Tuko
JF-Expert Member
- Jul 29, 2010
- 11,178
- 7,319
Katika kampeni ya mwaka 2005, kwa masikio yangu nilimsikia Kikwete katika campaign team ya CCM akisema anadhamiria kuwabadilisha jamii ya wafugaji Tanzania kutoka hali ya kuwa wachungaji, na kuwa wafugaji. Kikwete alitumia kauli moja maarufu sana kuwa wakati anazunguka nchini, alisikitishwa sana na kuwaona wafugaji wakiwa katika hali ile "Mifugo imekonda, na mchungaji amekonda"...
Leo ni miaka 8, na bado miaka miwili tu Kikwete aachie madaraka, inshaalah:
- Hakuna maboresho yeyote yaliyofanywa kwa sekta ya ufugaji...
- Hata wafugaji aliowaita wachungaji, leo hii baadhi yao hata mifugo ya kuchunga hawana...
- Wachungaji waliopo nchini, wamekuwa wakihamishwa kutoka eneo moja hadi jingine, wamekuwa wakimbizi katika nchi yao
- Kutokana na kuwa katika hali mbaya, wafugaji wamelazimika kuwa watoa rushwa na migogoro kati yao na wakulima imeongezeka
- Hakuna program yeyote ya ruzuku kwa wafugaji
- Hakuna Program yeyote significant ya breeding nchi hii, na aina ya mifugo waliyo nayo wafugaji ni duni sawa tu na kabla hajaingia Kikwete
- Hakuna program yeyote ya kutengenezwa kwa miundombinu ya kuwezesha upatikanaji wa maji ya kunywa kwa mifugo na hata wafugaji wenyewe
- Huduma za kijamii kama hospitali, shule, masoko nk zimezidi kuwa mbovu katika maeneo walikotupwa wafugaji...
Huu ni ulaghai, hii ni fedheha, hata kwa mwenyezi Mungu hii ni dhambi na ni ukiukwaji mkubwa wa haki za msingi za binadamu uliofanywa na raisi Kikwete na serikali ya CCM...
Leo ni miaka 8, na bado miaka miwili tu Kikwete aachie madaraka, inshaalah:
- Hakuna maboresho yeyote yaliyofanywa kwa sekta ya ufugaji...
- Hata wafugaji aliowaita wachungaji, leo hii baadhi yao hata mifugo ya kuchunga hawana...
- Wachungaji waliopo nchini, wamekuwa wakihamishwa kutoka eneo moja hadi jingine, wamekuwa wakimbizi katika nchi yao
- Kutokana na kuwa katika hali mbaya, wafugaji wamelazimika kuwa watoa rushwa na migogoro kati yao na wakulima imeongezeka
- Hakuna program yeyote ya ruzuku kwa wafugaji
- Hakuna Program yeyote significant ya breeding nchi hii, na aina ya mifugo waliyo nayo wafugaji ni duni sawa tu na kabla hajaingia Kikwete
- Hakuna program yeyote ya kutengenezwa kwa miundombinu ya kuwezesha upatikanaji wa maji ya kunywa kwa mifugo na hata wafugaji wenyewe
- Huduma za kijamii kama hospitali, shule, masoko nk zimezidi kuwa mbovu katika maeneo walikotupwa wafugaji...
Huu ni ulaghai, hii ni fedheha, hata kwa mwenyezi Mungu hii ni dhambi na ni ukiukwaji mkubwa wa haki za msingi za binadamu uliofanywa na raisi Kikwete na serikali ya CCM...