PakaJimmy
JF-Expert Member
- Apr 29, 2009
- 16,203
- 8,724
Childish!- Ukifanya kitu bila kukieleza ni sawa na kwamba hukukifanya
Zamani tukiwa watoto nakumbuka ukienda mtoni kuteka maji, basi wakati wa kurudi unakataa kupokelewa na mtu mwingine yeyote zaidi ya mama aU baba!... ha ha haaaa!
Sasa sentenso ya pale juu kwenye quote ni kitu kama hicho!
Unatumia gharama kutengeneza kitu, then unatumia gharama ingine kutangaza kuwa umefanya!
Nakumbuka serikali ya hawa MAGAMBA iliamua kutuma mawaziri wake wazunguke nchi nzima kueleza mafanikio ya serikali(my hairs!!!!) na fedha nyingi sana ililiwa kwa mtindo huo wa safari za upuuzi na upofu!
Mtu ukifanya jambo zuri huna haja ya kupitisha nyago kuwaambia watu kuwa umefanya kadha na kadha, watu wataona wenyewe bana!
Kweli MAGAMBA mmechoka, na haata MKIGAWA FEDHA KWA RAIA hakuna jinsi mnaweza kujitoa shombo la UFISADI!