Kikwete na Pinda walimuonea Dr. Magufuli! Waliongea naye kabla ya kumzuia kwenye bomoa bomoa?

Kwa matamshi na maamuzi haya ya viongozi wa juu wa Taifa...... kumbe bado nchi imekwama kwenye matope.... sasa sijui tufanyeje ili tuikwamue.....

KWA MUDA MREFU NIMEVUMILIA KUTOCHANGIA HII THREAD ILI ANGALAU NIONE KAMA WATAJITOKEZA MASHABIKI WA MAGUFULI WAKIWA NA VIELEE-LEZO AU WATAENDELEA KUMWAGA MANENO MATUPU KUWA MAGUFUOI ANASIMAMIA SHERIA BILA YA KUZITAJA KINAGAUBAGA SHERIA ANAZOSIMAMIA ILI KWA PAMOJA TUZIPIME KAMA ALIKUWA SAHIHI AU MAGUFULI ALICHEMKA.

NAANZA SASA:-

SABABU ZA MAGUFULI KUAKARIPIWA HIZI HAPA.
Sasa imebainika sababu za Mhe John Pombe Magufuli kukaripiwa na wakubwa wake serikalini ni kutokana na kuwa mbumbumbu wa sheria za barabara ambazo amekuwa akitamba kuwa aliapa kuzilinda.

Kama ambavyo Mhe John Magufuli aliliambia bunge lililoisha wakati akijibu swali kuhusu hifadhi ya barabara, alisema upana wa hifadhi hiyo nchi nizma ilikuwa ni Mita 22 kila upande kutoka katikati ya barabara, lakini upana huo uliongezwa kufikia Mita 30 kwa Kanuni za Sheria ya barabara namba 13 ya 2007 zilipopitishwa kwa Tangazo la Serikali namba 21 la Tar 23 Januari 2009 ibara ya 29 . Na akaongeza kuwa wananchi wanaoguswa na ongezeko hilo wana haki ya kulipwa fidia.

Ibara ya 27 (2) ya Kanuni za Sheria hiyo inamtaka Waziri wa Ujenzi atakaporidhika kuwa ardhi fulani inahitajika kwa ajili ya maendeleo ya barabara atawasiliana na Wizara wa Ardhi, kwa ajili ya ardhi hiyo kuhifadhiwa. Kutokea upana wa hifadhi ya barabara kuongezwa kwa MIta 8 kupitia Kanuni za 2009, hakuna Waziri yoyote wa Ujenzi wala Mhe John Magufuli mwenyewe aliyewasiliana na Wizara ya Ardhi ili itimize wajibu wake wa kuhifadhi eneo hilo kwa mujibu wa sheria? Kitendo cha Magufuli kuwatuma wafanyakazi wa TANROAD kuweka alama ya X katika nyumba zilizoko katika upana wa MIta 8 kimekiuka sheria, tena alizojitungia mwenyewe?.

Ibara ya 27 (3 na 4 ) inamataka Waziri wa Ujenzi baada ya kufanya mawasiliano na Waziri wa Ardhi atahakiksha ananunua ardhi hiyo kutoka kwa wananchi hao. Je Mhe John Magufuli alifanya hivyo? Badala yake Mhe Magufuli alitumia ubabe na kuwatuma kwa lazima na vitisho vya kufukuzwa kazi wafanyakazi wa TANROAD kuvamia nyumba za wananchi na kuweka alama za X katika Mita 8 zilizoongezeka 2009, huku kulikuwa ni kukiuka sheria ya barabara.

Ibara ya 27 (5) inatamka kuwa baada ya siku 60 tokea wananchi kulipwa fidia Wizara wa Ujenzi kupitia TANROAD atawataka wananchi husika kuhama au kutoendeleza chochote. Je wananchi ambao nyumba zao zilizowekewa alama za X wamewahi kuarifiwa chochote na Wizara ya Ardhi, sembuese kulipwa fidia? kwakuwa wananchi walioko ndani ya Mita 8 hawajalipwa fidia hawakutakiwa kubughudhiwa kwa lolote hadi hapo watakapokuwa wamelipwa fidia. Na Magufuli anafahamu hivyo ndio maana alijibu hivyo bungeni, lakini akafanya tofauti alipotoka bungeni.

Ibara ya 27 (6) inatamka kuwa baada ya wananchi kuarifiwa kuhusu ardhi hiyo kutwaliwa na Serikali watalipwa fidia. Kwa kuwa hakuna fidia zozote zilizolipwa ndio maan Waziri Mkuu Pinda na Raisi Kikwete wakamkaripia.

Kwa hali hii ni lazima tukubaliane kuwa Mhe John Pombe Magufuli ni mbumbumbu wa sheria, aidha ameshindwa hata kutafsiri na kutekeleza sheria alizojitungua mwenyewe. Je atawezaje kutekeleza sheria zingine?

Kwa hali hiyo Mhe JohnPombe Magufuli alistahili kufukuzwa kazi kwa kukiuka sheria za barabara na kuiletea aibu serikali.
 

Attachments

  • Roads Regulations Road Reserves 2.doc
    830 KB · Views: 29
  • Road Regulations Road Reserves.doc
    1.9 MB · Views: 27
KWA MUDA MREFU NIMEVUMILIA KUTOCHANGIA HII THREAD ILI ANGALAU NIONE KAMA WATAJITOKEZA MASHABIKI WA MAGUFULI WAKIWA NA VIELEE-LEZO AU WATAENDELEA KUMWAGA MANENO MATUPU KUWA MAGUFUOI ANASIMAMIA SHERIA BILA YA KUZITAJA KINAGAUBAGA SHERIA ANAZOSIMAMIA ILI KWA PAMOJA TUZIPIME KAMA ALIKUWA SAHIHI AU MAGUFULI ALICHEMKA.

NAANZA SASA:-

SABABU ZA MAGUFULI KUAKARIPIWA HIZI HAPA.
Sasa imebainika sababu za Mhe John Pombe Magufuli kukaripiwa na wakubwa wake serikalini ni kutokana na kuwa mbumbumbu wa sheria za barabara ambazo amekuwa akitamba kuwa aliapa kuzilinda.

Kama ambavyo Mhe John Magufuli aliliambia bunge lililoisha wakati akijibu swali kuhusu hifadhi ya barabara, alisema upana wa hifadhi hiyo nchi nizma ilikuwa ni Mita 22 kila upande kutoka katikati ya barabara, lakini upana huo uliongezwa kufikia Mita 30 kwa Kanuni za Sheria ya barabara namba 13 ya 2007 zilipopitishwa kwa Tangazo la Serikali namba 21 la Tar 23 Januari 2009 ibara ya 29 . Na akaongeza kuwa wananchi wanaoguswa na ongezeko hilo wana haki ya kulipwa fidia.

Ibara ya 27 (2) ya Kanuni za Sheria hiyo inamtaka Waziri wa Ujenzi atakaporidhika kuwa ardhi fulani inahitajika kwa ajili ya maendeleo ya barabara atawasiliana na Wizara wa Ardhi, kwa ajili ya ardhi hiyo kuhifadhiwa. Kutokea upana wa hifadhi ya barabara kuongezwa kwa MIta 8 kupitia Kanuni za 2009, hakuna Waziri yoyote wa Ujenzi wala Mhe John Magufuli mwenyewe aliyewasiliana na Wizara ya Ardhi ili itimize wajibu wake wa kuhifadhi eneo hilo kwa mujibu wa sheria? Kitendo cha Magufuli kuwatuma wafanyakazi wa TANROAD kuweka alama ya X katika nyumba zilizoko katika upana wa MIta 8 kimekiuka sheria, tena alizojitungia mwenyewe?.

Ibara ya 27 (3 na 4 ) inamataka Waziri wa Ujenzi baada ya kufanya mawasiliano na Waziri wa Ardhi atahakiksha ananunua ardhi hiyo kutoka kwa wananchi hao. Je Mhe John Magufuli alifanya hivyo? Badala yake Mhe Magufuli alitumia ubabe na kuwatuma kwa lazima na vitisho vya kufukuzwa kazi wafanyakazi wa TANROAD kuvamia nyumba za wananchi na kuweka alama za X katika Mita 8 zilizoongezeka 2009, huku kulikuwa ni kukiuka sheria ya barabara.

Ibara ya 27 (5) inatamka kuwa baada ya siku 60 tokea wananchi kulipwa fidia Wizara wa Ujenzi kupitia TANROAD atawataka wananchi husika kuhama au kutoendeleza chochote. Je wananchi ambao nyumba zao zilizowekewa alama za X wamewahi kuarifiwa chochote na Wizara ya Ardhi, sembuese kulipwa fidia? kwakuwa wananchi walioko ndani ya Mita 8 hawajalipwa fidia hawakutakiwa kubughudhiwa kwa lolote hadi hapo watakapokuwa wamelipwa fidia. Na Magufuli anafahamu hivyo ndio maana alijibu hivyo bungeni, lakini akafanya tofauti alipotoka bungeni.

Ibara ya 27 (6) inatamka kuwa baada ya wananchi kuarifiwa kuhusu ardhi hiyo kutwaliwa na Serikali watalipwa fidia. Kwa kuwa hakuna fidia zozote zilizolipwa ndio maan Waziri Mkuu Pinda na Raisi Kikwete wakamkaripia.

Kwa hali hii ni lazima tukubaliane kuwa Mhe John Pombe Magufuli ni mbumbumbu wa sheria, aidha ameshindwa hata kutafsiri na kutekeleza sheria alizojitungua mwenyewe. Je atawezaje kutekeleza sheria zingine?

Kwa hali hiyo Mhe JohnPombe Magufuli alistahili kufukuzwa kazi kwa kukiuka sheria za barabara na kuiletea aibu serikali.

Hongera kwa kurejea vifungu vya sheria....
Nimesoma maelezo ulioweka hapo ukinukuu sheria..... Lakini kama unakumbuka vizuri...
Magufuli alielezea kama hapo penye red juu panavyoonesha na pia utekelezaji wake ulipangwa kama alivyoeleza...... ndiyo maana ofisi ya mkoa wa DSM ya TANROADS ilibomolewa bila fidia..... Kitu kingine ambacho naomba nisikubaliane na wewe ni kuwa yeye alikuwa na lengo la kubomoa nyumba za wananchi bila fidia. Hicho si kweli kwa maana kuna sehemu mbali mbali hapa nchini ambako kuna miradi ya barabara inaendelea wananchi wamelipwa fidia MFANO Singida - Qatesh, Dodoma - Singida, Tunduma - S/wanga, Rombo - Holili n.k. Hivyo Magufuli kwa kushauriwa na wataalam alielezwa nani anastahili fidia na nani hastahili...
 
Hongera kwa kurejea vifungu vya sheria....
Nimesoma maelezo ulioweka hapo ukinukuu sheria..... Lakini kama unakumbuka vizuri...
Magufuli alielezea kama hapo penye red juu panavyoonesha na pia utekelezaji wake ulipangwa kama alivyoeleza...... ndiyo maana ofisi ya mkoa wa DSM ya TANROADS ilibomolewa bila fidia..... Kitu kingine ambacho naomba nisikubaliane na wewe ni kuwa yeye alikuwa na lengo la kubomoa nyumba za wananchi bila fidia. Hicho si kweli kwa maana kuna sehemu mbali mbali hapa nchini ambako kuna miradi ya barabara inaendelea wananchi wamelipwa fidia MFANO Singida - Qatesh, Dodoma - Singida, Tunduma - S/wanga, Rombo - Holili n.k. Hivyo Magufuli kwa kushauriwa na wataalam alielezwa nani anastahili fidia na nani hastahili...

KWA TAARIFA YAKO TANROAD HAIJAWAHI KUJEMNGA JENGO LOLOTE KATIKA HIFADHI YA BARABARA PALE UBUNGO. KAULI ZILE ZA KUDANGANYA TAIFA ZILIKUWA NI SEHEMU YA MBINU ZA MHE MAGUFULI KUWATISHA WATU WABOMOE NYUMBA ZAO ILI APATE SIFA KAMA ALIVYOPATA SIFA AKINA SOKOINE NA MREMA KWA WAT KUTUPA MALI ZA MAGENDO NA SILAHA.

KILICHOBOMOLEWA NI MAJENGO MAKUU MAKUU YALIYORITHIWA NA TANROAD KUTOKA KWA CONTRACTOR ALIYEIFANYIA BARABARA YA DAR-MLANDIZI UKARABATI MWAKA 2001 ALIYEITWA SCANPHIL KOLAS.

MAJENGO MAKUU MAKUU, KONTENA NA UZIO VILIKUWA NI SEHEMU YA YADI YA CONTRACTOR. KWA KAWAIDA CONTRACTORANBAPOKABIDHIWA SIET YA UJENZI, HATA BARABARA INAYOJENGWA MARA TU BAADA YA KUKABIDHIWA KWA CONTRACTOR HUITWA BUILDING SITE.

HIVYO UKWELI NI KWAMBA CONTARACTOR AITWAYE SCANPHIL KOLAS ALIJENGA YADI YAKE KATIKA SITE ALIYOKUWA AKIFANYA KAZI ZA UJENZI WA BARABARA YA MOROGORO NA MAGUFULI ALITAKIWA KUW AMKWELI KWA KUSEMA HIVYO NA SIO KUDANGANYA TAIFA KUWA TANROAD IMEJEMNGA KATIKA HIFADHI YA BARABARA.



HIVYO HAIKUWA SAHIHI KWA MAGUFULI KULIDANGANYA TAIFA KUWA TANROAD IMEJENGA KATIKAHIFADHI YA BARABARA. ALITAKIWA KUSEMA UKWELI KUWA MAJENGO HAYO YALIKUWA NI MALI YA CONTRACTOR SCANPHIL KOLAS.

Kitu kingine ambacho naomba nisikubaliane na wewe ni kuwa yeye alikuwa na lengo la kubomoa nyumba za wananchi bila fidia.MAGUFULI ALITAMK MWENYEWE KUWA WATU HAWATALIPWA FIDIA. NAOMBA UFUATILIE MATUKIO YA HAPACHINI HALAFU UNIAMBIE WANANCHI HAWA WALISTAHILI FIDIA AU LA? NA KWANINI MAGUFULI ALIWAWEKEA MAWE NA MABANGI YANAYOONYESHA MWISHO WA HIFADHI YA BARABARA MWAK 2001? MAGUFULIAKIAMUA JAMBO LAKE HANA CHA KUSIKILIZA WATAALAMU WALA NANI, NDIO MAAN HUWA HAUSISHI NGAZI ZA MKO, WILAYA N.K

Ibara ya 2 ya Kanuni za Sheria ya barabara (Tangazo la Serikali Namba 161 la tarehe 5/5/1967) inatamka kuwa hifadhi ya barabara kuu zote hapa nchini (Trunk roads) ni Futi 75 kila upande au Mita 22.86, kutoka katikati ya barabara. Ibara ya 4 ilitamka upana wa hifadhi ya barabara kwa barabara ya Morogoro, kati ya kati ya Ubungo hadi Kibaha kuwa ni kati ya Futi 300 hadi 400, sawa na Mita 120 kutoka katikati ya barabara. Ujenzi wa barabara ya Morogoro iliyokusudiwa na ibara ya 4 hapo juu, ulikamilka mwanzoni mwa miaka ya 1970.
Wakati huo huo, mwanzoni wa miaka ya 1970, Serikali ya awamu ya kwanza chini ya Mwalimu Nyerere ilitekeleza sera ya Vijiji vya Ujamaa nchi nzima. Eneo kati ya Ubungo hadi Kibaha pia vilianzishwa Vijiji vya Ujamaa vya Kimara, Mbezi, Kibamba na Kiruvia. Wananchi walihamishiwa katika vijiji hivi na kugawiwa ardhi ya kuishi na kulima. Maeneo haya yalikoma kuwa na hadhi ya vijiji mwaka 1985, baada ya kuwekwa chini ya Mipango Miji.

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilitunga Sheria mpya za Ardhi namba 4 na 5 mwaka 1999, wakati wa kupitishwa kwake Mhe John Magufuli alikuwa ni mbunge. Kifungu cha 15 cha Sheria ya Ardhi ya Vijiji namba 5 ya 1999 kinatamka kuwa "Ugawaji wa ardhi uliofanywa kwa mtu au kundi la watu waishio au waliotakiwa kuhamia na kuishi katika kijiji wakati wowote kati ya 01 Jan 1970 hadi 31 Des 1977 , kama ugawaji huo ulifanywa kwa mujibu wa sheria au kinyume cha sheria au bila kuzingatia sheria yoyote, sasa inathibitishwa kuwa ugawaji huo ni halali na kwamba daima ni wenye nguvu ya kutoa haki na wajibu wa kisheria kwa kundi la watu waliogawiwa ardhi hiyo....." Aidh kifungu cha 16 kinatamka .......... masharti ya kifungu 15 yatatumika kila mara ugawaji wa ardhi ya kijiji ulipofanywa na halmashauri ya kijiji au mamlaka nyingine yoyote mnamo na baada ya 01 jan 1978 hadi tarehe ya kuanza kutumika kwa sheria hii.

Mwaka 2000, (ikiwa ni miezi michache baada ya kupitishwa kwa Sheria ya Ardhi ya Vijiji ya 1999, Rais Benjamin Mkapa alimteua Mhe John Magufuli kushika wadhifa Waziri wa Ujenzi. Akiwa kiongozi mwandamizi wa Serikali alikuwa kifahamu kuwa Serikali haikuwa na fedha za kuchapa, kusambaza na kutoa elimu kwa wananchi ya sheria mbali mbali zinazopitishwa na bunge hususan Sheria ya Ardhi ya Vijiji namba 5 ya 1999, ambayo iliipitishwa miezi michache kabla ya uteuzi wake; hivyo kwa kukosa elimu hiyo wananchi hususan wa maeneo kati ya Ubungo hadi Kibaha hawakuwa wakifahamu haki za umiliki wa ardhi waliyokuwa nayo tokea enzi za vijiji (kabla na hadi 1985) kwa mujibu wa vifungu 15 na 16 vya Sheria ya Ardhi ya Vijiji namba 5 ya 1999.

Katika hali inayoashiria ukosefu wa uadilifu na uaminifu kwa sheria za barabara na Sheria ya Ardhi ya Vijiji namba 5 ya 1999, Mhe John magufuli alimwagiza mkandarasi aliyewekwa na TANROAD kukarabati barabara ya Morogoro kuingia Mita 120 ndani ya ardhi na makazi ya wananchi pande zote mbili za barabara ya Morogoro, na kupanda kwa mawe na mabango yanayoonyesha mwisho wa hifadhi ya barabara kati ya Ubungo hadi Kibaha. Wananchi wala ngazi za Mkoa, Wilaya, Manispaa, Tarafa, Kata na Serikali za Mitaa waliojulishwa nini kinaendelea ikizingatiwa wananchi walikuwa wakiishi hapo kwa miaka kati ya 40 hadi 50.

Wakati Mhe John Magufuli anatoa maagizo hayo kama Waziri wa Ujenzi, kama mmoja wa wabunge wa Bunge lililomaliza muda wake mwaka 2000 alikuwa akifahamu dhahiri kuwa ibara ya 4 ya Kanuni za Sheria ya barabara (Tangazo la Serikali Namba 161 la tarehe 5/5/1967) iliyoko kuwa ikitenga upana wa Futi 300 hadi 400 au Mita 120 kama hifadhi ya barabara ilikwisha poteza uhai mara tu baada ya kupitishwa kwa Sheria ya Ardhi ya Vijiji namba 5 ya 1999 na kuridhiwa na Rais wa Tanzania kwa mujibu wa Katiba tarehe 15 Mei 1999 ili kuanza kutumika kama sheria.

Kama Mhe John Magufuli angekuwa ni muumini mzuri wa sheria kama anavyodaiwa kuwa, alipaswa kutii na kutekeleza sheria iliyopitishwa na bunge 1999; badala ya kutii na kutekeleza Kanuni iliyotungwa na Waziri wa Ujenzi 1967, kwa kuwa sheria ya 1999 ilitamka bayana kuwa wananchi wana haki na ardhi waliyogawiwa chini ya operesheni vijiji hata kama ni kwa kukiuka sheria yoyote. Sheria yoyote sio ni pamoja na hiyo Kanuni ya Sheria ya brbr ya 1967? Ni kwa mantiki hiyo kauli za Waziri Mkuu na Rais zinakuwa za busara na hekima kwa kuwa zinazingatia historia ya Tanzania, hivyo ni lazima ubinadamu utumike.


VIPI KUHUSU KANUNI ZA SHERIA YA BARABARA NILIZOWEKA KWENYE THREAD YANGU YA AWALI, JE MAGUFULI ALIPATA WAPI MADARAKA YA KUWAAGIZA TAMROAD KIUINGI KATIK ARDHI NA MAZKI YA WANANCHI YALIYOKO MITA 8 ZILIZOONGEZWA MWAK 2009 BILA YA ENEO HILO KUWA LIMEHIADHIWA NA WIZARA YA ARDHI KAMA KANUNI ZAKE MWENYEWE ZINAVYOHITAJI?
 

Attachments

  • OPERESHENI VIJIJI KIFUNGU 15 NA 16.pdf
    773.9 KB · Views: 32
KWA TAARIFA YAKO TANROAD HAIJAWAHI KUJEMNGA JENGO LOLOTE KATIKA HIFADHI YA BARABARA PALE UBUNGO. KAULI ZILE ZA KUDANGANYA TAIFA ZILIKUWA NI SEHEMU YA MBINU ZA MHE MAGUFULI KUWATISHA WATU WABOMOE NYUMBA ZAO ILI APATE SIFA KAMA ALIVYOPATA SIFA AKINA SOKOINE NA MREMA KWA WAT KUTUPA MALI ZA MAGENDO NA SILAHA.

KILICHOBOMOLEWA NI MAJENGO MAKUU MAKUU YALIYORITHIWA NA TANROAD KUTOKA KWA CONTRACTOR ALIYEIFANYIA BARABARA YA DAR-MLANDIZI UKARABATI MWAKA 2001 ALIYEITWA SCANPHIL KOLAS.

MAJENGO MAKUU MAKUU, KONTENA NA UZIO VILIKUWA NI SEHEMU YA YADI YA CONTRACTOR. KWA KAWAIDA CONTRACTORANBAPOKABIDHIWA SIET YA UJENZI, HATA BARABARA INAYOJENGWA MARA TU BAADA YA KUKABIDHIWA KWA CONTRACTOR HUITWA BUILDING SITE.

HIVYO UKWELI NI KWAMBA CONTARACTOR AITWAYE SCANPHIL KOLAS ALIJENGA YADI YAKE KATIKA SITE ALIYOKUWA AKIFANYA KAZI ZA UJENZI WA BARABARA YA MOROGORO NA MAGUFULI ALITAKIWA KUW AMKWELI KWA KUSEMA HIVYO NA SIO KUDANGANYA TAIFA KUWA TANROAD IMEJEMNGA KATIKA HIFADHI YA BARABARA.



HIVYO HAIKUWA SAHIHI KWA MAGUFULI KULIDANGANYA TAIFA KUWA TANROAD IMEJENGA KATIKAHIFADHI YA BARABARA. ALITAKIWA KUSEMA UKWELI KUWA MAJENGO HAYO YALIKUWA NI MALI YA CONTRACTOR SCANPHIL KOLAS.

Kitu kingine ambacho naomba nisikubaliane na wewe ni kuwa yeye alikuwa na lengo la kubomoa nyumba za wananchi bila fidia.MAGUFULI ALITAMK MWENYEWE KUWA WATU HAWATALIPWA FIDIA. NAOMBA UFUATILIE MATUKIO YA HAPACHINI HALAFU UNIAMBIE WANANCHI HAWA WALISTAHILI FIDIA AU LA? NA KWANINI MAGUFULI ALIWAWEKEA MAWE NA MABANGI YANAYOONYESHA MWISHO WA HIFADHI YA BARABARA MWAK 2001? MAGUFULIAKIAMUA JAMBO LAKE HANA CHA KUSIKILIZA WATAALAMU WALA NANI, NDIO MAAN HUWA HAUSISHI NGAZI ZA MKO, WILAYA N.K

Ibara ya 2 ya Kanuni za Sheria ya barabara (Tangazo la Serikali Namba 161 la tarehe 5/5/1967) inatamka kuwa hifadhi ya barabara kuu zote hapa nchini (Trunk roads) ni Futi 75 kila upande au Mita 22.86, kutoka katikati ya barabara. Ibara ya 4 ilitamka upana wa hifadhi ya barabara kwa barabara ya Morogoro, kati ya kati ya Ubungo hadi Kibaha kuwa ni kati ya Futi 300 hadi 400, sawa na Mita 120 kutoka katikati ya barabara. Ujenzi wa barabara ya Morogoro iliyokusudiwa na ibara ya 4 hapo juu, ulikamilka mwanzoni mwa miaka ya 1970.
Wakati huo huo, mwanzoni wa miaka ya 1970, Serikali ya awamu ya kwanza chini ya Mwalimu Nyerere ilitekeleza sera ya Vijiji vya Ujamaa nchi nzima. Eneo kati ya Ubungo hadi Kibaha pia vilianzishwa Vijiji vya Ujamaa vya Kimara, Mbezi, Kibamba na Kiruvia. Wananchi walihamishiwa katika vijiji hivi na kugawiwa ardhi ya kuishi na kulima. Maeneo haya yalikoma kuwa na hadhi ya vijiji mwaka 1985, baada ya kuwekwa chini ya Mipango Miji.

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilitunga Sheria mpya za Ardhi namba 4 na 5 mwaka 1999, wakati wa kupitishwa kwake Mhe John Magufuli alikuwa ni mbunge. Kifungu cha 15 cha Sheria ya Ardhi ya Vijiji namba 5 ya 1999 kinatamka kuwa "Ugawaji wa ardhi uliofanywa kwa mtu au kundi la watu waishio au waliotakiwa kuhamia na kuishi katika kijiji wakati wowote kati ya 01 Jan 1970 hadi 31 Des 1977 , kama ugawaji huo ulifanywa kwa mujibu wa sheria au kinyume cha sheria au bila kuzingatia sheria yoyote, sasa inathibitishwa kuwa ugawaji huo ni halali na kwamba daima ni wenye nguvu ya kutoa haki na wajibu wa kisheria kwa kundi la watu waliogawiwa ardhi hiyo....." Aidh kifungu cha 16 kinatamka .......... masharti ya kifungu 15 yatatumika kila mara ugawaji wa ardhi ya kijiji ulipofanywa na halmashauri ya kijiji au mamlaka nyingine yoyote mnamo na baada ya 01 jan 1978 hadi tarehe ya kuanza kutumika kwa sheria hii.

Mwaka 2000, (ikiwa ni miezi michache baada ya kupitishwa kwa Sheria ya Ardhi ya Vijiji ya 1999, Rais Benjamin Mkapa alimteua Mhe John Magufuli kushika wadhifa Waziri wa Ujenzi. Akiwa kiongozi mwandamizi wa Serikali alikuwa kifahamu kuwa Serikali haikuwa na fedha za kuchapa, kusambaza na kutoa elimu kwa wananchi ya sheria mbali mbali zinazopitishwa na bunge hususan Sheria ya Ardhi ya Vijiji namba 5 ya 1999, ambayo iliipitishwa miezi michache kabla ya uteuzi wake; hivyo kwa kukosa elimu hiyo wananchi hususan wa maeneo kati ya Ubungo hadi Kibaha hawakuwa wakifahamu haki za umiliki wa ardhi waliyokuwa nayo tokea enzi za vijiji (kabla na hadi 1985) kwa mujibu wa vifungu 15 na 16 vya Sheria ya Ardhi ya Vijiji namba 5 ya 1999.

Katika hali inayoashiria ukosefu wa uadilifu na uaminifu kwa sheria za barabara na Sheria ya Ardhi ya Vijiji namba 5 ya 1999, Mhe John magufuli alimwagiza mkandarasi aliyewekwa na TANROAD kukarabati barabara ya Morogoro kuingia Mita 120 ndani ya ardhi na makazi ya wananchi pande zote mbili za barabara ya Morogoro, na kupanda kwa mawe na mabango yanayoonyesha mwisho wa hifadhi ya barabara kati ya Ubungo hadi Kibaha. Wananchi wala ngazi za Mkoa, Wilaya, Manispaa, Tarafa, Kata na Serikali za Mitaa waliojulishwa nini kinaendelea ikizingatiwa wananchi walikuwa wakiishi hapo kwa miaka kati ya 40 hadi 50.

Wakati Mhe John Magufuli anatoa maagizo hayo kama Waziri wa Ujenzi, kama mmoja wa wabunge wa Bunge lililomaliza muda wake mwaka 2000 alikuwa akifahamu dhahiri kuwa ibara ya 4 ya Kanuni za Sheria ya barabara (Tangazo la Serikali Namba 161 la tarehe 5/5/1967) iliyoko kuwa ikitenga upana wa Futi 300 hadi 400 au Mita 120 kama hifadhi ya barabara ilikwisha poteza uhai mara tu baada ya kupitishwa kwa Sheria ya Ardhi ya Vijiji namba 5 ya 1999 na kuridhiwa na Rais wa Tanzania kwa mujibu wa Katiba tarehe 15 Mei 1999 ili kuanza kutumika kama sheria.

Kama Mhe John Magufuli angekuwa ni muumini mzuri wa sheria kama anavyodaiwa kuwa, alipaswa kutii na kutekeleza sheria iliyopitishwa na bunge 1999; badala ya kutii na kutekeleza Kanuni iliyotungwa na Waziri wa Ujenzi 1967, kwa kuwa sheria ya 1999 ilitamka bayana kuwa wananchi wana haki na ardhi waliyogawiwa chini ya operesheni vijiji hata kama ni kwa kukiuka sheria yoyote. Sheria yoyote sio ni pamoja na hiyo Kanuni ya Sheria ya brbr ya 1967? Ni kwa mantiki hiyo kauli za Waziri Mkuu na Rais zinakuwa za busara na hekima kwa kuwa zinazingatia historia ya Tanzania, hivyo ni lazima ubinadamu utumike.


VIPI KUHUSU KANUNI ZA SHERIA YA BARABARA NILIZOWEKA KWENYE THREAD YANGU YA AWALI, JE MAGUFULI ALIPATA WAPI MADARAKA YA KUWAAGIZA TAMROAD KIUINGI KATIK ARDHI NA MAZKI YA WANANCHI YALIYOKO MITA 8 ZILIZOONGEZWA MWAK 2009 BILA YA ENEO HILO KUWA LIMEHIADHIWA NA WIZARA YA ARDHI KAMA KANUNI ZAKE MWENYEWE ZINAVYOHITAJI?

Aksante kwa maelezo yako mazuri yaliyojikita kwenye sheria/TARATIBU..........LAKINI SUALA LINABAKI PALE PALE........WAKUU WAKE BAADA YA KUGUNDUA MAKOSA ALIYOYAFANYA MAGUFULI KATIKA KUTEKELEZA MAJUKUMU YAKE WALIFANYA KIKAO NAYE AU KUZUNGUMZA NAYE KUWA JINSI ANAVYOFANYA KAZI HAZINGATII SHERIA .......??? AU WALIAMUA KUMUUMBUA TUUU...???....TENA MAJUKWAANI ILI WANANCHI WAMCHUKIEEE??????/
 
aksante kwa maelezo yako mazuri yaliyojikita kwenye sheria/taratibu..........lakini suala linabaki pale pale........wakuu wake baada ya kugundua makosa aliyoyafanya magufuli katika kutekeleza majukumu yake walifanya kikao naye au kuzungumza naye kuwa jinsi anavyofanya kazi hazingatii sheria .......??? Au waliamua kumuumbua tuuu...???....tena majukwaani ili wananchi wamchukieee??????/

nashukuru sana kwa uungwana wako wa kukubali ukweli, tofauti na mashabiki vipofu wa magufuli amabo hawahawahi kusoma hata sheria moja ya barabara lakini kila siku kujitia kutaka sheria zitekeelzwe hata kama ni sheria feki.

Gazeti la tanzania dima liliwahi kuripoti kuwa waziri mkuu kabla ya kwenda kageraa likuwa na mazungumzo na magufuli mara mbali kuhusu suala hilo hilo, lakini akitoka hapo anaendelea kusisitiza bomoa bomoa tena. Hivyo kitenda cha kwena kuwambia mbele ya wapiga kura wake ilikuwa ni kama vile barua ya onyo.

Kimsingi magufuli alistahili kufukuzwa kazi kwa kutumia vibya madaraka. Lakini kwa kuzingatia athri zake kisiasa ndio maan wakaamua kumkabili kinagaubaga.
 
nashukuru sana kwa uungwana wako wa kukubali ukweli, tofauti na mashabiki vipofu wa magufuli amabo hawahawahi kusoma hata sheria moja ya barabara lakini kila siku kujitia kutaka sheria zitekeelzwe hata kama ni sheria feki.

Gazeti la tanzania dima liliwahi kuripoti kuwa waziri mkuu kabla ya kwenda kageraa likuwa na mazungumzo na magufuli mara mbali kuhusu suala hilo hilo, lakini akitoka hapo anaendelea kusisitiza bomoa bomoa tena. Hivyo kitenda cha kwena kuwambia mbele ya wapiga kura wake ilikuwa ni kama vile barua ya onyo.

Kimsingi magufuli alistahili kufukuzwa kazi kwa kutumia vibya madaraka. Lakini kwa kuzingatia athri zake kisiasa ndio maan wakaamua kumkabili kinagaubaga.

Mimi sipingi wala siungi mkono kuwa Waziri mkuu Pinda aliongea na Waziri Dr. Magufuli.......Ila pia unaweza nirushia hilo gazeti hapa????

Ila hapo penye red umeenda mbali....mbona Waziri Ngereja ametuweka na anaendelea kutuweka kwenye giza hajafukuzwa????
Waziri Dr. Mwinyi kwenye suala la Gongo la Mboto mbona hajafukuzwaa????
 
Back
Top Bottom