Tetesi: Kikwete kupanda mlima Kilimanjaro kwa mara ya kwanza toka awe Rais wa Tanzania

chakii

JF-Expert Member
Sep 15, 2013
19,666
22,674
Habari wakuu.

Kuna taarifa kwamba Mhe Rais mstaafu Jakaya Kikwete kesho atapanda Mlima Kilimanjaro kwa mara ya kwanza kabisa toka awe Rais wa Tanzania.

Hizi ni habari njema japo inashangaza kidogo imekuwaje kwa kipindi chote hicho cha miaka kumi akiwa madarakani hakufanya jambo hili la Kizalendo ambalo huenda lingeongeza hamasa kwa watalii wa nje na ndani kuutembelea mlima huo mrefu kuliko yote Afrika.



Natoa pongezi kwa Mh Jk lakini vilevile viongozi wawe na Utamaduni wa kuvienzi vya nyumbani. Safari za Ughaibuni Jk hakukosa hata moja ila hapo Kilimanjaro alipasahau kabisa.


Namtakia kila la kheri kwa utalii huu wa ndani hapo kesho.

b90fd3cce8e5075bd99a52bdd074a4b8.jpg



Wasalaam...
 
Kiu salama hawezi kupanda mlima akiwa rais...hivo usilaumi.
Mpongeze sasa kwani anaokoa jahazi la utalii
 
wewe umeshapanda mlima mara ngapi ili kutekeleza hicho kitendo ulichookita cha kizalendo? mimi kila birthday yangu iki happen nipo tz huwa napanda
 
Huyu mzee apumzike, asije kuugua huko akasumbua watu, bado taifa na dunia inamuhitaji ingawa amestaafu
 
Akishuka mtujulishe.
Inachukua siku saba kupanda.
Au Tano ukichukua njia fupi .
 
Aende akatembelee tu pale chini ya mlima. ..lakini asithubutu kuupanda. ..hali ya afya yake haimruhusu na miaka imesogea. ..ache kabisa!
 
Aende akatembelee tu pale chini ya mlima. ..lakini asithubutu kuupanda. ..hali ya afya yake haimruhusu na miaka imesogea. ..ache kabisa!

tatizolako unataka kumfananisha na yule mwingine.
 
Habari wakuu.

Kuna taarifa kwamba Mhe Rais mstaafu Jakaya Kikwete kesho atapanda Mlima Kilimanjaro kwa mara ya kwanza kabisa toka awe Rais wa Tanzania.

Hizi ni habari njema japo inashangaza kidogo imekuwaje kwa kipindi chote hicho cha miaka kumi akiwa madarakani hakufanya jambo hili la Kizalendo ambalo huenda lingeongeza hamasa kwa watalii wa nje na ndani kuutembelea mlima huo mrefu kuliko yote Afrika.



Natoa pongezi kwa Mh Jk lakini vilevile viongozi wawe na Utamaduni wa kuvienzi vya nyumbani. Safari za Ughaibuni Jk hakukosa hata moja ila hapo Kilimanjaro alipasahau kabisa.


Namtakia kila la kheri kwa utalii huu wa ndani hapo kesho.

b90fd3cce8e5075bd99a52bdd074a4b8.jpg




Wasalaam...

Wacha uongo, wewe ndiyo ulikuwa unampangia safari zake hata useme hajaikosa hata moja? Au ulikuwa unampangia mabegi yake?
 
Nyerere na mkapa sina uhakika Kama walipanda,ila mwinyi.
Hata PM wote waliopita sijasijasikia kwalipanda.

Nadhani suala LA usalama huzingatiwa zaidi
 
Ulaya ilikuwa ni ishu ya muda akiwa madarakani ili wewe mtoa mada "UNYE",pia mlima hauhami wala hautaamua kukataa kupandwa,haraka ya nini?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom