Andindile
JF-Expert Member
- Mar 18, 2009
- 304
- 16
Habari zilizochapishwa na gazeti la Tanzania Daima la leo (Jumatano June 3 2009) zinaeleza kuwa Rais wa JMT ndugu Kikwete anatarajia kwenda Australia mnamo mwezi November au December. Aliyemtengenezea njia mkulu wetu ni waziri Membe aliyetembelea Australia hivi karibuni kutokana na mwaliko wa waziri wa mambo ya nje wa Australia ndugu Steven smith. Inasemekana kuwa safari tunazolaumu kuwa zimezidi kupita kiasi, mkulu hazitengenezi mwenyewe bali hutengenezewa na wizara ya mambo ya nje. Hii ni kutokana na kauli ya Mheshimiwa Masilingi ambaye ni mwenyekiti wa kamati ya bunge ya mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama alipokuwa ana kamati yake wakikagua mahesabu ya wizara hiyo nami namnukuu "kutokana na kazi nzuri inayofanywa na wizara hiyo (wizara ya mambo ya nje), tayari rais Kikwete amepata mwaliko mwingine wa kufanya ziara ya kikazi nchini australia, kati ya Novemba na Desemba" mwisho wa kunukuu.
Je Kikwete kabla ya kwenda Australia atatembelea nchi zipi?
Je kuna haja ya kumwekea limiti ya safari Rais wetu?
Je tuunde wizara ya mambo ya vijijini ili ishugulikie mialiko ya rais kwenda vijijini ili akahamasishe uzalishaji na uboreshaji wa miundombinu huko?
Je Kikwete kabla ya kwenda Australia atatembelea nchi zipi?
Je kuna haja ya kumwekea limiti ya safari Rais wetu?
Je tuunde wizara ya mambo ya vijijini ili ishugulikie mialiko ya rais kwenda vijijini ili akahamasishe uzalishaji na uboreshaji wa miundombinu huko?