abdulahsaf
JF-Expert Member
- Aug 31, 2010
- 858
- 130
[h=3][/h]
Rais Jakaya Kikwete wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Rais Jakaya Kikwete wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ameonya kuwa mchakato wa kuandika Katiba Mpya usifanywe kwa kuegemea udini, ukabila, ubinafsi, siasa ama kulenga kuvunja Muungano.
Rais Kikwete amesema hayo baada ya kuwaapisha wajumbe wa Tume ya Kuratibu Maoni ya Katiba Mpya, Ikulu, Dar es Salaam hapo Jana na kuwahutubu wajumbe wa tume hiyo akiwaambia, Tanzania hakuna udini wala ukabila, hivyo wajumbe wa Tume ya Katiba mnatakiwa kuongozwa na maoni ya wananchi siyo ya makundi mnayotoka, hatutaki ipatikane Katiba itakayoegemea udini, ukabila, siasa wala kulenga kuvunja Muungano, katiba ni ya Watanzania wote.
Tume hiyo itaanza kazi yake ya miezi 18, Mei mosi mwaka huu, kwa kukusanya maoni ya wananchi na kutengeneza rasimu ya katiba, baadaye zikifuata hatua mbili muhimu ambazo ni kuundwa kwa Bunge Maalumu la kuchambua rasimu hiyo, kisha wananchi kupiga kura ya maoni.
Rais Jakaya Kikwete wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Rais Jakaya Kikwete wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ameonya kuwa mchakato wa kuandika Katiba Mpya usifanywe kwa kuegemea udini, ukabila, ubinafsi, siasa ama kulenga kuvunja Muungano.
Rais Kikwete amesema hayo baada ya kuwaapisha wajumbe wa Tume ya Kuratibu Maoni ya Katiba Mpya, Ikulu, Dar es Salaam hapo Jana na kuwahutubu wajumbe wa tume hiyo akiwaambia, Tanzania hakuna udini wala ukabila, hivyo wajumbe wa Tume ya Katiba mnatakiwa kuongozwa na maoni ya wananchi siyo ya makundi mnayotoka, hatutaki ipatikane Katiba itakayoegemea udini, ukabila, siasa wala kulenga kuvunja Muungano, katiba ni ya Watanzania wote.
Tume hiyo itaanza kazi yake ya miezi 18, Mei mosi mwaka huu, kwa kukusanya maoni ya wananchi na kutengeneza rasimu ya katiba, baadaye zikifuata hatua mbili muhimu ambazo ni kuundwa kwa Bunge Maalumu la kuchambua rasimu hiyo, kisha wananchi kupiga kura ya maoni.