Kikwete (na serikali yake) anaogopa kumshtaki Balali

Mwafrika wa Kike

JF-Expert Member
Jul 5, 2007
5,185
56
Ukaguzi wa kawaida wa ndani ulifanyika ukagundua kuna tatizo kubwa sana. Deloitte wakafanya ukaguzi wakagundua kuna tatizo kubwa zaidi na walipoanza kupiga kelele wakafukuzwa. CAG nayo ikaingilia ikakuta tatizo ni kubwa zaidi. Wenye uchungu wakaanza kuvujisha mambo kwa wapinzani na Jamboforums.

Habari zikaenea kwa haraka sana kuwa kuna watu wachache wanafilisi nchi. Lipumba akaongea na waandishi wa habari lakini ccm wakapuuza maneno yake. Dr Slaa akataka kuwasilisha hoja bungeni lakini Spika akasema ni uzushi. Dr Slaa akasisitiza tena kuleta hoja bungeni, usalama wa taifa ukaandika barua kali ya onyo kwa Lowasa kuwa asimruhusu mbunge hata mmoja wa ccm kuijadili hoja ya Slaa- wabunge wa sisiem wote wakanywea.

Mwenye uchungu na nchi akavujisha barua ya usalama wa taifa (TISS) kwa Lowasa hapa JF na kwa wapinzani. Serikali ikashindwa kukana au kuikubali hiyo barua. Katika kipindi hicho hicho Zitto akaleta hoja binafsi kuhusu Buzwagi. Wabunge wa ccm chini ya Lowasa na Malecela wakamfukuza Zitto bungeni. Spika akaonya kuwa yeyote anayeleta hoja bungeni za kuipaka serikali matope kwa "maneno ya kizushi na uongo" ataadhibiwa na bunge.

Dr Slaa akatoa hoja yake bungeni na akaipa serikali muda hadi sep 15 kufanya uchunguzi wa wizi mkubwa kabisa benki kuu lakini serikali chini ya kikwete ikapuuzia. Dr Slaa akaishtaki serikali kwa wananchi kupitia mikutano ya hadhara. Zitto naye akaendelea kuishtaki serikali kwa wananchi kupitia mikutano ya hadhara. Wananchi wa Tanzania kwa mara ya kwanza kabisa wakaanza kuzomea viongozi wa ccm kila walikoenda. Lowasa akaulizwa swali na mtoto mdogo akakasirika sana na kumshambulia mtoto yule na mwalimu wake. Serikali ya ccm ikajua kuwa mambo yameanza kuharibika.

Dr Slaa akatembelea Marekani na kukutana na watu wengi tu. Wana JF wa America wakapeleka hoja ya Zitto na Slaa kwa serikali ya America na wafadhili. Serikali za nje zikamtia presha Kikwete afanye uchunguzi wa BOT. Serikali ikaingia mkataba na E&Y kuchunguza yaliyotokea BOT. E&Y ikapewa muda na ikatoa report yake. Report ikavuja JF, Serikali ikakalia report kwa zaidi ya mwezi mmoja. Balali akaandika barua ya kujiuzulu na serikali ikazuga kuwa haikupata barua ya Balali. Kikwete akatoa vipande tu vya report na kutaja makampuni 22 tu yasiyojulikana huku akiacha wapambe wake wa karibu nje. Wapinzani wauliza kupewa report ya E&Y wakaambiwa kuwa hilo ni jambo la usalama wa taifa.

Kikwete akatangaza kutengua uteuzi wa Balali na kuipa bodi ya BOT (ambayo ndiyo iliyoshiriki katika wizi wa awali) miezi sita kuchunguza kile kilichochunguzwa na waliochunguza ile kamati iliyochunguza ile kampuni iliyochunguza yale CAG aliyochunguza baada ya kampuni ya uchunguzi kuchunguza uchunguzi wa .....nimechanganyikiwa sasa.

Baada ya miezi sita, Kikwete anajiandaa kuunda kamati ambayo itahusisha viongozi wa dini na vyama vya upinzani ili vifanye uchunguzi wa kile bodi itamaliza kuchunguza baada ya miezi sita. Kuna habari kuwa hiyo kamati itapewa miezi 18 kumaliza kazi yake.

Pamoja na PR strategy na maneno ya vitisho ya kumfuta kazi na kutaka kumshitaki Balali, Kikwete na serikali yake iliyowekwa madarakani na pesa za wizi toka BoT, hawana ubavu kabisa wa kumshtaki Balali au yeyote aliyehusika na wizi wa BoT unless.........

Wana JF, watch this thread..............
 
Nilidhani nimechanganyikwa, sasa nina uhakika nimechanganyikiwa, yaani kuchunguza kamati iliyochunguza uchunguzi wa kile kilichochunguzwa?

Hii inanikumbusha ila kamati ya madini imbayo inapitia yale yaliyochunguzwa na kamati ya Masha na yale yaliyochunguzwa na Mboma ambaye naye alichunguza yaliyochunguzwa na Kilokola na Mangenya.

Sasa katika nchi hii ambao uchunguzi uliochunguzwa nao unachunguzwa basi uwezekano wa kuchunguza kilichochunguzwa huwa ni kawaida na wa daima (perpetual)

Tunakumbuka jinsi Muhimbili walivyochunguza wale wagonjwa wa Muhimbili ambapo baada ya uchunguzi wao ripoti yao ikakataliwa na kumfanya Mwakyusa aunde kamati nyingine ya uchunguzi wa kilichochunguzwa na kamati ya awali.

sasa, kwanini tusiamue kubadili jina la nchi yetu na kuwa Jamhuri ya Muungano wa Watu Wanaochunguzwa?
 
Nilidhani nimechanganyikwa, sasa nina uhakika nimechanganyikiwa, yaani kuchunguza kamati iliyochunguza uchunguzi wa kile kilichochunguzwa?

Hii inanikumbusha ila kamati ya madini imbayo inapitia yale yaliyochunguzwa na kamati ya Masha na yale yaliyochunguzwa na Mboma ambaye naye alichunguza yaliyochunguzwa na Kilokola na Mangenya.

Sasa katika nchi hii ambao uchunguzi uliochunguzwa nao unachunguzwa basi uwezekano wa kuchunguza kilichochunguzwa huwa ni kawaida na wa daima (perpetual)

Tunakumbuka jinsi Muhimbili walivyochunguza wale wagonjwa wa Muhimbili ambapo baada ya uchunguzi wao ripoti yao ikakataliwa na kumfanya Mwakyusa aunde kamati nyingine ya uchunguzi wa kilichochunguzwa na kamati ya awali.

sasa, kwanini tusiamue kubadili jina la nchi yetu na kuwa Jamhuri ya Muungano wa Watu Wanaochunguzwa?

Yup,

sasa ni JMWW - Jamhuri ya Muungano wa Watu Wanaochunguzwa
 
Mimi naona at-least awamu ya nne kuna viuchunguzi vinafanywa (BoT), watu wanapelekwa mahakamani (Balozi wa Tanzania Italy, Zombe, Dito), tume zinawaingiza mpaka wapinzani (Madini Zitto).

Awamu ya nyerere, BoT imepakuliwa mpaka ikachomwa moto! Hakuna tume wala uchunguzi wala kufikishwa mtu mahakamani. Lord Rajpar, kauziwa meli ya serikali kwa njia ya mkato, hakuna kilichotokea, kimya.

Awamu ya mwinyi, huyu ndio kila kitu ruksa...hakuna uchunguzi, wala tume, wala mahakamani, kimyaa.

awamu ya nkapa, kaunda tume ya warioba, mpaka leo kaikalia. kafunguwa biashara binafsi ikulu, kimya...

awamu ya nne, si at least tunayaona yanayofanyika..., "mnyonge mnyongeni haki yake mpeni", au hamuijuwi system ni nini?
 
Mimi naona at-least awamu ya nne kuna viuchunguzi vinafanywa (BoT), watu wanapelekwa mahakamani (Balozi wa Tanzania Italy, Zombe, Dito), tume zinawaingiza mpaka wapinzani (Madini Zitto).

Awamu ya nyerere, BoT imepakuliwa mpaka ikachomwa moto! Hakuna tume wala uchunguzi wala kufikishwa mtu mahakamani. Lord Rajpar, kauziwa meli ya serikali kwa njia ya mkato, hakuna kilichotokea, kimya.

Awamu ya mwinyi, huyu ndio kila kitu ruksa...hakuna uchunguzi, wala tume, wala mahakamani, kimyaa.

awamu ya nkapa, kaunda tume ya warioba, mpaka leo kaikalia. kafunguwa biashara binafsi ikulu, kimya...

awamu ya nne, si at least tunayaona yanayofanyika..., "mnyonge mnyongeni haki yake mpeni", au hamuijuwi system ni nini?

Ulisikia alichosema juzi Kikwete kuwa anataka kuchunguza wazazi wa wanaJF wanaopenda kulialia kama watoto kila mara? Uko kwenye nchi ya uchunguzi, kinachofuatia, hilo jina unalotumia hapa litachunguzwa kama linafanana na memba fulani hapa alikuwa na tabia ya kulialia kila mara ili apewe maziwa!
 
Ulisikia alichosema juzi Kikwete kuwa anataka kuchunguza wazazi wa wanaJF wanaopenda kulialia kama watoto kila mara? Uko kwenye nchi ya uchunguzi, kinachofuatia, hilo jina unalotumia hapa litachunguzwa kama linafanana na memba fulani hapa alikuwa na tabia ya kulialia kila mara ili apewe maziwa!
Wandugu zangu wa visiwani wana wimbo wao "ukichunguwa usichunguwe utayajuwa", kwa hiyo usiwe na shaka na uchunguzi, mradi mambo yaende na tuyaone, kama tunavyoyaona awamu hii yanavyokwenda. Au hujuwi system ni nini?
 
Wandugu zangu wa visiwani wana wimbo wao "ukichunguwa usichunguwe utayajuwa", kwa hiyo usiwe na shaka na uchunguzi, mradi mambo yaende na tuyaone, kama tunavyoyaona awamu hii yanavyokwenda. Au hujuwi system ni nini?

Consider yourself ignored by Mwafrika wa Kike from now on unless........
 
Mimi nafikiri sasa kuna haja ya kumzomea huyu Kikwete hadharani maana hana sifa ya kuwa Rais wa Watanzania.

Utakuwaje kiongozi wa nchi na wakati huo huo unaogopa kuwachukulia wahusika wa ufisadi na ubadhirifu hatua yoyote hata pale ambapo kuna ushahidi wa kutosha kabisa dhidi yao.

Mhindi wa rada aliyejipatia $12 millioni za Watanzania aliachwa huru mpaka akatoroka. Watuhumiwa wa kashfa ya BoT wako huru na mali zao hazijaguswa kabisa! baadhi yao si ajabu nao wakatoroka.

Mkapa ana kashfa chungu nzima dhidi yake ikiwemo ya kujipatia kiharamu KCM lakini mkuu wa nchi hajasema lolote!

Mawaziri wengi wamegubikwa katika wimbi la kashfa za utendaji mbovu, ufisadi na ubadhirifu, kusaini mikataba isiyo na maslahi kwa Tanzania, kuidhinisha malipo ya mabilioni toka BoT ambayo sasa kuna ushahidi wa kutosha kwamba pesa hizo zimeibiwa, lakini cha kushangaza hakuna hata waziri mmoja aliyepoteza kazi :confused: wote bado wanapeta tu!

Kikwete ni tatizo letu kubwa. Hatuwezi kuwa na kiongozi anayeogopa kutumia uwezo mkubwa aliopewa na katiba ya kuwashughulikia mafisadi, wezi, wabadhirifu n.k. Yeye bado anawaona hawa kama hawana dosari yoyote na bado anakaa nao meza moja kula, kunywa na kucheka nao na pia kuendelea kuwakabidhi utendaji ambao wameshaonyesha kwamba wameshindwa.

Sasa tuanze kampeni za kumzomea huyu jamaa iwe ndani au nje ya Tanzania dhidi ya usanii wake. Tumepiga kelele kiungwana lakini hatusikilizi labda tukianza kumzomea hadharani atauelewa ujumbe tunaomfikishia maana kiongozi wa nchi kuzomewa hadharani ni aibu kubwa sana. Kumbukeni miezi michache iliyopita mawaziri na watendaji wa juu wa CCM walipozomewa katika sehemu mbali mbali Tanzania walionekana kukerwa sana, labda na huyu naye litamkera hivyo aache usanii wake.
 
Mwafrika wa Kike,
Hata kama ungekuwa ni wewe, unaweza kukata tawi ulilokalia? Ripoti ya Slaa inamtaja Kikwete kwamba naye ni mchafu kama Balali, sasa amshitaki ili iweje? Aumbuke na yeye?
Ni ngumu sana.
Tumsubiri Balali aje aseme yale mabilioni alikula na nani!
 
Kikwete akatangaza kutengua uteuzi wa Balali na kuipa bodi ya BOT (ambayo ndiyo iliyoshiriki katika wizi wa awali) miezi sita kuchunguza kile kilichochunguzwa na waliochunguza ile kamati iliyochunguza ile kampuni iliyochunguza yale CAG aliyochunguza baada ya kampuni ya uchunguzi kuchunguza uchunguzi wa .....nimechanganyikiwa sasa.

Hapo lazima uchanganyikiwe dah ndo serikali yetu hiyo yaani usanii mtupu..Kuwazomea viongozi sidhani kama itasaidia sana maana wapo wengi waliozomewa kwenye kipindi cha uchanguzi na sasa wapo madarakani na ni mawaziri so hata kumzomea JK ambae ana imani ya kushinda kwa hizo 80% anaweza assume kumzomea kwenu ndio kumshangilia...Tanzania imepata kiongozi aliyekulia kijiweni yaani Yeye na mawaziri wote inaonekana wanacheza karata moja na lengo lao moja tu!!
 
Mwafrika wa Kike,
Hata kama ungekuwa ni wewe, unaweza kukata tawi ulilokalia? Ripoti ya Slaa inamtaja Kikwete kwamba naye ni mchafu kama Balali, sasa amshitaki ili iweje? Aumbuke na yeye?
Ni ngumu sana.
Tumsubiri Balali aje aseme yale mabilioni alikula na nani!

IDIMI,

Kila siku unasikia story huko Asia (esp Japan) za mawaziri kujiuzulu na kuacha madaraka pale inapodhihirika kuwa kuwepo kwao kunahatarisha maisha na uchumi wa mamilioni ya raia wenzao.

Kikwete anaweza kufanya the right thing hapa na kukata mzizi wa fitina na kuwatosa wenzake huku akitumia machine ya uongozi kuzima kila aina ya upizani watakaoanzisha.

Kusubiri Balali aje inaweza kuwa ni ndoto sasa hivi. Kuna uwezekano mdogo kuwa jamaa ataenda bongo. Kikwete pia haonekani hata kama ana mpango wa kumleta Balali ili ashtakiwe.

Kwa sasa mimi narudisha mpira kwa Kikwete. Yeye ana nafasi nzuri sana ya kuomba msamaha kwa MUNGU na kwa wananchi wa Tanzania na akasaidia kuwatosa kina Patel, Mramba, Mgonja, na wenzake ili nchi ikapumua kidogo.
 
Kifupi Jamani Sisi Hatuna Serikali Yaani From President Mpaka Kwa Mjumbe Sioni Kinachofanyika.

Jk Kwa Wale Msiomfahamu Ndio Uwezo Wake Sio Mtu Wa Kufanya Maamuzi Magumu-just Follow His Trail Wizara Zote Alizopita Hakuwahi Kufanya Maamuzi Magumu.pole Yetu Watanzania Masikini Tuko Kwenye Hii York Sijui Nani Wa Kututoa.
 
IDIMI,

Kila siku unasikia story huko Asia (esp Japan) za mawaziri kujiuzulu na kuacha madaraka pale inapodhihirika kuwa kuwepo kwao kunahatarisha maisha na uchumi wa mamilioni ya raia wenzao.

Kikwete anaweza kufanya the right thing hapa na kukata mzizi wa fitina na kuwatosa wenzake huku akitumia machine ya uongozi kuzima kila aina ya upizani watakaoanzisha.

Kusubiri Balali aje inaweza kuwa ni ndoto sasa hivi. Kuna uwezekano mdogo kuwa jamaa ataenda bongo. Kikwete pia haonekani hata kama ana mpango wa kumleta Balali ili ashtakiwe.

Kwa sasa mimi narudisha mpira kwa Kikwete. Yeye ana nafasi nzuri sana ya kuomba msamaha kwa MUNGU na kwa wananchi wa Tanzania na akasaidia kuwatosa kina Patel, Mramba, Mgonja, na wenzake ili nchi ikapumua kidogo.

Mwafrika wa Kike,
Jamaa hana utashi wa kisiasa wa kuweza kuwaunguza wenzake katika dili feki kama hizo kwani na yeye ni mhusika! Hiyo ndio haswa pointi ambayo ningeweza kuiwekea msisitizo. Naogopa kuwatosa kwa sababu anajua kwamba wao pia wanjua siri zake, kwa hito anaogopa kivuli chake! Kwamba "Akimwaga ugali, sisi tunamwaga mboga"! Mchezo wote uko hapa!
 
Wapinzani mnamtesa sana JK yaani kaja na kila mbinu sasa anagota .Karibia ataamua kukata tawi aanguke chini . JK seriously alikuja kuia CCM na CCM itakufa kwa mwendo huuu.Kama iafi basi JK ajiandae kutoa amri kama Kibaki ya shoot to kill.
 
Hodi wana JF wenzangu!

Mimi naona Kikwete hawezi kumshitaki bwana Balali ikiwa bwana Balali bado yuko USA.

Inaeleweka wazi kwamba Balali alikimbilia USA kupata matibabu ambayo yalikuwa ni ya kuokoa maisha yake.

Pia inajulikana kwamba bwana Balali ana baadhi ya wana familia yake huko USA ambayo imejitahidi kwa udi na uvumba kuhakikisha baba huyu anapona.

Halafu inajulikana kwamba ikiwa bwana Balali ataingia Tanzania, na kufanikiwa kutoa ushahidi wake dhidi ya tuhuma zinazomhusu, basi kwa kuwa watu wengi wanahusika akiwemo mheshimiwa Rais Kikwete, basi huo ndio utakuwa ndio mwanzo wa mwamko kwa wananchi wajinga wa Tanzania ambao bado mpaka leo tumelala usingizi mzito huku baadhi ya watu wenye funguo za iliko keki ya taifa wakifanza mambo ya ajabu.

Kwa hio juhudi yoyote ya kumpata bwana Balali inayofanzwa sasa itakuwa ni kazi bure kama yeye mwenyewe bwana Balali ameamua kwamba asipatikane.

Kitu kimoja ambacho mimi nimegundua ni ujinga wa baadhi ya wana JF ambao kwa makusudi kabisa wanapotosha mada hii muhimu na maalum na inayohusu mustakabali mzima wa hali ya kisiasa, kiuchumi na kijamii kwa taifa letu la Tanzania.

Ni tabia hii ya ujinga ambapo baadhi ya magazeti ya Uhuru na Mzalendo na yale ya Daily News na mengine,kupenda kuandika habari za kukoroga na kudanganya wananchi, habari ambazo kama bwana Balali bado atakuwa hai mpaka atakapotoa ushahidi wake, ndio itakuwa mwisho wa ujinga huo na wananchi kuelewa kwamba kwa miaka yote tokea tupate uhuru mzunguko wa pesa upo tu serikalini na CCM na makoloni yake.

Sasa nawaomba kama kuna mwana JF yeyote anaefahamu ukweli wa kwamba kwanini bwana Balali alikimbilia US kwa matibabu na kwanini hadi leo anatafutwa na asionekane, atuletee habari hapa jamvini hasa wana JF walio jikoni -US.
 
Wapinzani mnamtesa sana JK yaani kaja na kila mbinu sasa anagota .Karibia ataamua kukata tawi aanguke chini . JK seriously alikuja kuia CCM na CCM itakufa kwa mwendo huuu.Kama iafi basi JK ajiandae kutoa amri kama Kibaki ya shoot to kill.

Kwi kwi kwi kwi!
Nadhani hadi ifike 2010, jamaa atakuwa ashatoa amri hiyo. Si unaona jinsi maandamano ya wapinzani Danganyika yanavyozimwa kinamna na polisi? Ipo siku wenye nchi tutasema hapana! Liwalo na liwe! We have nothing to loose, except oulr lives!
 
Nadhani tuwe waelevu kidogo kwa kuwa ata tume ikishabaini wenye makosa inabidi uchunguzi ufanyike kujua nani alifanya nini ili ata kesi inapoandikwa kusiwepo ten na marekebisho ya mashtaka.sasa mnadhani kwakuwa tu ripoti imetoka kinachofata ni mahakamani!nchi haiendeshwi namna hio
 
Kama Kikwete ataifanya CCM iwe kama KANU ya Uhuru Kenyatta, that will be the best thing for Tanzania. Mistake ni kuwa JK aliingia ulingoni akiwa amefungwa mikono, how do you expect him to fight! Zawadi pekee anayoweza kutupa watanzani ni kufanya kuwe na true political competition, yaani kupunguza nguvu ya CCM iwe sawa na vyama vingine ili kuwe na level playing field. I want to look at this on this side!
 
Consider yourself ignored by Mwafrika wa Kike from now on unless........
Mwafrika wa kike kila kukicha inaonyesha ur not matured enough kua hapa JF.Or Usitake sisi watu wa zamani turejee ktk imani yetu ya zamani kua KINA DADA BADO MUDA WA KUWAPA PLATFORM ZA KUJADILI NA KUTOA MAAMUZI BADO MUENDELEE KUKAA JIKONI NA KULEA WATOTO.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom