahakuwa na mpango mbadala.


Ingeyasema huko nyuma, angalau JK angepata kauhalali ka-kusema: 'nilishazungumzia hili: kwamba Richmond ilikuwa ya kitapeli tu.'

Sasa anabwata nini? Kwa kuwa maji yanaanza kufika shingoni? Kama alilikoroga, si bora alinywe tu?


Hili limekuwa dhahiri sasa kuwa mpango wa kumsafisha Lowasa imekwama hivyo ni lazima JK ajaribu kujitenga na Richmond ili kuficha uhusika wake.

Na uko wapi ule 'ujasiri' wake aliouonyesha mwaka jana Bungeni (tarehe kama hizi) pale alipoligeuza Bunge kuwa mahakama yake na kujipachika u-CID, u-prosecutor na ujaji alipotoa hukumu dhidi ya wezi wa EPA?


Ujasiri imekwisha baada ya mipango ya kumsafisha Lowasa kushindikana.

Hatujasikia tena mkazo wa hukumu hasa kwa wale “waliorudisha’ hela na pia kutueleza nani alirudisha ngapi.

Au anataka tuamini kuwa mamilioni “yaliyorudishwa” yalishanunuliwa mbolea na wakulima mikoa kadha wameshafaidika, na kwa hiyo “file closed?”


Hakuna mkazo wa hukumu kwa kuwa kesi zenyewe ni kiini macho tuu ili kupunguza ghadhabu za wananchi dhidi wa wezi wa EPA.

Kwa nini safari hii asiende tena Bungeni na kulifanya tena mahakama na atoe “hukumu” dhidi yake mwenyewe na watu wake kwamba hawahusiki na Richmond na kwa hiyo “case closed?”


Amepoteza ujasiri na Bunge limegeuka mbogo aliyejeruhiwa,hakuna namna JK anaweza kulishawishi Bunge libadili msimamo juu ya Richmond.
 
Amepoteza ujasiri na Bunge limegeuka mbogo aliyejeruhiwa,hakuna namna JK anaweza kulishawishi Bunge libadili msimamo juu ya Richmond.

Yani shughuli aliyonayo sasa hivi ni pevu!, inabidi abadilike aache ushkaji.
 
Amepoteza ujasiri na Bunge limegeuka mbogo aliyejeruhiwa,hakuna namna JK anaweza kulishawishi Bunge libadili msimamo juu ya Richmond.

Namna wanayo, ila itakuwa 2010, watawapiga chini na kuweka vibaraka wapya. Ndiyo maana hawataki kuwepo na wagombea binafsi. Nyie ngojeni tu mtaona bunge la 2010 litakuwa rubber stamp zaidi ya hili.
 
Kama kikwete angekuwa safi basi angefanya usafi kwenye chama na serikali yake. lakini kwakuwa yeye ni fisadi kama hao wengine ndio maana anashindwa kuwachukulia hatua. asubiri 2010 kama mbeya aliwahi kurushiwa mawe basi mwakani kwenye majukwaa apande na helment.
 
Kama kikwete angekuwa safi basi angefanya usafi kwenye chama na serikali yake. lakini kwakuwa yeye ni fisadi kama hao wengine ndio maana anashindwa kuwachukulia hatua. asubiri 2010 kama mbeya aliwahi kurushiwa mawe basi mwakani kwenye majukwaa apande na helment.

Kshindwa kufanya hivyo, wanaCCM hawaoni hilo!

Ikiwa kuna watanzania walioisaliti nchi yao, na ambayo vizazi na vizazi vitakuja kuichukia basi ni CCM, hata kuifuta bendera yake kwenye uso wa nchi!

Ni rahisi kumfundisha paka asinye kwenye unga, kuliko kuwaambia CCM wafumbue macho yao!
katika asilimia 70% anayoisema Jk wafuata Mkumbo CCM wamo, na katika hii asilima 70% wamo akina

Mwakyembe, prof Bana, akina Kilango Malecela,CCM wote, akina Mwinyi, warioba,, Salim... YEEES kma wanaona CCM inanuka watoke tu, au waanzishe chama kipya, wanaogopa nini??

Mtu yeyote kwa namna yeyote anayetokea kumsifia JK, ni jini na mchawi!
 
Waondoke Chama Cha Majambazi thubutu! hawaondoki hao hata la mgambo likilia. Aliondoka Mrema tu.
 
Kshindwa kufanya hivyo, wanaCCM hawaoni hilo!

Ikiwa kuna watanzania walioisaliti nchi yao, na ambayo vizazi na vizazi vitakuja kuichukia basi ni CCM, hata kuifuta bendera yake kwenye uso wa nchi!

Ni rahisi kumfundisha paka asinye kwenye unga, kuliko kuwaambia CCM wafumbue macho yao!
katika asilimia 70% anayoisema Jk wafuata Mkumbo CCM wamo, na katika hii asilima 70% wamo akina

Mwakyembe, prof Bana, akina Kilango Malecela,CCM wote, akina Mwinyi, warioba,, Salim... YEEES kma wanaona CCM inanuka watoke tu, au waanzishe chama kipya, wanaogopa nini??

Mtu yeyote kwa namna yeyote anayetokea kumsifia JK, ni jini na mchawi!


CCM ya sasa hivi siyo chama cha wakulima na wafanyakazi bali ni genge la wezi na mafia ambao nia yao kuu ni moja tu kuchota mali ya watanzania.

Hao uliowataja hawana ujasiri na hawawezi kamwe kutoka huko kwani ni beneficiaires wa CCM na wakithubutu kutoka wanajua kuwa watakuwa ni targets wa CCM mafia.
 
Siwezi kukataa kwamba serekali ya awamu ya nne haijafanya jambo lolote kuleta maendeleo (positive changes) nchini. Kitu kinacho nifanya nishangae na kubaki mdomo wazi ni pale miradi ya maendeleo ya Taifa inapofunguliwa kama miradi ya chama tawala.

Wiki kadhaa zilizopita muheshimiwa rais akiwa ziarani kanda ya kusini alizindua barabara. Nilishangaa sana kuona uzinduzi ule ulivyokuwa umepambwa kwa rangi na mabango ya CCM huku wanaCCM wakiimba na kukisifia chama chao:confused:!!! (si jambo baya kusifia chama chako) Swali langu la msingi ni: Hivi ni kweli kwamba ile barabara imejengwa na wanaCCM au Chama chao kwa ujumla???

Mtazamo wangu naona serekali ya awamu ya nne ijue kutofautisha kati ya shughuli za kichama na kitaifa. Ukizingatia kwamba wakati wa campaini haujafika na maendeleo yanaletwa na watanzania wote kupitia kodi wanazolipa, nguvu kazi yao, elimu waliyonayo n.k. Chama tawala kinabaki kama msimazi wa shughuli zote za maendeleo ya taifa. kazi kubwa ya upinzani inabaki kuwa muangalizi wa pembeni "Watch Dog".

Taifa linajengwa na wananchi wote na ili ilani ya CCM ifanikiwe basi watanzania wote wanavua uwanachama na kuvaa umoja wa kitaifa wenye tija ya kuleta maendeleo kwa watanzania wote, na si kwa wanaCCM!!!
 
Back
Top Bottom