Kikwete kwanini hataki kujaza nafasi hizi? hakuna wanaofaa?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,460
39,928
Unajua tatizo moja la kupenda kuzungusha watendaji (recycling) ni kuwa unaweza ukafika mahali ukakuta hauna watu wa kuwazungusha tena. Sasa inabidi utegee tu. Kuna katabia ambako kamekubalika kuwa nafasi fulani za juu bado ni za kundi fulani la watu na hivyo ni hao hao watazungushwa kiasi kwamba wale makada wa ngazi ya kati ni vigumu kwela kupasua paa hilo la nafasi za juu.

Matokeo yake Mkurugenzi wa taasisi moja kubwa anahamishwa na kuwa Mkurugenzi wa taasisi nyingine na vivyo hivyo hadi inafika mahali wanapofika wakati wa kustaafu hatuko tayari wastaafu kwa sababu hatuna watu wengine wa kuingia katika nafasi hizo. Matokeo yake waliostaafu wanaoengezewa muda zaidi si kwa sababu wanahitajika sana la hasha; kwa sababu "hakuna" watu wa kuchukua nafasi zao.

Lakini hili pia linaelezea matokeo ya tatizo jingine ambalo naweza kusema ni sehemu ya "gharama ya ufisadi". Unapokuwa na mfumo wa kiutawala wa ufisadi (MUK) waliomafisadi na makuwadi wao ni wengi sana kwenye system kiasi kwamba ikitokea nafasi nyeti ya kujaza ni vigumu mno kwa sababu wale wote ambao unafikiria wajaze nafasi hizo tayari wana harufu ya ufisadi fisadi.

Pia ni dalili ya mfumo mbaya ambapo hata wakurugenzi wa makampuni ambayo hayahusiani na utendaji wa serikali moja kwa moja wanateuliwa na Rais! Kwanini mtendaji wa Shirika la Bima ateuliwa na Rais? Kwanini mtendaji wa Shirika la Tanesco ateuliwe na Rais? Vipi mtendaji wa ATCL ateuliwe na Rais na wakati huo huo Rais anatakiwa ateue Mkuu wa Usalama wa Taifa n.k ?

Kama wabunge wetu wangeamua kufikiri kidogo wangeondoa mzigo huu wa uteuzi kwenye makampuni yafanyayo biashara ili wakurugenzi wake waingie kwa kushindanishwa (kuomba) na kuteuliwa na Bodi ya Wakurugenzi ambayo nayo iundwe na wadau siyo na wanasiasa.

Matokeo yake Mtawala anaamua Kusettle; yaani kuteua mtu yule ambaye aidha ni fisadi "mdebe mdebe" (mdogo) au fisadi asiyejulikana sana. Na hili linaweza kuelezea kwanini hadi leohii Rais Kikwete anapata shida ya kuachia watu wastaafu na kuteu watendaji wengine.

Hebu angalia taarifa hii kutoka katoto ka "nzi"...

Mkuu Mwanakijiji;
...

Ndege moja ya Aribus ambayo sisis tulikuwa tunakodi(iliyotimika) bei yake ikiwa mpya ni dola million 50 ba inachukua muda wa miaka mitatu mpaka unakabidhiwa ndege yao;Jiulize serikali ilikuwa inakodi kwa bei gani?mara mbili zaidi ya bei ya kununulia

tatu,Mpaka leo mashirika haya pamoja na interview kufanyika na faili kupelekwa kwa mkuu ila hajateua watendaji wa mashirika haya;sijui muungwana anafanya kazi gani

1.Mkurugenzi wa Consolidated Holdings Corporation(miaka miwili)

2.Mkurugenzi wa National Insurance Corporation(NIC)

3.Mkurugenzi wa TANESCO

4.Mkurugenzi wa TTCL

5.Mkurugenzi wa ATCL

Hao wote nafasi zao ziko acted kwa muda mrefu na hakuna maamuzi yoyote yanayofanyika;watu hawahoji kwanini inachukua muda mrefu ila hii yote ni kwasasabu tunapenda mapmbo mepesi mepesi

Shirika la NBC tunatakiwa kuteua Mwenyekiti wa Bodi ila mpaka sasa yule Mpungwe anakaimu ;matokeo yake kunakuwa na maamuzi mabovu sana katika kufanikisha


Hapo bado kuna mambo mengi yanakwama tu ukiangalia hata Luhanjo muda wake umeisha ila naye sijui nani kamuongezea muda wa kukaa pale ila anatakiwa kustaafu;


suala la mambo mepesi mepesi limenikumbusha haya
 
Unajua tatizo moja la kupenda kuzungusha watendaji (recycling) ni kuwa unaweza ukafika mahali ukakuta hauna watu wa kuwazungusha tena. Sasa inabidi utegee tu. Kuna katabia ambako kamekubalika kuwa nafasi fulani za juu bado ni za kundi fulani la watu na hivyo ni hao hao watazungushwa kiasi kwamba wale makada wa ngazi ya kati ni vigumu kwela kupasua paa hilo la nafasi za juu.

Matokeo yake Mkurugenzi wa taasisi moja kubwa anahamishwa na kuwa Mkurugenzi wa taasisi nyingine na vivyo hivyo hadi inafika mahali wanapofika wakati wa kustaafu hatuko tayari wastaafu kwa sababu hatuna watu wengine wa kuingia katika nafasi hizo. Matokeo yake waliostaafu wanaoengezewa muda zaidi si kwa sababu wanahitajika sana la hasha; kwa sababu "hakuna" watu wa kuchukua nafasi zao.

Lakini hili pia linaelezea matokeo ya tatizo jingine ambalo naweza kusema ni sehemu ya "gharama ya ufisadi". Unapokuwa na mfumo wa kiutawala wa ufisadi (MUK) waliomafisadi na makuwadi wao ni wengi sana kwenye system kiasi kwamba ikitokea nafasi nyeti ya kujaza ni vigumu mno kwa sababu wale wote ambao unafikiria wajaze nafasi hizo tayari wana harufu ya ufisadi fisadi.

Pia ni dalili ya mfumo mbaya ambapo hata wakurugenzi wa makampuni ambayo hayahusiani na utendaji wa serikali moja kwa moja wanateuliwa na Rais! Kwanini mtendaji wa Shirika la Bima ateuliwa na Rais? Kwanini mtendaji wa Shirika la Tanesco ateuliwe na Rais? Vipi mtendaji wa ATCL ateuliwe na Rais na wakati huo huo Rais anatakiwa ateue Mkuu wa Usalama wa Taifa n.k ?

Kama wabunge wetu wangeamua kufikiri kidogo wangeondoa mzigo huu wa uteuzi kwenye makampuni yafanyayo biashara ili wakurugenzi wake waingie kwa kushindanishwa (kuomba) na kuteuliwa na Bodi ya Wakurugenzi ambayo nayo iundwe na wadau siyo na wanasiasa.

Matokeo yake Mtawala anaamua Kusettle; yaani kuteua mtu yule ambaye aidha ni fisadi "mdebe mdebe" (mdogo) au fisadi asiyejulikana sana. Na hili linaweza kuelezea kwanini hadi leohii Rais Kikwete anapata shida ya kuachia watu wastaafu na kuteu watendaji wengine.

Hebu angalia taarifa hii kutoka katoto ka "nzi"...

Kazi imemshinda jamani mnataka hadi awaambie basi. Tusimchague 2010 hawezi kazi ya urais. Agombee nafasi ya uwaziri wa mambo ya nje ataendelea kubembea, ni vizuri ajijenge kwa rais mtarajiwa..
 
Lakini kweli kuna ugumu wa kujaza nafasi hizi au ndiyo vetting process ni ndefu kiasi hiki?
 
Lakini kweli kuna ugumu wa kujaza nafasi hizi au ndiyo vetting process ni ndefu kiasi hiki?
Hakuna lolote sio vetting process. Kama kuna vetting mbona kunatakataka kibao zinaingia kwenye processing system. Hiyo sasa ni vetting gani?
Nahisi sasa hivi wale yes men/Ndio mzee wanapungua sasa kwa wengi wanaonekana wakaidi na wasiostahili kulipwa na wakubwa kwa ajiri ya utii wao.
Utii usio na kikomo wenye agenda ya kuwaridhisha wakuu bila kujari gharama zake ndio unafanya baadhi ya watu wanakuwa wateule kwelikweli wakizunguka kila upande na wengine pamoja na kufaa wanatupwa nje. Hivi unajua kwa mfano kama wakikugundua ni mchangiaji hapa JF wanakuchukulia kama ni traitor?
 
Mzee Mwanakijiji,

Kuna Power Struggle Tanzania ambayo imeota mizizi kotoka vyama vya kisiasa, kuelekea Serikalini na mpaka kwenye Taasisi.

Badala ya kuwa na Utamaduni wa kuchagua watu on merit basis, tunachagua watu kutumia loyalty and pleasing!
 
Mzee Mwanakijiji,

Kuna Power Struggle Tanzania ambayo imeota mizizi kotoka vyama vya kisiasa, kuelekea Serikalini na mpaka kwenye Taasisi.

Badala ya kuwa na Utamaduni wa kuchagua watu on merit basis, tunachagua watu kutumia loyalty and pleasing!

Well said rev. Hizo nafasi zina wenyewe waungwana wala usiulize kwanini hajachaguliwa mtu. Tanzania is technical know who and not technical know how.
Sasa nafasi hizo zinasubiri wenye nafasi zao waje kuchukua wengineo mtaandika CVs zenu nzuri but mwisho wa siku hamna kitu. Mtaambiwa dah ulifanya vizuri sana katika interview but jamaa alikuwa na experience, experience anaijua bwana mkubwa.
 
Unategemea nini wakati siasa zetu, katiba yetu, sheria zetu, haziendi na wakati?

Mh. Kikwete sio mwenye haya maamuzi(aidha achague au la) anafuata muongozo uliokuwepo, nao ni, uliopitwa na wakati?

Hata wawakilishi wetu hapa bungeni hususani kamati zile kuukuu utategemea kuna vichwa ambavyo vitapitia hizi 'rubbish' na kutoa ushauri unaoenda na wakati...
Very frustrating if not intriguing?
 
Labda anasubiri wale watakaomchangia bulungutu kubwa kwenye kampeni zake za 2010 wampe majina ya nani wanaofaa katika nafasi hizo. Si unakumbuka huyo Rweyemamu aliingizwa Ikulu kupitia mgongo wa Rostam, basi nafasi hizo labda zimeachwa ili akina Rostam, Jeetu, Manji, Subhash Patel na wengineo wakishatoa mabilioni yao wampe na majina ya wale watakaofaa kupewa nyadhifa hizo nzito.
 
Labda anasubiri wale watakaomchangia bulungutu kubwa kwenye kampeni zake za 2010 wampe majina ya nani wanaofaa katika nafasi hizo. Si unakumbuka huyo Rweyemamu aliingizwa Ikulu kupitia mgongo wa Rostam, basi nafasi hizo labda zimeachwa ili akina Rostam, Jeetu, Manji, Subhash Patel na wengineo wakishatoa mabilioni yao wampe na majina ya wale watakaofaa kupewa nyadhifa hizo nzito.

Huenda marafiki wa kuwapa hizo nafasi wameisha ndo tusubiri hadi baada ya uchaguzi ila hii inaonesha kwa jinsi gani tunaongozwa kisanii nchi makini na kiongozi makini hawezi weka viporo.
 
Huenda marafiki wa kuwapa hizo nafasi wameisha ndo tusubiri hadi baada ya uchaguzi ila hii inaonesha kwa jinsi gani tunaongozwa kisanii nchi makini na kiongozi makini hawezi weka viporo.

Ndiyo ari mpya, kasi mpya na nguvu mpya ya msanii wetu hiyo. Nchi nyingine asingeruhusiwa kugombea kutokana na utendaji wake dhaifu lakini kwetu tunaambiwa chama chake kina utamaduni wa kumuachia aliyeko madarakani akae awamu mbili bila kujali maslahi ya nchi hata kama anavurunda vipi. Kweli CCM imeshika utamu. Kigumu chama cha map...Ooops! cha mafisadi! Kigumu!
 
Ndiyo ari mpya, kasi mpya na nguvu mpya ya msanii wetu hiyo. Nchi nyingine asingeruhusiwa kugombea kutokana na utendaji wake dhaifu lakini kwetu tunaambiwa chama chake kina utamaduni wa kumuachia aliyeko madarakani akae awamu mbili bila kujali maslahi ya nchi hata kama anavurunda vipi. Kweli CCM imeshika utamu. Kigumu chama cha map...Ooops! cha mafisadi! Kigumu!
Swala la kuwa CCM imeshiaka utamu si la kuhiji lipo wazi sana na yule aliyesema mawazili wanajibu mbofumbofu angesema tu selikali yetu ni mbofumbofu maana hakuna hata kero moja ya wapiga kura Jk anaweza kujigamba na kusema amerekebisha zaidi ya kupindukia kuwa Vasco Dagama.
 
Mambo yanakwenda. Hakuna haraka. Si wapo wanaokaimu nafasi hizo? Tunatakiwa kuelewa tu kwamba wanaotakiwa kwenye nafasi hizo ni wale ambao wanajua ni jinsi gani wataisaidia CCM na makada/wagombea wake kwenye uchaguzi ujao.
 
Jk urais umemshinda hilo liko wazi. ccm tuoneeni huruma watanzania tupeni mtu mwingine 2010. huo utaratibu wenu wa kutaka rais atimize vipindi viwili pasipo kuangalia maslahi ya nchi mnatupoteza. Huyu mtu hawezi na mshaurini akubali kupumzika awapishe wengine. atakuwa amejijengea heshima. asiwasikilize wachovu wakina shekh Yahya hawana lolote wagaga njaa tu.
na hao ndio wanampoteza ushauri wa wasomi hafuati anafuata wa wachawi vp jk? leo hii serikari yako inamuondoa prof; baregu pale chuoni eti muda wake wa utumishi umekwisha. muda wa utumishi wa baregu umeisha vp wa luhanjo katibu wako? bado upo? JK please tuachie Tz yetu kapumzike kwenye mijumba yako ya kifahari hapo mikocheni na chalinze . pia miaka mitano si haba utakula pension mpaka unakufa.
 
umenikumbusha aisee.. nadhani kulikuwa na nafasi mbili za wazi!!

Na ideally alitakiwa kuwapa watu kumi anaoona wanafaa kuingia kwenye cabinet lakini hawana ubunge...hiyo ndio sababu ya kupewa nafasi hiyo lakini yeye anawapa maswahiba...sofia tu ndio yuko katika cabinet....

MMM by the way hivi Mama Anna Abdallah yuko bungeni kwa msingi gani?si aliingia kama mwenyekiti wa UWT ambao hana tena?
 
Unajua tatizo moja la kupenda kuzungusha watendaji (recycling) ni kuwa unaweza ukafika mahali ukakuta hauna watu wa kuwazungusha tena. Sasa inabidi utegee tu. Kuna katabia ambako kamekubalika kuwa nafasi fulani za juu bado ni za kundi fulani la watu na hivyo ni hao hao watazungushwa kiasi kwamba wale makada wa ngazi ya kati ni vigumu kwela kupasua paa hilo la nafasi za juu.

Matokeo yake Mkurugenzi wa taasisi moja kubwa anahamishwa na kuwa Mkurugenzi wa taasisi nyingine na vivyo hivyo hadi inafika mahali wanapofika wakati wa kustaafu hatuko tayari wastaafu kwa sababu hatuna watu wengine wa kuingia katika nafasi hizo. Matokeo yake waliostaafu wanaoengezewa muda zaidi si kwa sababu wanahitajika sana la hasha; kwa sababu "hakuna" watu wa kuchukua nafasi zao.

Lakini hili pia linaelezea matokeo ya tatizo jingine ambalo naweza kusema ni sehemu ya "gharama ya ufisadi". Unapokuwa na mfumo wa kiutawala wa ufisadi (MUK) waliomafisadi na makuwadi wao ni wengi sana kwenye system kiasi kwamba ikitokea nafasi nyeti ya kujaza ni vigumu mno kwa sababu wale wote ambao unafikiria wajaze nafasi hizo tayari wana harufu ya ufisadi fisadi.

Pia ni dalili ya mfumo mbaya ambapo hata wakurugenzi wa makampuni ambayo hayahusiani na utendaji wa serikali moja kwa moja wanateuliwa na Rais! Kwanini mtendaji wa Shirika la Bima ateuliwa na Rais? Kwanini mtendaji wa Shirika la Tanesco ateuliwe na Rais? Vipi mtendaji wa ATCL ateuliwe na Rais na wakati huo huo Rais anatakiwa ateue Mkuu wa Usalama wa Taifa n.k ?

Kama wabunge wetu wangeamua kufikiri kidogo wangeondoa mzigo huu wa uteuzi kwenye makampuni yafanyayo biashara ili wakurugenzi wake waingie kwa kushindanishwa (kuomba) na kuteuliwa na Bodi ya Wakurugenzi ambayo nayo iundwe na wadau siyo na wanasiasa.

Matokeo yake Mtawala anaamua Kusettle; yaani kuteua mtu yule ambaye aidha ni fisadi "mdebe mdebe" (mdogo) au fisadi asiyejulikana sana. Na hili linaweza kuelezea kwanini hadi leohii Rais Kikwete anapata shida ya kuachia watu wastaafu na kuteu watendaji wengine.

Hebu angalia taarifa hii kutoka katoto ka "nzi"...

Kinachotumika hapa ni kujuana tu !
Hakuna cha uwezo hapa na hii staili ya CCM anayoendeleza Jakaya Mrisho Kikwete aka Vasco Da Gama kwa kukosa ubunifu kwani hata yeye amekulia kwenye hizo mbeleko ni mwendelezo wa uswahiba tu. Sijui anachelea nini kumrudishia Dr. Idris Rashid Tanesco kwani kuna kipindi alijiuzulu akamwamrisha arudi ili atekeleze matakwa ya ROSTAM AZIZ na washirika wake akina Lowasa na Karamagi. Sasa mkataba ulikwisha mwaka jana November mpaka leo ana kigugumizi cha miguu. I once said this president is very funny and has no iota of seriousness lakini waTZ hamtaki kukubali. Sababu za kuliweka shirika nyeti limbo haziingii akilini labda anataka ile ripoti ya CAG ipoe au iingie vumbi but huo mshirika wa umeme ameuacha pabaya hoi bin taabani kwa over 400bn/= in areas. Net group waliacha deni halisi la over 150bn/= baada ya five years. Huyu mmatumbi kaacha almost three fold BAADA YA KUWEPO FOR only three years? Mwache amurudishe of course atakopa tena this time 500bn/= of course kuna kauchaguzi na tunataka uwe wa kishindo where is the money by the way . Baada ya his second term angalia asiishie kupelekwa the Heague!!!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom