Kikwete: Lowassa ni msafi, alisingiziwa!

Ina maana tume ya Mwakyembe wote ni wapumbavu na kazi waliyoifanya ni kazi bure?. Sasa kama Lowasa ni msafi kwanini JK alikubali na kubariki kujiuzulu kwa Lowasa?.

Ndugu zangu watanzania, nchi si yetu sote bali ni mali ya watu wachache sana. Wanafanya wapendacho na wako juu ya sheria.

Ni ukweli usiofichika kwamba watanzania wenye mapenzi ya kweli ya nchi yao wameshangazwa na kauli hii ya Jakaya (Lowasa ni MSAFI).

Tunakokwenda ni kubaya, itafika wakati watanzania wataanza kuvaa mabomu na kujilipua ama kulipua mali za mafisadi na familia zao.

Kwanini nilizaliwa mtanzania?

Hii ni kudharau bunge lote la jamhuri lililokubaliana kwa pamoja ELowasa ajiuzuru kwa sababu ya kuhusishwa katika kashfa ya Ricmond. Rais asiyeheshimu bunge ni hatari sana...ni rais asiyeweza kufuata utawala wa sheria.

Kwakweli Wa-Tz wenzangu huenda kwa maneno yetu makali na yanayoonesha chuki dhidi ya ufisadi hayatasaidia sana katika harakati za kuinasua nchi yetu kutoka mikono ya mafisadi. Nimeona na kusikia watu wengi ama kwa kujua au kutofahamu wanapenda kabisa kikwete ashinde. Yaani hawaoni kama Dr Slaa ni mkombozi wa nchi yetu kama tunavomuona siye.

Kutokana na hali hiyo nadhani itakuwa vizuri kama tukimshirikisha Mungu.

Chuki peke yake dhidi ya ufisadi inaweza kupandisha BP yako na ukafia ndani ya chumba chako peke yako. Na mtu akifa kwa sababu ya hasira dhidi ya ufisadi haina msaada sana katika harakati za kuikomboa nchi yetu kutoka kwa wezi wachache. Nawashauri watu waombe kwa Mungu, kila mtu kwa imani yake. Mungu anaweza kuleta mageuzi tunayotamani. Yeye huwainuwa wafalme na kuwashusha chini waovu. Nina imani kabisa kwamba Kikwete hakubaliki, hata mbele za Mungu, kama ilivyo kwa wanadamu hivi sasa. Mungu asipoingilia kati, pesa ina nguvu kuweza kununua kitu chochote hapa duniani kasoro uzima. Kumbukeni zile bilioni 50 .... lakini, mafisadi wapo tayari ku-spend hata mara tatu ya hiyo pesa ili kunusuru hatima yao. Hii kwa mafisadi ni struggle for survival. Ukweli ndio huo...
 
Siamini haya.kwa sababu mwakyembe ndio aöne upumbavu anaofanya.na lile li samwel sita liache kuropoka.ni hivi hao ni vibao tu vya mafisadi.wanayazunguka yanaimba kama mazuzu.unabii.sitta na mwakyembe mwisho wao mutauöna.as for kikwete,atakuwa ameshakufa.
 
Lini alifahamu kama Lowassa ni msafi? Mbona hakusema mapema hadi kampeni za 2010? Haya ni mambo ya 2015? Kweli mafisadi hawana aibu!
 
Baada ya kumpigia kampeni BAsil Mramba Rombo, JK saa Katika kampeni zake za mkoani Arusha anaelekea Monduli atakapomnadi na kufanya mazungumzo ya faragha na Lowassa

Lakini JK anatafuta kura - kwa kupitia wabunge waliopitishwa na "wananchi".
nafikiri kwa sababu hiyo lazima amsifie mbunge anayegombea hapo hata kama ni mbaya kiasi.
Lowasa ana wafuasi wengi sana kule monduli na huenda pia Arusha kwa ujumla, unafikiri JK ni mjinga amtukane EL hadharani?
 
wamasai huwaambii chochote kuhusu LOWASA.... JK hakuwa na haja ya kumnadi MONDULI wanamkubali lowasa

Ilishesemwa tangu zamani Kikwete amepewa urais na Lowasa. Kuna hadithi inasema kuwa hata iweje mbwa huwa hufurukuti kwa kobra, anajipeleka mwenyewe kumezwa.
 
Yaani Raisi ndio aliye msingizia EL au Serikali ndio iliyo msingizia Lowasa, maana kamati ya Bunge ni Sehemu ya Uongozi/utawala wa nchi yetu na Raisi aliridhia kwa kukubali kijiuzulu kwake na kuteua mwingine. "na Lowasa alililijua hilo ndio maana alitamka bayana kama shida ni uwaziri mkuu nitawapa mnachotaka"
 
Hivi Bunge liliunda kamati nyingine iliyochunguza kusingiziwa kwa EL na kumsafisha? Ladba Tido mhando na TBC. Even though EL hasafishiki kama alivyo jk (kagoda)
 
Hivi vichwa vya wa TZ vimejaa nini!??ama kweli sasa naanza kuamini kuna watu wana vichwa vigumu! yaani bado kuna watu wanampigia debe Lowasa??? Arrrghhh! Lord help!
 
Very confusing

Huyo ndiye Jakaya Mrisho Kikwete kwa wale ambao walikuwa bado hawajamfahamu - haoni, hasikii wala hashtuki. Bila haya, anawanadi Mramba na Lowassa na bila soni atawanadi Rostamu na Chenge lakini hivi vitendo vyake naamini vitamtokea puani. Hajagutuka kwamba hata CCM wenyewe sasa wamemshtukia kwamba hauziki tena na kabakiwa tu na mkewe na mwanawe. Wakereketwa wa CCM hivi sasa bila kusombwa na malori na mabasi baada ya kuahidiwa fweza, kanga, kofia na fulana, hawana muda naye tena. Hayo mabango ya picha yaliyoota kama uyoga yamekuwa kero kiasi cha wananchi walio wengi kutamani wayatemee mate.
Nasubiri kwa hamu exit msanii Kikwete, enter mpiganaji Dr. Slaa.
 
Mbona haya tuliyasema mapema jamani.. hakuna wakati wowote ambapo hawa wawili hawakuwa wamoja.. na chances ni kuwa EL atarudi kuwa Waziri Mkuu.. walianza pamoja watamaliza pamoja..si unajua tena "hawakukutana barabarani"?

Mwanakijiji,
Bunge gani hilo litakalompitisha FEL (Fisadi E. Lowassa) kuwa PM? Kama kuna serikali za majimbo wanaweza kumpa ugavana wa Monduli and NOT Tanzania. Watanzania wanaipenda sana nchi yao.
 
Kwa Jimbo la Monduli nani wa kumnadi mwingine kati ya Kikwete na Lowasa? Mimi nadhani wa kunadiwa ni Kikwete kwani Lowasa anakubalika vya kutosha
 
Kwanini huyo mmasai asipumzike akala alivyovipata kwa wizi???/
Wamasai fanyeni kama wahaya walivyomwondoa mwizi karamagi kwenye system.
Na Kikwete kumrudisha Lowassa itakuwa ni aibu kwa taifa letu.
 
Remember, the late PM Sokoine resigned, took a break and came back!
So did PM Netanyahu!
Why not Lowassa?

Red nose,
Are the circumstances similar for their resignations? BTW Sokoine > Lowassa by far.........Netanyahu lost elections....Sokoine resigned on his own accord to further his studies(and never complained about it)....Lowassa was forced to resign on corruption basis(and is complaining even this very minute over it)....see now?
 
Lazima Lowassa arudishwe Uwaziri Mkuu.. na mtakoma mliokuwa wapinzani wengine tulishaweka vichwa vyetu kwenye sahani..
 
Remember, the late PM Sokoine resigned, took a break and came back!
So did PM Netanyahu!
Why not Lowassa?


Netanyahu kichwa kingine mjomba.

Na wala akili za Wayahudi huwezi kulinganisha na matope yaliyojaa kichwani mwa wavaa vijifulana vya kijani na njano
 
Back
Top Bottom