Kikwete na CCM kuwahadaa wafugaji: Ni Aibu, ni Fedheha, na si Haki....

Tuko

JF-Expert Member
Jul 29, 2010
11,178
7,319
Katika kampeni ya mwaka 2005, kwa masikio yangu nilimsikia Kikwete katika campaign team ya CCM akisema anadhamiria kuwabadilisha jamii ya wafugaji Tanzania kutoka hali ya kuwa wachungaji, na kuwa wafugaji. Kikwete alitumia kauli moja maarufu sana kuwa wakati anazunguka nchini, alisikitishwa sana na kuwaona wafugaji wakiwa katika hali ile "Mifugo imekonda, na mchungaji amekonda"...

Leo ni miaka 8, na bado miaka miwili tu Kikwete aachie madaraka, inshaalah:

- Hakuna maboresho yeyote yaliyofanywa kwa sekta ya ufugaji...

- Hata wafugaji aliowaita wachungaji, leo hii baadhi yao hata mifugo ya kuchunga hawana...

- Wachungaji waliopo nchini, wamekuwa wakihamishwa kutoka eneo moja hadi jingine, wamekuwa wakimbizi katika nchi yao

- Kutokana na kuwa katika hali mbaya, wafugaji wamelazimika kuwa watoa rushwa na migogoro kati yao na wakulima imeongezeka

- Hakuna program yeyote ya ruzuku kwa wafugaji

- Hakuna Program yeyote significant ya breeding nchi hii, na aina ya mifugo waliyo nayo wafugaji ni duni sawa tu na kabla hajaingia Kikwete

- Hakuna program yeyote ya kutengenezwa kwa miundombinu ya kuwezesha upatikanaji wa maji ya kunywa kwa mifugo na hata wafugaji wenyewe

- Huduma za kijamii kama hospitali, shule, masoko nk zimezidi kuwa mbovu katika maeneo walikotupwa wafugaji...

Huu ni ulaghai, hii ni fedheha, hata kwa mwenyezi Mungu hii ni dhambi na ni ukiukwaji mkubwa wa haki za msingi za binadamu uliofanywa na raisi Kikwete na serikali ya CCM...
 
Zipo habari kuwa huko Morogoro leo kuna vurugu kati ya Wakulima na Wafugaji...
 
Katika kampeni ya mwaka 2005, kwa masikio yangu nilimsikia Kikwete katika campaign team ya CCM akisema anadhamiria kuwabadilisha jamii ya wafugaji Tanzania kutoka hali ya kuwa wachungaji, na kuwa wafugaji. Kikwete alitumia kauli moja maarufu sana kuwa wakati anazunguka nchini, alisikitishwa sana na kuwaona wafugaji wakiwa katika hali ile "Mifugo imekonda, na mchungaji amekonda"...

Leo ni miaka 8, na bado miaka miwili tu Kikwete aachie madaraka, inshaalah:

- Hakuna maboresho yeyote yaliyofanywa kwa sekta ya ufugaji...

- Hata wafugaji aliowaita wachungaji, leo hii baadhi yao hata mifugo ya kuchunga hawana...

- Wachungaji waliopo nchini, wamekuwa wakihamishwa kutoka eneo moja hadi jingine, wamekuwa wakimbizi katika nchi yao

- Kutokana na kuwa katika hali mbaya, wafugaji wamelazimika kuwa watoa rushwa na migogoro kati yao na wakulima imeongezeka

- Hakuna program yeyote ya ruzuku kwa wafugaji

- Hakuna Program yeyote significant ya breeding nchi hii, na aina ya mifugo waliyo nayo wafugaji ni duni sawa tu na kabla hajaingia Kikwete

- Hakuna program yeyote ya kutengenezwa kwa miundombinu ya kuwezesha upatikanaji wa maji ya kunywa kwa mifugo na hata wafugaji wenyewe

- Huduma za kijamii kama hospitali, shule, masoko nk zimezidi kuwa mbovu katika maeneo walikotupwa wafugaji...

Huu ni ulaghai, hii ni fedheha, hata kwa mwenyezi Mungu hii ni dhambi na ni ukiukwaji mkubwa wa haki za msingi za binadamu uliofanywa na raisi Kikwete na serikali ya CCM...
Hizo huduma ulizotaja kama zisingekuwepo wewe hapa ulipo ungefikaje.
 
Mkuu Tuko umenena kweli... Nakumbuka sana hotuba ya Kikwete ya kufunga kampeni pale jangwani mwaka 2005 (dakika kadhaa kabla hajaanguka), alisema kuwa amesikitishwa sana na hali ya wafugaji aliyoiona katika mizunguko yake nchi nzima, na kuahidi kuwa akiingia madarakani ataboresha sekta hiyo.

Leo anatoka akiwa amewaacha vibaya zaidi..
 
Sidhani kama CCM itapata tena kura hata moja kutoka kwa wafugaji mwaka 2015.
 
Kwani isingekuwa ni wizi na ufisadi wa CCM wewe ungefika hapo ulipo?

Mkuu wala usiangaike kupoteza mda wako kujibizana na huyu kilema wa akili... anatafuta buku saba ya kununua ubuyu leo...
 
Sidhani kama CCM itapata tena kura hata moja kutoka kwa wafugaji mwaka 2015.

CCM ni chama cha wote. Ni chama cha wafugaji na wakulima. Ni chama cha kila mmoja wetu ukiwemo wewe Ramos
 
Katika kampeni ya mwaka 2005, kwa masikio yangu nilimsikia Kikwete katika campaign team ya CCM akisema anadhamiria kuwabadilisha jamii ya wafugaji Tanzania kutoka hali ya kuwa wachungaji, na kuwa wafugaji. Kikwete alitumia kauli moja maarufu sana kuwa wakati anazunguka nchini, alisikitishwa sana na kuwaona wafugaji wakiwa katika hali ile "Mifugo imekonda, na mchungaji amekonda"...

Leo ni miaka 8, na bado miaka miwili tu Kikwete aachie madaraka, inshaalah:

- Hakuna maboresho yeyote yaliyofanywa kwa sekta ya ufugaji...

- Hata wafugaji aliowaita wachungaji, leo hii baadhi yao hata mifugo ya kuchunga hawana...

- Wachungaji waliopo nchini, wamekuwa wakihamishwa kutoka eneo moja hadi jingine, wamekuwa wakimbizi katika nchi yao

- Kutokana na kuwa katika hali mbaya, wafugaji wamelazimika kuwa watoa rushwa na migogoro kati yao na wakulima imeongezeka

- Hakuna program yeyote ya ruzuku kwa wafugaji

- Hakuna Program yeyote significant ya breeding nchi hii, na aina ya mifugo waliyo nayo wafugaji ni duni sawa tu na kabla hajaingia Kikwete

- Hakuna program yeyote ya kutengenezwa kwa miundombinu ya kuwezesha upatikanaji wa maji ya kunywa kwa mifugo na hata wafugaji wenyewe

- Huduma za kijamii kama hospitali, shule, masoko nk zimezidi kuwa mbovu katika maeneo walikotupwa wafugaji...

Huu ni ulaghai, hii ni fedheha, hata kwa mwenyezi Mungu hii ni dhambi na ni ukiukwaji mkubwa wa haki za msingi za binadamu uliofanywa na raisi Kikwete na serikali ya CCM...

Ushahidi wa haya ulioyaandika unao? Suala la wafugaji kuhama hama ni kutokana mabadiliko ya hali ya hewa kutoka eneo moja hadi lingine, sidhani kama hili liko chni ya uwezo wa JK. Hivi sasa masoko mazao yatokanayo na mifugo yameboreshwa sana ukilinganisha na zamani, Kule dodoma kuna machinjio makubwa sana yamejengwa. Madawa ya mifugo yameongezeka kwa kiasi kikubwa sana. Sina uhakika kama ulichokiandika umekifanyia utafiti au umetumia tu hoja za migogoro ya wakulima na wafugaji.
 
wewe unatafuta nini humu? kutwa kucha upo JF

huyo jamaa ndo wale waliokuwa na kazi ya kumchafua ZITTO Mitandaoni, sasa wamemaliza kazi zao na hawana la kufanya wanabaki kuandika hata wasilolijua.
 
Sidhani kama CCM itapata tena kura hata moja kutoka kwa wafugaji mwaka 2015.

Kwani wewe ni mfugaji? Wafuaji weneywe wanajua juhudi zinazofanywa na serikali kuhakikisha migogoro yao dhidi ya wakulima inamalizika, wewe kapuku tu unawezaje kuwasemea? Unapoteza muda.
 
Katika kampeni ya mwaka 2005, kwa masikio yangu nilimsikia Kikwete katika campaign team ya CCM akisema anadhamiria kuwabadilisha jamii ya wafugaji Tanzania kutoka hali ya kuwa wachungaji, na kuwa wafugaji. Kikwete alitumia kauli moja maarufu sana kuwa wakati anazunguka nchini, alisikitishwa sana na kuwaona wafugaji wakiwa katika hali ile "Mifugo imekonda, na mchungaji amekonda"...

Leo ni miaka 8, na bado miaka miwili tu Kikwete aachie madaraka, inshaalah:

- Hakuna maboresho yeyote yaliyofanywa kwa sekta ya ufugaji...

- Hata wafugaji aliowaita wachungaji, leo hii baadhi yao hata mifugo ya kuchunga hawana...

- Wachungaji waliopo nchini, wamekuwa wakihamishwa kutoka eneo moja hadi jingine, wamekuwa wakimbizi katika nchi yao

- Kutokana na kuwa katika hali mbaya, wafugaji wamelazimika kuwa watoa rushwa na migogoro kati yao na wakulima imeongezeka

- Hakuna program yeyote ya ruzuku kwa wafugaji

- Hakuna Program yeyote significant ya breeding nchi hii, na aina ya mifugo waliyo nayo wafugaji ni duni sawa tu na kabla hajaingia Kikwete

- Hakuna program yeyote ya kutengenezwa kwa miundombinu ya kuwezesha upatikanaji wa maji ya kunywa kwa mifugo na hata wafugaji wenyewe

- Huduma za kijamii kama hospitali, shule, masoko nk zimezidi kuwa mbovu katika maeneo walikotupwa wafugaji...

Huu ni ulaghai, hii ni fedheha, hata kwa mwenyezi Mungu hii ni dhambi na ni ukiukwaji mkubwa wa haki za msingi za binadamu uliofanywa na raisi Kikwete na serikali ya CCM...

Kila siku unabadilisha ID, kwa nini? badilisha basi na avatar yako tujue wewe ni mpya humu, japo michango yako isiyo na mashiko itakutambulisha tu kuwa ni wewe.
 
Ushahidi wa haya ulioyaandika unao? Suala la wafugaji kuhama hama ni kutokana mabadiliko ya hali ya hewa kutoka eneo moja hadi lingine, sidhani kama hili liko chni ya uwezo wa JK. Hivi sasa masoko mazao yatokanayo na mifugo yameboreshwa sana ukilinganisha na zamani, Kule dodoma kuna machinjio makubwa sana yamejengwa. Madawa ya mifugo yameongezeka kwa kiasi kikubwa sana. Sina uhakika kama ulichokiandika umekifanyia utafiti au umetumia tu hoja za migogoro ya wakulima na wafugaji.

1. Kikwete alipoahidi kuwa ataboresha hali ya wafugaji, na kuwabadilisha kutoka kuwa wachungaji hadi wafugaji, akiwajengea mazingira bora yatakayowafanya wasihame, alikuwa hajui kuwa liko nje ya uwezo wake?

2. Hayo mabadiliko yanatokea Tanzania peke yake?

3. Unajua ni ng'ombe elfu ndapi walikufa wakulima walipokuwa wanahamishwa kwa nguvu Ihefu na Kilombero?

4. Kuboresha masoko bila kuboresha ufugaji unataka wafugali wakachinje mawe?

5. Hakuna madawa yeyote ya mifugo yaliyoongezeka, maelfu ya ng'ombe hufa kila siku kutokana na Ndigana moto na Ndigana baridi

6. Hakuna program yeyote ya breeding ya ng'ombe kwa wafugaji, ranch zote za taifa kuanzia Kongwa, Ruvu, nk almost zimekufa katika uongozi wa serikali ya nne...
 
Kila siku unabadilisha ID, kwa nini? badilisha basi na avatar yako tujue wewe ni mpya humu, japo michango yako isiyo na mashiko itakutambulisha tu kuwa ni wewe.

Tangia mwaka 2010 nilipojiunga JF (kipindi hicho wewe hata hujajua kutumia computer), sijawahi hata kuwaza kuwa na ID nyingine, sembuse kubadilisha...
 
Back
Top Bottom