~ Kikwete na Simba wake wa Kuchora! ~

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,474
39,987
Na. M. M. Mwanakijiji
(Makala hii imetoka kwenye gazeti la Tanzania Daima leo. Kutokana na matatizo ya kiufundi gazeti hilo halikuwa kwenye mtandao)

Kuna msemo wa Kiswahili kuwa "mtu mzima hatishiwi nyau". Msemo huu unapotumika mara nyingi unataka kutuma ujumbe kwa mtu kuwa mtu mzima hapigwi mikwara ya kitoto. Hata hivyo msemo huu unakosa ukweli mmoja ambao ni dhahiri; paka akibanwa hupigana kama simba. Rafiki yangu mmoja hivi majuzi alijikuta yuko kwenye mapambano na paka wa jirani ambaye aliingia kwenye sebule yake bila kukaribishwa. Kwa vile jamaa yangu hapendi paka basi akaamua "kumtolea uvivu" kwenye eneo la baraza lililozungukwa kwa uzio wa nyavu nyavu za chuma huku mlango wa sebule ukiwa umefungwa na ule wa kutokea nje ukiwa umefungwa pia.

Mwenyewe aliliita hilo ni pambano la "karne". Paka wa watu hakutaka ugomvi na mtu alichotaka yeye ni kuruhusiwa kwenda zake nje. Jamaa akajifanya yeye jasiri akaanza kumtandika paka wa watu mangumi na mateke; paka akalia huku akikimbia kujificha akitafuta mahali pa kutokea. Mwishowe yule paka akaona hana la kufanya isipokuwa kujibu mashambulizi. Nilipopigiwa simu huyo bwana alikuwa amekimbizwa hospitali akiwa anavuja damu baada ya kupata kibano cha "nyau". Alipotoka hospitali na kunisimulia kisa hiki nilishindwa kujizuia kuhuzunika bali nilibakia kucheka hadi masikio yakaniuma.

Nikagundua kuwa hata mtu mzima akitishiwa nyau lazima ashtuke kwa maana akijifanya yeye mjanja anaweza kutoka na mikwaruzo na kutolewa nishai na paka. Hata hivyo ninaamini msemo mzuri ni ule usemao (nimeutunga mwenyewe) Simba wa karatasi haungurumi wala hang'ati. Yawezekana kabisa mtu akamchora simba mkali kabisa akiwa amekenua meno na manyoya yametoka huku macho yake makali yakiangalia kwa hasira lakini akimsimamisha na kumuelekeza hata kwa mtoto mdogo zaidi atakachofanya mtoto huyo ni kuigusa hiyo picha ya "simba mkali". Simba wa picha anaweza kutisha wale ambao hawajui vitu vya kuchora au picha (sidhani kama watu hao wapo). Mtu hata hawa na lengo gani akisimama na simba wake wa kuchora kuwatishia watu kinachofanyika watu watadhania ni msanii wa aina fulani ambaye anajaribu kuburudisha watu kwa vikatuni au vikaragosi. Naogopa kuwa mikwara ya Rais Kikwete imekuwa kama picha ya simba mkali asiyeunguruma wala kung'ata!

Akiwa katika ziara yake inayoendelea Mkoani Pwani, Rais Kikwete alipata nafasi ya kutembelea mradi wa miembe inayozaa kwa muda mfupi ambapo walengwa wakubwa ni watu wenye kipato cha chini. Mojawapo ya malalamiko ambayo yamekuwa yakisikika ni madai kuwa kuna baadhi ya viongozi ambao wanatakiwa kusimamia mradi huo wameanza kujigawia "miembe" na hivyo walengwa wenyewe hawanufaiki. Rais Kikwete aliposikia malalamiko hayo alishikilia picha yake ya kuchora ya simba na kusema kuwa "Naomba tuelewane kabisa Mkigawana miradi ya maendeleo ambayo imelengwa kuinua maisha ya wananchi maskini na kuwapatia kipato, mtakiona cha mtemakuni nitawasema hadharani mbele ya wananchi" Watu wakasimama na kuipigia makofi picha hiyo. Waliowajanja wakajisema moyoni, tumeshayasikia hayo huko nyuma.

Sijui lengo la Rais kuwasema hawa viongozi kwa wananchi lilikuwa ni nini na sielewi kama yeye anamaanisha kweli kuwa kukiona cha mtema kuni ni kuwasema hadharani. Ukweli ni kuwa mtu mzima hatishiwi nyau, na simba wa kuchora hang'ati wala hangurumi. Haya ya kusema hadharani na kuwataja hadharani wahalifu au wasiofuata taratibu siyo mambo mageni katika utawala wa Rais Kikwete. Mikwara hii ya Kikwete tumeanza kuizoea sasa kama vile picha ya kuchora ya simba mwenye masharubu ambaye amepanua mdomo! Tumeshatambua ni picha tu, simba haumi.

Huyu simba kama angekuwa anauma angeshauma zamani. Miaka miwili sasa vitisho vya serikali ya Rais Kikwete kwa waalifu vimekuwa ni vya kawaida na hasa kwa wale wahalifu wanaotumia kalamu huku wametinga tai zao nzuri na wakiendesha magari yanayoendeshwa kwa gharama za wananchi.

Nakumbuka vizuri ziara yake ya Musoma ambako alisimama na kushikilia picha hiyo ya simba asiyenguruma na kusema kuwa serikali yake haitavumilia viongozi wezi, wala rushwa na na wabovu katika halmashauri mbalimbali nchini. Tukatarajia kuwa "mshikemshike" kwenye halmashauri uko njiani. Kumbe ilikuwa ni picha tu ya simba anayeonekana kama anaunguruma.

Hiyo haikuwa mwisho, tarehe mbili Oktoba mwaka jana akizungumza na Wahariri wa vyombo vya habari nchini Ikulu jijini Dar-es-Salaam alikiri kupokea waraka wenye kutaja majina ya vigogo wanaojihusisha na madawa ya kulevya. Na hivi karibuni Inspekta Jenerali wa Polisi Bw. Saidi Mwema naye alisema kuwa wanayo majina karibu mia mbili na karibu nusu ya majina hayo ya "vigogo wa madawa" yalipelekwa Ikulu. Sasa msiniulize inakuwaje Polisi Mkuu na nambari uno anashindwa kufuata sheria ya kuwatia pingu wahalifu hawa na anaamua kupeleka majina Ikulu. Kumbe na Mwema naye ameshikilia picha ya simba asiyeng'ata.na kupeleka majina kwa Rais.

Bila ya shaka wengi bado wanakumbuka wakati ule Rais Kikwete akiwa ameshikilia picha yake ya simba asiyeng'ata aliwaambia wananchi kuwa anawajua pia viongozi wala rushwa na amewapa muda "wajirekebishe".

Sasa siyo Kikwete tu ambaye anashikilia picha ya simba aliyechorwa kwani yule kiongozi mahiri, shujaa aliyetamba Bungeni na yeye hivi karibuni alikuja na maneno mengine ambayo natumaini alidhani sikuyatilia maanani. Akiwa Morogoro kwenye kuadhimisha kusimikwa kwa Askofu mpya wa Dayosisi ya Morogoro Waziri Mkuu alisimama na kusema kuwa imetosha wananchi kulalamika kuwa kwenye vita dhidi ya madawa ya kulevya wenye kukamatwa ni watu wadogo wadogo huku vigogo wakiangaliwa tu. Akanukuliwa kusema kuwa "Jamani kwa muda mrefu nimekuwa nasikia wanaokamatwa kwa dawa za kulevya na rushwa eti ni watu wadogo wadogo huku vigogo wakitazamwa, tatizo ni kuwa mnasema tu vigogo, vigogo hamuwataji. Nasema watajeni, na ninaahidi tutawashughulikia bila kujali cheo cha mtu au nafasi aliyonayo katika taifa hili na nje ya taifa"

Sasa sisi wengine tunajiuliza hivi Ikulu hawawasiliani na ofisi ya Waziri Mkuu? Je inawezekana kinachofanyika Ikulu Waziri Mkuu hakijui. Wakati Rais wake amesema ameshayapata majina na IGP kasema majina yamepelekwa Ikulu iweje leo Mhe. Lowassa aseme wananchi hawana ujasiri wa kutaja majina ya vigogo hao? Labda anataka wananchi waitishe mkutano wa waandishi wa habari au wafanye kama wapinzani pale Jangwani na kuanza kuorodhesha vigogo wa madawa ya kulevya au waende polisi na kuwanong'oneza vigogo wao. Hata hivyo hapo kuna tatizo.

Tatizo ni kuwa kuwa wananchi wanapowataja vigogo wa ufisadi (na hapa inajumlisha rushwa, matumizi mabaya ya vyeo, madawa ya kulevya n.k) wanaambiwa "hizo ni tuhuma tu leteni ushahidi". Wakiwataja wale wanaowatambua kuwa ndio vilele vya ufisadi nchini Rais anaficha picha yake ya simba na kusema "msijifanye polisi, wapelelezi na mahakimu". Tatizo ni kuwa majina yakitajwa Chama cha Mapinduzi na wapambe wake watajitokeza na kusema "hizo ni kelele za wapinzani, wapuuzieni". Sasa hapa ndio wananchi wanachanganyikiwa. Wasipotaja wanaambiwa "mbona hamuwataji", wakitaja wanaambiwa "acheni kuwazulia viongozi tuhuma zisizothibitishwa". Sasa hata uamuzi wa kusuka au kunyoa siyo rahisi namna hiyo. Vinginevyo waseme kama watanzania wanaotakiwa kutaja wahalifu ni wana CCM peke yao.

Binafsi naamini kabisa kuwa Rais Kikwete na viongozi waliopo madarakani wananguvu zote za kisheria na Kikatiba za kuweza kukomesha ufisadi wa aina nyingi nchini. Hawahitaji nguvu zaidi bali dhamira za wazi za kufanya kile ambacho wamekuwa wakikitishia kwa miaka miwili sasa. Semina Elekezi ya ngurdoto hazikusaidia, hotuba Bungeni hazikusaidia, na sasa mikwara hii ya "hatua kali" haijawafanya wajanja kutetemeka. Imetosha kuwasikiliza, maneno yao yamekuwa matamu mno hadi yanatia kichefuchefu. Waoneshe kuwa wanaweza kutekeleza bila woga, haya, husuda, kisasi, au upendeleo.

Kuendelea kuwatishia wahalifu kwa picha ya simba wa kuchorwa haitoshi. Kama mnaye simba wa kweli kwanini msimuweke hadharani muone watu watakavyotimuana. Hata hivyo ninafahamu tatizo la msingi ambalo siyo tu linampa kusita Rais Kikwete lakini linamgwaisha Lowassa. Ni tatizo ambalo bado hawajaweza kulipatia majibu kwa sababu linahusu kuweka dawa kwenye kidonda kilicho kwenye ngozi zao wenyewe.

Kama wameamua kulindana watuambie tu ili tukubali yaishe. Labda umefika wakati Watanzania tuamue kuwaziria nchi ili watafune, wameze, na kusaza. Haina maana kuendelea kuwalalamikia au kuwaonesha mapungufu; Hakuna maana kuwakosoa maana kwao ni wimbo waliouzoea. Tuwaachie BoT, tuwaachie madini, tuwaachie mikataba ya nishati na kila kitu wanachotaka. Tusiwaulize tena, tuwasusie Tanzania ili watawale wanavyopenda maana hizi kelele zetu zinawakera na wanaona tunawatakia mabaya.

Hata tutakapoamua kuzira hivyo watambue kuwa kuna kizazi cha wananchi ambacho hakitazira kitaendelea kuwakalia kwenye shingo zao kama jinamizi na kuendelea kupiga kelele kama mtu aliyefumania. Kizazi hicho kitakapokuwa kimekata tamaa kweli watawala watakichukia. Leo hii tunasikia madini yanaibwa toka kwenye gari la CCM (msiniulize ilikuwaje); ndani ya wiki moja migodi mitatu inavamiwa na watu kuchukua madini kama utani. Tumeyaona Delta kule Nigeria pale wananchi walipokata tamaa baada ya kuona mali yao ya asili ikichotwa na kujenga nchi za watu wengine. Leo hii wameanzisha vitendo vya kuhujumu sekta ya mafuta kule Delta kwa kushambulia visima na kuteka watendaji wa makampuni ya mafuta.

Natumaini na ninaombea kwenye Mwenyezi Mungu mwingi wa Rehema na Mwenye Huruma kuwa yaliyotokea Mwadui, Bukombe na Mererani wiki iliyopita ni matukio ya uhalifu wa kawaida tu na ya nadra. Kwa sababu kama tunachoshuhudia ni mwanzo wa uhalifu wa kupangwa dhidi ya makampuni ya madini au sekta hiyo basi ndugu zangu huko mbeleni ni machozi na hofu. Naomba nitoe wito kwa heshima kubwa na taadhima; Mhe. Rais na wenzako, hatutaki vitisho tena, hatutaki kushikiwa picha ya simba wa kuchorwa, na kwa hakika tumechoka na kibwagizo cha "tumepewa majina ya wahalifu" . Wananchi wasitoe majina tena ya wahalifu hadi yale yaliyokwishatolewa yafanyiwe kazi. Vinginevyo tutaoneshana haya mazingaombwe hadi tusikie kizunguzungu. Simba ambaye mmemshikilia mbele ya wahalifu imegundulika ni mdoli tu na ni wapicha, haumi kwani meno yake ya plastiki! Mkitaka wahalifu wajue mko makini na mliodhamiria, acheni porojo za kisiasa na fanyeni kweli. Vinginevyo, tutawaziria nchi. Najua hilo liwafurahisha maana hatimaye mtaweka picha ya simba chini ili muendelee na "shughuli" zenu bila kusumbuliwa.



Niandikie: mwanakijiji(at)jamboforums.com
 
Mimi ninajiuliza sana, hivi kwanini ni vigumu kuchukua "hizo hatua kali".. na ni kwanini watu hawaogopi vitisho vya viongozi wa nchi? Inanikumbusha nilipokuwa shuleni, kuna mwalimu ambaye akiwapiga mkwara si utani hasa mkijua wiki ile ni zamu yake.. lakini kuna wengine ukijua wiki ile ni zamu ya mwalimu "fulani" basi ndio siku ya kuzamia miembeni; yaani darasa linaisha saa nne hivi watu mnaenda zenu Baharini kuogelea.. kwenye saa tisa na nusu hivi basi mnasubiri wenzenu wakitoka shule mnaunganika nao, unaazima madaftari, jioni unakwenda tuition, ka mtihani kakija unapasua vilevile!! Walimu kama wale walikuwa wanapendwa sana maana hata wakisamama kupiga mkwara mbele ya Mwalimu Mkuu, wanafunzi wanatabasamu kwa kukonyezana..
 
One important point is that when the president is aware of wrongdoing and does not act, his inaction becomes wrongdoing and he becomes an accomplice liable for the original wrongdoing.
 
Na. M. M. Mwanakijiji
(Makala hii imetoka kwenye gazeti la Tanzania Daima leo. Kutokana na matatizo ya kiufundi gazeti hilo halikuwa kwenye mtandao)

Kuna msemo wa Kiswahili kuwa "mtu mzima hatishiwi nyau". Msemo huu unapotumika mara nyingi unataka kutuma ujumbe kwa mtu kuwa mtu mzima hapigwi mikwara ya kitoto. Hata hivyo msemo huu unakosa ukweli mmoja ambao ni dhahiri; paka akibanwa hupigana kama simba.

Akiwa katika ziara yake inayoendelea Mkoani Pwani, Rais Kikwete alipata nafasi ya kutembelea mradi wa miembe inayozaa kwa muda mfupi ambapo walengwa wakubwa ni watu wenye kipato cha chini. Mojawapo ya malalamiko ambayo yamekuwa yakisikika ni madai kuwa kuna baadhi ya viongozi ambao wanatakiwa kusimamia mradi huo wameanza kujigawia "miembe" na hivyo walengwa wenyewe hawanufaiki. Rais Kikwete aliposikia malalamiko hayo alishikilia picha yake ya kuchora ya simba na kusema kuwa "Naomba tuelewane kabisa Mkigawana miradi ya maendeleo ambayo imelengwa kuinua maisha ya wananchi maskini na kuwapatia kipato, mtakiona cha mtemakuni nitawasema hadharani mbele ya wananchi" Watu wakasimama na kuipigia makofi picha hiyo. Waliowajanja wakajisema moyoni, tumeshayasikia hayo huko nyuma.

Hapa ndipo mahala ambapo imani ya wananchi kutomwamini Rais inapozaliwa


Sijui lengo la Rais kuwasema hawa viongozi kwa wananchi lilikuwa ni nini na sielewi kama yeye anamaanisha kweli kuwa kukiona cha mtema kuni ni kuwasema hadharani. Ukweli ni kuwa mtu mzima hatishiwi nyau, na simba wa kuchora hang'ati wala hangurumi. Haya ya kusema hadharani na kuwataja hadharani wahalifu au wasiofuata taratibu siyo mambo mageni katika utawala wa Rais Kikwete. Mikwara hii ya Kikwete tumeanza kuizoea sasa kama vile picha ya kuchora ya simba mwenye masharubu ambaye amepanua mdomo! Tumeshatambua ni picha tu, simba haumi.

Huyu simba kama angekuwa anauma angeshauma zamani. Miaka miwili sasa vitisho vya serikali ya Rais Kikwete kwa waalifu vimekuwa ni vya kawaida na hasa kwa wale wahalifu wanaotumia kalamu huku wametinga tai zao nzuri na wakiendesha magari yanayoendeshwa kwa gharama za wananchi.

Nakumbuka vizuri ziara yake ya Musoma ambako alisimama na kushikilia picha hiyo ya simba asiyenguruma na kusema kuwa serikali yake haitavumilia viongozi wezi, wala rushwa na na wabovu katika halmashauri mbalimbali nchini. Tukatarajia kuwa "mshikemshike" kwenye halmashauri uko njiani. Kumbe ilikuwa ni picha tu ya simba anayeonekana kama anaunguruma.

Hiyo haikuwa mwisho, tarehe mbili Oktoba mwaka jana akizungumza na Wahariri wa vyombo vya habari nchini Ikulu jijini Dar-es-Salaam alikiri kupokea waraka wenye kutaja majina ya vigogo wanaojihusisha na madawa ya kulevya. Na hivi karibuni Inspekta Jenerali wa Polisi Bw. Saidi Mwema naye alisema kuwa wanayo majina karibu mia mbili na karibu nusu ya majina hayo ya "vigogo wa madawa" yalipelekwa Ikulu. Sasa msiniulize inakuwaje Polisi Mkuu na nambari uno anashindwa kufuata sheria ya kuwatia pingu wahalifu hawa na anaamua kupeleka majina Ikulu. Kumbe na Mwema naye ameshikilia picha ya simba asiyeng'ata.na kupeleka majina kwa Rais.

IGP ni kama refaa au mshika kibendera kwani hayo majina kabla hajafungua aliunguruma sana sasa baada ya kuyafungua alikaa kimya, au alilikuta jina lake au la ndugu yake mbona kimya???

Bila ya shaka wengi bado wanakumbuka wakati ule Rais Kikwete akiwa ameshikilia picha yake ya simba asiyeng'ata aliwaambia wananchi kuwa anawajua pia viongozi wala rushwa na amewapa muda "wajirekebishe".

Kuwapa muda wala rushwa ni kutukejeli maana ni sisi wananchi tumekuwa katika mateso hayo tangu enzi hizo na nyie viongozi mmekuwa na wimbo huo huo wa kumaliza tatizo la rushwa nchini.

Sasa siyo Kikwete tu ambaye anashikilia picha ya simba aliyechorwa kwani yule kiongozi mahiri, shujaa aliyetamba Bungeni na yeye hivi karibuni alikuja na maneno mengine ambayo natumaini alidhani sikuyatilia maanani. Akiwa Morogoro kwenye kuadhimisha kusimikwa kwa Askofu mpya wa Dayosisi ya Morogoro Waziri Mkuu alisimama na kusema kuwa imetosha wananchi kulalamika kuwa kwenye vita dhidi ya madawa ya kulevya wenye kukamatwa ni watu wadogo wadogo huku vigogo wakiangaliwa tu. Akanukuliwa kusema kuwa "Jamani kwa muda mrefu nimekuwa nasikia wanaokamatwa kwa dawa za kulevya na rushwa eti ni watu wadogo wadogo huku vigogo wakitazamwa, tatizo ni kuwa mnasema tu vigogo, vigogo hamuwataji. Nasema watajeni, na ninaahidi tutawashughulikia bila kujali cheo cha mtu au nafasi aliyonayo katika taifa hili na nje ya taifa"

Sasa sisi wengine tunajiuliza hivi Ikulu hawawasiliani na ofisi ya Waziri Mkuu? Je inawezekana kinachofanyika Ikulu Waziri Mkuu hakijui. Wakati Rais wake amesema ameshayapata majina na IGP kasema majina yamepelekwa Ikulu iweje leo Mhe. Lowassa aseme wananchi hawana ujasiri wa kutaja majina ya vigogo hao? Labda anataka wananchi waitishe mkutano wa waandishi wa habari au wafanye kama wapinzani pale Jangwani na kuanza kuorodhesha vigogo wa madawa ya kulevya au waende polisi na kuwanong'oneza vigogo wao. Hata hivyo hapo kuna tatizo.

Inasemekana baadhi ya mawaziri wanajihusisha na biashara ya madawa ya kulevya, kuna ndugu yangu wa karibu sana baada ya kuhitimu chuo kikuu alienda kwa naibu waziri mmoja sasa si waziri tena alikwenda kuomba msaada apate ajira. Yule naibu waziri akamweleza kuwa ajira hakuna isipokuwa labda amtafutie passport ili wafanye biashara. Yule ndugu yangu akamuuliza biashara gani? Hakuamini masikio yake yake baada ya kuelezwa kwamba biashara yenyewe iwe ni siri yao wawili, akamwambia kuwa mbona mawaziri wengi ndivyo wanavyoishi? Sasa kwangu mimi kuona zoezi hili linasua sua sioni geni kwani biashara hii ni wao wenyewe ndiyo wanaofanya.


Tatizo ni kuwa wananchi wanapowataja vigogo wa ufisadi (na hapa inajumlisha rushwa, matumizi mabaya ya vyeo, madawa ya kulevya n.k) wanaambiwa "hizo ni tuhuma tu leteni ushahidi". Wakiwataja wale wanaowatambua kuwa ndio vilele vya ufisadi nchini Rais anaficha picha yake ya simba na kusema "msijifanye polisi, wapelelezi na mahakimu". Tatizo ni kuwa majina yakitajwa Chama cha Mapinduzi na wapambe wake watajitokeza na kusema "hizo ni kelele za wapinzani, wapuuzieni". Sasa hapa ndio wananchi wanachanganyikiwa. Wasipotaja wanaambiwa "mbona hamuwataji", wakitaja wanaambiwa "acheni kuwazulia viongozi tuhuma zisizothibitishwa". Sasa hata uamuzi wa kusuka au kunyoa siyo rahisi namna hiyo. Vinginevyo waseme kama watanzania wanaotakiwa kutaja wahalifu ni wana CCM peke yao.

Binafsi naamini kabisa kuwa Rais Kikwete na viongozi waliopo madarakani wananguvu zote za kisheria na Kikatiba za kuweza kukomesha ufisadi wa aina nyingi nchini. Hawahitaji nguvu zaidi bali dhamira za wazi za kufanya kile ambacho wamekuwa wakikitishia kwa miaka miwili sasa. Semina Elekezi ya ngurdoto hazikusaidia, hotuba Bungeni hazikusaidia, na sasa mikwara hii ya "hatua kali" haijawafanya wajanja kutetemeka. Imetosha kuwasikiliza, maneno yao yamekuwa matamu mno hadi yanatia kichefuchefu. Waoneshe kuwa wanaweza kutekeleza bila woga, haya, husuda, kisasi, au upendeleo.

Kuendelea kuwatishia wahalifu kwa picha ya simba wa kuchorwa haitoshi. Kama mnaye simba wa kweli kwanini msimuweke hadharani muone watu watakavyotimuana. Hata hivyo ninafahamu tatizo la msingi ambalo siyo tu linampa kusita Rais Kikwete lakini linamgwaisha Lowassa. Ni tatizo ambalo bado hawajaweza kulipatia majibu kwa sababu linahusu kuweka dawa kwenye kidonda kilicho kwenye ngozi zao wenyewe.

Kama wameamua kulindana watuambie tu ili tukubali yaishe. Labda umefika wakati Watanzania tuamue kuwaziria nchi ili watafune, wameze, na kusaza. Haina maana kuendelea kuwalalamikia au kuwaonesha mapungufu; Hakuna maana kuwakosoa maana kwao ni wimbo waliouzoea. Tuwaachie BoT, tuwaachie madini, tuwaachie mikataba ya nishati na kila kitu wanachotaka. Tusiwaulize tena, tuwasusie Tanzania ili watawale wanavyopenda maana hizi kelele zetu zinawakera na wanaona tunawatakia mabaya.


Nakumbuka siku moja Mh Rais baada ya kutangzwa rasmi kuwania urais wake kupitia CCM alitoa hotuba ambayo iliashiria haya tunayojadili sitamnukuu kwa usahihi kama ilivyokuwa najaribu kumnukuu ".....I may wear smile but tough in decision" mwisho wa kujaribu kumnukuu

Maneno haya yamenifanya kukumbuka kwamba huenda ni kweli tuliangalia uzuri wa jalada la kitabu, badala ya kufungua ndani kujisomea tukajua content of the book. Hata hivyo Mh. Rais anayonafasi ya kufanya marekebisho katika serikali yake kabla wananchi HAWAJA BWAGA MIOYO YAO
 
mzee mwanakijiji umegusia mambo mengi ambayo kwakweli yameibua hisia zangu nyingi na kwa wengine waliyo soma thread hii pia.leo kwenye gazeti la tanzania Daima lime-report kwamba kuna hakimu aliyetajwa kwa jina la jamila nzoa,alitiwa mbaroni na PCCB wakati akiwa mbioni kwenda kupokea rushwa,kulingana na taarifa hiyo,mtego wenyewe ulitegwa kuanzia saa tisa mchana hadi saa sita usiku,hatimaye mtuhumiwa akakamatwa akipokea sh.70000/=yapo matukio mengi tu ambayo utasikia watu wamekamatwa na Takukuru wakipokea rushwa.lakini ni categoly gani,sanasana,maafisa watendaji,makatibu tarafa na kata serikali za mitaa na maofisa wa chini serikalini.kitu kinachonisikitisha mimi nikuona jinsi namna hawa Takukuru walivyo bussy wakiangaika na vijidagaa vidogo hadi saa sita usiku wakiacha mapapa yaliyobobea kwenye rushwa yakipeta,na kama si hawa mafisadi wanaodidimiza uchumi wa nchi,hivi vijidagaa vidogo visingelikuwa vinakula rushwa,vimishahara kiduchu ndiyo chanzo kikubwa,kwanini hawa PCCB wasishughulikie mafisadi kwanza na taarifa wanazo.je huyo bosi wao ambaye nikinara wa rushwa atachunguzwa na nani?hata wafanyakazi walioko chini yake wamekuwa wakimlalamika,kwa ufupi nakubaliana na mzee mwanakijiji kwamba rais wetu kama siyo rahisi amebeba picha ya simba,uswahili mwingi yaani ni mbabaishaji hakuna,ogopa mtu anayechekacheka,ni vigumu kuchukua hatua.hata msichana akiwa na tabia ya kuchekacheka anawakaribisha wanaume wamtongoze.lakini akiwa serious wanaume wanajiuliza namna ya kumuingia.naona tuandike maumivu,tuendelee kuomba na kusali sana,tupo kwenye chombo hakina naodha kinategema nguvu za upepo tukifika inshaal.
 
Watanzania maneno yana tuburudisha mno!
Haujawahi kijiuriza kwanini muziki wa taarabu unapendwa!? Mipasho... ndio hasa inayopendwa.
Sasa mimi nimejigawia mali ya Umma ukinitaja hadhalani ndio umefanya nini?Niwajibishe niwe mfano....!
Lakini utanipasha hadhalani watu wacheke na kukupiga makofi huku ukiniambia nijirekebishe au siyo..!
Kama Rais aliweza kuwaambia polisi (alipokua ana wapa vyeo wiki hii)waache kuongea na waarifu wanaovunja sheria mbele yao,kwani kwa kufanya hivyo wanadhalaulika na kwamba hawana lolote na wako "Nyoronyoro...." (kwa maneno yake mwenyewe Rais) na hii inawapunguzia heshima alfu anatoka huko na yeye anafanya yale YALEle wanayo fanya police 'nyoronyoro' kuwaambia waharifu atawataja hazalani.
Mie mwenzenu naona mkang'anyiko mkubwa na naona kizunguzungu.
 
Watanzania maneno yana tuburudisha mno!
Haujawahi kijiuriza kwanini muziki wa taarabu unapendwa!? Mipasho... ndio hasa inayopendwa.


Kwa kweli hata mie sijui. Tueleze mkuu. Ngoja nibuni. May be ni shauri ya maneneo rahisi yanayotumika kila siku hasa na wanawake, au wengi hushindwa kujua maana ya huo wimbo wakalewa na midundo tu?
 
Kwa kweli hata mie sijui. Tueleze mkuu. Ngoja nibuni. May be ni shauri ya maneneo rahisi yanayotumika kila siku hasa na wanawake, au wengi hushindwa kujua maana ya huo wimbo wakalewa na midundo tu?[/QUOTE]

majibu yote yako hapa.............

Sasa mimi nimejigawia mali ya Umma ukinitaja hadhalani ndio umefanya nini?Niwajibishe niwe mfano....!
Lakini utanipasha hadhalani watu wacheke na kukupiga makofi huku ukiniambia nijirekebishe au siyo..!
Kama Rais aliweza kuwaambia polisi (alipokua ana wapa vyeo wiki hii)waache kuongea na waarifu wanaovunja sheria mbele yao,kwani kwa kufanya hivyo wanadhalaulika na kwamba hawana lolote na wako "Nyoronyoro...." (kwa maneno yake mwenyewe Rais) na hii inawapunguzia heshima alfu anatoka huko na yeye anafanya yale YALEle wanayo fanya police 'nyoronyoro' kuwaambia waharifu atawataja hazalani.
 
Asante Jafar.. natumaini tunawasha moto wa fikra ili wananchi watakaposikia tena Rais anapiga mkwara wawaze "picha ya simba"...
 
Mwanakijiji,
Yaani inakatisha tamaa kabisa.Kama kweli tunahitaji maendeleo ya haraka Raisi lazima awe mkali kuwashughulikia mara moja wale wanaoturudisha nyuma.Ila cha kushangaza Raisi wetu anakuwa Champion wa mikwara na maneno mengi bila ya vitendo!
Hivi kweli mpaka leo ile listi ya wauza madawa ya kulevya aliyopewa Raisi imefikia wapi? maana tumekuwa wavumilivu vya kutosha lakini kwa staili hii mheshimiwa Raisi hutoi mfano mzuri wa utendaji.
Hivi kweli tutaiona ile Tanzania yenye neema katika kizazi hiki???

Wembe
 
mkjj......

hutaki tena kujiunga na CCM? au ndio mambo ya SUNGURA KIKOSA ZABIBU HUSEMA.....SIZITAKI MBICHI HIZI...........nakuuliza tu kaka.
 
Wananchi wasiishie 'kuwaza' tu; wamwambie 'live' kwamba vitisho hivyo ni sawa na picha ya simba. Havina nguvu yoyote.

Unayosema ni kweli kuwa wananchi wafanye kweli, lakini yote yatafanyika baada ya wananchi kufahamu kwa kina kinachoendelea katika jamii ya watawala wa Tz. Nani alitegemea kuwa wananchi wanaweza kuwazomea wabunge? Vilevile JK alionja joto ya mabango kule Kondoa na Kahama. Hili ni suala la muda tu, kwa jinsi wananchi wanavyoendelea kupigika si muda mrefu watavunja ukimya "kwani hata sponge ukigandamiza sana inafikia sehemu inagoma kuukubali huo msukumo pamoja na ulaini wake".
 
Na. M. M. Mwanakijiji
(Makala hii imetoka kwenye gazeti la Tanzania Daima leo. Kutokana na matatizo ya kiufundi gazeti hilo halikuwa kwenye mtandao)
...
Nikagundua kuwa hata mtu mzima akitishiwa nyau lazima ashtuke kwa maana akijifanya yeye mjanja anaweza kutoka na mikwaruzo na kutolewa nishai na paka. Hata hivyo ninaamini msemo mzuri ni ule usemao (nimeutunga mwenyewe) Simba wa karatasi haungurumi wala hang’ati. Yawezekana kabisa mtu akamchora simba mkali kabisa akiwa amekenua meno na manyoya yametoka huku macho yake makali yakiangalia kwa hasira lakini akimsimamisha na kumuelekeza hata kwa mtoto mdogo zaidi atakachofanya mtoto huyo ni kuigusa hiyo picha ya “simba mkali”. Simba wa picha anaweza kutisha wale ambao hawajui vitu vya kuchora au picha (sidhani kama watu hao wapo). Mtu hata hawa na lengo gani akisimama na simba wake wa kuchora kuwatishia watu kinachofanyika watu watadhania ni msanii wa aina fulani ambaye anajaribu kuburudisha watu kwa vikatuni au vikaragosi. Naogopa kuwa mikwara ya Rais Kikwete imekuwa kama picha ya simba mkali asiyeunguruma wala kung’ata!...

Si vibaya kusema msemo huu umeiga msemo wa chui wa karatasi.

Paper tiger is a literal English translation of the Chinese phrase zhǐ lǎohǔ (Chinese: 紙老虎 meaning something which seems as threatening as a tiger, but is really harmless.

The phrase is an ancient one in Chinese, but sources differ as to when it entered the English vocabulary. Although some sources may claim it dates back as far as 1850, it seems the Chinese phrase was first translated when it was applied to describe the United States using propaganda tactics. In 1956, Mao Zedong said of the United States:

In appearance it is very powerful but in reality it is nothing to be afraid of; it is a paper tiger. Outwardly a tiger, it is made of paper, unable to withstand the wind and the rain. I believe the United States is nothing but a paper tiger.

In Mao Zedong's view, the term could be applied to all allegedly imperialist nations, particularly the United States and the Soviet Union (following the Sino-Soviet split): Mao argued that they appeared to be superficially powerful but would have a tendency to overextend themselves in the international arena, at which point pressure could be brought upon them by other states to cause their sudden collapse. Soviet PremierNikita Khrushchev at some point may have remarked that although the "U.S. is a paper tiger, it has atomic teeth".
source: wikipedia
 
Anatuzuga kwamba ameanza, kwa kuamua kumpangia kazi nyingine mtu kama Severe badala ya kumfukuza.

Labda muda wa kuipa uhai hiyo picha ya simba ndo umewadia!
 
Back
Top Bottom