Nawaomba watanzania wenzangu tuondokane na dhana kwamba rais ni kama Mungu kwa hiyo hasogelewi wala haguswi kwa maana ya kukemewa. Woga huu ndiyo uliotufikisha hapa tulipo na mambo kuharibika huku tukiona na kujua ni nani anaharibu lakini tunakaa kimya eti kwa sababu tunamuogopa mjomba,huo si uzalendo. Kwa walio madarakani kama mtamuonea haya Rais Kikwete kama mnavyomuonea haya Rais Mstaafu Mkapa,eti kwa sababu mtapoteza mkate wenu wa kila siku,basi hamuitakii mema Tanzania na ubinafsi utawahukumu. Na kwa mpendwa Rais,lionee huruma taifa lako hakika linaweza kuangamia likiwa mikononi mwako kama utakwenda na mwendo huu wa sasa. Wanaokupigia makofi,wanakupongeza sasa utambue kuwa wengi wao wanakupaka mafuta kwa mgongo wa chupa huku wakijua fika kuwa mambo hayaendi sawa. Usimuonee haya mtu yeyote, chonde chonde nchi inakwenda pabaya. Mafisadi wanakudai nini kiasi cha kuwaogopa hivi!!