MAGAMBA MATATU
JF-Expert Member
- Jul 2, 2011
- 646
- 1,174
RAIS Jakaya Kikwete ameandaa chakula cha jioni kwa wahitimu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), pamoja na wadau wengine wa elimu kuchangisha shilingi bil. 17 kwa ajili ya mradi wa kujenga kituo cha wanafunzi chuoni hapo.
Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam kwa niaba ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, Waziri Mkuu mstaafu ambaye ni Mwenyekiti wa Baraza UDSM, na rais wa wahitimu wote chuoni hapo, Jaji Joseph Warioba, alisema kituo hicho kina lengo la kupunguza tatizo la uhaba wa majengo.
Aliongeza kuwa chakula hicho ni harakati za kuelekea kilele cha maadhimisho ya miaka 50 tangu kuanzishwa kwa chuo hicho.
Warioba alisema UDSM imepata mafanikio mengi lakini inakabiliwa na uchakavu wa majengo, upungufu wa majengo ya kufundishia na maeneo ya kupumzikia.
"Idadi ya wanafunzi imeongozeka sana, ingawa wengi wao hawakai hapa wanakaa nje ya chuo. Majengo hayatoshi na mengine yamezeeka, wakati mwingine mwanafunzi ana kipindi asubuhi na jioni anakosa mahali pa kupumzikia kwa sababu anaishi nje ya chuo," alisema Warioba.
Maswali yangu ni machache tu;
1: kama hawa ndoo lile kundi linalokosa mikopo , je hizo pesa za kuchanga watazitoa wapi???
2: Kama wajibu wa serikali ni kuhakikisha kuwa miundo mbinu ya chuo kikuu kama cha UDSM inakarabatiwa ila hakuna kinachofanyika na pesa za walipa kodi zinawekwa mifukoni kwa manufaa yao na kuja tena kuwachangisha hawa walala hoi wanafunzi ili wajenge wenyewe je nini kazi ya hii serikali ya JK na kodi za watanzania zinaenda wapi?????
3: Je nikisema huu mchakato wa kutaka kuchangisha hizi pesa bilion 17 ni kwa manufaa ya BMW (Baba Mama na Watoto) kwa ajili ya huyu JK nitakuwa nimekosea????
Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam kwa niaba ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, Waziri Mkuu mstaafu ambaye ni Mwenyekiti wa Baraza UDSM, na rais wa wahitimu wote chuoni hapo, Jaji Joseph Warioba, alisema kituo hicho kina lengo la kupunguza tatizo la uhaba wa majengo.
Aliongeza kuwa chakula hicho ni harakati za kuelekea kilele cha maadhimisho ya miaka 50 tangu kuanzishwa kwa chuo hicho.
Warioba alisema UDSM imepata mafanikio mengi lakini inakabiliwa na uchakavu wa majengo, upungufu wa majengo ya kufundishia na maeneo ya kupumzikia.
"Idadi ya wanafunzi imeongozeka sana, ingawa wengi wao hawakai hapa wanakaa nje ya chuo. Majengo hayatoshi na mengine yamezeeka, wakati mwingine mwanafunzi ana kipindi asubuhi na jioni anakosa mahali pa kupumzikia kwa sababu anaishi nje ya chuo," alisema Warioba.
Maswali yangu ni machache tu;
1: kama hawa ndoo lile kundi linalokosa mikopo , je hizo pesa za kuchanga watazitoa wapi???
2: Kama wajibu wa serikali ni kuhakikisha kuwa miundo mbinu ya chuo kikuu kama cha UDSM inakarabatiwa ila hakuna kinachofanyika na pesa za walipa kodi zinawekwa mifukoni kwa manufaa yao na kuja tena kuwachangisha hawa walala hoi wanafunzi ili wajenge wenyewe je nini kazi ya hii serikali ya JK na kodi za watanzania zinaenda wapi?????
3: Je nikisema huu mchakato wa kutaka kuchangisha hizi pesa bilion 17 ni kwa manufaa ya BMW (Baba Mama na Watoto) kwa ajili ya huyu JK nitakuwa nimekosea????