Kikwete kuzindua Bunge Nov.17

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,437
113,445
Wanabodi,
Uchaguzi umemalizika, japo ni kwa mtindo wa sadakalawe, mwenye kupata, kupata hata kama ni kwa kuiba, bado kapata tuu na mwenye kukosa, kakosa hata kama ni kwa kuibiwa, kudhulumiwa, kuonewa na kunyanyaswa, the bottom line ni kakosa.

Japo ni muhimu sana kukaa chini na kutafakari historia ya tulikotoka, tulipo ili tuone tunapokwenda, pia ni muhimu zaidi kutokumbatia yaliyopita ni ndwele, tungange yajayo for 2015, hivyo sasa macho yetu yote tuyaelekeze Dodoma.

Wabunge wanakusanyika rasmi Dodoma kuanzia kesho, kwanza watasajiliwa. Baada ya hapo, wataaungana na wenzao wa viti maalum. Siku ya Ijumaa asubuhi, Watamchagua Spika na naibu spika na zoezi la kuwaapisha litaanza rasmi. Watapumzika wikiendi hii kujilia kuku zao na wengi wao kutambulishwa rasmi eneo la Mnadani.

Update:
Rais, ameshaitisha tangazo la kuitisha bunge kuanzia leo.
Wabunge walioko Dar, wanajisajili pale ofisi ya Bunge, wengine watajisajilia Dodoma.
KAikao cha kwanza cha Bunge, kitaanza Alhamisi kwa vikao vya kamati za siasa za vyama kupendekeza majina ya wagombea uspika.

Saa 10:00 jioni ya Alhamisi ndipo bunge litapokea majina ya wagombea uspika.
Mkutano wa kwanza wa Bunge, utaITISHWA Ijumaa asubuhi kwa kusomwa tangazo la rais kuitisha Bunge kikifuatiwa na uchaguzi wa spika atakayeapishwa na Katibu wa Bunge, wimbo wa Taifa utapiogwa ukifuatiwa na dua na kiapo cha utii kwa wabunge wote.
Jumamosi, Jumatatu kuapishwashwa kutaendelea.

Jumanne ndio jina la waziri mkuu litafichuliwa, Waziri Mkuu atatoa hotuba ya shukrani, na utafuatia uchaguzi wa naibu spika.

Jumatano asubuhi, Waziri Mkuu mpya (wa zamani kama alivyo rais mpya) ataapishwa rasmi Ikulu ya Chamwino, saa 10:00 jioni ndipo rais atalihutubia Bunge kwa hotuba ya malengo mfano wa 'State of Nation Address' ambapo litaahirishwa rasmi mpaka kikao cha Januari, 2011 na kumalizia kwa tukio la kugonganisha glasi usiku pale katika viwanja vya bunge.

Alhamisi atatangaza baraza jipya la mawaziri. Jumamosi asubuhi, baraza hili litaapishwa rasmi katika viwanja vya Ikulu. Jumatatu inayofuatia, mawaziri wa zamani, watakabidhi ofisi kwa mawaziri wapya, serikali mpya ndio itaingia kazini rasmi.
 
mkuu mbona hiyo itakua nje ya siku saba
Acid, ni kweli iko nje ya siku 7, ila katibu inatamka kuwa bunge jipya lazima likutane ndani ya siku 7 tangu kuapishwa kwa rais. Hivyo bunge jipya liaanza kukutana Jumatano which is ndani ya siku 7 kwa majibu wa katiba, labda niirudie tena katiba nijiridhishe kama imetamka rais lazima alihutubie bunge ndani ya siku 7, then lazima tupige kelele, asiuanze muhula wake wa lala salama kwa kupindisha katiba.
 
Update:
Rais, ameshaitisha tangazo la kuitisha bunge kuanzia leo.
Wabunge walioko Dar, wanajisajili pale ofisi ya Bunge, wengine watajisajilia Dodoma.
KAikao cha kwanza cha Bunge, kitaanza Alhamisi kwa vikao vya kamati za siasa za vyama kupendekeza majina ya wagombea uspika.

Saa 10:00 jioni ya Alhamisi ndipo bunge litapokea majina ya wagombea usipika.
Mkutano wa kwanza wa Bunge, utaITISHWA Ijumaa asubuhi kwa kusomwa tangazo la rais kuitisha Bunge kikifuatiwa na uchaguzi wa spika atakayeapishwa na Katibu wa Bunge, wimbo wa Taifa utapiogwa ukifuatiwa na dua na kiapo cha utii kwa wabunge wote.
Jumamosi, Jumatatu kuapishwashwa kutaendelea.

Jumanne ndio jina la waziri mkuu litafichuliwa, Waziri Mkuu atatoa hotuba ya shukrani, na utafuatia uchaguzi wa naibu spika.

Jumatano asubuhi, waziri mkuu ataapishwa rasmi ikulu ya Chamwino, saa 10:00 jioni ndipo rais atalihutubia Bunge na kumalizia kwa tukio la kugonganisha glasi usiku pale katika viwanja vya bunge.
 
Mhh nachelea watakakuwepo kwenye hilo baraza la mawaziri je mtoto wa makamba atakuwepo? Sijui mana ameshasema mwanae asipokuwepo atashangaa kwanza anamshangaa nani wakati wao ndio wanaweka mawaziri

mzee gomezi
 
Mhh nachelea watakakuwepo kwenye hilo baraza la mawaziri je mtoto wa makamba atakuwepo? Sijui mana ameshasema mwanae asipokuwepo atashangaa kwanza anamshangaa nani wakati wao ndio wanaweka mawaziri mzee gomezi

mzee gomezi, ukiachilia mbali maneno ya baba mtu, kijana ni briliant na smart upstairs hivyo ana uwezo mkubwa kumsaidia sana JK kwenye hilo baraza jipya. Nawaombeni sana sana sana, tusiwe wepesi kuwahukumu watoto kwa majina ya baba zao.
 
mzee gomezi, ukiachilia mbali maneno ya baba mtu, kijana ni briliant na smart upstairs hivyo ana uwezo mkubwa kumsaidia sana JK kwenye hilo baraza jipya. Nawaombeni sana sana sana, tusiwe wepesi kuwahukumu watoto kwa majina ya baba zao.

Hata pale wanapoyatumia kwa maslahi yao binafsi tusiseme mkuu?
 
Jamani,

Wako wapi wakereketwa wa Dk. Slaa? Sisi wengine tulisema tangu awali kuwa kura hazitatosha! Wabunge wa Chadema walioshinda, kina Mnyika, Lisu, Lema nao wamechakachua?Karata yake ya mwisho ilikuwa kufanya uchochezi wa kuanzisha vurugu, kwa kuwasingizia Usalama wa Taifa kuwa wamechakachua ili akamatwe na kusweka rumande na baadaye wafuasi wake waandamane na kuleta fujo na baadaye iwe vurugu kubwa na hata watu wapoteze maisha katika kuzima fujo hizo! Mtego huo umemnasa mwenyewe. Matokeo yake ametahayari hata haonekani hadharani! Ameshinda jambo moja: Kuiongezea Chadema ruzuku, naye, kama mkataba aliokubaliana na kina Mbowe ulivyo, atakula Sh. Milioni 12.5 kwa mwezi! Dk. Slaa kwa Urais: Not reachable. Try again later!

Bwassa
 
Back
Top Bottom