Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,475
- 39,988
Hakuna ulazima wowote wa Rais Kikwete kufanya "mdahalo hewa" baada ya kura kupigwa na kujijenga kama bado ni Rais wakati wananchi wanasubiri matokeo ya Uchaguzi. Ninawashauri kina kinana kama lengo la "mdahalo hewa" wa Rais Kikwete kuwavutia wapiga kura waufanye wakati wa kampeni yaani (hadi Jumamosi). Watanzania wana haki ya kumsikiliza Kikwete ili awasaidie kufanya uamuzi wa kupiga kura.
Kitendo cha kupanga kufanya "mdahalo hewa" siku ya Jumapili, wakati kura zinasubiliwa na matokeo hayajatoka ni kitendo chenye lengo la kuandaa mazingira ya vitisho na hata kutangaza hali ya hatari hasa kama exit polls zinaonesha CCM kufanya vibaya.
Matokeo yake Rais Kikwete atatumia nguvu ya EPACT ya 1986 ambapo vyombo vyote vya habari vinaweza kupigwa marufuku kutangaza na radio zote kuanza kuimba nyimbo wanazozitaka na hivyo kuchakachua utaratibu wa kutangaza matokeo.
Kwa kufanya mazungumzo hayo usiku wa kuhesabu kura na kabla ya matokeo yote kutoka CCM inawataka wananchi wajikusanye kuandamana au kufanya vurugu ili hatimaye waweze kufungulia virungu dhidi yao.
Tutumie hekima basi tunapopanga baadhi ya mambo. Kwa vile uchaguzi utakuwa umeshapita sidhani kama kuna ulazima wa Kikwete kuzungumza usiku wa kuhesabu kura.
Kama atashinda basi atazungumza na wananchi siku ya kuapishwa. Is that too much to ask?
Kitendo cha kupanga kufanya "mdahalo hewa" siku ya Jumapili, wakati kura zinasubiliwa na matokeo hayajatoka ni kitendo chenye lengo la kuandaa mazingira ya vitisho na hata kutangaza hali ya hatari hasa kama exit polls zinaonesha CCM kufanya vibaya.
Matokeo yake Rais Kikwete atatumia nguvu ya EPACT ya 1986 ambapo vyombo vyote vya habari vinaweza kupigwa marufuku kutangaza na radio zote kuanza kuimba nyimbo wanazozitaka na hivyo kuchakachua utaratibu wa kutangaza matokeo.
Kwa kufanya mazungumzo hayo usiku wa kuhesabu kura na kabla ya matokeo yote kutoka CCM inawataka wananchi wajikusanye kuandamana au kufanya vurugu ili hatimaye waweze kufungulia virungu dhidi yao.
Tutumie hekima basi tunapopanga baadhi ya mambo. Kwa vile uchaguzi utakuwa umeshapita sidhani kama kuna ulazima wa Kikwete kuzungumza usiku wa kuhesabu kura.
Kama atashinda basi atazungumza na wananchi siku ya kuapishwa. Is that too much to ask?